Jamaa kapaniki sana hasira eti hao hata hawajui pesa ziko wapi!? Wala sikukopa nimeyakamua mafisadi (Watanzania!?) Hizi zarau na ubaguzi kwa kuwagawa Watanzania.
 
Hahaha Magufuli kafanya kampeni tangu 2015 peke yake na akina Pole pole na Bashiru.

Waligawa pesa barabarani, leo hawajui hata waanzie wapi?!

Tume ingeweka orodha ya matusi tujifunze, badala yake wanatishia kuengua wagombea.
Hili bila shaka watajibiwa vyema na Lissu leo.
 
Katika Kampeni za Uchaguzi Mkuu-2020 zinazoendelea njini ni Wagombea 2 wanaochuana vikali ulingoni kwa Tanzania Bara nao ni Rais Magufuli na Tundu Lissu.

Kama kuna mgombea wa Urais anayempa Taabu Sana Rais Magufuli basi ni Tundu Antipas LISSU wa CHADEMA.
Unaposikiliza hoja za Tundu Lissu na ukasiliza hoja za Magufuli, basi Toto Tundu anaonekana yuko Smart zaidi kuliko Magufuli.



Hebu sikiliza hoja hizi za Tundu Lissu kuhusu Uwanja wa ndege wa Chattle na sera za CHADEMA za Uhuru, Haki na Maendeleo.
 
Leo JPM atakuwa biharamulo alipo anzia siasa atapiga kura za haja acha Tundu ashike tu huko kubaya.
 
Wasalaam, natumai kila mtu anayeingia mtandaoni anajionea mada Kali zinazomzungumzia zaidi T. Lisu. Kusema ukweli Lisu ameshangaza watu wengi kwa ujasili alio nao wa kumsema waziwazi Magufuri. Kutokana na Lisu kulitumia vyema jukwaa la siasa, ccm wamejikuta wakichanganyikiwa, Magufuri bado anaamini Mpaka Sasa yeye Ni Raisi kwa kutumia kivuli Cha Katiba mbovu tuliyonayo, ndiyo maana hataki kuvunja baraza la mawaziri Kama alivyofanya do Shein. Ni kweli katiba inampa kivuli hicho lakini haiondoi matumizi ya BUSARA kwa kiongozi mwanasaisa, Magufuri alipaswa kutumia busara na KUINGIA kwenye kampeni zaidi Kama watangulizi wake walivyofanya, ndiyo maana inawapa wakati mgumu watetezi wake kumtetea maana hawawezi Tena kujibu hoja za wapinzani. Bado Magufuri anapewa coverage kubwa na media lakini unashaangaa Tume inasema kuna mtu anachochea vulugu, KWANI ANAHAMASISHA KUPITIA VYOMBO VIPI VYA HABARI? yaan Mpaka watu watumie bando kumuona Lisu ufananishe na Magufuri tunayemuona kuanzia anatoka nyumbani asubuhi Mpaka anaenda kula.? Ccm ielewe, Lisu anatumia vyema jukwaa la kampeni ndo maana halisi ya siasa. CCM wajikumbushe kampeni za awamu zilizopatikana, Viongozi wa CCM walijipanga kwa kila sector, mipasho kejeli no ili kujihakikishia mgombea wao anatamba jukwaani. Lakini saivi hawana msemaji mwenye mvuto wa kulichangamsha jukwaa, CHADEMA wamejipanga kweli kweli, jukwaa lao linavutia kwa kila mtu, ukisogea kwenye jukwaa la CHADEMA, hata Kama hukuwa na mpango wa kuokoka, unajikuta umeokoka na kukabiliana na Sera za CHADEMA. CCM isitumie jukwaa la kampeni kumtisha Lisu, zaidi ianze upya kujinadi, Tundu Lisu amekuwa mjadala mkubwa vijiweni na maeneo ya kazi. Anawapa nguvu na hoja kwa watetezi wake nakuwafanya watetezi wa Magufuri kujikuta wanasema, Lisu HAWEZI KUPEWA NCHI, HAPO NDO SIELEWI, KUMBE NCHI INAPEWA KWA MAAMZI YA WATU WACHACHE? safari hii watamtangaza Lisu. Kampeni ndo baado zinaanza.
Good morning
Ni kweli katiba inampa kivuli hicho lakini haiondoi matumizi ya BUSARA kwa kiongozi mwanasaisa.

**************
Wewe ni Ile sehemu ya kukalia kabisa aisee
 
Ni jambo lililo wazi na lisilopingika kwamba Lissu unahitaji kwenda vijijini kutafuta kura huko. Huko vijijini watu wamepigika kweli kimaisha. Kama ni umasikini wa kipato huko umetamalaki sana. Ukijua kucheza karata yako vizuri naamini utapindua meza asubuhi na mapema. Nenda Lissu! Nendaaa! Nendaaaa! Neeeendaaaaaa!
 
Tundu Lissu ana upendo wa kweli kwa Watanzania

Angalia upendo anaouonyesha kwa watu duh.

Sio yule anayewatukana watu kila siku
IMG_20200916_141851.jpg
 
Watu wa DAR ES SALAAM huwa hawajifichi wakiamua kukudharau wala hawakufichi ona huu msafara wa Lissu siku unaenda kwenye uzinduzi wa kampeni MBAGALA ulivyodharaulika na watu wa Dar es salaa hadi unaingia uwanjani njia nzima watu walionyesha kutokujali wala kuwa na habari naye ndio maana akakimbia mji kukimbilia mikoani kwa aibu



LAKINI ona mahudhurio ya uzinduzi hapa chini wa siku ya kwanza ya LOWASSA Dar es salaam 2015 LINGANISHA na hayo ya LISSU hapo juu
Lissu watu wa DAR hawamtaki

 
68 Reactions
Reply
Back
Top Bottom