Spika awauliza mawaziri kwa nini wanapeleka miradi kwa wapinzani wakati hawaungi mkono bajeti

Nucky Thompson

JF-Expert Member
Sep 20, 2016
1,817
4,058
Spika wa bunge la Tanzania Job Ndugai amewashangaa mawaziri kupeleka miradi ya maendeleo kwenye majimbo ya upinzani wakati wabunge hao wamepiga kura ya hapana kwenye bajeti ya serikali

Spika alitoa ufafanuzi huo baada ya mbunge wa Mbeya mjini Sugu kuhoji juu ya maelekezo ya awali aliyoyatoa juu ya watakaopiga kura za hapana, ndio na ku abstein

 
kwani walengwa wa hiyo bajeti ni kina nani?hovyo hili zee.yani kodi zetu wanaamua wampe nani na nani wasimpe?ukichaa gani unawapata hawa maccm ya awamu hii?mimi nalipa kodi ikamsaidie hata mwananchi wa tandahimba huko,sasa yeye nani kutuamulia matumizi ya kibaguzi haya??????mbona hawa watu wanalewa madaraka kupitiliza jamaniii??.nawalaaani.kama hawataki kura za hapana huo upigaji kura wa nini????
 
Huyo spika anayetokana na chama chao yeye Jimbo lake lina maendeleo gani?Jimbo la Kongwa watu wake na mazingira ni dhalili kabisa,bora Kibaigwa na bado watu wanashare maji na ng'ombe na punda......

Hapo hawawakomoi wabunge, wanawakomoa wananchi ambao wengine walimchagua JPM, Mawaziri wasiingie kwenye mtego huo watajikuta wanatumbuliwa kwa uzembe...hii nchi mbona viongozi wanatutenganisha sana?
 
Huyu mama aliechangia mwisho mi kilaza kweli sasa kama ina mapungufu wakubali kwa kigezo hawatapelekewa huduma hizo sasa huu si ni ubaguzi ambao hatuu utaki waseme tu kwamba nchi hii jimbo likiongozwa na upinzani hawapati huduma za serikari baas ili tuvunje nchi kwa mikoa na tutengane kabisa
 
Viongozi wengi wa CCM wapo very average Vichwani,
Ndio maana wabunge wengi wa CCM siku ile bajeti inasomwa walikurupuka kushangilia kufutwa Load License bila kufahamu kuwa imehamishiwa kwenye mafuta hivyo hata anaewasha Generator atalipia..

Na kuthibitisha hili angalia baadhi ya Wakuu wa Wilaya na Mikoa wa awamu hii wanavyofanya Maamuzi,

Au angalia hata mikoa mingi ambayo CCM hupata kura nyingi Kama sio kupita bila kupingwa, utagundua walio wengi ni wenye Vipato Duni, Wenye Elimu Duni na Wazee. (Insecure groups)

Utafiti wa Twaweza uliofanywa hivi Karibuni una mengi ya Kutueleza.
 
kwani walengwa wa hiyo bajeti ni kina nani?hovyo hili zee.yani kodi zetu wanaamua wampe nani na nani wasimpe?ukichaa gani unawapata hawa maccm ya awamu hii?mimi nalipa kodi ikamsaidie hata mwananchi wa tandahimba huko,sasa yeye nani kutuamulia matumizi ya kibaguzi haya??????mbona hawa watu wanalewa madaraka kupitiliza jamaniii??.nawalaaani.kama hawataki kura za hapana huo upigaji kura wa nini????
Ndio maana ilishasemekana ukisomesha manamba hamtaendelea hata kwa nini, itabaki tu ubaguzi usio na tija. Wote tunalipa kodi haijalishi mpinzani au chama dola.
 
Namuunga Mkono wasipeleke,ila kwa masharti kwamba wawaambie watanzania kwanini Serikali haitapeleka Pesa za maendeleo huko.Maana huwezi kusema ndiyo kwenye Bajeti unayojua haitekelezeki na inamuumiza mtu wa kawaida.

Ni vyema wakasema Bajeti hii ni kwa ajili ya wanaCCM tu,na kodi zitolewe na wanaccm tu.Ili wale tusio wanaCCM tutoe kodi kwenye maeneo yetu ili kujiletea maendeleo.Mbona tunaweza bila hata hiyo pesa ya serikali?
 
Kama ni kweli kasema....basi majimbo ya upinzani yasilipe kodi watafute maendeleo yao wenyewe.......wajitenge...
Duuhh .........hatari huwa ina anza hivi.

Ni kweli Kasema na Jenista Mhagama akampongeza.
 
bora bunge limehairishwa kwa sasa maana naona siku zilivyokuwa zinaendelea Spika Ndugai alikuwa anazidi kupoteza hekima, busara na utu na chuki dhidi ya wabunge wa upinzani ikiongezeka. Hivi wabunge kukataa bajeti imeanza bunge hili au imeanza Tanzania tu? kama wanahitaji mfanano wa mawazo kwa 100% ni kufuru kwa Mwenyezi Mungu
 
Bora iwe hivyo ili kila watu walipe kodi kwenye maeneo na kujitegemea kufanya maendeleo kwenye maeneo yao
 
Jenista kapiga swali la msingi sana hawa wabunge wanaopinga bajeti wasiruhusiwe kabisa kuuliza maswali yakimaendeleo kwakuwa hawataki maendeleo.
Wabunge wengi wa CCM wapo very small minded, huwa ni ndio mzee, hawana uwezo wa kudadavua na kuelewa mambo,
Hawana uwezo wa kuhoji au kugundua technical mistakes kwenye writen documents, ndiomaana kila kinachokuja toka serikalini huwa kinapitishwa tu.
Pathetic.
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom