Bwana Utam
JF-Expert Member
- Feb 15, 2016
- 16,637
- 31,134
Endeleeni kujifarijiSidhani Kama kuna kuchezeana akili hapo.
Me nadhani Urusi bado anatumia tactics za Ww2 kwenye hii vita akisahau Kama Ukraine walikua wakipatiwa mafunzo na NATO toka alipoichukua Crimea.
Hivi unakumbuka ule msafara wa Urusi wa 64km uliokua ukielekea Kiev?! Unatumaje msafara mrefu vile bila kua na air cover?! Hatima yake ni nini?! Si ule msafara wote uliharibiwa na Ukraine Kwa Javellin na NLAW za Ukraine alizopewa na Marekani na Uingereza,had warusi wakachanganyikiwa ikabidi wabadili mawazo waachane na Kiev waende kule South ambako walikua wapo kabla hata ya Vita kuanza.
Sasa Leo tena wamejirundika hapo na mavifaa kibao bila hata air cover matokeo yake battalion nzima imeliwa kichwa. Na sasa hivi Ukraine imepewa hizo artillery na nyingine ziko njiani sitashangaa nikiona warusi wakifurushwa mpaka hayo maeneo waliyoteka,mfano ni Kharkiv kule Ukraine wamewarudisha warusi karibu kabisa na mpaka wao (mpaka wa Russia) na wamechukua maeneo na vijiji kadhaa ambavyo vilikua chini ya Urusi na bado wanasonga mbele.
Sent using Jamii Forums mobile app