wende
JF-Expert Member
- Sep 6, 2009
- 714
- 65
Nadhani Kyela hakuna KKKT au nimesahau?!!!Leo ilikuwa siku ya kumsindikiza mwendazao shemeji yetu kule Kyela.Tunamtakia pumziko la Milele,mwenyezi Mungu ampunguzie adhabu na kumfikisha katika ufalme wa mbinguni,kule ambapo siku moja tuna imani tutakutana na kufurahia pamoja na malaika wake wakuu,Gabriel,Mikael na Rafael.
Kilichotawala leo wakati wa "Hotuba za Tanzia" si maneno ya kufarijiana na kuusiana juu ya uhai na kiama,bali siasa na vitisho vilitawala.Kuanzia Mchungaji,PM,Spika na Mwenyekiti wa CCM Mkoa.
Katika hotuba yake,Spika Job Ndugai amesema mbele ya waombolezaji kuwa ingekuwa si taratibu na kanuni,basi kuna wabunge mle ndani hasa wa "upande wa pili" angewacharaza bakora kila wanaposimama na kuongea bungeni.
Job Ndugai akasisitiza kuwa kuna wabunge wa "upande wa pili" wana midomo michafu,kauli za hovyo na za kuudhi.Kila wanaposimama ni kumsimanga na kumshambulia Rais na serikali yake pamoja na yeye spika.Wabunge hao wanapaswa kushukuru tu kuwa kuna taratibu za kibunge,lakini kwa nidhamu zao mbovu,spika angekuwa alishawachapa viboko ili washike adabu.
Mh.Spika anasema,kwa bahati mbaya au nzuri,wabunge hao watovu wa nidhamu,wana vigazeti vyao ambavyo wanavitumia kueneza matusi na lugha zao chafu.Ni heri hata hivyo vigazeti visingekuwepo ili wakose hapa pa kutolea maneno yao machafu.M.Ndugai alinukuliwa akisema "Tena wengine wana vigazeti vyao vya ovyoovyo,kila siku vinakashifu watu"
Wakati Ndugai akiyasema hayo,Mchungaji aliyetoa mahubiri wakati wa mazishi anasema kuna wanasiasa kazi yao kumsema na kumsimanga Rais.Hawa wanatakiwa kuonywa na kushughulikiwa na serikali,kwani kumtukana au kumkshifu Rais ni sawa na kuwakashifu Watanzania.
Mchungaji anasema yeye hatakubali kuona Rais anaendelea kusemwa semwa na kutukanwa,kwani kwa kufanya hivyo ni sawa na kutukanwa yeye na familia yake,kwani ndani ya nyumba yake,wao wote walimpigia kura Rais Magufuli.
Kwa kweli msiba huu,uligeuka vijembe na vitisho kwa "Upande wa pili".Kiasi watu wengi wa eneo la msiba walikuwa wanajiuliza,hawa "wenzetu wa upande wa pili" ni kina nani?Maana ukiwa Kyela ukasema "Wa upande wa pili",unamaanisha majirani zetu wa Malawi.
Kwahiyo wataanza na nani?!!Mh. Spika afuate ushauri wa Rc Makonda kuhusu kuwapima wabunge kabla hawazama mjengoni
Sent using Jamii Forums mobile app
Leo ilikuwa siku ya kumsindikiza mwendazao shemeji yetu kule Kyela.Tunamtakia pumziko la Milele,mwenyezi Mungu ampunguzie adhabu na kumfikisha katika ufalme wa mbinguni,kule ambapo siku moja tuna imani tutakutana na kufurahia pamoja na malaika wake wakuu,Gabriel,Mikael na Rafael.
Kilichotawala leo wakati wa "Hotuba za Tanzia" si maneno ya kufarijiana na kuusiana juu ya uhai na kiama,bali siasa na vitisho vilitawala.Kuanzia Mchungaji,PM,Spika na Mwenyekiti wa CCM Mkoa.
Katika hotuba yake,Spika Job Ndugai amesema mbele ya waombolezaji kuwa ingekuwa si taratibu na kanuni,basi kuna wabunge mle ndani hasa wa "upande wa pili" angewacharaza bakora kila wanaposimama na kuongea bungeni.
Job Ndugai akasisitiza kuwa kuna wabunge wa "upande wa pili" wana midomo michafu,kauli za hovyo na za kuudhi.Kila wanaposimama ni kumsimanga na kumshambulia Rais na serikali yake pamoja na yeye spika.Wabunge hao wanapaswa kushukuru tu kuwa kuna taratibu za kibunge,lakini kwa nidhamu zao mbovu,spika angekuwa alishawachapa viboko ili washike adabu.
Mh.Spika anasema,kwa bahati mbaya au nzuri,wabunge hao watovu wa nidhamu,wana vigazeti vyao ambavyo wanavitumia kueneza matusi na lugha zao chafu.Ni heri hata hivyo vigazeti visingekuwepo ili wakose hapa pa kutolea maneno yao machafu.M.Ndugai alinukuliwa akisema "Tena wengine wana vigazeti vyao vya ovyoovyo,kila siku vinakashifu watu"
Wakati Ndugai akiyasema hayo,Mchungaji aliyetoa mahubiri wakati wa mazishi anasema kuna wanasiasa kazi yao kumsema na kumsimanga Rais.Hawa wanatakiwa kuonywa na kushughulikiwa na serikali,kwani kumtukana au kumkshifu Rais ni sawa na kuwakashifu Watanzania.
Mchungaji anasema yeye hatakubali kuona Rais anaendelea kusemwa semwa na kutukanwa,kwani kwa kufanya hivyo ni sawa na kutukanwa yeye na familia yake,kwani ndani ya nyumba yake,wao wote walimpigia kura Rais Magufuli.
Kwa kweli msiba huu,uligeuka vijembe na vitisho kwa "Upande wa pili".Kiasi watu wengi wa eneo la msiba walikuwa wanajiuliza,hawa "wenzetu wa upande wa pili" ni kina nani?Maana ukiwa Kyela ukasema "Wa upande wa pili",unamaanisha majirani zetu wa Malawi.
Kutema juice diyo shida shida ni kuropoka kama Tundu Lisu.View attachment 546157
Hii tabia haifai kabisa...Inaweza kukuudhi mpaka ukatema juice ya passion katikati ya utamu kwa hasira tu
Hizi chuki zinatupeleka pabaya mkuu Ushimen
Hayuko sawa hyo!Huyu ni lazima atakuwa na utaahira wa kwenda kugeuza msiba kuwa ni jukwaa la kuonyesha chuki zale za kutisha dhidi ya Chadema. Kuna mafisadi mle wa chama cha wahuni na mafisadi wapokea rushwa aanze kuwachapa viboko wao.
kuna vitu hata mimi kijana mdogo nashindwa kuamini ka vinaweza kufanywa ama kusemwa na watu wazima wenye elimu na dhamana ya uongozi,ni kitu gani huwafanya watu wenye akili na upeo kupindisha ukweli na kufanya vitu vya ajabu ajabu?,siku hizi misiba imekuwa platform ya kisiasa?.
kaama hawana adabu awatandike tu watanzania tutamteteaLeo ilikuwa siku ya kumsindikiza mwendazao shemeji yetu kule Kyela.Tunamtakia pumziko la Milele,mwenyezi Mungu ampunguzie adhabu na kumfikisha katika ufalme wa mbinguni,kule ambapo siku moja tuna imani tutakutana na kufurahia pamoja na malaika wake wakuu,Gabriel,Mikael na Rafael.
Kilichotawala leo wakati wa "Hotuba za Tanzia" si maneno ya kufarijiana na kuusiana juu ya uhai na kiama,bali siasa na vitisho vilitawala.Kuanzia Mchungaji,PM,Spika na Mwenyekiti wa CCM Mkoa.
Katika hotuba yake,Spika Job Ndugai amesema mbele ya waombolezaji kuwa ingekuwa si taratibu na kanuni,basi kuna wabunge mle ndani hasa wa "upande wa pili" angewacharaza bakora kila wanaposimama na kuongea bungeni.
Job Ndugai akasisitiza kuwa kuna wabunge wa "upande wa pili" wana midomo michafu,kauli za hovyo na za kuudhi.Kila wanaposimama ni kumsimanga na kumshambulia Rais na serikali yake pamoja na yeye spika.Wabunge hao wanapaswa kushukuru tu kuwa kuna taratibu za kibunge,lakini kwa nidhamu zao mbovu,spika angekuwa alishawachapa viboko ili washike adabu.
Mh.Spika anasema,kwa bahati mbaya au nzuri,wabunge hao watovu wa nidhamu,wana vigazeti vyao ambavyo wanavitumia kueneza matusi na lugha zao chafu.Ni heri hata hivyo vigazeti visingekuwepo ili wakose hapa pa kutolea maneno yao machafu.M.Ndugai alinukuliwa akisema "Tena wengine wana vigazeti vyao vya ovyoovyo,kila siku vinakashifu watu"
Wakati Ndugai akiyasema hayo,Mchungaji aliyetoa mahubiri wakati wa mazishi anasema kuna wanasiasa kazi yao kumsema na kumsimanga Rais.Hawa wanatakiwa kuonywa na kushughulikiwa na serikali,kwani kumtukana au kumkshifu Rais ni sawa na kuwakashifu Watanzania.
Mchungaji anasema yeye hatakubali kuona Rais anaendelea kusemwa semwa na kutukanwa,kwani kwa kufanya hivyo ni sawa na kutukanwa yeye na familia yake,kwani ndani ya nyumba yake,wao wote walimpigia kura Rais Magufuli.
Kwa kweli msiba huu,uligeuka vijembe na vitisho kwa "Upande wa pili".Kiasi watu wengi wa eneo la msiba walikuwa wanajiuliza,hawa "wenzetu wa upande wa pili" ni kina nani?Maana ukiwa Kyela ukasema "Wa upande wa pili",unamaanisha majirani zetu wa Malawi.
Mtu anayempiga mwenzake kwa rungu kichwani baada ya kuzidiwa hoja anapaswa kufungiwa wodini kwenye kliniki za Apollo India.Au wasiwe wanaangia baada ya Kuvuta Bangi hii Ingesaidia akina Mdee, Tundu na Lema kuacha lugha Chafu
Since wa Judicial ni kaimu tu lazima amnyenyekee Nduli ali apewe cheo kamili.Hatimaye mkuu wa executive branch imefanikiwa kupandikiza chuki kwa mkuu legislative branch
Yule wa judicial branch bado anatafutwa
Sent from my Exclusive Y30-U00 using JamiiForums mobile app