Spika Aendelea Kuvurunda

M-bongo

JF-Expert Member
Feb 29, 2008
338
71
Katika kile kinachoonekana kujipangia mkakati wa kuendelea kuwa kinara wa CCM mkoa wa Tabora Mbunge wa Jimbo la Urambo Mashariki ambaye pia ni Spika bunge la jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh Samuel Sita amemsogeza karibu ya ofisi yake (BUNGENI)Kijana mmoja kutoka Tabora(Bw kwikima) kufanya kazi sehemu ya utawala. kibaya zaidi wakati vijana wa kitanzania wakilia usiku na mchana juu ya tatizo la ajira Mh spika amemuachisha kijana kazi ofisi ya Madini mkoa wa Dodoma. habari kutoka chanzo cha uhakika wa habari hizi zinadai kuwa Mh Spika amemsogeza karibu yake kijana huyo na kumshawishi agombee Uenyekiti wa Vijana mkoani kwake ili aendelee kujiwekea matumaini ya kisiasa jimboni urambo kwani kama atafanikisha kijana huyo kuikwaa nafasi hiyo basi atakuwa na ngome katika Kamatiya siasa Mkoa wa Tabora. Swali bwana Spika ni lazima amueke mtu ofisi kwake mtu kutoka Tabora ambaye tayari kijana alishakuwa kibosile katika ofisi ya Madini Mkoa wa Dodoma au ndiyo mikakati ya kila mtu kuchukua chake mapema? kazi kwenu Tabora Bw Spika anawaletea Mkiti wa Kuchonga
 
YALE YALE ..... Sitta aanafikiri watu wamelala au hajui ni nini kinachoendelea!!
 
Swali bwana Spika ni lazima amueke mtu ofisi kwake mtu kutoka Tabora ambaye tayari kijana alishakuwa kibosile katika ofisi ya Madini Mkoa wa Dodoma au ndiyo mikakati ya kila mtu kuchukua chake mapema?

Hoja isiwe ni kijana kutoka wapi, bali hoja iwe ni je ajira hiyo ilifuata taratibu? Kama aliomba kazi na akafanya vyema kwenye interview, then swali lako linakuwa halina mashiko na huwezi ukalitetea.

Kuhusu mtu kuacha kazi sehemu ambayo tayari ulishakuwa kibosile na kwenda sehemu tofauti ambayo unakuwa ofisa wa kawaida, mimi sioni shida iko wapi. Watu wanaangalia maslahi zaidi. Kuna faida gani niitwe Director ama CEO halafu mwisho wa mwezi ninapokea laki 5, wakati nikienda sehemu nyingine nikiwa staff wa kawaida ninalipwa milioni 2? Hapo nadhani swala ni maslahi/mshiko na kuwa kibosile siyo hoja tena.

Mtoa hoja ongeza mashiko kwenye hoja yako, vinginevyo watu wanaweza kuelekea kwenye udaku na siasa chafu za kiwango cha chini kabisa za majitaka!
 
Bwana Keil inawezekana kabisa zikawa ni siasa za maji taka kwa tafsiri yako sahihi japo sina hakika kama umeisoma thread yangu kwa makini na kujua kila kilichoulizwa vinginevyo siasa za maji taka zaweza kuwafaa sana watu waishio katika kiwango hicho cha maji taka hivyo kufanya siasa za maji taka ikawa sahihi kabisa kufikishiana ujumbe wa maji taka
 
Kwa ufafanuzi zaidi wa hoja hii na kwa maana halisi ya utawala bora katika sekta za umma, nafasi yoyote inapotokea lazima itangazwe ili wenye sifa husika waombe na kisha kuitwa kwa kufanyiwa usaili kitu ambacho hakikufanywa maneno haya ili ndugu yangu aliyetaka ufafanuzi ni kwamba Bw Kwikima ameajiriwa kwa mlango wa nyuma, nafasi haikutangazwa wala hakukuwa na uasaili wowote ulifanyika nadhani mmenipata wakuu Au?
 
Alipochaguliwa kuwa Spika wengi tulifurahi kwa sababu aliyekuwepo alionesha kuchoka, na inaonekana busara zake zimekwisha, lakini huyu SPEED AND STANDARDS ameonekana kutokuwa na mwelekeo hata kidogo, bunge la sasa ni too much kuliko uwezo wake. hawa ndio watu wa kustaafu kwa manufaa ya umma.
 
Nimeshasema kuwa hawa viongozi wanachukua chao mapema, ila sasa siku watanzania hawahawa wakiamua tutakwenda sawa.Kwa hilo la spika wa Bunge letu kupachika kilichochake pale bungeni amejidhalilisha kama ni kweli, namshauri alitazame upya, ajue bado tunamwamini sana na hututegemei afanye vitu kama hivyo
 
Katika kile kinachoonekana kujipangia mkakati wa kuendelea kuwa kinara wa CCM mkoa wa Tabora Mbunge wa Jimbo la Urambo Mashariki ambaye pia ni Spika bunge la jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh Samuel Sita amemsogeza karibu ya ofisi yake (BUNGENI)Kijana mmoja kutoka Tabora(Bw kwikima) kufanya kazi sehemu ya utawala. kibaya zaidi wakati vijana wa kitanzania wakilia usiku na mchana juu ya tatizo la ajira Mh spika amemuachisha kijana kazi ofisi ya Madini mkoa wa Dodoma. habari kutoka chanzo cha uhakika wa habari hizi zinadai kuwa Mh Spika amemsogeza karibu yake kijana huyo na kumshawishi agombee Uenyekiti wa Vijana mkoani kwake ili aendelee kujiwekea matumaini ya kisiasa jimboni urambo kwani kama atafanikisha kijana huyo kuikwaa nafasi hiyo basi atakuwa na ngome katika Kamatiya siasa Mkoa wa Tabora. Swali bwana Spika ni lazima amueke mtu ofisi kwake mtu kutoka Tabora ambaye tayari kijana alishakuwa kibosile katika ofisi ya Madini Mkoa wa Dodoma au ndiyo mikakati ya kila mtu kuchukua chake mapema? kazi kwenu Tabora Bw Spika anawaletea Mkiti wa Kuchonga

Binafsi sioni mantiki ya hoja hii. Ninachokiona ni majungu yasiyo na msingi wowote. Inaonekana wazi kwamba mtoa hoja anauadui au ni challenger wa Mhe Sitta au huyo Kijana. Ninasema haya kutokana na sababu zifuatazo: -
a) Hujabainisha kama utaratibu uliotumika kumpatia kazi ya utawala katika ofisi ya Bunge ulikiuka utaratibu.

b) Suala la vijana wengi kukosa ajiri halimzuii mtu kubadilisha kazi. Huenda huyo kijana kapendezewa na kazi ya utawala katika ofisi za bunge kuliko u-bossi aliokuwa nao huko madini-Dodoma. Hili ni suala la mtu binafsi.

c) Suala la kumtaka angombee Uenyekiti wa CCM huko Tabora, wewe linakukera nini? Kwani wanaoshauriwa kugombea nafasi mbalimbali za uongozi si wapo wengi tu? tena unaposhauri hivyo inaonyesha jinsi unavyokubalika tofauti na kuamua mwenyewe.

d) Kuhusu kuwashauri vijana wa CCM wa Tabora waamini kwamba kijana huyo unapelekwa na Mhe. SItta ili amlindie maslahi yake katika kamati ya siasa halina mshiko. hata likiwa la kweli si ndiyo siasa?

e) Ni vipi unahusisha suala hili na kuchukua chako mapema? labda sijakuelewa.

In all, sioni umaana wa hoja hii zaidi ya kuwa jungu kwa wana-CCM wenzako, na kuleta chuki za wazi kwa Mhe. Sitta na huyo Kijana.
 
Jamani hebu ifuatiliwe hii maana post ya pili ya mtoa hoja hii inasema kuwa ajira haikufata taratibu za kisheria kwamba ameajiriwa kwa mlango wa nyuma! ingefuatiliwa hii ingekuwa tamu sana kuliko kuanza kumtupia mawe mtoa hoja, tunachoamini JF ni mtambo wa kurekebisha tabia so ifuatiliwe ili haki ijulikane kama ni jungu au la? hasa kwa ndugu zetu wana JF mliopo Dodoma fuatilieni kama kweli kulikuwa na mtu aitwaye Kwikima ofisi ya madini Dodoma na sasa ameacha kazi na kuanza ofisi mpya Bungeni, na anatokea Dodoma, na ajira yake haikufata taratibu za ajira thats all
 
Wakulugo ! naomba nikushukuru kwa ufafanunuzi makini ulionisaidia, natumai hoja yako sasa yaweza kuifanya hoja yangu kuwa yenye mashiko kama Nziku alivyoomba vinginevyo itaniwia vigumu sana kumwelewa Nziku endapo katika hoja yangu hajapata chochote cha maana kwa faida ya wana JF japo kaongelea kuwa inawezakana yakawa ni majungu fitina au uhasama issue ni je hoja zitolewazo zina msingi wa ukweli wowote au?
 
Back
Top Bottom