South Africa msije Sio kuzuri

Lusungo Simu,Radio,TV,Gari ni vitu vya kawaida tuu na bei zipo chini sana....Nikikueleza bei za magari tunavyonunua mnadani huko na aina ya gari lenyewe huwezi amini nimeshangaa unashangaa Simu ya Touch
Sawa mkuu isanga
 
Vumilia kaka, ila usijiunge na magenge ya uhalifu maana ukikamatwa utahukumiwa kwa sheria za huko kwa maagizo ya Mjomba Magu.
 
Ni Siku nyingi Sana sijakuja hapa kuleta mrejesho,
Ndugu zangu South Africa, Sio kabisa msoto ni mkuu,
Sina muda wa kusema Mengi Ila point yangu kuu km huna mtu Huku, km huna mtaji Pls watanzania wenzangu msije

Nimemaliza sim hii nimeazima japo tu niwasalim na kuwapa tahadhari,
Vijana wengi hasa wa Tanzania wanateseka Jamani
Sijui nisemeje, asie Sikia la mkuu basi azamie tu. View attachment 569601View attachment 569602
Wapo walio sema nimekufa Ila Mimi najichanga nirudi.

Sent using Jamii Forums mobile app
wewe ilikuaje ukaenda huko, nini ilikua target yako kwanza .....pengine hukujipanga wala hukuwa na plan yoyote au ishu yoyote ya kueleweka,

maana kuna wengine wanampango wa kuja kusoma, kazi labda na vitu kama ivo, pengine ueleweshe vizuri ilikuaje kwako
 
Usikate tamaa kijana,jaribu nchi jirani na hapo kama Namibia au Botswana
 
Ebwana hivi ukipata fursa ya kupata uraia huko kwa ndoa, unamshauri mtu aichukue? Na process yake inachukua muda gani?

Ukiwa raia, ni maeneo gani unaona yana fursa (ambayo umeshuhudia wahamiaji wenye legal status wanafanya na kufanikiwa)?
 
Ila pamoja na yote, SA ni bonge moja is nchi! Hiyo Joburg ni next level. Kuanzia barabara, majengo, aina ya magari barabarani ni hatari tupu. Sandton City siyo ya Africa hii! Gautrain, aisee! Noma sana
 
Habari zenu Ba ndugu,
Kwa takribani miaka michache iliyopita Hapa Jf nyuzi za watu kwenda South Africa kila wiki zilikuwa zina postiwa,
Ila kwasasa tunamshukuru Mungu hizo Thierd siku hizi zimekwisha,

Inaonekana walio taka kwenda wamesha fika kwa madiba.

Sijui kwanin watu wengi waliipenda SA kuliko nchi nyingine .
Mwenye jibu anipe.
 
Kwenu pamekushinda Tanzania huwezi kwenda kule ukaweza.umetoka mkoa uko mjini uko resi je ukienda south?pamechafukwa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom