Special thread: The Vatican secrets and treasures of the Holy City

Mmh mbona mambo magumu hayo, ilithibitiswaje kwamba papa Francis n Moja wapo ya jesuit?
Jesuit siyo jamii ya siri kiasi kwamba isijulikane, kwa sasa imejiweka wazi zaidi na inajulikana kila sehemu duniani kote japo bado inaendesha mipango yake kwa siri.

Kuthibitisha ni kufanya uhakiki wa taarifa mbali mbali wanazozikusanya waandishi wa hivi vitabu, na kufanya mahojiano na members kadhaa wa jamii hiyo, kutokana na hilo wamemtaja kama mojawapo ya watu waliokuwa viongozi wakuu wa Jesuit duniani kabla ya kuchaguliwa kuwa Papa.
 
Na mossad pia uizungumzie. Hyo picha nimechek kwa kina sijamtambua yeyote aisee
Mossad imekuja miaka ya 1980s baada ya Jaribio la kumuua Papa kushindikana, wakatumia mwanya huo kujipenyeza VATICAN ili wasaidie kutoa taarifa ni nani walihusika na mipango hiyo, wakapokelewa kwa mikono miwili na Papa John Paul II, na hatimaye akazuru Jerusalem.

Kwahiyo usijali ntawazungumzia pia.
 
Kwenye ubatizo wala huhitaji swimming pool,ni nia tu ya kufanya the right thing and spiritually sound inahohitajika! You need for example only a brick 3m×3m×4m water tank to the job.Haya mawazo kwamba unahitaji swimming pool ni upotoshaji.By the way,hivi unajua maana ya ubatizo?Tafadhali soma hii👇.Mkuu narudia,hatuwezi kufanya mambo kama tuonavyo sisi,"ni lazima" tufuate muongozo wa Biblia.

Jibu la Biblia​

Ubatizo unarejelea mtu kuzamishwa majini na kuinuliwa tena. Hilo linatusaidia kuelewa kwa nini Yesu alibatizwa katika mto mkubwa. (Mathayo 3:13, 16) Vivyo hivyo, mwanamume Mwethiopia aliomba abatizwe walipofika “mahali penye maji.”Matendo 8:36-40.

Maana ya ubatizo​

Biblia inalinganisha ubatizo na kuzikwa. (Waroma 6:4; Wakolosai 2:12) Ubatizo wa maji unawakilisha mtu kufa kutokana na mambo aliyokuwa akifanya maishani na kuanza maisha mapya akiwa Mkristo aliyejiweka wakfu kwa Mungu. Hatua zinazoongoza kwenye ubatizo pamoja na ubatizo wenyewe ni mpango wa Mungu wa kumsaidia mtu kupata dhamiri safi kwa msingi wa imani katika dhabihu ya Yesu Kristo. (1 Petro 3:21) Kwa hiyo, Yesu alifundisha kwamba wanafunzi wake wanapaswa kubatizwa(Mathayo 28:19, 20).

Je, ubatizo wa maji unasafisha dhambi?​

Hapana. Biblia inafundisha kwamba tunaweza kuoshwa kutokana na dhambi kupitia damu ya Yesu iliyomwagwa. (Waroma 5:8, 9; 1 Yohana 1:7).Hata hivyo, ili mtu anufaike kutokana na dhabihu ya Yesu, anapaswa kumwamini Yesu, abadili njia yake ya maisha ili aishi kupatana na mafundisho ya Yesu, kisha abatizwe.(Matendo 2:38; 3:19).

Je, Biblia inafundisha kuhusu ubatizo wa watoto?​

Hapana, haifundishi jambo hilo. Wazo la kuwabatiza watoto halipatikani katika Biblia. Makanisa fulani hufanya sherehe ya kuwabatiza watoto (kwa kuwamiminia au kuwamwagilia maji kichwani) na kuwapa majina. Ubatizo wa Kikristo ni kwa ajili ya watu walio na umri wa kutosha kuelewa na kuamini “habari njema ya ufalme wa Mungu.” (Matendo 8:12) Unahusianishwa na kusikiliza neno la Mungu, kulikubali, na kutubu,mambo ambayo mtoto hawezi kufanya.(Matendo 2:22, 38, 41).
Mbali na hilo, Biblia inaonyesha kwamba Mungu huwaona watoto wadogo wa Wakristo kuwa watakatifu, au safi machoni pake, kwa sababu ya uaminifu wa wazazi wao. (1 Wakorintho 7:14) Ikiwa ubatizo wa watoto ni halali, basi watoto hao hawangehitaji kutegemea kibali ambacho mtu mwingine anaonyeshwa.

Maoni yasiyo sahihi kuhusu ubatizo wa Kikristo​

Uwongo: Kumimina au kummwagilia mtu maji ni njia inayofaa badala ya kumzamisha kabisa.
Ukweli: Matukio yote ya ubatizo unaotajwa katika Biblia yalihusisha kuzamisha. Kwa mfano, mwanafunzi Filipo alipombatiza mwanamume Mwethiopia, ‘walishuka na kuingia ndani ya maji’ kwa ajili ya ubatizo huo. Baadaye, ‘walipanda kutoka ndani ya maji.’(Matendo 8:36-39.)
Uwongo: Biblia inaposema kwamba nyumba nzima ilibatizwa, inamaanisha watoto pia walibatizwa,hapana. Kwa mfano, inasema hivi kuhusu mlinzi wa jela huko Filipi: “Wote, yeye na walio wake wakabatizwa.”(Matendo 16:31-34.)
Ukweli: Simulizi kuhusu kugeuzwa imani kwa mlinzi huyo wa jela linaonyesha kwamba wale waliobatizwa walielewa “neno la Yehova” na kwamba ‘wakashangilia sana.’ (Matendo 16:32, 34). Mambo hayo yanatusaidia kuamini kwamba watoto wowote waliokuwepo katika nyumba ya mlinzi huyo wa jela wasingeweza kubatizwa, kwa sababu hawangeweza kuelewa neno la Yehova.
Uwongo: Yesu alifundisha kwamba watoto wadogo wanabatizwa kwa kusema kwamba Ufalme ni wa watoto wachanga.(Mathayo 19:13-15; Marko 10:13-16).
Ukweli: Yesu hakuwa akizungumzia ubatizo aliposema maneno hayo. Badala yake, alikuwa akionyesha kwamba wale wanaostahili kuingia katika Ufalme wa Mungu wanapaswa kuwa kama watoto,wapole na wenye kufundishika.(Mathayo 18:4; Luka 18:16, 17.)
Shina la neno la Kigiriki linalotafsiriwa “ubatizo” linamaanisha “kuzamisha.” Ona kitabu Theological Dictionary of the New Testament, Buku la Kwanza, ukurasa wa 529.
Kulingana na kitabu The International Standard Bible Encyclopedia, “hakuna sehemu katika Agano Jipya inayounga mkono ubatizo wa watoto.” Pia inataja kwamba zoezi hilo lilitokana na “mawazo yenye makosa na yaliyotiwa chumvi kuhusu thamani ya ubatizo,” yaani, kwamba ubatizo unasafisha dhambi kabisa.Buku la 1, ukurasa wa 416-417.
Kitabu cha New Catholic Encyclopedia kinasema hivi chini ya kichwa “Ubatizo katika Biblia”: “Ni wazi kwamba ubatizo uliofanywa katika Kanisa la mapema ulikuwa wa kuzamisha watu katika maji.”Buku la 2, ukurasa wa 59.

Kwa mitazamo ya aina hii ni ngumu mno. Yohana alikuwa anabatizia Watu Mto Yordan maji yanayo tembea. Ni Andiko gani lilitutoa hapo Jordan? Sasa kwa nini wewe uzungumzie bricks 3mx3mx3m. Na kama umetoka mto Yordan mpaka hako kabwawa kasaizi hiyo unashindwa nini kutoka kwenye kabwawa ukafika maji ya saizi ya kiganja cha mkono. Hamna tofauti na hawa watu Matendo ya Mitume 15:1
 
Thankyou,this further proves that Catholicism is a demonic entity,as proved by it's symbology.The brave can see,but the stupid cannot,very sad.
Hayo umesema wewe ila kwangu mimi katoliki siyo demonic entity.

Dini ni falsafa, na kila falsafa ina kanuni zake. Dini ikishageuka na kuwa dhehebu, dhehebu nje na mafundisho ya Biblia ni lazima liwe na utaratibu, sheria na kanuni za kuongoza wafuasi wake.


Dini lazima iambatane na utamaduni, hivyo kila dhehebu linafuata utamaduni wake kutokana na chimbuko lake, Katoliki chimbuko lake ni Yesu Kristu.

Reformation ni kitu muhimu sana kwa sasa katika suala la zima la kuendesha na kusimamia misingi ya maadili ya kanisa husika. Katoliki likiwa ndilo dhehebu kubwa duniani ni lazima liende na mabadiliko ya wakati husika ili kukabaliana na changamoto mpya.

Wakatoliki wamepewa uhuru wa kuabudu, kukosoa na hata kushauri mambo mbali mbali yanoyohusu dhehebu lao. Leo hii mkatoliki anaweza kusali KKKT, angalicana, TAG, Sabath, orthodox n.k ila imani yake isiteteleke wala kuyumba. Hili limefanya kanisa katoliki liendelee kustahimili ukosoaji wote. Na hili linafanyika kwa sababu imani yao ni kwa Yesu Kristo tu bila kujalisha mafundisho ya madhehebu mengine.

Kanisa katoliki kwa kutambua kwamba tatizo la Unyanyasaji wa kingono limeendelea kuliandama, lipo njiani kubadili sheria na kufanya mageuzi mapya hili kuwadhibiti priests wote watakaojihusisha na vitendo hivyo.

Kwa nini kanisa lishilikiane na jamii za siri, vyombo vya ujasusi n.k ?

Sababu mojawapo ni kwamba kanisa katoliki lina mamlaka duniani, na mamlaka hiyo inatambulika, hivyo kuimarisha ulinzi na usimamizi dhidi ya wafuasi wake na kanisa ni muhimu sana. Hii inafanyika kwa sababu dini ni utawala, kwahiyo kama ni utawala ni lazima ujiimarishe.


Lakini tukirudi katika theolojia, madhehebu ya dini zote yanafuata falsafa ya theolojia, kwa kuzitizama theories & principles of theology, utakuta dini zote na madhehebu yake unayaita ya shetani na siyo Mungu.

Kwahiyo huwezi kuendesha kanisa kwa kufuata mafundisho ya Biblia tu, ni lazima ziwepo kanuni, taratibu na hata sheria mbali mbali za kuweka mambo sawa pale yanapokwenda ndivyo sivyo na kusimamia misingi ya utamaduni wa kanisa husika.
 
Kwa mitazamo ya aina hii ni ngumu mno. Yohana alikuwa anabatizia Watu Mto Yordan maji yanayo tembea. Ni Andiko gani lilitutoa hapo Jordan? Sasa kwa nini wewe uzungumzie bricks 3mx3mx3m. Na kama umetoka mto Yordan mpaka hako kabwawa kasaizi hiyo unashindwa nini kutoka kwenye kabwawa ukafika maji ya saizi ya kiganja cha mkono. Hamna tofauti na hawa watu Matendo ya Mitume 15:1
Ugumu hapo siuoni,Dini ndiyo iliyokuaminisha kwamba ni ngumu,it is simple,na nimeshakuonyesha how simple it is.Concept kwamba huwezi kupata maji mengi everywhere is rubbish,kwani ya kunywa unapata wapi? Na nisisitize,unahitaji maji yanayotosha kuzamishwa mtu,si lazima yawe yanayotiririka.Ukipata yanayotiririka na yanayotosha kuzamishwa sawa.

Andiko la toashi hili hapa.👇

Matendo ya Mitume 8:36-39
36 Wakawa wakiendelea njiani, wakafika mahali penye maji; yule towashi akasema, Tazama, maji haya; ni nini kinachonizuia nisibatizwe?
37 Filipo akasema, Ukiamini kwa moyo wako wote, inawezekana. Akajibu, akanena, Naamini ya kwamba Yesu Kristo ndiye Mwana wa Mungu.]
38 Akaamuru lile gari lisimame; wakatelemka wote wawili majini, Filipo na yule towashi; naye akambatiza.

39 Kisha, walipopanda kutoka majini, Roho wa Bwana akamnyakua Filipo, yule towashi asimwone tena; basi alikwenda zake akifurahi.

Kufuatana na mtiririko wa mazungumzo haya,na mtiririko mzima wa swala la ubatizo kwenye Biblia,ni wazi kwamba haya maji yalikuwa mengi na toashi alizamishwa kama Bwana Yesu,unless mtu una nia ovu ya kupotosha maandiko!Kama hapakuwa na haja ya kuzamishwa toashi asingeshuka kwenye gari,wangechota maji kidogo tu halafu toashi akanyunyiziwa kichwani!

But finally naonya, unaposoma Biblia ni lazima u-flush out mapokeo ya Dini yote kichwani,mapokeo ni kongwa au sumu mbaya sana kwenye kuielewa Biblia.
 
Ugumu hapo siuoni,Dini ndiyo iliyokuaminisha kwamba ni ngumu,it is simple,na nimeshakuonyesha how simple it is.Concept kwamba huwezi kupata maji mengi everywhere is rubbish,kwani ya kunywa unapata wapi? Na nisisitize,unahitaji maji yanayotosha kuzamishwa mtu,si lazima yawe yanayotiririka.Ukipata yanayotiririka na yanayotosha kuzamishwa sawa.

Andiko la toashi hili hapa.👇

Matendo ya Mitume 8:36-39
36 Wakawa wakiendelea njiani, wakafika mahali penye maji; yule towashi akasema, Tazama, maji haya; ni nini kinachonizuia nisibatizwe?
37 Filipo akasema, Ukiamini kwa moyo wako wote, inawezekana. Akajibu, akanena, Naamini ya kwamba Yesu Kristo ndiye Mwana wa Mungu.]
38 Akaamuru lile gari lisimame; wakatelemka wote wawili majini, Filipo na yule towashi; naye akambatiza.

39 Kisha, walipopanda kutoka majini, Roho wa Bwana akamnyakua Filipo, yule towashi asimwone tena; basi alikwenda zake akifurahi.

Chanzo ni Ubatizo wa Yohana Mbatizaji ambao aliufanyia Yordan kwenye maji yanayo tembea. Hii ya kuzamisha kwenye maji mengi tofauti na Yordan imepatikana vipi?

Bwana Yesu alichukua mikate mitano na samaki wawili Akavibariki akalisha maelfu. So kwa Imani na kwa Nguvu ya jina la Yesu maji ya kwenye kiganja cha mkono yaliyo barikiwa kwa Neno na Jina la Yesu ya kimwagiwa kichwani yana uwezo sawa na yale ya kuzamisha mwili mzima ya Mto Yordan.
 
Hayo umesema wewe ila kwangu mimi katoliki siyo demonic entity.

Dini ni falsafa, na kila falsafa ina kanuni zake. Dini ikishageuka na kuwa dhehebu, dhehebu nje na mafundisho ya Biblia ni lazima liwe na utaratibu, sheria na kanuni za kuongoza wafuasi wake.


Dini lazima iambatane na utamaduni, hivyo kila dhehebu linafuata utamaduni wake kutokana na chimbuko lake, Katoliki chimbuko lake ni Yesu Kristu.

Reformation ni kitu muhimu sana kwa sasa katika suala la zima la kuendesha na kusimamia misingi ya maadili ya kanisa husika. Katoliki likiwa ndilo dhehebu kubwa duniani ni lazima liende na mabadiliko ya wakati husika ili kukabaliana na changamoto mpya.

Wakatoliki wamepewa uhuru wa kuabudu, kukosoa na hata kushauri mambo mbali mbali yanoyohusu dhehebu lao. Leo hii mkatoliki anaweza kusali KKKT, angalicana, TAG, Sabath, orthodox n.k ila imani yake isiteteleke wala kuyumba. Hili limefanya kanisa katoliki liendelee kustahimili ukosoaji wote. Na hili linafanyika kwa sababu imani yao ni kwa Yesu Kristo tu bila kujalisha mafundisho ya madhehebu mengine.

Kanisa katoliki kwa kutambua kwamba tatizo la Unyanyasaji wa kingono limeendelea kuliandama, lipo njiani kubadili sheria na kufanya mageuzi mapya hili kuwadhibiti priests wote watakaojihusisha na vitendo hivyo.

Kwa nini kanisa lishilikiane na jamii za siri, vyombo vya ujasusi n.k ?

Sababu mojawapo ni kwamba kanisa katoliki lina mamlaka duniani, na mamlaka hiyo inatambulika kama nchi, hivyo kuimarisha ulinzi na usimamizi dhidi ya wafuasi wake na kanisa ni muhimu sana. Hii inafanyika kwa sababu dini ni utawala, kwahiyo kama ni utawala ni lazima ujiimarishe.


Lakini tukirudi katika theolojia, madhehebu ya dini zote yanafuata falsafa ya theolojia, kwa kuzitizama theories & principles of theology, utakuta dini zote na madhehebu yake unayaita ya shetani na siyo Mungu.

Kwahiyo huwezi kuendesha kanisa kwa kufuata mafundisho ya Biblia tu, ni lazima ziwepo kanuni, taratibu na hata sheria mbali mbali za kuweka mambo sawa pale yanapokwenda ndivyo sivyo na kusimamia misingi ya utamaduni wa kanisa husika.
Mm,sawa mkuu ila to me what you have put forward only proves further how Catholicism is penetrated by Satan.It's unfortunate that you do not see this truth and instead you are defending evil stances.
 
Chanzo ni Ubatizo wa Yohana Mbatizaji ambao aliufanyia Yordan kwenye maji yanayo tembea. Hii ya kuzamisha kwenye maji mengi tofauti na Yordan imepatikana vipi?

Bwana Yesu alichukua mikate mitano na samaki wawili Akavibariki akalisha maelfu. So kwa Imani na kwa Nguvu ya jina la Yesu maji ya kwenye kiganja cha mkono yaliyo barikiwa kwa Neno na Jina la Yesu ya kimwagiwa kichwani yana uwezo sawa na yale ya kuzamisha mwili mzima ya Mto Yordan.
Nimesasema kuzamishwa na kuibuliwa majini kuna-signify kuzikwa na kufuka kwa Bwana Yesu,sasa kunyunyiziwa maji kichwani kuna-signify tendo gani?Jamani mbona this is straight forward and easy to understand.Nadhani tuachane siwezi kukusaidia.Umepotoshwa sana.
 
Sasa kama maji
Nimesasema kuzamishwa na kuibuliwa majini kuna-signify kuzikwa na kufuka kwa Bwana Yesu,sasa kunyunyiziwa maji kichwani kuna-signify tendo gani?Jamani mbona this is straight forward and easy to understand.Nadhani tuachane siwezi kukusaidia.Umepotoshwa sana.

Maji yaliyopewa Nguvu na Uweza kwa Jina la Bwana Yesu Kristo na Neno lake kwa IMANI yana uwezo huo huo wakusignify hicho hicho 'Kuzikwa na kufufuka kwa Bwana Yesu.'

Kama vile ambavyo Mkate waweza kugeuzwa kuwa Mwili wa Kristo na Divai kuwa Damu ya Bwana Yesu iliyo mwagika pale Msalabani kwa ajili ya ondoleo la dhambi.
 
Nimesasema kuzamishwa na kuibuliwa majini kuna-signify kuzikwa na kufuka kwa Bwana Yesu,sasa kunyunyiziwa maji kichwani kuna-signify tendo gani?Jamani mbona this is straight forward and easy to understand.Nadhani tuachane siwezi kukusaidia.Umepotoshwa sana.
Unajua vipo vitu ukivijua vitakutoa kwenye giza.

5 Yesu akajibu, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa kwa maji na kwa Roho, hawezi kuuingia ufalme wa Mungu.
Yohana 3:5

Wapi aliposema isipokuwa watoto? Mnatumia andiko lipi kutenga watoto? Mtoto ni mtoto kimwili ila ni roho kamili! Ndio maana anarithi dhambi ya asili inayoondoka kwa ubatizo tu!

Yesu aliposema waacheni watoto waje kwangu msiwazuie unaelewa maana yake? Maana mnaweka wakfu watoto badala ya kuwabatiza mkisingizia Yesu aliwabariki tu hakuwabatiza! Kwani Yesu amewahi kubatiza akiwa duniani? Unaweza kwenda kwa Yesu bila kubatizwa?

Ndugu Catholic Church linasimamia maandiko na mapokeo kama tulivyoachiwa kuanzia mitume hadi leo. Tumerithishana imani miaka 2000 sasa! Hakuna nyakati kanisa ndio lilianzisha tu kubatiza watoto ni practise toka awali hata kimapokeo!

Kafatilie historia ujue ubishi wa kutobatiza watoto umeanza lini! Purely heretics! Ukitaka kutafuta kweli nenda kwenye sites rasmi za Kanisa ujifunze lakini ukiamua kungangana na hilo endelea nalo.
 
Mm,sawa mkuu ila to me what you have put forward only proves further how Catholicism is penetrated by Satan.It's unfortunate that you do not see this truth and instead you are defending evil stances.
Kwani Yesu si alimshinda shetani pale msalabani? Au mission ilifeli?
 
Mmh mbona mambo magumu hayo, ilithibitiswaje kwamba papa Francis n Moja wapo ya jesuit?
Pope Francis kuwa mjesuit siyo taatifa za kiintelejensia, inajulikana kama inavyojulikana askofu wa Jimbo la dar es salaam (Ruwaichi) ni wa shirika la wafransisko wa capuchin, shirika la Jesuit limewahi kutoa maaskofu ila halijawahi kutoa papa, Pope Francis ndiyo wa kwanza katika shirika lao (Jesuit) kuwa papa. Hadi tarehe aliyoingia noviciate katika malezi ya utawa inajulikana
 
Pope Francis kuwa mjesuit siyo taatifa za kiintelejensia, inajulikana kama inavyojulikana askofu wa Jimbo la dar es salaam (Ruwaichi) ni wa shirika la wafransisko wa capuchin, shirika la Jesuit limewahi kutoa maaskofu ila halijawahi kutoa papa, Pope Francis ndiyo wa kwanza katika shirika lao (Jesuit) kuwa papa. Hadi tarehe aliyoingia noviciate katika malezi ya utawa inajulikana
Huwezi kuwa Jesuit ukawa kiongozi wa Kanisa la kiroho,no way,unaweza tu kuwa Kanisa la Shetani!No wonder Pope Francis kasema kaifuta Biblia.By the way mbona sijapata comments about this na issue ya kuua watoto na kubaka.Na comment ya Francis kwamba Kanisa la Roma ndilo lililobadilisha siku ya ibada to Sunday umeisikia?Amesema siku halali ya ibada ni Jumamosi?What is your take on this .
 
Sasa kama maji

Maji yaliyopewa Nguvu na Uweza kwa Jina la Bwana Yesu Kristo na Neno lake yana uwezo huo huo wakusignify hicho hicho 'Kuzikwa na kufufuka kwa Bwana Yesu.'

Kama vile ambavyo Mkate waweza kugeuzwa kuwa Mwili wa Kristo na Divai kuwa Damu ya Bwana Yesu iliyo mwagika pale Msalabani kwa ajili ya ondoleo la dhambi.
Aisee,upotoshwaji mbaya kabisa huu.Amini matakataka mkuu,uko huru.
 
Huwezi kuwa Jesuit ukawa kiongozi wa Kanisa la kiroho,no way,unaweza tu kuwa Kanisa la Shetani!No wonder Pope Francis kasema kaifuta Biblia.By the way mbona sijapata comments about this na issue ya kuua watoto na kubaka.Na comment ya Francis kwamba Kanisa la Roma ndilo lililobadilisha siku ya ibada to Sunday umeisikia?Amesema siku halali ya ibada ni Jumamosi?What is your take on this .
Haya yote wametuletea wazungu, Kuna kitu naona hakipo sawa kwenye hizi dini, kama wakituletea biblia mpya ntapata shauku ya kujua kama contradictions zitendelea au codes tusizozielewa zitafunguliwa, maana nasikia biblia yenyewe Ile kabla haijapunguzwa, ilikuwa inawafanya wasomaji wake kuwa "mageneous"
 
Back
Top Bottom