Spika amkataza Waziri wa Fedha kusifia na kuwazuia wabunge kuimba nyimbo za kumsifia Rais wakati bajeti ikisomwa

Abraham Lincolnn

JF-Expert Member
Apr 12, 2018
2,510
4,224
Wakati waziri wa fedha akisoma bajeti ambayo ndiyo msingi na hatma ya watanzania 2022/2023 Spika wa JMT Mh Dr.Tulia Ackson amemzuia waziri wa fedha Mh Mwigulu Nchemba kuimba nyimbo za sifa na kurudia rudia kauli za pongezi kwa Rais.

Je, huu ni mwanzo wa mwisho wa tabia za kuingiza siasa na pongezi zisizokuwa na tija hususan kwenye mambo nyeti na muhimu kwa taifa kama bajeti kuu ya serikali?

Tabia hii ya kutoa pongezi na kusifia hovyo hovyo hata pale pasipokuwa na ukweli au ulazima wa kufanya hivyo imekuwa jambo la kawaida kwa viongozi wengi hususan mawaziri.Hali hii imepelekea hata katika mambo ya msingi na nyeti viongozi kushindwa kuongea ukweli na kuingiza siasa kwa lengo la kujinufaisha wao binafsi mbele ya Rais.

Hali hii huwafanya viongozi wa juu hususan Rais kushindwa kuupata ukweli na endapo hatachukua hatua za ziada katika kuutambua na kutafuta ukweli na uhalisia basi hali hubaki midomoni na siasa za hapa na pale huku wananchi wa chini wakiumia.

Je, Nini kifanyike kukomesha tabia hii?
 
Spika mwenyewe huwa anamsifia hovyo Rais.

Chakufanya ili kukomesha hiyo tabia kwanza Rais ambaye ni mwenyekiti wa CCM asiwe na mamlaka ya kuteua wabunge kupitia chama chake, asiteue mawaziri, na asihusike kupitisha jina la Spika na NS wa bunge la JMT.
 
Muda mwingi bungeni na kwenye mikutano umekuwa ukitumika kusifia, matokeo wengi wamesusa kusikiliza au kutazama hizo hotuba. Ni siku ya budget lakini hata sijajua nini kimeendelea kwani ni kupotezeana muda.

Mimi hii tabia ya kumsifia rais na kutoa sifa za kijinga kwa chama zilinifanya niache kusikiliza bunge kabisa. Hao wenye moyo wa kuangalia hilo bunge la kitoto sijui wanaweza vipi.
 
Wakati waziri wa fedha akisoma bajeti ambayo ndiyo msingi na hatma ya watanzania 2022/2023 Spika wa JMT Mh Dr.Tulia Ackson amemzuia waziri wa fedha Mh Mwigulu Nchemba kuimba nyimbo za sifa na kurudia rudia kauli za pongezi kwa Rais...
Sifia sifia ilianza kipindi cha bwana yule ila kwa sasa ishaota mizizi
 
Hakuna kitu kina kera kama kila muda mtu anamsifia Rais.........Kwa zaidi ya miaka kadhaa sijawahi kusikia mbunge akiukosoa mhimili ulijishindilia zaidi
 
Back
Top Bottom