Spika Ndugai aache kupotosha umma kwamba ajira zinatolewa kwa upendeleo wa kikabila na kikanda

Mheshimiwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Ndugai amepotosha umma mchana kweupe kudai ajira za ualimu zilizopita zilitolewa kwa misingi ya kikanda na ukabila kwa sababu ukiachilia mbali jina moja lililojirudia kila ukurasa, mchakato wa ajira zilizopita ulifanyika kwa haki na kila mwenye sifa alipata nafasi ya kuajiriwa.

Pia soma > Spika Ndugai: Ajira ziwe zinazingatia usawa wa Kijografia

Katika hatua nyingine Job Ndugai anauliza wabunge kama wapiga kura wa majimbo yao waliajiriwa kwenye ajira zilizopita. Ebu tujiulize, wapiga kura anaowasema Job ndugai ni akina nani..? Je, ni watanzania? Kama ni watanzania walitokea wapi kama sio huko huko majimboni anakokusema spika Ndugai?

Je, Spika Ndugai ana majina mfukoni ya vijana wa jimbo lake waliompigania kwenye uchaguzi anaotaka kushinikiza waajiriwe?

Nauliza hivi kwa sababu kabla mchakato wa ajira kutangazwa baadhi ya wabunge walichukua majina ya vijana majimboni kwao kwa madai kwamba wanaenda kuwapigania wapewe kipaumbele cha ajira kwa kisingizio kwamba wanajitolea. Kwa hiyo inawezekana Spika Ndugai nae yupo kwenye kundi hili ndio maana anapiga kelele ili ajenda yake ifanikiwe.

Na, kama ajira zilizopita anasema zilikuwa zimegubikwa na ukabila mbona hakusema kipindi hicho anakuja kulisema hilo leo?

Kwa kipindi chote ambacho ajira zimekuwa zikitolewa enzi za magufuli spika Ndugai alikuwa kimya wala hatukusikia akiagiza kamati za kisekta kufanya uchunguzi lakini leo kwenye utawala wa Rais Samia anaibuka na kudai kamati hizo zifanye kazi yake. Je hiki ni kielelezo kwamba Spika Ndugai alimwogopa magufuli na anamchukulia poa Rais Samia?

Kimsingi kelele za spika ndugai zimebeba ajenda binafsi nyuma yake na kama Tamisemi watazisikiliza zitakuja kuharibu mchakato wa ajira kwa sababu kama yeye amekuja na kigezo cha ukabila, mwingine atashauri kigezo kiwe umri na mwingine anaweza kushauri kigezo kiwe ni rangi nyeupe, mwisho wa siku vigezo vinakuwa vingi kuliko ajira zenyewe.

Kwa hiyo ni vyema Tamisemi mkafanya kazi yenu kwa vigezo mlivyojiwekea ili kila mwenye sifa aajiriwe as long as amehitimu mafunzo ya ualimu na ana vyeti halali lakini kutaka kusikiliza kila anachosema mwanasiasa ndio kiwe mtakuja kuharibu mchakato mzima kwa sababu wanasiasa naturally ni wabinafsi ambao kazi yao kubwa ni kulinda maslahi yao hasa ya kibunge.

Spika aboreshe shule za Kongwa kwanza ili awe na kigezo cha kulalamika. Huyu spika mlimtolea wapi?
 
Utumishi wa umma ni Dhamana tu sio mali ya mtu binafsi au kampuni ya mtu binafsi.

kuna baadhi ya viongozi wanajisahau sana wana dhani kuwa kiongozi ndani ya utumishi ni sawa na kumiliki kampuni yako binafsi na hivyo unaweza kumuweka mtu unaye jisikia au kumpenda na kumuacha usiye mpenda.....hapana!.

unaweza kufanya hayo endapo tu una miliki kampuni yako binafsi lkn sio ktk utumishi wa umma.
 
Ukiangalia kwa jicho la Tatu Ndugai yupo sahihi kabisa.
Usahihi wake uko wapi kwa sababu ukichunguza vizuri hoja aliotoa utagundua ana jambo lake analotaka lifanikiwe. Kwa kuthibitisha hilo leo bungeni amekataa wazi wazi walimu wa kike kupewa kipaumbele cha ajira. Maana yake nini kama sio kuwa ana majina yake mfukoni anayotaka yapewe kipaumbele?
 
Nafasi hitajika ni 6000 waombaji wenye sifa ni zaidi ya 700,000 iv kwann serikal isirejeshe mazingira mazurinya private sectors kujazilizia uhaba wa ajira
 
Ajira zilikuwa zinaangalia watu wa kanda ya ziwa,,

Kwaiyo ndugai yupo sahihi,,, dikteta aliharibu Nchi
Huku ni kujishuku upumbavu tu.

Magu hakuwahi kupendelea watu wa kanda ya ziwa wala wasukuma.

Magu alikuwa na genge lake maalum alilotoka nalo wizara ya ujenzi hasa TANROADS ndio alikuwa anakomaa nalo.

Watu wake wengi wa karibu siyo watu wa kanda ya ziwa.
  • Mfugale
  • Kijazi
  • Kabudi
  • Ndugai
-

Na mnaposema kanda ya ziwa mnaijua vizuri, ni mtu gani alikuwa na ukaribu na Magu kutokea Mara ?
 
Hata nami namuunga mkono maana ukanda ulizidi sana kila kitu ilikuwa ni masanjah
Sikatai ukanda ulikuwepo kwenye nafasi za uteuzi lakini kwenye ajira za utumishi wa umma hapakuwepo upendeleo wowote, watu waliajiriwa kwa usawa. Kwa hiyo hoja yako ya ukanda unataka kutuaminisha kwamba ajira zilizopita waliajiriwa wasukuma au watu wa kanda ya ziwa tu?
 
Sikatai ukanda ulikuwepo kwenye nafasi za uteuzi lakini kwenye ajira za utumishi wa umma hapakuwepo upendeleo wowote, watu waliajiriwa kwa usawa. Kwa hiyo mnataka kuniambia ajira zilizopita waliajiriwa wasukuma tu?
Ni 60%
 
Kwa ujumla, binadamu hatustahili kufurahia kifo cha mwanadamuwenzetu awaye yeyote.

Mimi sifurahiibkifo cha Mwendazake lakini nimefurahia sana kuondoka kwake kwenye nafasi ya Urais. Maana kama angeendelea, sijui huko mbeleni kungetokea nini!!

Alikuwa ameanza kupandikiza mbegu mbaya ya ukabila, ukanda na undugu. Ukuaji wa uchumi alikuwa anaudondosha kwa kasi ya ajabu.
 
Alichosema Job kina ukweli sana tu.

Mfano ni wizara ya Afya,alivyokuwepo Ummy mwalimu,watu wa Tanga wengi wamepata shavu sana.

Mfano tu baraza la wafamasia.Watu waliopata scholarship wakati wake kutoka Tanga ni wengi.
Wapare nao wameingia kwa kasi ya ajabu.
Kifupi tu ni kwamba ubaguzi wa jinsi hii ulianza kuthaminiwa wakati wa JK na ukapigwa muhuri wakati wa JPM.
Sasa mama wanampima imani.
 
Ndugai anakumbukumbu kwa sababu ameyaishi kwa kushuhudia ajira zilivyokua zikitolewa kwa ukanda na ukabila enzi za mwendazake

Sina maana naye ni mtu safi sababu yote yaliyokua yakitokea ni mbele ya macho yake, mbele ya mmoja ya mihimili ya nchi na yeye mwenyewe akiwa kiongozi wake, tena akiwa kapewa kinga ya kutoshtakiwa mahakamani kwa atakayoyatenda mjengoni. Alishindwa nini kuunda kamati ya Bunge kuchunguza hayo enzi zile?
Kama aliyaishi na kuyashuhudia mbona hakuyasema kipindi cha mwendazake?
Ndo mjue spika ana ajenda yake iliyojificha nyuma ya hizi ajira
 
Kwa ratio hiyo sioni tatizo hapo. Kumbuka kanda ya ziwa ndio kanda yenye mikoa mingi na watu wengi kwahivyo ata namba ya wahitimu lazima iwe kubwa kulinganisha na kanda zingine.
Jiwe alikuwa mbaguzi sana
 
Back
Top Bottom