Spika Makinda amfagilia David Kafulila bungeni leo

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
46,993
144,329
Katika hali isiyo ya kawaida,Spika Makinda leo hii asubuhi wakati wa mjadala wa wizara ya fedha alisifu mchango wa mh.Kafulila alipochangia katika bajeti ya wizara ya fedha.

Kilichotokea ni kuwa muda wa mh.Kafulila kuchangia ulikuwa umeisha ila spika alikuwa amapetiwa kuangalia muda na hivyo Kafulila akaendelea kuchangia kidogo huku muda wake ukiwa umeisha.Baaada ya spika kugundua kuwa muda wa Kafulila umekwisha na sijui ilikuwa ni baada ya kushituliwa na wasaidizi wake au ni yeye mwenyewe tu alisema maneno matamu ya Kafulila yamemfanya apitiwe kuangalia muda.

Ni kweli leo Kafulila alifunguka kwa kiasi kikubwa kwa kuiponda serikali kwa kushindwa kuhakikisha makampuni mengi ya kibiashara yanaingizwa katika list ya Dar-es-salaam Stock Exchange(DSE) na hivyo kukwepa kulipa kodi na hivyo serikali kupoteza mapato. Kafulila alieleza kwa kirefu na kwa kutoa mifano ya makampuni kama vile airtel n.k yanavyoibia serikali kwasababu tu hayajaorodheshwa katika orodha hiyo ya DSE huku akiishushia lawama nzito serikali kwa uzembe huu.Mh.Kafulila aliisifu kampuni ya bia ambayo imeorodheshwa katika soko la hisa Dar-es-salaam(DSE) kwa kulipa kodi kubwa serikali licha ya serikali kuwa na hisa ya asilimia 4 tu huku kampuni ya airtel ambayo serikali ina hisa ya asilimia 40 ikilipa kiasi kidogo cha kodi serikalini.Kafulila ameishangaa serikali ni kwanini makampuni mengine hayaorodheshwe katika list hiyo ya DSE.Mh.Kafulila amedai kuna watu wanafaidika na uzembe huu na ndio mana makampuni hayo hayaorodheshwe katika list ya DSE.

Mchango huo wa Kafulila ndio ulimfanya spika ajisahau kuangalia muda na kukiri kuwa Kafulila alikuwa na maneno matamu ya kumsililiza.
 
  • Thanks
Reactions: mij
Sasa YATOSHA wakiingia tena kwenye DSE sijui watajiiteje maana wahindi kwa kukwepa kodi ndiyo zao, kuna sehemu flani wahindi wanaingiziwa hela direct kwenye account zao.Mfano utakuta mshahara wa Wahindi Expart ni shilingi milioni 8 take home lakini kwenye salary slip wanaandika eti anapata laki 8 huku zingine zote hizo zinakwenda direct kwenye account zao.kwa kusema hivo ina maana wanailipa serikali PAY ES YOU EARN ndogo sana na pia na expatriate fee nayo inakuwa ndogo.But sishangai kwa sababu tunaoibomoa nchi ni sisi wenyewe Watanzania maana Finance Director ni Mtanzania tena ana masters na CPA na hivi navoongea yupo bungeni eti kusikiliza budget ya wizara ya fedha.UKITAKA JINA LA KAMPUNI NINALO NA USHAHIDI WA MISHAHARA YA MIEZI KUMI NTAWALETEA
 
Sasa YATOSHA wakiingia tena kwenye DSE sijui watajiiteje maana wahindi kwa kukwepa kodi ndiyo zao, kuna sehemu flani wahindi wanaingiziwa hela direct kwenye account zao.Mfano utakuta mshahara wa Wahindi Expart ni shilingi milioni 8 take home lakini kwenye salary slip wanaandika eti anapata laki 8 huku zingine zote hizo zinakwenda direct kwenye account zao.kwa kusema hivo ina maana wanailipa serikali PAY ES YOU EARN ndogo sana na pia na expatriate fee nayo inakuwa ndogo.But sishangai kwa sababu tunaoibomoa nchi ni sisi wenyewe Watanzania maana Finance Director ni Mtanzania tena ana masters na CPA na hivi navoongea yupo bungeni eti kusikiliza budget ya wizara ya fedha.UKITAKA JINA LA KAMPUNI NINALO NA USHAHIDI WA MISHAHARA YA MIEZI KUMI NTAWALETEA
Mkuu naomba tuletee huo ushahidi mapema iwezekanavyo
 
Serikali yenyewe kwani inasikia ama inaona? Hata ukitoa mawazo mazuri kiasi gani lakini ukweli unabaki kuwa serikali ya ccm imevaa miwani ya mbao.
 
Mkuu naomba tuletee huo ushahidi mapema iwezekanavyo

Nakuhakikishia ushahidi ninao tena sio wa maneno nina list ya mishahara ya kuanzia mwezi wa 1 mpaka mwezi wa tano ikionyesha mtu analipwa shilingi ngapi wakati siyo kweli hata kidogo
 
Nakuhakikishia ushahidi ninao tena sio wa maneno nina list ya mishahara ya kuanzia mwezi wa 1 mpaka mwezi wa tano ikionyesha mtu analipwa shilingi ngapi wakati siyo kweli hata kidogo

Mkuu,action speaks louder than words.
 
Mkuu,action speaks louder than words.

Mbona una haraka what do you want to achieve, nishirikishe kwanza maana hii sehemu ndiyo nayopatia ugali so kuisiliba kwanza lazima nihakikishiwe wapi naweza kupata ugali, otherwise wait until that time when I will be ready.lakini ukweli ndio huo tena hata ukitaka wa maandishi ntakuletea watu wanapata take home milion nane then accounting wanawaandikia gross ya 1.4 zilizobaki wanazipeleka moja kwa moja kwenye account za wahusika, but to disclose the company nihakikishie mkate wangu kwanza maana Tanzania yetu bwana hata ufanye jambo la ushujaa wa namna gani watakuona kichaa tu ndiyo maana kila mtu analinda mkate wake huku nchi ikichanwa vipandevipande maana no hero in our country
 
Mbona una haraka what do you want to achieve, nishirikishe kwanza maana hii sehemu ndiyo nayopatia ugali so kuisiliba kwanza lazima nihakikishiwe wapi naweza kupata ugali, otherwise wait until that time when I will be ready.lakini ukweli ndio huo tena hata ukitaka wa maandishi ntakuletea watu wanapata take home milion nane then accounting wanawaandikia gross ya 1.4 zilizobaki wanazipeleka moja kwa moja kwenye account za wahusika, but to disclose the company nihakikishie mkate wangu kwanza maana Tanzania yetu bwana hata ufanye jambo la ushujaa wa namna gani watakuona kichaa tu ndiyo maana kila mtu analinda mkate wake huku nchi ikichanwa vipandevipande maana no hero in our country
Mkuu umesomeka.Wacha niwe mvumilivu kusubiri muda muafaka!
 
Mkuu umesomeka.Wacha niwe mvumilivu kusubiri muda muafaka!

Nakushukuru sana, nina imani muda sio mrefu ntaachana na hawa jamaa then ndo utakuwa muda mwafaka.Tanzania yetu ndugu yangu ni pana no hero,utajitaidi sana lakini watu wanakuona kichaa tu.Kama nilivosema awali hata warudishe JKT na mgambo uzalendo ulishatutoka zamani.Si unaniona mimi hapa nilipo najua kabisa tena nina ushahidi wa maandishi na shift code zote zinazotumika kupeleka hela nchi za nje lakini siwezi kusema neno maana sisi hatuna utamaduni wa kumlinda mtu alie tayari kwa ajili ya kulipigania taifa.Mfano wa harakaharaka expert wapo 10 na kati ya hao hakuna anelipwa chini ya milioni 6 take home na wote hao wameandika kuwa gross yao ni 1.6 mpaka 1.2 sasa kwa harakaharaka PAY ES YOU EARN inayopotea hapo ni shilingi ngapi kwa mwezi? Lakini siwezi ndugu yangu nalinda mkate wangu wa kila siku
 
Back
Top Bottom