Speed ya CHADEMA, CCM hoi Mwanza, Tabora, Shinyanga, Kigoma...

Crashwise

JF-Expert Member
Oct 23, 2007
22,227
8,735
Speed ya chama cha Demokrasia na Maendeleo mikoa ya Shinyanga, Kigoma, Tabora na Mwanza ilikopamba na fitna nyingi za CCM na wasaliti waliokuwa wanachama wa chama hicho Zitto, Matata, Habibu, Amani Kabouru (Mwenyekiti CCM Kigoma) kwa usimamizi wa karibu kabisa na chama cha majagili,mafisadi, Dr Slaa alifanikikiwa kuziteketeza mbinu zao zote ambazo zilitishia uhai wa Dr Slaa, lakini Dr Slaa aliwaambia 'naenda Kigoma kaskazini na kama ni risasi wanipige' tukashuhudia thread nyingi sana humu jamvini mara chadema imekufa, Dr Slaa apigwa mawe lakini wenye akili tulijua niporojo za maccm maana tulijiuliza hivi Dr. Slaa kila siku anapigwa mawe lakini anayakwepa tu lazima atakuwa hodari sana na nilitamani akamfundishe namna ya kukwepa mawe Mabina!, juzi ilikuwa safari ya Mwanza chini ya kamanda wa anga sauti ya zege Mhe. Freeman Mbowe huko aliwazika Dr Asha Rose Migiro aliyejaribu kujipima na kamanda wa anga pamoja na kutishwa kuwa asikanyage Mwanza na alipofika mwanza kuongea na wanafunzi wa vyuo vikuu jijini Mwanza, CCM chini ya Asha Rose Migiro na Antony Diallo(Mmiliki Sahara Communication yaani Startv, Kissfm, RFA na gazeti linalopatikana kanda ya ziwa) nao waliitisha mkutano wa wanafunzi wa vyuo vikuu na kutoa usafiri pamoja na chakula kwa wote ambao wangefika kwenye mkutano huo lakini kuonyesha Watanzania wameshajua ujinga wa CCM waliamua kupuua na kuachana na ubwabwa na usafiri huo wa bwerere na kuamua kujilipia gharama zote hizo ili kushiriki mkutano wa Chadema.
Jana tarehe 15.12.2013 ndiyo ilikuwa funika mbaya Kwa Mwanza na Tabora Huku Dr Slaa kule Mbowe baada ya watu mwengi sana kujitokeza kwenye mikutano ya Mwanza na Tabora..Bila shaka utabiri wa Dr Dr Kikwete kuwa wasipoangalia CCM inakufa inaenda kutimia chadema ina tisha na inazidi kukubarika sana kuelekea chaguzi za serikali ya mitaa ambazo kimusingi ndizo zinazoongoza serikali kama mwendo huu utaendelea na bilasha CCM hawana tena binu za kuizibiti baada ya Video ya kichina kubuma, wasaliti ambao ndiyo walikuwa wanawapa kiburi na kujiaminisha kuwa chadema ingekufa ndani ya mwaka huu na kutembea kifua mbele wakijiaminisha ushetani wao sasa zinashindwa vibaya hakika Mungu anaendelea kuibariki sana chadema maovu yote ya CCM Mungu anazidi kuwaumbua na ataendelea kuwaumbua...
Ombi langu kwa chadema ni kufukuza kila anae leta usaliti na tusonge mbele muda wa kufuga wasaliti umekwisha tulimvumilia tangu siku nyingi sana sasa tunangoa Mizizi mpaka matawi ili jeshi likiingia uchaguzi ujao liwe moja siyo mpuuzi anae sema hawezi kumpigia kampeni fulani kwa sabau mgombea wa CCM ni rafiki yake.
View attachment 127034
Kamanada wa anga Freeman Mbowe akikamua jijini Mwanza
2552_343451445796353_1652870020_n.jpg
Dr. Slaa akikamua - Tabora​
=====Mikutano ya Kata kwa kata

View attachment 127080
Msafara wa mapokezi ya Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Willibrod Slaa alipowasili mjini Tabora jana, kuanza ziara yake ya kujenga chama katika mikoa ya Kigoma, Tabora na Singida. (Picha na Joseph Senga)
View attachment 127083 Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Willibrod Slaa akiwahutubia wananchi wa kijiji cha Shitange katika jimbo la Tabora Kaskazini jana, ikiwa ni sehemu ya zira yake ya kujenga chama katika mikoa ya Kigoma, Tabora na Singida. (Picha na Joseph Senga)
View attachment 127085Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Willibrod Slaa akiwahutubia wananchi wa kijiji cha Bukumbi katika jimbo la Tabora Kaskazini jana, ikiwa ni sehemu ya zira yake ya kujenga chama katika mikoa ya Kigoma, Tabora na Singida. (Picha na Joseph Senga)
 
SPEECH KALI KAMA HIZI NDIO MSIBA KWA CCM

[h=2]DR. Slaa: Tukishika Dola tutaruhusu utengenezaji wa pombe ya gongo kisheria[/h]
Saturday, 14 December 2013 ·

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimetoa mpya baada ya kueleza kuwa kitakapofanikiwa kushika dola kitaruhu Shirika la Viwanda Vidogo Vidogo (SIDO) kutengeneza mitambo ya kutengenezea pombe aina ya gongo. Katibu Mkuu wa Chadema, Dk.Willbroad Slaa, akizungumza na wananchi wa Jimbo la Kasulu Vijijini alisema kama gongo itatengenezwa kwa mitambo maalum itaondoa mianya ya rushwa kwa polisi ambao wamekuwa wakiwakamata wanaotengeneza kwa kificho na kuwafanya vitega uchumi vyao.

"Gongo sasa hivi ni haramu sababu inatengenezwa kwa kificho katika mazingira machafu, tukishika dola tutataka SIDO itengeneze mitambo ya kutengeneza gongo ili iwe katika hali ya usafi," alisema.

Mitambo hiyo itakayotengenezwa na SIDO itakapouzwa itaiingizia mapato serikali pia wauzaji wa gongo watafanya biashara hiyo kwa amani tofauti na sasa ambapo wanaifanya kwa kificho na wakikamatwa fedha zote wananufaika polisi.

Dk. Slaa alisema hata suala la kukamata watu wanaotengeneza silaha linapaswa kuangaliwa upya kwani wanaokamatwa wakifanya kazi hiyo wangekuwa wanashikiliwa kwa muda na baadaye wanapelekwa katika kiwanda cha serikali cha kutengenezea silaha ili watuhumiwa hao wapeleke ujuzi huo huko badala ya kuwafunga jela.

Dk. Slaa alisema matatizo yote yanatokana na wasomi kutofikiri namna ya kuisogea nchi mbele kimaendeleo.

"Nchi hii imelala, imechoka sababu waliopewa madaraka wamelala, wamejisahau hawatambui kuwa wamepewa nafasi hizo ili kuwatumikia wananchi," alisema.


CHANZO: NIPASHE​


 
....

...Hakuna kulala mpaka majangili yatokomezwe!!!!

...Mwendo wa subaru ... Moro kimenuka sultan anapumulia mashine ....
 
....

...Hakuna kulala mpaka majangili yatokomezwe!!!!

...Mwendo wa subaru ... Moro kimenuka sultan anapumulia mashine ....
hakuna kulala mpaka walisha watu sumu, wamwagia watu tindikali, walipua watu na mabomu na wapora wake za watu watokomezwe!!!!!!!!!!!!!!
 
Unaweweseka mchana, bado kidogo to utakaa chini.

Kuweweseka mara nyingi kunasababishwa na GONGO HARAMU!
Ambayo chadema inataka kuhalalisha!

Nchi za wenzetu zilizoendelea kila ikifika bajeti zao za mwaka WANAPANDISHA USHURU WA POMBE NA SIGARA ili kuwafanya wananchi wao WAPUNGUZE MATUMIZI YA POMBE!
Tena huko wanaongelea POMBE kama bia na mvinyo ambayo HUWEZI KULINGANISHA NA GONGO!

Wakati bia iliyo na asilimia 2% ya alcohol inafanyiwa kampeni ya kupunguzwa matumizi yake kwa wananchi! Tena kwa wale wavumbuzi wenyewe!!

Leo CHADEMA inataka kuhalalisha GONGO YENYE asilimia zaidi ya 70% ya alcohol NDANI YAKE!!

Sasa tukisema sera za cdm zina lengo la kuleta ATHARI KUBWA SANA KWA WANANCHI na Uwezekano mkubwa wa kuahatarisha maisha ya wananchi
Mtasema sisi WAONGO??

Halafu mtu na busara zake anasema tuige uganda!!

Nyie mabaya tu ndio ya KUIGA! Mazuri aaaaaaa!

Mnfnsssssssss!
 
picha za mwaka 2010 zinatumiwa leo na wafuasi wa chadema kudanganya umma. si kwenye mitandao ya kijamii, gazeti la tz daima na hata itv
 
Back
Top Bottom