Spika Makinda ampiga Stop Stephen Ngonyani kumshambulia Dr Ulimboka

[h=3]Hii ndiyo hasara ya kuchagua waganga wa kienyeji na matapeli kuwa wabunge[/h]

Profesa+maji+marefu.JPG

Nani angeamini kuwa mbunge ambaye ni mwakilishi wa wananchi angeshangilia uvunjaji sheria na haki za binadamu? Imetokea tena bungeni ambapo mbunge wa Korogwe Vijijini Steven Ngonyani aka Maji Marefu kusema eti kipigo alichopata mwenyekiti wa Jumuia ya Madaktari, Dk Steven Ulimboka kilistahili. Laiti bunge letu lingekuwa ni bunge huyu alipaswa kuwajibishwa mara moja. Maana hii si kashfa ya kawaida.

weka picha yake ile amabyo inamuonesha na P.o.P,anasema amechanganyikiwa na ugonjwa pamoja na kuzushiwa kifo thats why amesema asitibiwe,,,,
 
Kweli shukrani ya punda ni mateke!
Huyu maji marefu kaja Muhimbili hata miezi mitatu haijapita alikuwa NA Hali mbaya sana anaharisha damu tumemsaidia sana mpaka mwishowe tukampeleka India Leo hii shukurani yake kwa madaktari ni kushangilia Jemedari wetu kupigwa NA watu wa secret service.
Nina imani ule ugonjwa wake atakua hajapona, ole wake alete makanyagio Muhimbili, atatujua sisi ni nani!
Usitukane Wakunga Uzazi Ungalipo!
 
Mbunge kusema alichosema ni jambo moja, lakini response ya Spika ndio itasumbua wengi. Hivi ange-react hivyo hivyo kama angekuwa ni mbunge wa upinzani? Spika anawaundia zengwe wabunge wa ccm na wananchi.
 
hajui alitendalo ameshazoea kuua watu kwa uchawi wake.... kwa hiyo kwa hili yeye ni kawaida sana... mungu amsaidie kwa kweli
 
Hasara na nitatizo kwa mstakabali wa maendeleo ya taifa letu kuwa na wawakilishi kama hawa waliozoea kurubani watu kwa mapepo.Watu wenye roho mbaya kama huyu hawawezi kutetea wananchi.Umaskini wetu utaendelea kututafuna hadi hapo watanzania tutakapoamuka maana tumezidi kulala
 
katika mchango wake bungeni leo mbunge wa Korogwe kawatonesha madaktari kidonda! Kasema kama madaktari wamegoma kutibu watu kwa nini wanamtibu dr. Ulimboka? Madam Spika ikabidi amzuie kwamba swala liko mahakamani! Mi nadhani afya yake mgogoro angeishauri serikali yake

anafikiri kwakutumia masaburi, yeye anafikiri haki inapatikana kwa kuuwa ama kwa nguvu?
 
Huyu ni mchawi, tanzania ni nchi ya pekee kuwa na mchawi bungeni
 
Ndiyo matatizo ya kuwa na Wabunge DHAIFU ambao hawana hata sifa ya kuwa wajumbe wa nyumba kumi kumi....Pumbavu kabisa!!
 
Hata kama mtu nia adui yako vipi, si busara linapofikia swala la matatizo kufurahia
 
Mbunge wa Korogwe-CCM Stephen Ngonyani(Profesa Maji Marefu) amemshambulia vikali Dr Stephen Ulimboka na kuwataka madaktari wasimtibu.Spika Makinda ilibidi aingilie kati na kumuamuru Ngonyani kuacha mara moja kuzungumzia suala hilo ndani ya bunge kwa sababu liko mahakamani.Ngonyani akajitetea kuwa amechanganyikiwa kwa sababu aliumwa sana na watu wakamzushia kifo.Kabla ya kuwa Mbunge Ngonyani amewahi kuwa mganga wa kienyeji.Kauli hiyo ya Ngonyani ilionekana kushangiliwa sana na wabunge wenzake wa CCM.

Ngonyani ni sehemu tu wabunge genius wa SISIEMU. Sasa go-figure waliobaki ambao si ma-genius wakoje?
 
ni bora alikiri mwenyewe kukataa Jemedar Ulimboka asitibiwe ni ukweli mtupu kwamba alikuwakachanganyikiwa + kupandwa na pepo mchafu
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom