Tushauriane kuhusu applications kwa vyuo vilivyopo nje ya Tanzania

ESPRESSO COFFEE

JF-Expert Member
Sep 6, 2014
6,170
7,661
Habarini

Najua Hapa JF kuna watu wapo wanao ishi nje ya Tanzania,pia wapo wanao Soma nje ya Tanzania kwa pesa yao wenyewe,kwa scholarship au kwa Sponsorship! Kozi mbali mbali

Pia kuna wale wanao Tegemea kwenda kusoma nje ya Nchi kwa njia mojawapo ya hizo hapo juu,hata kama si wewe anaweza kuwa ndugu,jamaa, rafiki,mwanao au mtu wako wa karibu yeyote yule!

Lakini likija Suala la Applications hapo ndipo shida huwa inaanzia,kwa sababu ufanyaji wa applications kwa nje Ya Tanzania ni tofauti kabisa! Ndio maana wapiga pesa kama Global Education link wakaanzishwa! Naomba huu uwe uzi maalumu wa kuwasaidia wale wenye nia na malengo ya kwenda kusoma chuo nje ya Tanzania!

Nakumbuka wakati namaliza Form six Nilikuwa na malengo ya kwenda kusoma china Kozi fulani....lakini sikuwa na Idea yoyote wapi kwa kuanzia hadi kwa kumalizia,Ndipo nilipo fanya maamuzi ya kwenda GLOBAL education Link ofisini kwao wakati huo nilikuwa Arusha! Tulienda na Rafiki yangu yeye Alikuwa anataka kwenda kusoma India lakini tulipo fika Global waliniambia niwe na Million 15.5! Kwa kuanza hiyo ikiwa ni hela kwa ajiri ya application,ada,nauli ya kwenda na wakasema Mwaka unaofuata hela itapungua hadi kufikia million 6! Kiukweli nilishindwa lakini Rafiki angu aliamua kuwatumia Global na akaenda India kusoma Mambo ya Moyo! Alipo Rudi aliniambia Global walinila hela nyingi sana ningejua ningefanya Mwenyewee siwataki hata kuwasikia! Kupitia rafiki angu nilijua kuwa watu wanapigwa sana hela kufanya application kwa vyuo vya nje ya Tanzania

Tuwasaidie/Tusaidieni sisi wenye Malengo ya kusoma nje ya Tanzania....

1.Nchi ipi ni nzuri kusoma kozi fulani kwa bei nafuu

2.Ubora wa chuo utaujua vipi(Kuepuka kwenda vyuo vibovu)

3.Namna Ya kufanya applications kuanzia applications Fee,Muda wa kufanya Applications,Vitu vinavyo hitajika!

4.Matokeo Je yawaje na kupitia matokeo yako utajua vipi kuwa unaweza soma chuo fulani (equavalent inafanyikaje?)

5.Utasoma kwa muda gani? Na utaratibu wao upoje je ni Part Time au Full Time mfano najua kuna Tofauti ya Alie maliza Diploma na Fresh from School i mean Form four au Form six kwa nchi zingine!

6.Vitu vya kuzingatia kabla ya kufanya Maombi....Ulipwaji wa Ada,Accomodation na Mambo mengine

Tusaidie na utwambie mwenztu upo chuo gani nje ya Tanzania na Uliomba Vipi,ukweli ni upi wa malipo na vitu vya kujiandaa mapema! Najua wapo watakao beza lakini ulichangia kidogo utakuwa umemsaidia yule asie jua kbisa kuhusu hichi kitu,utakuwa umemuokoa kutoka kwa Matapeli! Kama ikitokea mmoja Kaeleza kifupi kwa ufasaha Mods nitaomba mupdate huu uzi!

Natarajia mwezi Wa nne Kufanya Applications Nchini South Afrika nimeona gharma ni ndogo kuliko kusoma Kenya na Uganja!

Karibuni
 
Mkuu kama uko serious waone hao!!! Watakusaidia sana, kuanzia process ya kwanza mpaka ya Mwisho.

TanSAO
(Tanzania Student Achievement Organization)
Seeking University Admissions and Scholarship Opportunities Worldwide

Plot [HASHTAG]#1820[/HASHTAG] Toure Drive
Golden Tulip Hotel
Msasani Peninsula
PO Box: 23134
DSM, Tanzania
Cell phone: +255 655 493 060
 
Ingia kwenye mtandao Google cucas na cicas. Hawa ni kwa upande wa China. Ni link au ni agents wa vyuo vyote vilivyoko China.
Una apply online. Fanya hivyo if you are serious. Na ukikwama au ukihitaji msaada nitafute.
 
Mkuu kama uko serious waone hao!!! Watakusaidia sana, kuanzia process ya kwanza mpaka ya Mwisho.

TanSAO
(Tanzania Student Achievement Organization)
Seeking University Admissions and Scholarship Opportunities Worldwide

Plot [HASHTAG]#1820[/HASHTAG] Toure Drive
Golden Tulip Hotel
Msasani Peninsula
PO Box: 23134
DSM, Tanzania
Cell phone: +255 655 493 060
Hawa si wanataka Malipo hawa?
 
Ingia kwenye mtandao Google cucas na cicas. Hawa ni kwa upande wa China. Ni link au ni agents wa vyuo vyote vilivyoko China.
Una apply online. Fanya hivyo if you are serious. Na ukikwama au ukihitaji msaada nitafute.
Hawa hawahitaji Malipo je wewe unasoma nje ya Tanzania?
 
Back
Top Bottom