Ajira zilikuwa zinaangalia watu wa kanda ya ziwa,,Ndugai ni spika wa hovyo kabisa asipo angaliwa vizuri atasabisha chuki kubwa sn
Siyo kweli, nje na nafasi za uteuzi ajira zilikuwa kawaida snAjira zilikuwa zinaangalia watu wa kanda ya ziwa,,
Kwaiyo ndugai yupo sahihi,,, dikteta aliharibu Nchi
Mheshimiwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Ndugai amepotosha umma mchana kweupe kudai ajira za ualimu zilizopita zilitolewa kwa misingi ya kikanda na ukabila kwa sababu ukiachilia mbali jina moja lililojirudia kila ukurasa, mchakato wa ajira zilizopita ulifanyika kwa haki na kila mwenye sifa alipata nafasi ya kuajiriwa.
Pia soma > Spika Ndugai: Ajira ziwe zinazingatia usawa wa Kijografia
Katika hatua nyingine Job Ndugai anauliza wabunge kama wapiga kura wa majimbo yao waliajiriwa kwenye ajira zilizopita. Ebu tujiulize, wapiga kura anaowasema Job ndugai ni akina nani..? Je, ni watanzania? Kama ni watanzania walitokea wapi kama sio huko huko majimboni anakokusema spika Ndugai?
Je, Spika Ndugai ana majina mfukoni ya vijana wa jimbo lake waliompigania kwenye uchaguzi anaotaka kushinikiza waajiriwe?
Nauliza hivi kwa sababu kabla mchakato wa ajira kutangazwa baadhi ya wabunge walichukua majina ya vijana majimboni kwao kwa madai kwamba wanaenda kuwapigania wapewe kipaumbele cha ajira kwa kisingizio kwamba wanajitolea. Kwa hiyo inawezekana Spika Ndugai nae yupo kwenye kundi hili ndio maana anapiga kelele ili ajenda yake ifanikiwe.
Na, kama ajira zilizopita anasema zilikuwa zimegubikwa na ukabila mbona hakusema kipindi hicho anakuja kulisema hilo leo?
Kwa kipindi chote ambacho ajira zimekuwa zikitolewa enzi za magufuli spika Ndugai alikuwa kimya wala hatukusikia akiagiza kamati za kisekta kufanya uchunguzi lakini leo kwenye utawala wa Rais Samia anaibuka na kudai kamati hizo zifanye kazi yake. Je hiki ni kielelezo kwamba Spika Ndugai alimwogopa magufuli na anamchukulia poa Rais Samia?
Kimsingi kelele za spika ndugai zimebeba ajenda binafsi nyuma yake na kama Tamisemi watazisikiliza zitakuja kuharibu mchakato wa ajira kwa sababu kama yeye amekuja na kigezo cha ukabila, mwingine atashauri kigezo kiwe umri na mwingine anaweza kushauri kigezo kiwe ni rangi nyeupe, mwisho wa siku vigezo vinakuwa vingi kuliko ajira zenyewe.
Kwa hiyo ni vyema Tamisemi mkafanya kazi yenu kwa vigezo mlivyojiwekea ili kila mwenye sifa aajiriwe as long as amehitimu mafunzo ya ualimu na ana vyeti halali lakini kutaka kusikiliza kila anachosema mwanasiasa ndio kiwe mtakuja kuharibu mchakato mzima kwa sababu wanasiasa naturally ni wabinafsi ambao kazi yao kubwa ni kulinda maslahi yao hasa ya kibunge.
Usahihi wake uko wapi kwa sababu ukichunguza vizuri hoja aliotoa utagundua ana jambo lake analotaka lifanikiwe. Kwa kuthibitisha hilo leo bungeni amekataa wazi wazi walimu wa kike kupewa kipaumbele cha ajira. Maana yake nini kama sio kuwa ana majina yake mfukoni anayotaka yapewe kipaumbele?Ukiangalia kwa jicho la Tatu Ndugai yupo sahihi kabisa.
Huku ni kujishuku upumbavu tu.Ajira zilikuwa zinaangalia watu wa kanda ya ziwa,,
Kwaiyo ndugai yupo sahihi,,, dikteta aliharibu Nchi
Yuko sahihi kwakuwa hamjajua lengo lake. Right mngejua dhamira yake kuhusu hizi ajira wala msinge mtetea.Yuko sahihi kwenye hili.
Sikatai ukanda ulikuwepo kwenye nafasi za uteuzi lakini kwenye ajira za utumishi wa umma hapakuwepo upendeleo wowote, watu waliajiriwa kwa usawa. Kwa hiyo hoja yako ya ukanda unataka kutuaminisha kwamba ajira zilizopita waliajiriwa wasukuma au watu wa kanda ya ziwa tu?Hata nami namuunga mkono maana ukanda ulizidi sana kila kitu ilikuwa ni masanjah
Ni 60%Sikatai ukanda ulikuwepo kwenye nafasi za uteuzi lakini kwenye ajira za utumishi wa umma hapakuwepo upendeleo wowote, watu waliajiriwa kwa usawa. Kwa hiyo mnataka kuniambia ajira zilizopita waliajiriwa wasukuma tu?
Kwa ratio hiyo sioni tatizo hapo. Kumbuka kanda ya ziwa ndio kanda yenye mikoa mingi na watu wengi kwahivyo ata namba ya wahitimu lazima iwe kubwa kulinganisha na kanda zingine.Ni 60%
Kama aliyaishi na kuyashuhudia mbona hakuyasema kipindi cha mwendazake?Ndugai anakumbukumbu kwa sababu ameyaishi kwa kushuhudia ajira zilivyokua zikitolewa kwa ukanda na ukabila enzi za mwendazake
Sina maana naye ni mtu safi sababu yote yaliyokua yakitokea ni mbele ya macho yake, mbele ya mmoja ya mihimili ya nchi na yeye mwenyewe akiwa kiongozi wake, tena akiwa kapewa kinga ya kutoshtakiwa mahakamani kwa atakayoyatenda mjengoni. Alishindwa nini kuunda kamati ya Bunge kuchunguza hayo enzi zile?
Jiwe alikuwa mbaguzi sanaKwa ratio hiyo sioni tatizo hapo. Kumbuka kanda ya ziwa ndio kanda yenye mikoa mingi na watu wengi kwahivyo ata namba ya wahitimu lazima iwe kubwa kulinganisha na kanda zingine.
Ndani ya ccm bado hakuna msafiKama aliyaishi na kuyashuhudia mbona hakuyasema kipindi cha mwendazake?
Ndo mjue spika ana ajenda yake iliyojificha nyuma ya hizi ajira
Atuambie uchaguzi wa LG 2019 na GE 2020 ilikuwaje kwanza ?mbona mmezoea huo upendeleo shauri yenu siku zaja ndio mtajua hamjui&€*£%/=÷×??Ccm, Ndugai! Wote ni janga tu la Taifa.