Spika aandamwa kwa visasi - Bunge

Kimbembe

Senior Member
May 14, 2006
122
15
na Mwandishi Wetu

OFISI ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, imesema Spika wa Bunge, Samuel Sitta, ana maadui wanaoathirika na maamuzi ya Bunge pamoja na wafanyakazi wachache wa ofisi hiyo wenye nongwa na ambao wameshindwa kwenda na dhana ya viwango na kasi katika utendaji wao.

Kutokana na hali hiyo, ofisi hiyo imesema inazo taarifa za njia mbalimbali zinazotumika na mahasimu wake (Spika) kumchafua kutokana na msimamo wake wa kuliimarisha Bunge liwe chombo madhubuti zaidi cha uwakilishi wa wananchi.

Ofisi hiyo ya Bunge imelazimika kueleza hayo kufafanua tuhuma mbalimbali zinazotolewa dhidi ya Spika kwa njia ya mtandao wa inteneti.

Taarifa iliyotolewa jana na Kaimu Katibu wa Bunge, Dk. Thomas Kashililah, inaeleza kuwa tuhuma hizo zinazotolewa zinaelekea kuwa ni wa makusudi na usiostahili na unaenezwa na makundi hasimu dhidi ya Spika.

“Ni vema vyombo vya habari vijihadhari na taarifa za kuokoteza ambazo zinaeneshwa kwa misingi ya chuki.

“Tujiulize kwa nini haya yanatokea mara baada ya maamuzi ya Bunge kuhusu Richmond? Ofisi ya Bunge inatambua muhimu wa wananchi kupewa taarifa sahihi kuhusu Bunge na uendeshaji wake kwa vile ni chombo chao cha uwakilishi,” ilieleza sehemu ya taarifa hiyo.

Taarifa hiyo inaeleza kuwa Ofisi ya Bunge inasikitishwa na tuhuma zinazoelekezwa kwa Spika na kusema ikiwa kuna yeyote ambaye anazo tuhuma halisi dhidi ya Spika, anapaswa kuziwasilisha kwa uwazi, ili zifikishwe kwenye mamlaka husika zifanyiwe kazi kwa utaratibu ulio bayana.

“Vinginevyo minong’ono dhidi ya viongozi ndio zitakuwa habari za nchi yetu. Hapo sio tu tunawadhalilisha viongozi walengwa bali zaidi tunaidhalilisha nchi,” ilieleza taarifa hiyo.

Taarifa hiyo inakanusha Ofisi ya Bunge kumlipia Spika sh milioni mbili kwa kila wiki kwa ajili ya dawa au matibabu na kwamba hajawahi kuhojiwa kuhusu matumizi ya gari la umma.

Inaelezwa kuwa Spika ana magari ya walinzi na ya huduma za nyumbani licha ya gari rasmi na kwamba magari yote yanatumika kuzingatia bajeti iliyopangwa, kwa ajili ya Ofisi ya Spika.

Aidha, inaelezwa kuwa Bunge linasimamia vema matumzi kwake na yangekuwepo matumizi ya hovyo ya fedha, yangedhihirishwa katika taarifa za kila mwaka za wakaguzi.



Source:
TanzaniaDaima
 
Mzee wa vimada na kukurupuka - Samweli Sitta - alionya watu kuwa makini na taarifa za internet (akiongelea JF) kuhusu BoT na leo hii imefahamika kuwa mwizi na mkoloni mwenye uraia wa utata - Rostam Azizi - ni miongoni mwa waliofilisi hazina.

Katika hili la kukataa, historia ya spika inamweka kwenye wrong side of the issue! Clean your house na usilaumu mwanga ambao unatumika kukuonyesha namna ulivyo mchafu!
 
Sioni ajabu hata kidogo kwa huyu bwana kukanusha yote yatakayosemwa. Mlikuwa mmezoea kufanya madhambi bila kuwa na yeyote wa kusema. sasa yanafunuka moja baada ya lingine.

mimi sijaona jambo lolote la ajabu alilofanya huko bungeni kupelekea kuwekewa visasi sana sana amewabeba hao mafisadi huku bunge ameligeuza kama nyumba ya washabiki. Change your ways.
 
Sioni ajabu hata kidogo kwa huyu bwana kukanusha yote yatakayosemwa. Mlikuwa mmezoea kufanya madhambi bila kuwa na yeyote wa kusema. sasa yanafunuka moja baada ya lingine.

mimi sijaona jambo lolote la ajabu alilofanya huko bungeni kupelekea kuwekewa visasi sana sana amewabeba hao mafisadi huku bunge ameligeuza kama nyumba ya washabiki. Change your ways.

Mshangao wangu ni mmoja .Namuuliza huy Dr.sijui nani jina lake .Kama Spika anazuliwa mambo mbona ukweli wa matumizi ya shilingi 2m toka pale Oysterbay Pharmacy uko nje ? Kama kuna ukweli kwenye hili nani anauzuia ukweli kwenue haya mengine ?
 
OFISI ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, imesema Spika wa Bunge, Samuel Sitta, ana maadui wanaoathirika na maamuzi ya Bunge pamoja na wafanyakazi wachache wa ofisi hiyo wenye nongwa na ambao wameshindwa kwenda na dhana ya viwango na kasi katika utendaji wao.

Viwango gani na kasi gani? Viwango vya uoga, kuwa coward na political pandering to the people in power?

Kutokana na hali hiyo, ofisi hiyo imesema inazo taarifa za njia mbalimbali zinazotumika na mahasimu wake (Spika) kumchafua kutokana na msimamo wake wa kuliimarisha Bunge liwe chombo madhubuti zaidi cha uwakilishi wa wananchi.
Hivi kunyamazisha wapinzani nako kuna count kama "kuliimarisha bunge"?

Ofisi hiyo ya Bunge imelazimika kueleza hayo kufafanua tuhuma mbalimbali zinazotolewa dhidi ya Spika kwa njia ya mtandao wa inteneti.
Si aseme tu JamiiForums

Taarifa iliyotolewa jana na Kaimu Katibu wa Bunge, Dk. Thomas Kashililah, inaeleza kuwa tuhuma hizo zinazotolewa zinaelekea kuwa ni wa makusudi na usiostahili na unaenezwa na makundi hasimu dhidi ya Spika.
Sasa hawa si walisema juzi wanaendesha uchunguzi? Uchunguzi umekwisha katika siku tatu au? Wanatoa kauli kama hii kabla ya kumaliza uchunguzi au?...

"Ni vema vyombo vya habari vijihadhari na taarifa za kuokoteza ambazo zinaeneshwa kwa misingi ya chuki.
Hata Lowassa naye alisema kuhusu chuki, is this a trend now? Kila mtu akibanwa analia chuki?

"Tujiulize kwa nini haya yanatokea mara baada ya maamuzi ya Bunge kuhusu Richmond? Ofisi ya Bunge inatambua muhimu wa wananchi kupewa taarifa sahihi kuhusu Bunge na uendeshaji wake kwa vile ni chombo chao cha uwakilishi," ilieleza sehemu ya taarifa hiyo.
Hapa wanataka ku spin kama wao ndiyo walikuwa vinara wa kutaka Lowassa atemwe. Wewe Sitta si ndiye ulitaka kukimbia nchi uende Marekani na kumuagiza mama Makinda naibu wako asiiguse hii issue? Mpaka ikabidi umuombe msamaha baada ya kuwa forced kuiweka mbele ya bunge hii issue? Au unafikiri tuna kumbukumbu fupi sana hivyo?

Taarifa hiyo inaeleza kuwa Ofisi ya Bunge inasikitishwa na tuhuma zinazoelekezwa kwa Spika na kusema ikiwa kuna yeyote ambaye anazo tuhuma halisi dhidi ya Spika, anapaswa kuziwasilisha kwa uwazi, ili zifikishwe kwenye mamlaka husika zifanyiwe kazi kwa utaratibu ulio bayana.
This is a challenge we ought to gladly take.Hapa tunatakiwa kuwafanya wajute kwa nini walijitutumua na kusema hivi. Wanataka waletewe picha kama za kaka Ditto na ankara za malipo, kama sio uzushi hii ni challenge nzuri tu.
 
Kuna mahali walisema kwaba Spika alikuwa kesha tumia 2m ka dawa pekee za mguu ama kitu gani na risiti ni za mgando .Mimi nadhani katika haya kuna ukweli mwingi sana .Wanaficha ficha kuwaita wat wabaya kwa kuwa walipokula wote hawakusema na sasa wanasema baada ya kundi lao kuvurugana.
 
Back
Top Bottom