Spika aliahirisha Bunge Ijumaa (8/4/2011) kwa Shughuli za CCM?

Gurudumu

JF-Expert Member
Feb 5, 2008
2,349
261
Alisoma waraka ulioonekana wazi kwamba ulikuwa umeandaliwa kabla.

Katika waraka huo alidai kwamba kuna vyama vya siasa vinavyotumia fursa ya Mswada wa kutunga Katiba mpya kujijenga kisiasa. Alidai pia kwamba vyama hivyo vinachochea vijana kuleta vurugu katika zoezi la kukusanya maoni.

Alikemea vyama hivyo na kuahirisha Bunge ili kuwapa wabunge fursa ya kushiriki katika zoezi la kutoa maoni.

Kimantiki, hii ilikuwa na tafsiri ya kuwapa wabunge nafasi kwenda kudhibiti hilo wimbi la wananchi waliochochewa kuleta vurugu kwenye mikutano ya kukusanya maoni. Nalazimika kufikiri hivyo kwa sababu Spika hakutoa hoja iliyothibitisha kwamba Wabunge walikuwa hawana muda wa kutoa maoni yao kwenye Public hearing na kwamba hiyo ndiyo siku pekee iliyobakia wao kutoa maoni.

Zaidi, sina uhakika kama Spika alikusudia kutuambia kwamba polisi walishindwa kudhibiti hizo vurugu na kwamba anawafungulia Wabunge wake ili wakaifanye hiyo kazi kikamilifu.

Lakini, nini kazi ya kamati ya Bunge ya Sheria na Katiba? Je, Public hearing ni ya wabunge au wananchi? Je, si Mswada huu utafikishwa Bungeni ili Wabunge wajadili na kutoa maoni yao kisha waupitishe au kuukataa? Na kwa mantiki, Wabunge wanatoa maoni kwa nani?

Je, ni wabunge wangapi na wa chama gani waliojiorodhesha katika mikutano ya kutoa maoni siku hiyo ya Ijumaa katika mikoa ya Dar, Dodoma na Zanzibar? Idadi hiyo waliojiorodhesha/waliohudhuria inapelekea kuahirisha Bunge zima?

Je, nini ilikuwa ratiba ya kikao cha Bunge cha siku hiyo na ni namna gani yaliyokuwa yajadiliwe siku hiyo yanapata kujadiliwa? Kwa nini ni rahisi kiasi hicho Spika (bila kuuliza maoni ya wabunge wote) kuamua aahirishe bunge bila kujali maslahi na matarajio ya Wabunge na Wananchi katika hoja ambazo zilikuwa zijadiliwe siku hiyo?

Je, ni sahihi kufikiri kwamba Makinda aliamrishwa (na mamlaka fulani ambayo siifahamu) kuahirisha Bunge ili kutoa muda wa wabunge wa ccm ambao walikuwa kwenye mchakato wa vikao vya juu vya chama kujiandaa/kushiriki?

Kama fikra hizo zikiwa sahihi (natamani zisiwe sahihi), Je, ni pesa kiasi gani zilitumika kuweka wabunge Dodoma siku hiyo aliyoahirisha Bunge? Ni nani anabeba hizo gharama, ccm au serikali (wananchi)?

I am just thinking aloud, Naomba tujadili na wenye taarifa sahihi watupatie please
 
Kwenye Kikao cha leo hata hawajagusia tena kuhusu swala hili
 
Kuna wabunge, mawaziri, WM na Spika mwenyewe ni mjumbe muhimu wa CC ya CCM. Kuahirisha kikao cha Bunge kwa ajili ya kikao cha CC inawezekana kabisa. Jinsi watu wanavyogawana madaraka, vyeo na nyadhifa mbalimbali nchi hii ni KATIBA MPYA ikiandikwa vizuri ndio itakayotusaidia tu.
 
Kuna wabunge, mawaziri, WM na Spika mwenyewe ni mjumbe muhimu wa CC ya CCM. Kuahirisha kikao cha Bunge kwa ajili ya kikao cha CC inawezekana kabisa. Jinsi watu wanavyogawana madaraka, vyeo na nyadhifa mbalimbali nchi hii ni KATIBA MPYA ikiandikwa vizuri ndio itakayotusaidia tu.

Kama hivyo ndivyo mimi sioni tatizo kama ccm wangeingia gharama hizo. Kwa nini wanajichomeka kwenye ratiba ya Bunge hivyo kupelekea uwezekano wa kutumia pesa za serikali katika vikao vya chama
 
Kama hivyo ndivyo mimi sioni tatizo kama ccm wangeingia gharama hizo. Kwa nini wanajichomeka kwenye ratiba ya Bunge hivyo kupelekea uwezekano wa kutumia pesa za serikali katika vikao vya chama

Ndugu yangu posho za Wabunge zipo tu 24/7/31/12 kwa miaka mitano. Wasipokuwa bungeni wanakuwa kwenye kamati au ziarani. Tunaendesha SIASA kwa gharama kubwa sana NCHI hii.
 
nategemea aliambiwa juu ya watoto wa Karimjee Hall na kama hakuambiwa ameona picha. Je, anajua ni kikundi gani kiri organize hao watoto, walitumia gharama gani na zilitoka wapi!!?
 
Ndugu yangu posho za Wabunge zipo tu 24/7/31/12 kwa miaka mitano. Wasipokuwa bungeni wanakuwa kwenye kamati au ziarani. Tunaendesha SIASA kwa gharama kubwa sana NCHI hii.

Na wabunge walivyo wengi, tungepata data za uhakika pengine tungeweza kuona namna ya kuliweka kwenye Katiba mpya
 
Na wabunge walivyo wengi, tungepata data za uhakika pengine tungeweza kuona namna ya kuliweka kwenye Katiba mpya
Data zipo pale kwa mhasibu mkuu wa Bunge. Tatizo kubwa tulilonalo posho, maslahi na mishahara yao wanajipangia wao wenyewe. Hakuna chombo huru kinachoweza kuhoji wala kuzuia hili. Serikali yetu kwa madudu inayofanya haiwezi kuthubutu hata kuulizia. Wanaridhia kila kitu na kulipa haraka sana. Ndio maana huku kungine kama kwenye huduma za jamii kama elimu, matibabu, kuko hoi. Polisi, walimu, wanafunzi wetu wako hoi.
 
Data zipo pale kwa mhasibu mkuu wa Bunge. Tatizo kubwa tulilonalo posho, maslahi na mishahara yao wanajipangia wao wenyewe. Hakuna chombo huru kinachoweza kuhoji wala kuzuia hili. Serikali yetu kwa madudu inayofanya haiwezi kuthubutu hata kuulizia. Wanaridhia kila kitu na kulipa haraka sana. Ndio maana huku kungine kama kwenye huduma za jamii kama elimu, matibabu, kuko hoi. Polisi, walimu, wanafunzi wetu wako hoi.

Mifumo yote ya kuandaa bajeti nchi hii bana inawapendelea wanaoandaa wanaofanya maamuzi na siyo wanaohudumiwa (wananchi)

Katiba mpya!!!
 
Ndio maana tunataka kuwa na kofia mbili Spika asitokane na chama chochote awe mtu independent toka kwenye jamii,hakuna ubishi na hilo kwamba spika aliharisha bunge kwa kusingizia muswaada mbona leo hajatolea maelezo yeyote alipoanza kikao cha bunge,kwa hiyo serikali imefadhili wajumbe/wabunge wa CCM, nani asie jua janja ya nyani yao
 
Ndio maana tunataka kuwa na kofia mbili Spika asitokane na chama chochote awe mtu independent toka kwenye jamii,hakuna ubishi na hilo kwamba spika aliharisha bunge kwa kusingizia muswaada mbona leo hajatolea maelezo yeyote alipoanza kikao cha bunge,kwa hiyo serikali imefadhili wajumbe/wabunge wa CCM, nani asie jua janja ya nyani yao

Hapo kwenye red pagumu kweli kutekeleza kwa sababu hutajua. Nadhani tunatakiwa kwenye katiba mpya tuweke masharti ambayo ikigundulika tu kwamba Spika amefanya maamuzi kupendelea chama chake au kutokana na maelekezo ya chama chake basi kuwe na taratibu za kumuwajibisha
 
Kuna umuhimu wa Katiba mpya ku-specify baadhi ya majukumu maana tunaona Katiba iliyopo sasa hivi ndio imekuwa strong hold ya CCM
 
Na wabunge walivyo wengi, tungepata data za uhakika pengine tungeweza kuona namna ya kuliweka kwenye Katiba mpya
Na ndio maana nasema hii Katiba ni ya wananchi na sio chama chochote kile kwa wabunge wengi wa CCM walivyo na jinsi wanavyopenda kusema "Ndio Mzee" hawa wako tayari kupitisha katiba bila kujali maslahi ya msingi ya nchi hii nikimaanisha wananchi
 
Na ndio maana nasema hii Katiba ni ya wananchi na sio chama chochote kile kwa wabunge wengi wa CCM walivyo na jinsi wanavyopenda kusema "Ndio Mzee" hawa wako tayari kupitisha katiba bila kujali maslahi ya msingi ya nchi hii nikimaanisha wananchi

Mkuu ikitinga bungeni tu ni lazima ipitishwe hata kama ina mapungufu gani kwa sababu kama umeshaona sasa hivi hili swala kwa upande wa bara ni ccm dhidi ya chadema na huko visiwani ni wananchi against vyama tawala! Pia katiba tuliyonayo sasa hivi inakataza bunge kukataa kupitisha mswada uliwawasilishwa na serikali vinginevyo rais atavunja bunge. Ndiyo maana wabunge (wa ccm) wanann'gang'ng'ania kwamba toeni maoni tu bunge litayapokea na kuyajadili
 
Data zipo pale kwa mhasibu mkuu wa Bunge. Tatizo kubwa tulilonalo posho, maslahi na mishahara yao wanajipangia wao wenyewe. Hakuna chombo huru kinachoweza kuhoji wala kuzuia hili. Serikali yetu kwa madudu inayofanya haiwezi kuthubutu hata kuulizia. Wanaridhia kila kitu na kulipa haraka sana. Ndio maana huku kungine kama kwenye huduma za jamii kama elimu, matibabu, kuko hoi. Polisi, walimu, wanafunzi wetu wako hoi.
Very right hakuna wa kuwaaudit, waseme nini wabunge wasipewe.
 
Very right hakuna wa kuwaaudit, waseme nini wabunge wasipewe.

Inatia uchungu sana Remmy, ndiyo maana ubunge inaonekana ni kazi inayolipa kuliko ajira zote hapa tz na mtu yuko tayari kwa lolote ili aupate ubunge. Tukifanikiwa kugeuza hiyo mizania tu ubunge ukawa ni kazi ya kawaida basi hata tusingehitaji kutumia nguvu nyingi sana kuzungumza na serikali kama ilivyo sasa hivi
 
Mkuu ikitinga bungeni tu ni lazima ipitishwe hata kama ina mapungufu gani kwa sababu kama umeshaona sasa hivi hili swala kwa upande wa bara ni ccm dhidi ya chadema na huko visiwani ni wananchi against vyama tawala! Pia katiba tuliyonayo sasa hivi inakataza bunge kukataa kupitisha mswada uliwawasilishwa na serikali vinginevyo rais atavunja bunge. Ndiyo maana wabunge (wa ccm) wanann'gang'ng'ania kwamba toeni maoni tu bunge litayapokea na kuyajadili
Wabunge wengi wa CCM wanajua vipengele fulani kwenye katiba vikibadilishwa basi wao na Rais watakuwa hawana mamlaka ya kufanya au kupiga kura kutokana na wingi wao sababu wingi wao kwenye Bunge ndio added advantage yao kwenye hii Katiba na wanajua kwamba Wananchi wakitoa maoni halafu hayo maoni yakaenda bungeni kujadiliwa uwezekano wa kuyatupilia mbali mambo ya msingi ni mkubwa
 
Back
Top Bottom