tatanyengo
JF-Expert Member
- Mar 30, 2011
- 1,134
- 280
Katika hali ya kushangaza viongozi wa ngazi za juu wametoa kauli zinazokidhalilisha Chuo kikuu Cha Dodoma (UDOM) kuwa chuo hicho kimejaa rushwa ya ngono na udhalilishaji kwa watoto wa kike. Viongozi hao ni Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano Mh. Anne Makinda na Naibu waziri wa Jamii, Jinsia na Watoto - Ummy Mwalimu.
Naibu Ummy Mwalimu alimuuza mbunge Murtaza Mangungu (CCM) aliyekuwa angombea ujumbe wa Baraza la chuo kikuu cha Dodoma kuwa UDOM imejaa rushwa ya ngono yeye (mgombea) atafanya nini ili kuondoa kero hiyo. Ndipo Mh.Musa Haji Kombo (CUF) akaomba swali hilo lifutwe kwani linakidhalilisha chuo. Mh. Spika akadai "hakifutwi kitu hapa, hali ndivyo ilivyo".
Ndugu wanajamvi:
1. Kama hali ya udhalilishaji ni mbaya kiasi hicho, viongozi hao walishawahi kuchukua hatua yoyote ili kuondoa au kupunguza unyanyasi huo?
2. Kama kuna mtumishi mmoja au wawili ambao walishawahi kuwa na tabia hiyo kwanini ionekane kuwa tatizo hilo ni kubwa kiasi hicho?
3. Je tatizo la lushwa ya ngono likoje katika vyuo vingine vya umma hapa Tanzania?
4. Tunaomba kusikia kutoka kwa wasemaji wa chuo kuhusu hayo yanayodaiwa na viongozi wetu.
Naibu Ummy Mwalimu alimuuza mbunge Murtaza Mangungu (CCM) aliyekuwa angombea ujumbe wa Baraza la chuo kikuu cha Dodoma kuwa UDOM imejaa rushwa ya ngono yeye (mgombea) atafanya nini ili kuondoa kero hiyo. Ndipo Mh.Musa Haji Kombo (CUF) akaomba swali hilo lifutwe kwani linakidhalilisha chuo. Mh. Spika akadai "hakifutwi kitu hapa, hali ndivyo ilivyo".
Ndugu wanajamvi:
1. Kama hali ya udhalilishaji ni mbaya kiasi hicho, viongozi hao walishawahi kuchukua hatua yoyote ili kuondoa au kupunguza unyanyasi huo?
2. Kama kuna mtumishi mmoja au wawili ambao walishawahi kuwa na tabia hiyo kwanini ionekane kuwa tatizo hilo ni kubwa kiasi hicho?
3. Je tatizo la lushwa ya ngono likoje katika vyuo vingine vya umma hapa Tanzania?
4. Tunaomba kusikia kutoka kwa wasemaji wa chuo kuhusu hayo yanayodaiwa na viongozi wetu.