Spika Ana Makinda ni mnyanyasaji wa kijinsia: {Aombe radhi}

Kisanduku

JF-Expert Member
Jul 9, 2009
284
482
Kwa nini nasema Spika Anne Makinda awaombe radhi wanaume?

Ni kwa sababu maana yake binafsi ya ufisadi. Sihangaiki sana na kujadili kauli yake mwaka juzi alivyoufahamu ufisadi maana imejadiliwa sana humu na wataalamu wameshtuonyesha nini kamusi zinavyosema kwamba fisadi ni mtu aliyekosa uadilifu (Bonyeza hapa).

Licha ya kamusi kuonyesha vile Anna makinda aliishia kuwasakama wanaume alipotumia neno fisadi.

Je, kama ufisadi ni aina ya ufusaka anaousema Makinda, kwa nini basi anaikwepesha jinsia ya kike kuwajibika kitendo kilekile cha kifisadi? Je, anataka kutuambia kwamba kuchaguliwa kwake mwanamke wa kwanza ngazi ile ni kusukuma uozo wote wa jamii kwenye jinsia ya kiume hata kama uozo ule unafanywa na jinsia ya kike pia?

Anne Makinda angekuwa muumini wa usawa wa jinsia walau angesema fisadi ni mhuni anayeingilia ndoa za watu. Japo si sahihi sana lakini walau kuna gender balance kidogo, jinsia zote zimeguswa.

Natoa wito kwamba spika huyu Anne Makinda aombe radhi kwa matumizi mabaya ya matamshi yake. Kwa sababu amedanganya umma kwa kujaribu kutunga maana mpya ya ufisadi wakati tukipekua dictionary na kamusi tunaona alichokisema ni aina mojawapo ya matumizi ya neno hilo bila msisitizo maalumu. Ufisadi ni kukosa uadilifu yaani corrupt person.

Hivyo hata mwanamke asiye na ndoa ni fisadi iwapo atachukua mwanaume mwenye ndoa waziwazi au kwa kujificha. Bila kujali mwanamke huyo ni mfagiaji barabarani, ni karani, ni sekretari. Pia bila kujali kuwa mwanamke huyo ni spika wa bunge la muungano.

Najua wapo wataotaka kupindisha mada kwamba wanaume sasa tunaanza kumashambulia spika kwa ajili ni mwanamke.

Wanaowaza kuleta madai hayo inabidi tuwanyamazishe mapema kwa kuwapa mfano wa yaliyompata spika mwenzake yaani Pius Msekwa mwaka 2003. Nakumbuka zilipigwa kelele nyingi kuhusu yeye kuwa Mwenyekiti wa board ya kampuni ya simu za mikononi yaani Vodacom wakati huohuo akiwa kama spika wa bunge.

Yeye alifafanua uenyekiti wake usivyoathiri uspka wake wa bunge. Na mwisho akatoa kauli kwamba wanaomsakama wanamuonea wivu. Alitumie neno "wana wivu wa kike"

Neno hili "wana wivu wa kike" wanaharakati wa kijinsia walilivalia njuga hadi kuipindisha mada ya msigi ya maslahi ya Msekwa, Vodacom na bunge. Mashambulizi ya wanaharakati hao yalimshinikiza spika Msekwa aseme kuwa hakujua kuwa neno "wana wivu wa kike" lingechukuliwa bango namna ile kwani ni neno la kawaida kwenye jamii.

Leo tuna spika mwangine. Si mwanaume tena, ni mwanamke, Anne Makinda. Wakati wa Msekwa kelele zilipigwa kwamba ni unyanyasaji wa kijinsia. Leo wale wanaharakati wote wako kimya kwa sababu Anne Makinda ni mwanamke mwenzao.

Kama Anne Makinda asipoomba radhi na ana baraka za ukimya wa wanaharakati wale sasa ndiyo tuone kuwa harakati za kijinsia zinamaanisha nini.

Tujihadhari.
 
Weed usimguse Huyu mama kuna wakubwa humu wamempiga BAN kigogo kwa kumgusa huyu mama,,,she is untouchable..yaani tumekuwa yatima humu jf
 
Weed usimguse Huyu mama kuna wakubwa humu wamempiga BAN kigogo kwa kumgusa huyu mama,,,she is untouchable..yaani tumekuwa yatima humu jf

Sijamtukana mama Anne Makinda.

Ninaiheshimu JF lakini wakinipiga BAN kwa kusema ukweli huu sibabaiki. Nitahamia online forum zingine na mada hiihii.
 
Kwa nini nasema Spika Anne Makinda awaombe radhi wanaume?

Ni kwa sababu maana yake binafsi ya ufisadi. Sihangaiki sana na kujadili kauli yake mwaka juzi alivyoufahamu ufisadi maana imejadiliwa sana humu na wataalamu wameshtuonyesha nini kamusi zinavyosema kwamba fisadi ni mtu aliyekosa uadilifu (Bonyeza hapa).

Licha ya kamusi kuonyesha vile Anna makinda aliishia kuwasakama wanaume alipotumia neno fisadi.

Je, kama ufisadi ni aina ya ufusaka anaousema Makinda, kwa nini basi anaikwepesha jinsia ya kike kuwajibika kitendo kilekile cha kifisadi? Je, anataka kutuambia kwamba kuchaguliwa kwake mwanamke wa kwanza ngazi ile ni kusukuma uozo wote wa jamii kwenye jinsia ya kiume hata kama uozo ule unafanywa na jinsia ya kike pia?

Anne Makinda angekuwa muumini wa usawa wa jinsia walau angesema fisadi ni mhuni anayeingilia ndoa za watu. Japo si sahihi sana lakini walau kuna gender balance kidogo, jinsia zote zimeguswa.

Natoa wito kwamba spika huyu Anne Makinda aombe radhi kwa matumizi mabaya ya matamshi yake. Kwa sababu amedanganya umma kwa kujaribu kutunga maana mpya ya ufisadi wakati tukipekua dictionary na kamusi tunaona alichokisema ni aina mojawapo ya matumizi ya neno hilo bila msisitizo maalumu. Ufisadi ni kukosa uadilifu yaani corrupt person.

Hivyo hata mwanamke asiye na ndoa ni fisadi iwapo atachukua mwanaume mwenye ndoa waziwazi au kwa kujificha. Bila kujali mwanamke huyo ni mfagiaji barabarani, ni karani, ni sekretari. Pia bila kujali kuwa mwanamke huyo ni spika wa bunge la muungano.

Najua wapo wataotaka kupindisha mada kwamba wanaume sasa tunaanza kumashambulia spika kwa ajili ni mwanamke.

Wanaowaza kuleta madai hayo inabidi tuwanyamazishe mapema kwa kuwapa mfano wa yaliyompata spika mwenzake yaani Pius Msekwa mwaka 2003. Nakumbuka zilipigwa kelele nyingi kuhusu yeye kuwa Mwenyekiti wa board ya kampuni ya simu za mikononi yaani Vodacom wakati huohuo akiwa kama spika wa bunge.

Yeye alifafanua uenyekiti wake usivyoathiri uspka wake wa bunge. Na mwisho akatoa kauli kwamba wanaomsakama wanamuonea wivu. Alitumie neno "wana wivu wa kike"

Neno hili "wana wivu wa kike" wanaharakati wa kijinsia walilivalia njuga hadi kuipindisha mada ya msigi ya maslahi ya Msekwa, Vodacom na bunge. Mashambulizi ya wanaharakati hao yalimshinikiza spika Msekwa aseme kuwa hakujua kuwa neno "wana wivu wa kike" lingechukuliwa bango namna ile kwani ni neno la kawaida kwenye jamii.

Leo tuna spika mwangine. Si mwanaume tena, ni mwanamke, Anne Makinda. Wakati wa Msekwa kelele zilipigwa kwamba ni unyanyasaji wa kijinsia. Leo wale wanaharakati wote wako kimya kwa sababu Anne Makinda ni mwanamke mwenzao.

Kama Anne Makinda asipoomba radhi na ana baraka za ukimya wa wanaharakati wale sasa ndiyo tuone kuwa harakati za kijinsia zinamaanisha nini.

Tujihadhari.
Hata sikuelewi...
Fisadi wala sio neno jipya kwa watu wa pwani kwani limekuwa likitumika miaka mingi tu kwa maana hiyo na limetokana na neno la kiarabu Fasad isipokuwa limepanuka zaidi ktk matumizi yake ndani ya kiswahili. Yapo pia maneno yanayowalenga wanawake ambayo leo hii yakitumiwa kijinsia itakuwa matusi kwa mfano neno Kahaba hili linawalenga wanawake zaidi ya wanaume ktk msamiati (kamusi), lakini pia ktk kiswahili kipya mwanamme anayeuza uzalendo wake kwa tamaa ya fedha anaweza kuitwa kahaba (malaya) ingawa tamaa hiyo haina mahusiano ya kijinsia.

Naweza kabisa kumwita Mkapa, JK au Karamagi kuwa ni makahaba (malaya) pasipo kuwa na maana ya kwamba wanauza miili yao wakijishabihisha kama wanawake, au wenye tamaa ya fedha ni wanawake tu hivyo kumwita mwanamme Malaya ni sawa na kuwatukana wanawake kiaina, laaa hasha ila matumizi ya neno hili yanalengakuonyesha mtu yeyote kuuza nchi yetu kwa tamaa ya fedha pasipo kujali jinsia yake. Kwa hiyo matumizi ya maneno haya yanaweza tumika ktk maana zaidi ya moja na sii lazima pawepo na mahusiano ya kijinsia ili kuleta maana halisi ya maneno haya.

Lakini pia hutumika kwa maana hiyo hiyo ya kijinsia kuwa Fisadi ni laghai mwanamme kwa wanawake ktk mapenzi au Kahaba ni mwanamke malaya...Hivyo ni muhimu kwa msikilizaji kuelewa msemaji amelenga kuzungumzia kitu gani zaidi ya maana ya neno lenyewe kama linavyotafsiriwa ktk kamusi.

Ila yanapotumika maneno haya wakati wote ni matusi ikiwa hakuna ushahidi kwa sababu haya yote maneno (Fisadi na Kahaba (malaya)) ni act of sin, ni uvunjaji wa sheria ambao unahitaji ushahidi kila unapoyatumia ili kumweka mhusika ktk nafasi hiyo na sio accusation ambazo huwezi kuzi back up na evidence...
 
Hata sikuelewi...
Fisadi wala sio neno jipya kwa watu wa pwani kwani limekuwa likitumika miaka mingi tu kwa maana hiyo na limetokana na neno la kiarabu Fasad isipokuwa limepanuka zaidi ktk matumizi yake ndani ya kiswahili. Yapo pia maneno yanayowalenga wanawake ambayo leo hii yakitumiwa kijinsia itakuwa matusi kwa mfano neno Kahaba hili linawalenga wanawake zaidi ya wanaume ktk msamiati (kamusi), lakini pia ktk kiswahili kipya mwanamme anayeuza uzalendo wake kwa tamaa ya fedha anaweza kuitwa kahaba (malaya) ingawa tamaa hiyo haina mahusiano ya kijinsia.

Naweza kabisa kumwita Mkapa, JK au Karamagi kuwa ni makahaba (malaya) pasipo kuwa na maana ya kwamba wanauza miili yao wakijishabihisha kama wanawake, au wenye tamaa ya fedha ni wanawake tu hivyo kumwita mwanamme Malaya ni sawa na kuwatukana wanawake kiaina, laaa hasha ila matumizi ya neno hili yanalengakuonyesha mtu yeyote kuuza nchi yetu kwa tamaa ya fedha pasipo kujali jinsia yake. Kwa hiyo matumizi ya maneno haya yanaweza tumika ktk maana zaidi ya moja na sii lazima pawepo na mahusiano ya kijinsia ili kuleta maana halisi ya maneno haya.

Lakini pia hutumika kwa maana hiyo hiyo ya kijinsia kuwa Fisadi ni laghai mwanamme kwa wanawake ktk mapenzi au Kahaba ni mwanamke malaya...Hivyo ni muhimu kwa msikilizaji kuelewa msemaji amelenga kuzungumzia kitu gani zaidi ya maana ya neno lenyewe kama linavyotafsiriwa ktk kamusi.

Ila yanapotumika maneno haya wakati wote ni matusi ikiwa hakuna ushahidi kwa sababu haya yote maneno (Fisadi na Kahaba (malaya)) ni act of sin, ni uvunjaji wa sheria ambao unahitaji ushahidi kila unapoyatumia ili kumweka mhusika ktk nafasi hiyo na sio accusation ambazo huwezi kuzi back up na evidence...

Mkubwa,

Msingi wa post yangu si mawazo yangu ni reference za dictinonary. Hivyo usieme hunielewi, sema huzielewi dictonary zote zinazorejea msamiati huu.

Na kutoielewa reference si jambo geni kama ambavyo tulipokuwa sekondari mtu hakuielewa Abbot au Nelkon na matokeo yake akaishia kupata "F" kwenye physics.
 
Hivyo hata mwanamke asiye na ndoa ni fisadi iwapo atachukua mwanaume mwenye ndoa waziwazi au kwa kujificha. Bila kujali mwanamke huyo ni mfagiaji barabarani, ni karani, ni sekretari. Pia bila kujali kuwa mwanamke huyo ni spika wa bunge la muungano.

Yeye mwenyewe ni mpweke hana mume...ninavyosikia na kama hii ni kweli tunaweza kumwelewa kwa nini hawezi kujishambulia nafsi yake............
 
Du Mipasho imeshaanza mapemaaaa! Next one will be " Na nyie wa upinzani mnikome" kwi kwi kwi kwi!:doh:
 
Kwa nini nasema Spika Anne Makinda awaombe radhi wanaume?

Ni kwa sababu maana yake binafsi ya ufisadi. Sihangaiki sana na kujadili kauli yake mwaka juzi alivyoufahamu ufisadi maana imejadiliwa sana humu na wataalamu wameshtuonyesha nini kamusi zinavyosema kwamba fisadi ni mtu aliyekosa uadilifu (Bonyeza hapa).

Licha ya kamusi kuonyesha vile Anna makinda aliishia kuwasakama wanaume alipotumia neno fisadi.

Je, kama ufisadi ni aina ya ufusaka anaousema Makinda, kwa nini basi anaikwepesha jinsia ya kike kuwajibika kitendo kilekile cha kifisadi? Je, anataka kutuambia kwamba kuchaguliwa kwake mwanamke wa kwanza ngazi ile ni kusukuma uozo wote wa jamii kwenye jinsia ya kiume hata kama uozo ule unafanywa na jinsia ya kike pia?

Anne Makinda angekuwa muumini wa usawa wa jinsia walau angesema fisadi ni mhuni anayeingilia ndoa za watu. Japo si sahihi sana lakini walau kuna gender balance kidogo, jinsia zote zimeguswa.

Natoa wito kwamba spika huyu Anne Makinda aombe radhi kwa matumizi mabaya ya matamshi yake. Kwa sababu amedanganya umma kwa kujaribu kutunga maana mpya ya ufisadi wakati tukipekua dictionary na kamusi tunaona alichokisema ni aina mojawapo ya matumizi ya neno hilo bila msisitizo maalumu. Ufisadi ni kukosa uadilifu yaani corrupt person.

Hivyo hata mwanamke asiye na ndoa ni fisadi iwapo atachukua mwanaume mwenye ndoa waziwazi au kwa kujificha. Bila kujali mwanamke huyo ni mfagiaji barabarani, ni karani, ni sekretari. Pia bila kujali kuwa mwanamke huyo ni spika wa bunge la muungano.

Najua wapo wataotaka kupindisha mada kwamba wanaume sasa tunaanza kumashambulia spika kwa ajili ni mwanamke.

Wanaowaza kuleta madai hayo inabidi tuwanyamazishe mapema kwa kuwapa mfano wa yaliyompata spika mwenzake yaani Pius Msekwa mwaka 2003. Nakumbuka zilipigwa kelele nyingi kuhusu yeye kuwa Mwenyekiti wa board ya kampuni ya simu za mikononi yaani Vodacom wakati huohuo akiwa kama spika wa bunge.

Yeye alifafanua uenyekiti wake usivyoathiri uspka wake wa bunge. Na mwisho akatoa kauli kwamba wanaomsakama wanamuonea wivu. Alitumie neno "wana wivu wa kike"

Neno hili "wana wivu wa kike" wanaharakati wa kijinsia walilivalia njuga hadi kuipindisha mada ya msigi ya maslahi ya Msekwa, Vodacom na bunge. Mashambulizi ya wanaharakati hao yalimshinikiza spika Msekwa aseme kuwa hakujua kuwa neno "wana wivu wa kike" lingechukuliwa bango namna ile kwani ni neno la kawaida kwenye jamii.

Leo tuna spika mwangine. Si mwanaume tena, ni mwanamke, Anne Makinda. Wakati wa Msekwa kelele zilipigwa kwamba ni unyanyasaji wa kijinsia. Leo wale wanaharakati wote wako kimya kwa sababu Anne Makinda ni mwanamke mwenzao.

Kama Anne Makinda asipoomba radhi na ana baraka za ukimya wa wanaharakati wale sasa ndiyo tuone kuwa harakati za kijinsia zinamaanisha nini.

Tujihadhari.

Huyu ndo mzuri kuliko nduguai eti .. wapinzani bana
 
Back
Top Bottom