Spika amfuma Naibu Waziri kuleta majibu mawili yanayokinzana. Awataka Mawaziri na Manaibu kuyapa maswali uzito

Replica

JF-Expert Member
Aug 28, 2017
1,444
7,808
Leo Spika, Tulia Ackson ametoa mrejesho wa muongozo uliiombwa 20 May 2022 na mbunge wa Handeni, Reuben Kwagilwa ambapo aliuliza lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Handeni-Singida kiwango cha lami.

Naibu waziri wa ujenzi, mhandisi Msongwe alisema Serikali imeanza ujenzi kwa awamu na taratibu za manunuzi kipande cha Handeni-Mafuleta(KM 20) zipo katika hatua za mwisho kusaini mkataba na ilitwakiwa kusainiwa kabla ya June.

Kwenye swali la nyongeza, Naibu waziri alimhakikishia mbunge kwamba kazi ya ujenzi imeshaanza na mkandarasi amepatikana na kunaza 'Mobilization' kupeleka vifaa 'site' na handeni mjini kwenda Turiani aliomba isubiriwe bajeti ipitishwe.

Mbunge alihoji inawezekana vipi mkandarasi yupo site ilhali mkataba haujasainiwa!
 
Back
Top Bottom