Sabung'ori
JF-Expert Member
- Jul 19, 2011
- 2,166
- 1,247
...wabunge sasa nawahoji...wanaokubali waseme ndio...wasiokubali waseme sio...NADHANI waliosema ndio wameshinda.Huu ndio utaratibu unaotumika ktk bunge letu kupitisha au kutopisha mambo muhim ya nchi.Ndugu zangu wana-jamii nimelileta kwenu jambo hili mnisaidie kwani nimekuwa nikitatizwa sana na huo utaratibu wa bunge.Labda niweke wazi kile kinacho nitatiza,1.nashidwa kuelewa speka anatumia kipimo gani cha sauti kutambua kuwa walioshinda au shindwa ni wangapi?.2. Kuwatangaza washindi na walioshindwa bila ya kuwa na uhakika yaani kwa KUDHANIA tu.Baada ya kuutafakali kwa kina utaratibu huu nmegundua yakuwa baadhi ya matatizo yanayoikabili nchi hii yametokana na huo utaratibu wa viongozi wetu wa KUDHANI badala ya kufanya tafiti na kupata majibu yasokuwa na shaka.Leo taifa limekwama kwenyetope la ufukala kwa sababu viongozi wanakaa maofisi kutwa wakidhania tu,spika anadhani waliosema ndio wameshinda,waziri mkuu anadhan tatizo la wauza mafuta alimuhusu,raisi anadhani mgao wa umeme ni ukame,daktari anadhani mgonjwa anaumwa kichwa anampasua mguu nk.Mwisho ngependa kuwahasa wabunge wabadiri huo utaratibu kwani haufai na unalea uzembe,kudhani ktk mambo ya msingi ni sawa na kuyachezea kamali maisha ya watanzania...UMDHANIAE NDIYE KUMBE SIYE!