Ndg yangu weee! unasema tu! kwa sababu hujui! nini unasema!! kuvaa kustarehe inategemea na hobby ya mtu ndg yangu weyeee!Utajiri wa masharti huo sio utajiri ni laana tu.
Yaani pesa ninayo lakini naogopa kula na kuvaa vizuri kisa nitafilisika huo ni upumbavu.
Mtu anayeonea ubahili hata tumbo lake anaweza kumsaidia maskini mwenye njaa kweli?
Kwangu mimi utajiri ni kua na uwezo wa kuihudumia familia yangu vizuri (kukidhi mahitaji yooote ya familia) pamoja na kuwasaidia watu wangu wa karibu ndugu, jamaa, marafiki na wote wasiojiweza wanaonizunguka katika jamii.
Mambo ya kufungia mabilioni ya pesa bank huku kuna watu walionizunguka wanakufa kwa njaa au wanapoteza maisha kwa kukosa huduma ya matibabu huo kwangu sio utajiri ni ufahari usio na faida yoyote kwangu.
Wewee, tema mate chini! Unatamani biashara na utajiri wa Wakinga? Kama wewe ni mcha Mungu wa ukweli, waombee tu ndugu hawa.Uchawi pekee wa wakinga ni wanapeana michongo yaani ni kabila wanalobebana lakini pia, Uaminifu huwezi kukuta mkinga mdhulumati kwenye biashara, matumizi bora ya pesa yao, wanawekeza zaidi kwa mfano unakutana nae chuoni nyumbani toka akiwa form one anashamba la miti ekari 20 la kwake hivo hata mkimaliza mkaajiriwa pamoja anakua anasubiri kuuza miti akajiajiri mwenyewe na kumbuka ataenda kujiajiri sehemu sahihi maana atakua na taarifa toka kwa wenzake
Baelezee! Kwa kifupi ni kwamba, Ni ngumu mno mno kufanya biashara za Bongo ukafanikiwa bila kuhusisha nguvu za giza. Nasema hivyo kwa sababu nimekuwemo humo. Mifumo ya biashara Nchi hii siyo rafiki kwa biashara. Lazima utumie rough. Uloge, uzindike, uibe, udhulumu, ukwepe kodi, utoe rushwa, uuze bidhaa counterfeit, na kadhalika. Ukimwona mtu ni tajiri Nchi hii, mwogope sana. Na umheshimu pia.Ni kweli unachosema ila tatizo wanakumbwa mno na vifo vya utatanishi wakiwa wadogo na miaka michache tu baada ya kupata utajiri. Ukienda Njombe na Makambako kuna wajane hadi utasikitika
Wakinga Siri yao ya mafanikio ni moja tu, WABAHILI.
HAWAHONGI, HAWAVAI VIZURI, HAWALI VIZURI HADI KIELEWEKE.
kitu ambacho wengi kinatushinda, tukipata faida kidogo tu lazima jamii itufahamu sisi ni nani, ila mkinga unaweza pishana nae kavaa ndala na Rambo yake mkononi ukamchulia poa, kumbe anaenda zake benki kuweka mamilioni ya MAUZO, alitoka hapo anapiga viazi vitamu vya kuchemsha na maji....
Sisi wengine sasa.....sisiiiiiiii.......hehehehe tutazungukwa walinzi kisa kafaida kaduchu tu
UnachekeshaWakinga Siri yao ya mafanikio ni moja tu, WABAHILI.
HAWAHONGI, HAWAVAI VIZURI, HAWALI VIZURI HADI KIELEWEKE.
kitu ambacho wengi kinatushinda, tukipata faida kidogo tu lazima jamii itufahamu sisi ni nani, ila mkinga unaweza pishana nae kavaa ndala na Rambo yake mkononi ukamchulia poa, kumbe anaenda zake benki kuweka mamilioni ya MAUZO, alitoka hapo anapiga viazi vitamu vya kuchemsha na maji....
Sisi wengine sasa.....sisiiiiiiii.......hehehehe tutazungukwa walinzi kisa kafaida kaduchu tu
Wakinga ndugu zako kama ujuavyo wanapuliza vibaya na utaona tu jinsi wanavyofekana na hawatafika mbali sana.Kuna jambo la kustukiza sana katika miaka ya hivi karibuni kuanzia 2010, kuna hawa jamaa wanaitwa wakinga wamejipatia umaarufu ndani ya miaka hii michache kwa spidi ya 4g.
Ni kabila dogo sana ambalo haliingii hata kwenye orodha ya makabila 20 yenye watu wengi hapa nchini, Ni kabila ambalo lipo chini mno kwenye elimu lakini wana kipaji cha kufanya biashara, kama samaki alipewa kipaji cha kuogelea, farasi alipewa mbio, basi wakinga walipewa akili ya biashara, siongei maneno matupu maana nayashuhudia kwa macho yangu.
leo hii ukienda pale kariakoo ni ya wakinga, kiukweli inastua.
Kwa mimi binafsi nikiwa chuoni, kuna mkinga flani alimaliza form 4 akaja kuanza certificate, nilipata kumjua, yule dogo hata hakumaliza certificate alianza kuuza mitumba ya nguo ila leo hii ana duka lake la simu za iphone hajafika hata miaka 25 na maisha yake yamebadilika.
Kuna mwengine alipomaliza chuo alipata ajira, analipwa vizuri tu kama 1.3 M take home na allowances kibao, ila alikaa kazini mwaka moja tu, aliacha hio kazi watu walimshangaa sana, alifungua biashara yake, hatua aliyofikia kwa sasa inavutia kwa kweli,
Mwengine namjua alimaliza chuo, hata hakuhangaika kitafuta kazi, alichangiwa mtaji wa biashara, nilitegemea atafungua duka mkoa anaoishi ila alivuka mategemeo yangu, huyu kaenda huko Zambia kwenye mikoa ya kawaida kabisa tena ndani ndani huko hata hana ndugu, bwana! bwana! bwana! duka ni la vitu general kama kina mangi ila anauza si mchezo! ndani ya miezi 8 tu aliweza kupanua duka lake, na saizi kaongeza duka la ziada basi ni mwendo wa bampa to bampa,
Nafkiri kuna namna tunaweza jifunza kupitia hili kundi,
Kumekua na fununu za ndumba na uchawi ila kwa bidii nayoona waliyo nayo unaona kabisa the juice is worth the squeeze, kama unahisi ni ndumba basi na wewe karoge,!!
Nime ipenda Spirit ya WakingaKuna jambo la kustukiza sana katika miaka ya hivi karibuni kuanzia 2010, kuna hawa jamaa wanaitwa wakinga wamejipatia umaarufu ndani ya miaka hii michache kwa spidi ya 4g.
Ni kabila dogo sana ambalo haliingii hata kwenye orodha ya makabila 20 yenye watu wengi hapa nchini, Ni kabila ambalo lipo chini mno kwenye elimu lakini wana kipaji cha kufanya biashara, kama samaki alipewa kipaji cha kuogelea, farasi alipewa mbio, basi wakinga walipewa akili ya biashara, siongei maneno matupu maana nayashuhudia kwa macho yangu.
leo hii ukienda pale kariakoo ni ya wakinga, kiukweli inastua.
Kwa mimi binafsi nikiwa chuoni, kuna mkinga flani alimaliza form 4 akaja kuanza certificate, nilipata kumjua, yule dogo hata hakumaliza certificate alianza kuuza mitumba ya nguo ila leo hii ana duka lake la simu za iphone hajafika hata miaka 25 na maisha yake yamebadilika.
Kuna mwengine alipomaliza chuo alipata ajira, analipwa vizuri tu kama 1.3 M take home na allowances kibao, ila alikaa kazini mwaka moja tu, aliacha hio kazi watu walimshangaa sana, alifungua biashara yake, hatua aliyofikia kwa sasa inavutia kwa kweli,
Mwengine namjua alimaliza chuo, hata hakuhangaika kitafuta kazi, alichangiwa mtaji wa biashara, nilitegemea atafungua duka mkoa anaoishi ila alivuka mategemeo yangu, huyu kaenda huko Zambia kwenye mikoa ya kawaida kabisa tena ndani ndani huko hata hana ndugu, bwana! bwana! bwana! duka ni la vitu general kama kina mangi ila anauza si mchezo! ndani ya miezi 8 tu aliweza kupanua duka lake, na saizi kaongeza duka la ziada basi ni mwendo wa bampa to bampa,
Nafkiri kuna namna tunaweza jifunza kupitia hili kundi,
Kumekua na fununu za ndumba na uchawi ila kwa bidii nayoona waliyo nayo unaona kabisa the juice is worth the squeeze, kama unahisi ni ndumba basi na wewe karoge,!!