Spika Ndugai aeleza mafanikio ya Bunge la Awamu ya Tano

Lituye

JF-Expert Member
Dec 27, 2015
1,862
5,679
Yaani ukistaajabu ya Kihiyo utayaona ya bwana Ngugai. Jioni hii nimewasha TV yangu nakutana na tangazo ITV likisema Usikose kuangalia kipindi maalumu siku ya Alhamisi saa tatu usiku cha mafanikio ya Bunge la AWAMU ya Tano.

Nilicho baini kama huyu jamaa kuwa kweli ile kauli yake kuwa analo faili kule Milembe ni mahojiano mafupi yaliyo rekodiwa ktk Tangazo hilo yakimnukuu Ngugai na baadhi ya wabunge kama Mbatia.

Ngugai anaeleza mafanikio makubwa sana yaliyo patikana Katika Bunge la AWAMU ya Tano ni kuwanunulia Wabunge IPAD na kudai kuwa wamekuwa Bunge la kisasa kabisa hapa Duniani.

Hivi kweli Ngugai na wenzie wanajua mahitaji ya wananchi ?
Katika nchi ambayo wanafunzi wamefaulu wanakosa nafasi kidato cha kwanza. Serikali yake inakazana kununua Ndege tena kwa keshi.

Katika nchi ambayo watu wanatekwa na kuuwa, watu wanabambikiwa kesi za kuhujumu uchumi na utakatishaji Pesa. Watu wanapigwa risasi milangoni mwao na wanafunzi wa vyuo vikuu wanakosa mikopo.

Katika nchi ambayo Bunge linajadili mambo ya wananchi likiwa halioneshwi moja kwa moja. Limezuiwa kuoneshwa na muhimili wa serikali kwa kibri tuu.

Katika nchi ambayo Bunge linatunga sheria za kukandamiza raia wake na upinzani, Ngugai anasema watanzania tujivunie kuwa Wabunge wamenunuliwa IPAD.

Hii ni Kejeli ya kiwango cha juu kabisaa inaweza ikafika kiwango cha standard gauge. Hawa ndio aina ya wabunge tulio wachagua wakaisimamie serikali na kuishauri.

Tusifanye tena mzaha ndugu zangu October mwaka huu katika box la kupigia kura. Watu aina ya Ngugai wabakie tuu kulea wajukuu.

Asante sana.
 
Wabunge wana ipad lakini hoja wanazotoa hazina mashiko, na sheria wanazopitisha zinawakandamiza wananchi.
 
ongelea tume huru tu hakuna jipya mambo mbele kwa mbele wala hawana wasi wasi
 
Hivi mimi niwaulize tulishawahi kushinda lipi dhidi ya serikali dhidi ya uonevu wowote?
 
Mkuu Lituye ngoja nikupe taarifa tu kuwa hili Bunge la awamu ya tano, chini ya huyu "agwe" Ndugai, linashikilia rekodi ya kuwa ndiyo Bunge bovu zaidi katika historia ya nchi yetu, tokea tupate Uhuru wetu mwaka 1961!

Bunge gani linakubali kupokea maagizo toka serikalini kwa Jiwe?
 
Ebu nikumbusheni ile sheria ya kikokotoo alichokikataa mheshimiwa isitumike kilipitishwa na bunge hili au ni bunge la mama makinda
 
Lituye,
Mkuu kweli umeandika kwa hasira, mpaka umeshindwa kutaja ni TV Station gani atakuwepo kuelezea hayo mafanikio ya iPad?
 
Saivi mnajadiri iPad..Nyumbu bhana

Tuonyeshe uzi wenu watekaji mkijadili viwanda tuje tuone mnajadili nini ili tuige. We ni wale bendera fuata upepo, umesikia neno nyumbu basi na ww unaliiga ili uonekane unaenda na wakati.

Ukiambiwa uonyeshe ni uzi gani ulianzisha wenye tija humu ndani, zaidi ya kufuata nyuzi hizi hizi wanazoanzisha wanaume na ww unabaki humu humu kujadili. Sasa kuna unyumbu zaidi ya huo?
 
Bunge hili hili??
Ule utatu tuliokua tunafundishwa wa Mungu baba, Mungu mwana, na Mungu roho mtakatifu wakifanya kaz katika hali ya kugawana majukumu haupo tena saiz inatekelezwa kauli ya mtukufu Jiwe

Sent using Jamii Forums mobile app
 
..wabunge wana ipad lakini hoja wanazotoa hazina mashiko, na sheria wanazopitisha zinawakandamiza wananchi.
Bunge linalotunga sheria zisizo na maslahi ya taifa ila kandamizi na zinazolenga kudhibiti maoni mbadala ya vyama vya upinzani!
Kwa mtazamo na unafiki wenu mnaamini bunge na serikali ya awamu hii inatumikia na inapendwa na watanzania?

Shame upon you.
 
8 Reactions
Reply
Back
Top Bottom