Spidi ya wakinga kwenye biashara inatisha, tuna lipi la kujifunza?

Nimeyaamini maneno ya Nyerere kuwa baada ya kuuvunja muungano watanganyika watagundua hakuna kitu kimoja kinachoitwa Tanganyika

Nje ya muungano kuna wahaya,wakinga,wajaluo,wasukuma nk
 
Utajiri wa masharti huo sio utajiri ni laana tu.
Yaani pesa ninayo lakini naogopa kula na kuvaa vizuri kisa nitafilisika huo ni upumbavu.
Mtu anayeonea ubahili hata tumbo lake anaweza kumsaidia maskini mwenye njaa kweli?
Kwangu mimi utajiri ni kua na uwezo wa kuihudumia familia yangu vizuri (kukidhi mahitaji yooote ya familia) pamoja na kuwasaidia watu wangu wa karibu ndugu, jamaa, marafiki na wote wasiojiweza wanaonizunguka katika jamii.
Mambo ya kufungia mabilioni ya pesa bank huku kuna watu walionizunguka wanakufa kwa njaa au wanapoteza maisha kwa kukosa huduma ya matibabu huo kwangu sio utajiri ni ufahari usio na faida yoyote kwangu.
Ndg yangu weee! unasema tu! kwa sababu hujui! nini unasema!! kuvaa kustarehe inategemea na hobby ya mtu ndg yangu weyeee!
Kwa mfano mie tajiri sana!! siwezi kufakamia, Nyama choma, vinono, kutembelea gari masaa 24, mazoezi ni muhimu mnoo!

Mademu, sijui Pombe kwa sana, sababu najua hii itaniletea pressure!!! Kisukari,! Obesenk! nk na matokeo ya haya yoote ni nini??? ... Kifo cha ghafla! ukiona tajiri yuko km wewe atakufa mapema mnoo! utajiri unahitaji nidhamu! umaskini unahitaji nidhamu!

Hayo unayoosema masharti!! basi ni nidhamu ya utajiri!.....hkn cha masharti ya kichawi km ni ivo Mbagalla kote huko wangekuwa matajiri shida zoote zile unadhani wanapenda kuwa hivo??

Na pia jua kuwa mchawi ni ndugu hasa!! au kikulacho ki nguoni mwako!! haya yoote wakinga wanaya jua sasa ogopa sana Mtu ndgu, Yusuf aliuzwa na nduguze, Daudi alitaka kuuawa na mwane Abosalom ili arithi ufalme wa Babae!!

Abel aliuawa na nduguye!! sababu ya wivu tu!! weye ni nani umpe nduguyo, mwanao, jasho lako na akupende daima?

hii yoote ni Mungu katupatia ilimu au funzo tuelewe!! ajabu sasa km huelewi hapa yeye Mungu hayumo tena! atakuacha ufe tu! na mbinguni hupokelewi maana utaangamia kwa kukosa maarifa!

Sawa ni ufahari si Mungu kakupa!! kosa lake ni nini? ujue kwamba hayo unayo yaona eti ni ufahari kuna Tairi mwingine anaona ni u chochoro tu! yaani unahangaika tu! huna kitu! wala si kitu!

Mwingine kumiliki Mbuzi, Punda ving'ombe tu kwake ni ufahari mpaka wana kijiji wanamjalia kwake! wkt huo huo kuna familia wana utajiri wa karne kumi na tano huko nyuma lkn wala hawa tetemeki! tena wakula vyakula vya hovyoooo!

shida kubwa kwao ni uhai kabisaaa! teantajiri hswa hanywi chai! yeye ni uji waulezi tu, na viazi vya kuchemsha, sasa kwa akili zako utasema Bahiri! Kikwete wakt wa sherehe nyumbani kwake watakula vijana. yeye na matajiri ni kunywa maji maji tu!
 
Uchawi pekee wa wakinga ni wanapeana michongo yaani ni kabila wanalobebana lakini pia, Uaminifu huwezi kukuta mkinga mdhulumati kwenye biashara, matumizi bora ya pesa yao, wanawekeza zaidi kwa mfano unakutana nae chuoni nyumbani toka akiwa form one anashamba la miti ekari 20 la kwake hivo hata mkimaliza mkaajiriwa pamoja anakua anasubiri kuuza miti akajiajiri mwenyewe na kumbuka ataenda kujiajiri sehemu sahihi maana atakua na taarifa toka kwa wenzake
Wewee, tema mate chini! Unatamani biashara na utajiri wa Wakinga? Kama wewe ni mcha Mungu wa ukweli, waombee tu ndugu hawa.
 
Hao wakinga ni wote wana hela au..mana mnakuza mambo watu wenyewe hata buku hawafiki kabila zima.

#MaendeleoHayanaChama
 
Ni kweli unachosema ila tatizo wanakumbwa mno na vifo vya utatanishi wakiwa wadogo na miaka michache tu baada ya kupata utajiri. Ukienda Njombe na Makambako kuna wajane hadi utasikitika
Baelezee! Kwa kifupi ni kwamba, Ni ngumu mno mno kufanya biashara za Bongo ukafanikiwa bila kuhusisha nguvu za giza. Nasema hivyo kwa sababu nimekuwemo humo. Mifumo ya biashara Nchi hii siyo rafiki kwa biashara. Lazima utumie rough. Uloge, uzindike, uibe, udhulumu, ukwepe kodi, utoe rushwa, uuze bidhaa counterfeit, na kadhalika. Ukimwona mtu ni tajiri Nchi hii, mwogope sana. Na umheshimu pia.
Aidha, haya mambo hayatushangazi wakristo tuliookoka; tena tuliookoka kwelikweli. Shetani-ibilisi alimshawishi Bwana Yesu Kristo amsujudie ili ampatie mali na utajiri kwani rasilmali zote za Dunia hii zipo chini ya udhibiti wake, na kuwa humpa yeyote kama apendavyo. Bwana Yesu alikataa ujinga huo. Akina Dangote hawa. Si rahisi. Wengine yalitushinda ya Wakinga. Wewe ingia kwenye biashara hata na mtaji mkubwa namna gani na usiwaone "wazee", utakosana na mke au mume kuwa anakuibia pesa. Mtaji badala ya kukua, Unapungua siku baada ya siku. Waulize wastaafu serikalini. Utasema ni uzoefu wa biashara; Uzoefu?! Dunia hii ina Mambo ndugu. Anyway, nawakumbusha ndugu zangu Wakinga kuwa hapa Duniani tulikuja uchi, na tutaondoka uchi hali kadhalika. Ndugu zangu Wachagga nao wameingizwa kwenye kamchezo ka Wakinga. Nenda Kilimanjaro na utulie, utakutana na story za ajabu za ushirikina. Wanatoana ndagu kwa kwenda mbele. Milango ya wizi serikalini si imedhibitiwa! Ndiyo hivyo.
 
Siri ya ukwasi kwenye shughuli yoyote inatokana na mambo makuu matatu:-

1. Bidii katika kutafuta na kuwekeza pesa(thrifty and investment)

2. Nidhamu katika matumizi ya pesa(frugality).

3. Kuweka akiba(savings)

Huo ndio utamaduni wa pesa ambao makundi makubwa ya watu wenye asili ya kufanya biashara(mf. wahindi) wameujua na kuutekeleza kwa vizazi vingi.

Lakini huu utamaduni sio attribute ya kabila fulani kama ambavyo ujinga unawatuma wengine kufikiria. Mtu yoyote anayeingia kwenye utafutaji akiwa na akili timamu anaweza kufikia kiwango kikubwa cha ukwasi kama akifuata utamaduni huu na mambo mengine kama kuvutia wateja kwenye biashara yake, kushirikiana na wengine katika kuibua mitaji, kufanya biashara sahihi kwenye mazingira na wakati sahihi n. k.

Hapana shaka hao wafanyabiashara wakinga wanaokuja juu wamegundua huu utamaduni wa pesa na wanaufanyia kazi. Mganga anapokuambia usijenge nyumba ya fahari ya kuishi itakayokata mtaji wako, au uvae yeboyebo na sio moccasin anakufundisha kuwa frugal.
Na ni siri iliyopaswa kuwa wazi kuwa sehemu kubwa ya utajiri inatokana na matumizi ya mali kwa nidhamu ya hali ya juu.

Hizo habari nyingine za ushirikina na mazindiko(wahindi huwa wanasemwa sana pia kwa haya) na kwamba kabila la mtu lina uhusiano na business acumen yake ni ujinga tu ambao umekataa kuondoka kwenye vichwa vya waafrika walio wengi na hivyo kuendeleza umasikini.
 
Wakinga Siri yao ya mafanikio ni moja tu, WABAHILI.

HAWAHONGI, HAWAVAI VIZURI, HAWALI VIZURI HADI KIELEWEKE.

kitu ambacho wengi kinatushinda, tukipata faida kidogo tu lazima jamii itufahamu sisi ni nani, ila mkinga unaweza pishana nae kavaa ndala na Rambo yake mkononi ukamchulia poa, kumbe anaenda zake benki kuweka mamilioni ya MAUZO, alitoka hapo anapiga viazi vitamu vya kuchemsha na maji....

Sisi wengine sasa.....sisiiiiiiii.......hehehehe tutazungukwa walinzi kisa kafaida kaduchu tu
 
Wakinga Siri yao ya mafanikio ni moja tu, WABAHILI.

HAWAHONGI, HAWAVAI VIZURI, HAWALI VIZURI HADI KIELEWEKE.

kitu ambacho wengi kinatushinda, tukipata faida kidogo tu lazima jamii itufahamu sisi ni nani, ila mkinga unaweza pishana nae kavaa ndala na Rambo yake mkononi ukamchulia poa, kumbe anaenda zake benki kuweka mamilioni ya MAUZO, alitoka hapo anapiga viazi vitamu vya kuchemsha na maji....

Sisi wengine sasa.....sisiiiiiiii.......hehehehe tutazungukwa walinzi kisa kafaida kaduchu tu

Huo sio ubahili(misery) bali ni matumizi yenye nidhamu na kipimo(frugality).
 
Wakinga Siri yao ya mafanikio ni moja tu, WABAHILI.

HAWAHONGI, HAWAVAI VIZURI, HAWALI VIZURI HADI KIELEWEKE.

kitu ambacho wengi kinatushinda, tukipata faida kidogo tu lazima jamii itufahamu sisi ni nani, ila mkinga unaweza pishana nae kavaa ndala na Rambo yake mkononi ukamchulia poa, kumbe anaenda zake benki kuweka mamilioni ya MAUZO, alitoka hapo anapiga viazi vitamu vya kuchemsha na maji....

Sisi wengine sasa.....sisiiiiiiii.......hehehehe tutazungukwa walinzi kisa kafaida kaduchu tu
Unachekesha
 
Hawa jamaa ni wachapa kazi,wavumilivu,hawana makuu,waaminifu ndio siri ya mafanikio yao
 
Kuna jambo la kustukiza sana katika miaka ya hivi karibuni kuanzia 2010, kuna hawa jamaa wanaitwa wakinga wamejipatia umaarufu ndani ya miaka hii michache kwa spidi ya 4g.

Ni kabila dogo sana ambalo haliingii hata kwenye orodha ya makabila 20 yenye watu wengi hapa nchini, Ni kabila ambalo lipo chini mno kwenye elimu lakini wana kipaji cha kufanya biashara, kama samaki alipewa kipaji cha kuogelea, farasi alipewa mbio, basi wakinga walipewa akili ya biashara, siongei maneno matupu maana nayashuhudia kwa macho yangu.

leo hii ukienda pale kariakoo ni ya wakinga, kiukweli inastua.


Kwa mimi binafsi nikiwa chuoni, kuna mkinga flani alimaliza form 4 akaja kuanza certificate, nilipata kumjua, yule dogo hata hakumaliza certificate alianza kuuza mitumba ya nguo ila leo hii ana duka lake la simu za iphone hajafika hata miaka 25 na maisha yake yamebadilika.

Kuna mwengine alipomaliza chuo alipata ajira, analipwa vizuri tu kama 1.3 M take home na allowances kibao, ila alikaa kazini mwaka moja tu, aliacha hio kazi watu walimshangaa sana, alifungua biashara yake, hatua aliyofikia kwa sasa inavutia kwa kweli,

Mwengine namjua alimaliza chuo, hata hakuhangaika kitafuta kazi, alichangiwa mtaji wa biashara, nilitegemea atafungua duka mkoa anaoishi ila alivuka mategemeo yangu, huyu kaenda huko Zambia kwenye mikoa ya kawaida kabisa tena ndani ndani huko hata hana ndugu, bwana! bwana! bwana! duka ni la vitu general kama kina mangi ila anauza si mchezo! ndani ya miezi 8 tu aliweza kupanua duka lake, na saizi kaongeza duka la ziada basi ni mwendo wa bampa to bampa,

Nafkiri kuna namna tunaweza jifunza kupitia hili kundi,

Kumekua na fununu za ndumba na uchawi ila kwa bidii nayoona waliyo nayo unaona kabisa the juice is worth the squeeze, kama unahisi ni ndumba basi na wewe karoge,!!
Wakinga ndugu zako kama ujuavyo wanapuliza vibaya na utaona tu jinsi wanavyofekana na hawatafika mbali sana.
 
Kuna jambo la kustukiza sana katika miaka ya hivi karibuni kuanzia 2010, kuna hawa jamaa wanaitwa wakinga wamejipatia umaarufu ndani ya miaka hii michache kwa spidi ya 4g.

Ni kabila dogo sana ambalo haliingii hata kwenye orodha ya makabila 20 yenye watu wengi hapa nchini, Ni kabila ambalo lipo chini mno kwenye elimu lakini wana kipaji cha kufanya biashara, kama samaki alipewa kipaji cha kuogelea, farasi alipewa mbio, basi wakinga walipewa akili ya biashara, siongei maneno matupu maana nayashuhudia kwa macho yangu.

leo hii ukienda pale kariakoo ni ya wakinga, kiukweli inastua.


Kwa mimi binafsi nikiwa chuoni, kuna mkinga flani alimaliza form 4 akaja kuanza certificate, nilipata kumjua, yule dogo hata hakumaliza certificate alianza kuuza mitumba ya nguo ila leo hii ana duka lake la simu za iphone hajafika hata miaka 25 na maisha yake yamebadilika.

Kuna mwengine alipomaliza chuo alipata ajira, analipwa vizuri tu kama 1.3 M take home na allowances kibao, ila alikaa kazini mwaka moja tu, aliacha hio kazi watu walimshangaa sana, alifungua biashara yake, hatua aliyofikia kwa sasa inavutia kwa kweli,

Mwengine namjua alimaliza chuo, hata hakuhangaika kitafuta kazi, alichangiwa mtaji wa biashara, nilitegemea atafungua duka mkoa anaoishi ila alivuka mategemeo yangu, huyu kaenda huko Zambia kwenye mikoa ya kawaida kabisa tena ndani ndani huko hata hana ndugu, bwana! bwana! bwana! duka ni la vitu general kama kina mangi ila anauza si mchezo! ndani ya miezi 8 tu aliweza kupanua duka lake, na saizi kaongeza duka la ziada basi ni mwendo wa bampa to bampa,

Nafkiri kuna namna tunaweza jifunza kupitia hili kundi,

Kumekua na fununu za ndumba na uchawi ila kwa bidii nayoona waliyo nayo unaona kabisa the juice is worth the squeeze, kama unahisi ni ndumba basi na wewe karoge,!!
Nime ipenda Spirit ya Wakinga
 
Back
Top Bottom