South Africa declared 5 days of mourning for Nyerere!

K.Msese

JF-Expert Member
Apr 1, 2012
2,384
3,007
Africa ya Kusini ilitangaza siku (5) tano za maombelezo ambapo bendera zilipepea nusu mlingoti! Tumuunge mkono Jk kwa maombelezo ya siku tatu ya nchi yetu juu ya kifo cha Madiba!

....If Mwalimu Julius Nyerere had been the founding father of South Africa and not Tanzania, he would hardly have received a more dignified farewell here than he has done.
South Africans from across the political spectrum, including many who once denounced him as puppet of the evil communist masterminds in Beijing and Moscow, if not as a demon himself, praised the former Tanzania head of state as a great African and a fine human being.

South African President Thabo Mbeki ordered that the country's flags be flown at half-mast for five days of mourning in recognition of Nyerere's role in South Africa's move from apartheid and the achievement of a multi-party democracy.

Mr. Mbeki, who was one of several heads of state to attend Mwalimu Nyerere's funeral, shared the sentiments of the many posters bearing the wording: Farewell Father of the Nation.

Mr. Mbeki was heading a high-powered South African delegation that included Inkatha Freedom Party President and Home Affairs Minister Mongosuthu Buthelizi, Foreign Affairs Minister Nkosazana Zuma, and Speaker in Parliament Frene Ginwala.

Although Mwalimu Nyerere's passing, aged 77, from leukaemia in a London hospital came as no great surprise, his death has hit hard many South Africans, especially those who were involved in the liberation struggle against apartheid and racism in this country and region.

Like so many African leaders who praised Mwalimu Nyerere, most South Africans feel they have lost a beloved godfather to their young nation.

In the media and on the streets, Mwalimu has been praised for his selfless contributions to the cause of African liberation.

He has been described as a tireless defender of just causes and a worthy architect of the African people's victory in gaining their rightful place among the nations of the world.

Just as Nelson Mandela is widely known by his nickname of Madiba, many South Africans fondly refer to Nyerere as Mwalimu.

From streetsweepers to parliamentarians, there was a general sense that Africa had lost a great man and that South Africans of all races and creeds owed him a huge debt.

Such is the feeling towards Mwalimu that not one but two formal memorial services were held for him.

Deputy President Jacob Zuma and representatives of all parties in the National Assembly also paid tribute to Mwalimu. They unanimously adopted a motion expressing National Assembly's condolences and support to his family and the people of Tanzania.

Mr. Zuma said Mwalimu had been "one of the giants" of the African continent.
His name permeated all the significant moments of the continent's development from its colonial past, and he had played a key supportive role in South Africa's path to freedom.

"The best way to remember Mwalimu is to continue the struggle to free all Africans from hunger and starvation; from homelessness; from diseases that are killing millions of our people; from joblessness; illiteracy, conflict and war; from tyranny and from oppression," Mr. Zuma said.

Dr Ginwala said prior to her departure for Mwalimu's funeral that under Dr Nyerere, she had hosted thousands of exiles from Southern Africa.

Africa would be the poorer from his death......."
 
Hao na walimwengu wengine ndiyo wanaomjua Mwalimu. Hapa mkianza kumjadili mnamtukana kana kwamba hakuna lolote wala chochote kwa ustawi wa ulimwengu huu. Mwalimu ni Mwalimu wa ukweli. Alipendwa na kuthaminiwa kutokana na maono yake ya kuwatetea wanyonge. Vijana wa Tanzania wamezama kwenye Bongo Movie na Bongo Fleva, hawajui watu muhimu kama hawa. Sana sana kwao John Cina ni wa maana na muhimu kwao kuliko wazee kama Mwalimu, Madiba, Samora, Kwame, Sankor, Kaunda na wengine wengi.
 
Hao na walimwengu wengine ndiyo wanaomjua Mwalimu. Hapa mkianza kumjadili mnamtukana kana kwamba hakuna lolote wala chochote kwa ustawi wa ulimwengu huu. Mwalimu ni Mwalimu wa ukweli. Alipendwa na kuthaminiwa kutokana na maono yake ya kuwatetea wanyonge..
Hizo ni rambirambi zao wakati amekufa, ulitegemea wakati wa maombolezo ya kifo chake wazungumzie nini zaidi ya maneno ya kuwafariji watu wake?

Yaliyozungumzwa wakati wa kifo chake yachukulie kuwa ni maneno ya kuwafariji watu wake katika kipindi kigumu cha msiba.
 
...kuna watu walibeza juu ya Tanzania kuomboleza kifo cha Mandela (RIP) kwa siku tatu...kana kwamba wao (RSA) hawakuomboleza wakati wa kifo cha Julius Nyerere!..kwamba ni kujipnd tu....kwa JK!
 
Kwenye maombolezo haya, hapa Tanzania, ofisi za serikali zitafunguliwa kama kawaida?
 
^^
Hawa walikuwa marafiki waliopatana! Hata kama hatuna ujasiri wa kuyafuata waliyoyaacha basi hata hilo la siku 3 lisitushinde
^^
 
Kwenye maombolezo haya, hapa Tanzania, ofisi za serikali zitafunguliwa kama kawaida?


Hivi mkuu ina maana hujui maombolezo ya kitaifa yanakuwagaje? In short ni kwamba bendera zinapepea nusu mlingoti, mzigo ni kama kawaida. Sharti lingine, masuala ya starehe yanatakiwa kudhibitiwa; kwa mfano kumbi za starehe marufuku kuendekeza starehe zilizopindukia, n.k. Lakini kazini ni kama kawaida kwani kufanya kazi nayo ni sehemu ya kumuenzi marehemu.
 
Hao na walimwengu wengine ndiyo wanaomjua Mwalimu. Hapa mkianza kumjadili mnamtukana kana kwamba hakuna lolote wala chochote kwa ustawi wa ulimwengu huu. Mwalimu ni Mwalimu wa ukweli. Alipendwa na kuthaminiwa kutokana na maono yake ya kuwatetea wanyonge. Vijana wa Tanzania wamezama kwenye Bongo Movie na Bongo Fleva, hawajui watu muhimu kama hawa. Sana sana kwao John Cina ni wa maana na muhimu kwao kuliko wazee kama Mwalimu, Madiba, Samora, Kwame, Sankor, Kaunda na wengine wengi.

Mwalimu anatukanwa katika Awamu hii ya nne, ushahidi upo wa wapi matusi yaha yanapoanzia japo ni kwa sababu za kishenzi.
 
Hao na walimwengu wengine ndiyo wanaomjua Mwalimu. Hapa mkianza kumjadili mnamtukana kana kwamba hakuna lolote wala chochote kwa ustawi wa ulimwengu huu. Mwalimu ni Mwalimu wa ukweli. Alipendwa na kuthaminiwa kutokana na maono yake ya kuwatetea wanyonge. Vijana wa Tanzania wamezama kwenye Bongo Movie na Bongo Fleva, hawajui watu muhimu kama hawa. Sana sana kwao John Cina ni wa maana na muhimu kwao kuliko wazee kama Mwalimu, Madiba, Samora, Kwame, Sankor, Kaunda na wengine wengi.

Lazima tukubali Mwalimu alikuwa na pande mbili kama wat wengine, so usishagae wtu wakikosa sana sana leo na kesho watu wakasifia sana sana.
 
Kati ya watu ambao hata kama kimwili hawapo pamoja na sisi lakini wanaendelea kuishi ni Mwalimu na Madiba. Wapo wengine pia lakini hawa ni mifano ya haraka sana!

Hawa waliamini kwenye falsafa ya "Living Today for Tomorrow"! Walipojifikiria wao walifikiria na ustawi wa binadamu wengine pia.

Nasikitika kuona kuwa watu wa kariba hili siku hizi hawapo popote na waliopo hawapewi fursa zozote zile!

Tumeendekeza umimi, ubaguzi, kujilimbikizia mali, utajiri wa haraka haraka kwa gharama/mbinu zozote na matendo mengine maovu huku tukiendelea kuzaliana! Laiti tungejua kuwa siku zetu za baadaye zitakuwa za kulia na kusaga meno kutokana na misingi ya kinyang'au tunayoijenga leo!

Mimi ni mwanafunzi wa maisha ya Nyerere na Madiba. Ninapotafakari maisha ya hawa ndugu zetu naona kwamba walikuwa binadamu zaidi ya watu wengi tulionao duniani.
Walikuwa na madhaifu yao lakini hayawezi kamwe kulinganishwa na mazuri waliyoifanyia dunia.

Ingependeza kama kila mtu akutane na moyo wake;kutoka humo aone ni jinsi gani anashiriki kuifanya dunia kuwa sehemu nzuri/salama ya kuishi leo na kesho! Living Today for Tomorrow!

Ee MUNGU naomba utuinulie akina Nyerere na Madiba wengine...!
 
Mwalimu anatukanwa katika Awamu hii ya nne, ushahidi upo wa wapi matusi yaha yanapoanzia japo ni kwa sababu za kishenzi.

Kweli mkuu,watu ambao sio waadilifu wanamwogopa Mwalimu,maadili ya uongozi yamedidimia kabisa awamu hii ya nne.
 
Thabo Mbeki ilikuwa si tu mchango wa Nyerere ktk ukombozi wa S.Afrika,bali mchango wa Nyerere kwa maisha binafsi ya Thabo Mbeki.
Mwaka 2007 nilihudhuria mdaharo wa Mbeki ktk ukumbi wa Nkurumah,siku ambayo Mbeki aliwashangaa Watanzania kwanini Tanzanite inazalishwa Tz lkn A.Kusini ktk soko la Dunia ndio wanaongoza kwa uuzaji,akashangaa kwanini wanampokea kwa mbwembwe wakati yeye hapa ni kama nyumbani.
Thabo akasimulia akasema,miaka ya sabini alikuwa anatoroka S.Afrika kupitia S.Rhodesia,bahati mbaya akakamatwa,na sbb pale alikuwepo Ian Smith swaiba wa makaburu, wakawa wanamrudisha S.Afrika.....Zuma Jacob akiwa Mozambique exile,Nyerere alimtumia ujumbe Smith akamwambia Mbeki aachiwe mana ni raia wake,kwa kutumia majasusi wake Mwalimu akampenyezea Mbeki passport ya ”uraia“ wa Tanzania,ijionyesha Mbeki kazaliwa Nachingwea,Mbeki akatoka kupitia Tanzania akaenda UK...na ktk safari zake mpaka miaka ya tisini alikuwa akitumia passport ya Tanzania,hali iliyomsaidia kuendesha harakati za kupinga ubaguzi kwa urahisi...na akasema ajabu ni kuwa jina la kwenye passport lilikuwa la ”kimakonde“...hata walipomkamata wakijua ni Mbeki,passport yake ilionyesha hina kinyume,na ikamtambulisha kama raia wa Tz.
Kwa mtindo huu,ilikuwa ni sahihi kwa Mbeki kutangaza siku tano,maana zaidi ya Nyerere kuwa Rais wa Tz,lkn kwa Mbeki alikuwa ni baba,mshauri na mentor wake....
 
Sijui tutafanya nii walau tuwe hata na theluthi tu ya moyo wa hawa waasisi. Kimeibuka kizazi cha watu wenye tamaa ya mali bila kutumia njia halali na kujaa ubinafsi na kiburi. Mungu atusaidie
 
Aise inapokuja mijadala inayomhusu mwalimu huwa naingia woga kupitia comments.....tangu nikutanage na post za wanaopenda kuponda tuuuu........na wapondaji hao ukisoma comments zao, wanaonekana kabisa wana ufahamu finyu wa historia......matokeo yake huishia kuporomosha matusi.

Mpaka kuna wakati huwa najiuliza....kama mtu anathubutu kumuita mwalimu mbaguzi......ni binadamu gani basi duniani atakuwa na sifa za kuonekana sio mbaguzi.

Aliimba Marijani Rajabu.........KILA MTENDA WEMA ATAKUMBUKWA KWA WEMA.

Kama kuna makosa ya kibinadamu.....yatakuwepo tu kwani sie ni hao binaadamu, sio MUNGU.

Walale pema peponi Mwalimu na mzee Madiba.
 
Mpaka kuna wakati huwa najiuliza....kama mtu anathubutu kumuita mwalimu mbaguzi......ni binadamu gani basi duniani atakuwa na sifa za kuonekana sio mbaguzi.
Tupatie tafsiri ya neno Ubaguzi halafu tuangalie kama wanaomuita nyerere ni mbaguzi wapo sahihi au la.
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom