Uchaguzi 2020 Special Thread: Taarifa za Kampeni za Wagombea Urais kupitia CCM, Dkt. John Pombe Magufuli na Samia Suluhu

Mh sana Rais na Mgombea Urais wa CCM ndugu John Magufuli pokea ushauri wangu huu wa bure kabisa.

Mosi, nakushauri sana tena sana. Usimjibu Tundu Lissu maana kwa kufanya hivyo utaendelea kutapata aibu kubwa.

Level za Lissu ni za juu sana sioni mwanaccm wa sasa wa kuweza kushindana nae kwa hoja kwahiyo kwa heshima yako na ya chama chako jikite tu kwenye sera zenu. Hilo la kwanza.

La pili nakushauri usipende kuiga na kutaka kutembelea nyota ya Lissu. Usidandie treni kwa mbele hasa ahadi ambazo chama chako haijazifanyia utafiti hivyo kutoka na uwezo wa kuzitekeleza km mlivocopy sera ya Chadema ya elimu bora na bure. Hili pia litakufedhehesha ww binafsi na chama chako iwapo utaendelea.

Ni hayo tu kutoka kwangu, kukubali au kukataa ni uamuzi wako. Ushauri kama huu huwezi kupewa na mwanaccm wao kazi yao kubwa ni kujipendekeza ili wapate vyeo kwa kukudanganga kua unakubalika unapendwa wkt hali halisi mtaani wewe mwenyewe umeshaiona.

Nukuu ya kwenye katiba: "Rais hatawajibika kufuata ushauri wa mtu yeyote"
Yuko vizuri, Sera zake zinaeleweka kamanda, sio lazima kila mgombea aongee kama Lissu. CCM mbele kwa mbele, CCM tano tena.
 
Eh!Eh!Eh!Eh! Yule Mzilankende anaenda tena huko? Na sasa mmeongeza maafa ya moto! Sijui wasanii wataendelea na burudani zao wakati kuna msiba? Je bila wasanii wananshomile watakuja kusikiliza vidonge vyao? Nadhani habari ya MV Victoria Hapa Kazi Tu itakuwa imewafuta machozi ya tetemeko, ukimwi, Katerero, mto ngono, vita ya kamera na huo moto wa shule ya Byamungu Islamic?!!?!? Poleni wana Kagera kuweni na moyo wa upendo na subira!
 
Kwanini mtu azidi kung'ang'ania mateso? Kama kazi yenyewe ni mateso, kwani ni lazima ugombee tena? Jitoe kiroho safi

Screenshot_20200915-181440.png
 
Hapo ndipo huwa ananiacha hoi. Inakuwaje mtu unatumia muda na nguvu nyingi kupigania kitu cha kukitesa wakati kwako una miradi na mazingira ya kukuwezesha kujipumzisha tu! Yaani unaishi bila shaka lolote?!
 
Kwakweli CCM imejiimalisha sana. Kuna watu wanaponda mfumo wa kampeni za kuambatana na wasanii lakini ukweli ni kwamba wanaumia kimoyomoyo.

Kampeni za CCM ni raha, burudani mda mwingi, mtu unasikiliza sera huku ukiburudika.
Kuna watu wanasema kazi na bata, hii ya ccm ni kampeni na bata wakubwa wakubwa.

Hongereni sana wasanii na ccm kwa ujumla. Tuko nanyi kila sehemu.
 
.. Salaaam

Kumekuwa na Sintofahamu juu ya chama cha CCM na mgombea wake Dr John Pombe Magufuli juu Upatikanaji wa Tume Huru na Katiba Mpya.

Tofauti na vyama vingine Kama CHADEMA, ACT WAZALENDO N.K Ambao wao katika Ilani na Sera zao wameipa Kipaumbele KATIBA MPYA NA TUME HURU YA UCHAGUZI, Tena wameenda mbali na kusisitiza kuwa Litakuwa jambo la kwanza kulifanya Tena kwa Haraka kupitia Rasimu ile ya JAJI WARIOBA.

Chama cha CCM wao hawana muda Kabisa na Katiba Mpya na Tume Huru Tena katika Miaka mitano (5) ya Magufuli aliipinga vikali wakati ni hitaji la Watanzania.

Sasa kwa kuwa Hawa ccm wanajifanya kuikwepa Katiba na Tume Huru hatuna haja ya kuchagua watu wanaopenda Katiba ya KUTUTAWALA badala ya KUTUONGOZA.


Tundu Lissu Anatosha ndugu zangu.
 
Necccm ndo inayowabakiza madarakani ccm na katiba iliyopo ndo inayowaweka watoto wa dada kwenye vitengo nyeti...
 
.. Salaaam

Kumekuwa na Sintofahamu juu ya chama cha CCM na mgombea wake Dr John Pombe Magufuli juu Upatikanaji wa Tume Huru na Katiba Mpya.

Tofauti na vyama vingine Kama CHADEMA, ACT WAZALENDO N.K Ambao wao katika Ilani na Sera zao wameipa Kipaumbele KATIBA MPYA NA TUME HURU YA UCHAGUZI, Tena wameenda mbali na kusisitiza kuwa Litakuwa jambo la kwanza kulifanya Tena kwa Haraka kupitia Rasimu ile ya JAJI WARIOBA.

Chama cha CCM wao hawana muda Kabisa na Katiba Mpya na Tume Huru Tena katika Miaka mitano (5) ya Magufuli aliipinga vikali wakati ni hitaji la Watanzania.

Sasa kwa kuwa Hawa ccm wanajifanya kuikwepa Katiba na Tume Huru hatuna haja ya kuchagua watu wanaopenda Katiba ya KUTUTAWALA badala ya KUTUONGOZA.


Tundu Lissu Anatosha ndugu zangu.
Ulipozungumzia ilani umenikosha sana maana tokea kampeni zimeanza nimekua naitafuta ilani ya uchaguzi ya chadema bila mafanikio. Naomba unisaidie kuiweka hapa comrade nipate kuisoma.
 
Ndugu mimi kama kawaida natumia platform kama hii nikiamini kipenzi changu mh ataona

Mh nilikuwepo leo pale Gymkana mjini Bukoba na nilishangaa kuona maaskari wakiwakamata sijui waliozomea kuwa hawakutaki baada ya ww kuwauliza kama wanakutaka. Sasa mh hili jambo la hasira ulipunguze tubaki kunadi sera zetu maana hata Yesu kunawaliompinga na pia hili jambo limeleta hasira kwa baadhi ya wana Bukoba mpaka kwa baadhi ya wana CCM wenzetu huku tukizokewa baada ya ww kuondoka hapa.

Sasa sisi watafuta kura tutapata wakati mgumu kuwafikia hawa wapga kura maana walishaanza kutengeneza na kuamini maneno atupashayo huyu kilema wa mguu Lissu. Rekebisha sana hasira mh
 
11 Reactions
Reply
Back
Top Bottom