Spika Ndugai aache kupotosha umma kwamba ajira zinatolewa kwa upendeleo wa kikabila na kikanda

Mhe. Ndugai amenena jambo la muhimu sana kwa Taifa letu, jambo ambalo wengi walilifumbia macho lkn lina hatarisha umoja wa taifa letu nalo ni mgawanyo wa ajira na nafasi za uteuzi serikalini ulio sawia na wa haki, kimaeneo na hata kiimani, sio sahihi kujaza ktk utumishi wa umma watu wa aina mmoja halafu wengine wengi wakatupwa nje, hilo sio sahihi kabisa kwa ustawi na uzalendo wa taifa letu, lazima jambo hilo.litazamwe kwa kuzingatia sifa, usawa wa maeneo na hata usawa wa imani zote kushiriki ktk ujenzi wa taifa lao utaleta na kuimarisha uzalendo.

kama tuna bisha kauli ya Mhe. Spika nashauri kila taasisi ya Serikali ifanye utafiti kubaini ukweli, na utaona kuna aina ya watu fulani ndio wame hodhi karibu nafasi zote ktk taasisi za serikali.
dini,kabila na maeneo atokayo mtu sio kigezo cha kupewa kazi au uteuzi, ujuzi,elimu na weledi ktk kazi ndivyo vinaamua, dini wakachuguane huko kwenye dini zao, na makabila huko wanakoenda kutambika. Tanzania haina dini wala haina kabila, Tanzania ni ya Watanzania wote.
 
Naunga mkono 100%
Sioni usahihi wa Spika kwenye hili, wabunge wanatofautiana ushawishi na uwezo wa kuzonga na kuzengea.Hi inaweza kupelekea baadhi ya wabunge wasio na ushawishi kukosa au kupata idadi ndogo kwenye majimbo yao,na wale ma veterani kwenye ushawishi kujizolea idadi kubwa kwenye majibo yao.

Bunge lilitakiwa kuhakikisha kuwepo kwa rationaleya mgao kwa majimbo yote.
Spika kushawishi wabunge wafanye lobbying ni kiashiria cha Bunge kupoteza mwelekeo.
 
...
Mhe. Ndugai amenena jambo la muhimu sana kwa Taifa letu, jambo ambalo wengi walilifumbia macho lkn lina hatarisha umoja wa taifa letu nalo ni mgawanyo wa ajira na nafasi za uteuzi serikalini ulio sawia na wa haki, kimaeneo na hata kiimani, sio sahihi kujaza ktk utumishi wa umma watu wa aina mmoja halafu wengine wengi wakatupwa nje, hilo sio sahihi kabisa kwa ustawi na uzalendo wa taifa letu, lazima jambo hilo.litazamwe kwa kuzingatia sifa, usawa wa maeneo na hata usawa wa imani zote kushiriki ktk ujenzi wa taifa lao utaleta na kuimarisha uzalendo.

kama tuna bisha kauli ya Mhe. Spika nashauri kila taasisi ya Serikali ifanye utafiti kubaini ukweli, na utaona kuna aina ya watu fulani ndio wame hodhi karibu nafasi zote ktk taasisi za serikali.
Hilo Jambo limeanza leo? Yeye alikuwa wapi? Wakati jpm anateua viongozi wote wa vyombo nyeti toka Kanda moja yeye alikuwa wapi? Acheni unafiki.Aseme mwingine Sio spika ndugai
 
dini,kabila na maeneo atokayo mtu sio kigezo cha kupewa kazi au uteuzi, ujuzi,elimu na weledi ktk kazi ndivyo vinaamua, dini wakachuguane huko kwenye dini zao, na makabila huko wanakoenda kutambika. Tanzania haina dini wala haina kabila, Tanzania ni ya Watanzania wote.
hakuna tatizo kama hawalalamiki, lkn kama wana lalamika ujue kuna tatizo lina nyemelea, jambo la msingi kama alivyo sema Spika ni kuweka mseto, nchi imara ni ile inayo jengwa na watu wote, wote wahisi hii ni nchi yao.

yaliyo semwa wakati ule na Mwalimu yali kidhi mahitaji ya kipindi kile sio nyakati hizi tena.
lazima viongozi wetu wabadilike haraka sana.
 
...wakati unzidi spika wa bunge alikuwa nani
Alikuwepo palepale kwenye kiti chake cha enzi,
Lkn kutokana na mfumo wa utawala ulivyokuwa ni kuwa kila mtu alikuwa anakimbiza bawa lake ili maisha yasonge.

Leo hii tunamuona mama Samia akiyakataa yale yote yaliyokuwa yanakubalika kipindi cha awamu ya 5 na yeye alikuwa mwana familia ya hiyo awamu.
 
Yeye mwenyewe tu ameingiza wabunge feki bungeni, huo uhalali wa kuhoji watumishi kwenye kada zilizotangazwa anapata wapi?

Sawa kabisa, yeye Ndugai na wabunge wenzake wa ccm waseme wameingiaje bungeni, mpaka yeye leo aweze kuhoji weledi wa taasisi nyingine.
 
Haahaa
Alikuwepo palepale kwenye kiti chake cha enzi,
Lkn kutokana na mfumo wa utawala ulivyokuwa ni kuwa kila mtu alikuwa anakimbiza bawa lake ili maisha yasonge.

Leo hii tunamuona mama Samia akiyakataa yale yote yaliyokuwa yanakubalika kipindi cha awamu ya 5 na yeye alikuwa mwana familia ya hiyo awamu.
Unafiki mtupu....
 
...
hakuna tatizo kama hawalalamiki, lkn kama wana lalamika ujue kuna tatizo lina nyemelea, jambo la msingi kama alivyo sema Spika ni kuweka mseto, nchi imara ni ile inayo jengwa na watu wote, wote wahisi hii ni nchi yao.

yaliyo semwa wakati ule na Mwalimu yali kidhi mahitaji ya kipindi kile sio nyakati hizi tena.
lazima viongozi wetu wabadilike haraka sana.
Huo mseto umuhimu wake unaonekana leo? Spika alikuwa wapi wakati Jpm anaweka watu toka Kanda moja?
 
Mheshimiwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Ndugai amepotosha umma mchana kweupe kudai ajira za ualimu zilizopita zilitolewa kwa misingi ya kikanda na ukabila kwa sababu ukiachilia mbali jina moja lililojirudia kila ukurasa, mchakato wa ajira zilizopita ulifanyika kwa haki na kila mwenye sifa alipata nafasi ya kuajiriwa.

Pia soma > Spika Ndugai: Ajira ziwe zinazingatia usawa wa Kijografia

Katika hatua nyingine Job Ndugai anauliza wabunge kama wapiga kura wa majimbo yao waliajiriwa kwenye ajira zilizopita. Ebu tujiulize, wapiga kura anaowasema Job ndugai ni akina nani..? Je, ni watanzania? Kama ni watanzania walitokea wapi kama sio huko huko majimboni anakokusema spika Ndugai?

Je, Spika Ndugai ana majina mfukoni ya vijana wa jimbo lake waliompigania kwenye uchaguzi anaotaka kushinikiza waajiriwe?

Nauliza hivi kwa sababu kabla mchakato wa ajira kutangazwa baadhi ya wabunge walichukua majina ya vijana majimboni kwao kwa madai kwamba wanaenda kuwapigania wapewe kipaumbele cha ajira kwa kisingizio kwamba wanajitolea. Kwa hiyo inawezekana Spika Ndugai nae yupo kwenye kundi hili ndio maana anapiga kelele ili ajenda yake ifanikiwe.

Na, kama ajira zilizopita anasema zilikuwa zimegubikwa na ukabila mbona hakusema kipindi hicho anakuja kulisema hilo leo?

Kwa kipindi chote ambacho ajira zimekuwa zikitolewa enzi za magufuli spika Ndugai alikuwa kimya wala hatukusikia akiagiza kamati za kisekta kufanya uchunguzi lakini leo kwenye utawala wa Rais Samia anaibuka na kudai kamati hizo zifanye kazi yake. Je hiki ni kielelezo kwamba Spika Ndugai alimwogopa magufuli na anamchukulia poa Rais Samia?

Kimsingi kelele za spika ndugai zimebeba ajenda binafsi nyuma yake na kama Tamisemi watazisikiliza zitakuja kuharibu mchakato wa ajira kwa sababu kama yeye amekuja na kigezo cha ukabila, mwingine atashauri kigezo kiwe umri na mwingine anaweza kushauri kigezo kiwe ni rangi nyeupe, mwisho wa siku vigezo vinakuwa vingi kuliko ajira zenyewe.

Kwa hiyo ni vyema Tamisemi mkafanya kazi yenu kwa vigezo mlivyojiwekea ili kila mwenye sifa aajiriwe as long as amehitimu mafunzo ya ualimu na ana vyeti halali lakini kutaka kusikiliza kila anachosema mwanasiasa ndio kiwe mtakuja kuharibu mchakato mzima kwa sababu wanasiasa naturally ni wabinafsi ambao kazi yao kubwa ni kulinda maslahi yao hasa ya kibunge.
Hawa wote yani Ndugai na TAMISEMI wote wana matatizo hasa TAMISEMI kuna figisu sana kwenye suala la ajira upendeleo na vimemo ndio kinachoendelea pale kwa hiyo huu msuguano unazidi kutuonyesha sisi wananchi sarakasi zilivyo huko lakini tukumbuke tu kuwa nafasi mlizonazo sasa hivi ipo siku mtatolea hesabu kwa Mungu hii nchi ni yetu sote hivi tukiendekeza upendeleo kiasi hiki je watoto wa masikini wasio na watu wao TAMISEMI au kujuana na watu watu wakubwa kama spika ina maana hawatapata ajira? je kama hawatapa ajira hamuoni manawaumiza?
 
hakuna tatizo kama hawalalamiki, lkn kama wana lalamika ujue kuna tatizo lina nyemelea, jambo la msingi kama alivyo sema Spika ni kuweka mseto, nchi imara ni ile inayo jengwa na watu wote, wote wahisi hii ni nchi yao.

yaliyo semwa wakati ule na Mwalimu yali kidhi mahitaji ya kipindi kile sio nyakati hizi tena.
lazima viongozi wetu wabadilike haraka sana.
Hata kama wanalalamika wanatakiwa wajue ukweli, huwezi kupewa kazi au cheo kwa sababu ya dini,ukabila au ukanda. kwani watu wataanza kulalamika huduma mbovu, maendeleo hakuna na uonevu. kama we ni wa dini nenda kafanya kazi kwenye dini yako, kama ni kabila kahudumia mizimu na kutambika kama unataka Ukanda baki nyumbani kwenu ukiangalia milima na mabonde. kama ni kazi ya serikali lazima uwe na Elimu, ujuzi na weledi
 
Ukiangalia kwa jicho la Tatu Ndugai yupo sahihi kabisa.
Sahihi kuanzia lini? Alikuwa wapi miaka Mitano iliyopita, ambayo ilikuwa imejaa Kila Aina ya injustice. Anatoa wapi moral authority kusema hayo wakati yeye mwenyewe ni unjust. Unakataliaje wabunge ambao wamefukuzwa kwenye chama Chao kwa sababu ya irreguraties walizocheza na unawapa haki kinyume Cha Sheria za nchi.
Uliona wapi Ndugai akiwa mtu mwenye haki na sober?
Apuuzwe!
 
Mheshimiwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Ndugai amepotosha umma mchana kweupe kudai ajira za ualimu zilizopita zilitolewa kwa misingi ya kikanda na ukabila kwa sababu ukiachilia mbali jina moja lililojirudia kila ukurasa, mchakato wa ajira zilizopita ulifanyika kwa haki na kila mwenye sifa alipata nafasi ya kuajiriwa.

Pia soma > Spika Ndugai: Ajira ziwe zinazingatia usawa wa Kijografia

Katika hatua nyingine Job Ndugai anauliza wabunge kama wapiga kura wa majimbo yao waliajiriwa kwenye ajira zilizopita. Ebu tujiulize, wapiga kura anaowasema Job ndugai ni akina nani..? Je, ni watanzania? Kama ni watanzania walitokea wapi kama sio huko huko majimboni anakokusema spika Ndugai?

Je, Spika Ndugai ana majina mfukoni ya vijana wa jimbo lake waliompigania kwenye uchaguzi anaotaka kushinikiza waajiriwe?

Nauliza hivi kwa sababu kabla mchakato wa ajira kutangazwa baadhi ya wabunge walichukua majina ya vijana majimboni kwao kwa madai kwamba wanaenda kuwapigania wapewe kipaumbele cha ajira kwa kisingizio kwamba wanajitolea. Kwa hiyo inawezekana Spika Ndugai nae yupo kwenye kundi hili ndio maana anapiga kelele ili ajenda yake ifanikiwe.

Na, kama ajira zilizopita anasema zilikuwa zimegubikwa na ukabila mbona hakusema kipindi hicho anakuja kulisema hilo leo?

Kwa kipindi chote ambacho ajira zimekuwa zikitolewa enzi za magufuli spika Ndugai alikuwa kimya wala hatukusikia akiagiza kamati za kisekta kufanya uchunguzi lakini leo kwenye utawala wa Rais Samia anaibuka na kudai kamati hizo zifanye kazi yake. Je hiki ni kielelezo kwamba Spika Ndugai alimwogopa magufuli na anamchukulia poa Rais Samia?

Kimsingi kelele za spika ndugai zimebeba ajenda binafsi nyuma yake na kama Tamisemi watazisikiliza zitakuja kuharibu mchakato wa ajira kwa sababu kama yeye amekuja na kigezo cha ukabila, mwingine atashauri kigezo kiwe umri na mwingine anaweza kushauri kigezo kiwe ni rangi nyeupe, mwisho wa siku vigezo vinakuwa vingi kuliko ajira zenyewe.

Kwa hiyo ni vyema Tamisemi mkafanya kazi yenu kwa vigezo mlivyojiwekea ili kila mwenye sifa aajiriwe as long as amehitimu mafunzo ya ualimu na ana vyeti halali lakini kutaka kusikiliza kila anachosema mwanasiasa ndio kiwe mtakuja kuharibu mchakato mzima kwa sababu wanasiasa naturally ni wabinafsi ambao kazi yao kubwa ni kulinda maslahi yao hasa ya kibunge.
Ndugai angalia na kutunza ulimi. Ya bandari Bagamoyo hatujasahau umeanza ajira za ualimu.
 
Back
Top Bottom