Speed ya Sauli bus: Mabasi yanayokimbia sana hayana vidhibiti mwendo?

kashibaba

Senior Member
Nov 26, 2019
191
269
1599480522207.png

Wadau salaam kwenu,

Kwa sasa bus la Sauli ndio linaweza kuwa bas linalokimbia sana barabarani (dhania) kwa Tanzania.

Nnafikir na Mfalme Zakaria wa Mwanza Musoma hatoshi, naona tunaanza taratibu kurudi kwa kina Leina tours, City boy na Kisbo kwa njia ya Kahama Dar, Buffalo na Ngorika enzi zile.

Swali langu vidhibiti mwendo Sauli hana au nini? Naamini ana gari mpya kabisa na ni Scania but speed alizonazo huwa zinaogopesha kiasi.

Mimi nimepanda mara chache tu, watu wa Moro wanaiita ndege ya chini, kama ambavyo wale wa Mwanza na Kahama tulizoea kuyaita mabasi ya Allys miaka ya 2007 na kuendelea maana Kahama - Dar saa 1 ulikuwa unaikuta Masbine pale Oilcom inapumua toka Kahama na Dar saa 2 tu mnaingia.

Sina chuki na kampuni hii lakina usalama wa abiria wenzangu ndio unanisukuma kutaka kujua.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sio kwamba kila siku ni Sauli tu,wapo washindani wake mkuu,Kuna mwekezaji (Golden Deer) anamwaga maji na wengine wengi tu,na sio kwamba eti Sauli ndio gari inayokimbia kuliko zote Tanzania hiyo ni dhana uliyoibuni ww mleta uzi.

Screenshot_20200114-200649.jpeg
Screenshot_20200114-200701.jpeg
 
kashibaba,
Polisi/ Traffic wapo barabarani saa zote na vidhibiti mwendo vimefungwa kwenye gari zote vipi pawe na mwendo hatarishi? bila ushahidi usiokuwa na shaka basi uzi wako huu utakuwa umekaa kimbeambea na inaonyesha kule RSA wamekuchokeni sasa mmevamia JF kuleta hoja mfu.
 
Polisi/Traffic wapo barabarani saa zote na vidhibiti mwendo vimefungwa kwenye gari zote vipi pawe na mwendo hatarishi?...
Si hoja mfu ndugu, na siongei kwa upande wowote, sina nia mbaya na kampuni ya sauli naipenda sababu ya mabasi yake yako vizuri kwa maana ya uimara na ni luxury buses, kuulizia mwendo ni haki yangi kama abiria na kwa abiria wengine, maana hata nisipopanda mim wanapanda watanzania wenzangu na wanadamu wengine kama mim,,ninaangazia hilo tu mkuu, si mzoefu sana wa njia ile,,ila mara chache

Sent using Jamii Forums mobile app
 
kwani mabasi yanayokimbia polepole hamuyaoni mpaka mje kuanzisha nyuzi, tuachieni mabasi yetu yanayokimbia siungi mkono vidhibiti mwendo speed sio chanzo pekee cha ajali
Kuhusu chanzo pekee cha ajali nakubaliana na wew,,lakini ni moja ya chanzo tena kikubwa, unakumbuka miaka ya karibuni ajali zimepungua,,na zikitokea madhara yake ni ya kawaida kama ajali imetokea kawaida,,ndg nafikir unakumbuka ajali za city boy pale singida,,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivi Happy Nation na Hai bado zipo?

Wale wapuuzi ndio basi la kwanza kulikubali baada ya miaka mingi ya kupotea kwa Kiswele

Kuna hiyo siku jamaa wa Happy Nation alitoka Mbeya 12 asubuhi, saa tisa na dakika zake akapaki gari Natioil ya Mbezi Luguruni/Mbezi Mwisho akivuta muda.
 
Kuhusu chanzo pekee cha ajali nakubaliana na wew,,lakini ni moja ya chanzo tena kikubwa, unakumbuka miaka ya karibuni ajali zimepungua,,na zikitokea madhara yake ni ya kawaida kama ajali imetokea kawaida,,ndg nafikir unakumbuka ajali za city boy pale singida...
isuue ya city boy haikusababishwa na speed ilikua mbwembwe tu za madereva, narudia tena kama hupendi basi linaloenda speed mtuachie pandeni hizo luxury zenu tuachini mabasi yetu tuwahi kufika mambo ni mengi muda ni mchache.
 
Si hoja mfu ndg, na siongei kwa upande wowote, sina nia mbaya na kampuni ya sauli naipenda sababu ya mabasi yake yako vizuri kwa maana ya uimara na ni luxury buses,,kuulizia mwendo ni haki yangi kama abiria na kwa abiria wengine,,maana hata nisipopanda mim wanapanda watanzania wenzangu na wanadamu wengine kama mim,,ninaangazia hilo tu mkuu, si mzoefu sana wa njia ile,,ila mara chache

Sent using Jamii Forums mobile app

Naomba nikupe mfano mmoja, Nimeondoka Iringa saa 12 asubuhi na Upenda Bus gari ambayo kila kituo inasimama kutafuta abiria na magari yanayotoka Njombe yalitupita kabla ya Mikumi na bahati mbaya siku hiyo tuliingia Dar saa 2 wakati magari ya Njombe yaliwahi kufika Ubungo mapema tu je hapo utasema gari hizo zinakimbia sana na ku overspeed?

Hivyohivyo ukitaka kuchelewa kufika Iringa panda gari za Iringa ambazo hawaendi na muda kabisa tofauti na wenzao ambao wanazingatia muda kitu ambacho hakiwezi kuitwa Overspeeding na ni vizuri endapo ungetueleza kuwa abiria tumemwonya dereva wa Sauli baada ya kuona kuwa anaendesha kwa ma speed kuliko kuja kuchonga huku mtandaoni, Tukeemee udereva mbovu bila upendeleo na tuendelee kuelimishana kwa uwazi
 
Back
Top Bottom