Spika amvaa Mwigulu bungeni kushindwa kujibu swali la Mpina

saidoo25

JF-Expert Member
Jul 4, 2022
602
1,407
Spika wa Bunge Dkt. Tulia Akson ameitaka wizara ya Fedha na Mipango kujibu upya swali namba 129 lililoulizwa na Mbunge Kisesa Luhaga Mpina, ambaye aliitaka serikali kutoa maelezo ya kwanini kesi 1,097 za kodi zenye thamani ya shilingi trilioni 360 na dola za Marekani milioni 181.4 hazijaamuliwa hadi sasa.

Hatua hiyo ya Spika imekuja baada ya majibu ya Naibu waziri wa Fedha na Mipango Hamadi Hassan Chande kwenda kinyume na swali la msingi la Mbunge Mpina.

Hata waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Mwigulu Nchemba alipojaribu kutoa ufafanuzi, maelezo yake hayakufanana na swali la msingi la Mbunge huyo wa Kisesa.

Baada ya Spika kuwahoji viongozi hao wa wizara ya Fedha na Mipango na kukosa majibu yanayoridhisha, ndipo akaamuru swali hilo likajibiwe tena kama ambavyo limeulizwa na Mbunge Luhaga Mpina.

CHANZO: TBC

308541459_609615547327121_5107204235206310616_n.jpg
 
Spika wa Bunge Dkt. Tulia Akson ameitaka wizara ya Fedha na Mipango kujibu upya swali namba 129 lililoulizwa na Mbunge Kisesa Luhaga Mpina, ambaye aliitaka serikali kutoa maelezo ya kwanini kesi 1,097 za kodi zenye thamani ya shilingi trilioni 360 na dola za Marekani milioni 181.4 hazijaamuliwa hadi sasa.

Hatua hiyo ya Spika imekuja baada ya majibu ya Naibu waziri wa Fedha na Mipango Hamadi Hassan Chande kwenda kinyume na swali la msingi la Mbunge Mpina.

Hata waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Mwigulu Nchemba alipojaribu kutoa ufafanuzi, maelezo yake hayakufanana na swali la msingi la Mbunge huyo wa Kisesa.

Baada ya Spika kuwahoji viongozi hao wa wizara ya Fedha na Mipango na kukosa majibu yanayoridhisha, ndipo akaamuru swali hilo likajibiwe tena kama ambavyo limeulizwa na Mbunge Luhaga Mpina.

CHANZO: TBC

View attachment 2364512
Swali zuri kabisa,wake na majibu..

Pili waje na majibu zile Til.1.3 za CAG zilienda wapi?
 
Mbona swali rahisi sana hilo?
Ni kuwa kuna madai makubwa kiasi hicho kwa sababu ya ule utopolo wa Magufuli eti anawadai Accacia kodi ya trilioni mwaka 360 za makinikia
 
Hana lolote la maana mnafiki tu, akipewa uwaziri hutosikia Tena akikosoa
Waziri hakosoi serikali, Bali anawajibika kwa yale yanayotokea kwa serikali.

Mbunge yeye ndio kazi yake kuisimamia serikali na kuiwajibisha. Hata Bashe alikuwa akikosoa serikali Ila alipopata uwaziri hakuweza kuendelea kwa sababu nilizokupatia.

Hata huko kwenu chadema, Mjumbe kamati kuu hawezi kukosoa chama. Ila mwanachama wa kawaida anaweza kukosoa
 
Waziri hakosoi serikali, Bali anawajibika kwa yale yanayotokea kwa serikali.

Mbunge yeye ndio kazi yake kuisimamia serikali na kuiwajibisha. Hata Bashe alikuwa akikosoa serikali Ila alipopata uwaziri hakuweza kuendelea kwa sababu nilizokupatia.

Hata huko kwenu chadema, Mjumbe kamati kuu hawezi kukosoa chama. Ila mwanachama wa kawaida anaweza kukosoa
Sawa msukule wa dikteta Jiwe
 
Back
Top Bottom