Sophia simba hana hadhi ya kuwa waziri, JK kachemsha saaana!!! Nitachambua hili...

eliesikia

JF-Expert Member
Oct 29, 2010
787
755
WAZIRI wa zamani Nchi, Ofisi ya Rais (Utawala Bora), Sophia Mnyambi Simba, huko nyuma amewahi pia kutoa kauli zenye ukakasi akimshambulia mfanyabiashara (Mengi kuwa sio mwanaCCM )na mmoja wa wafadhili wa chama tawala kilichomweka waziri huyo madarakani.

Ni huyu huyu Sophia ambaye chama chake kimekanusha matamshi aliyotatoa mbele ya kadamnasi kuwashambulia wabunge wa kuchaguliwa walio mume na mke – John Malecela na Anne Kilango Malecela.

Ni huyu Sophia mwenye dhamana ndani ya wizara nyeti ya Utawala Bora, yenye wajibu wa kusimamia mienendo ya watumishi wa umma, iliyo chini ya Ofisi ya Rais.

Ni Sophia ndiye anayewajibika katika kusimamia na kutekeleza kiapo chake cha utii na kumshauri vema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, katika masuala mbalimbali yenye maslahi kwa taifa, bila migogoro yoyote.

Ni huyu Sophia, ambaye ndani ya chama chake, amekabidhiwa dhamana ya uenyekiti wa Jumuiya ya Wanawake (UWT) - wanaokiamini, kukipenda na kukitumikia chama tawala, yaani CCM.

Ni huyu Sophia aliyedaiwa kumwangushia kipigo, aliyekuwa mwenyekiti wa jumuiya hiyo, Janeth Kahama, wakati wa mchakato na kampeni za kumtafuta mwenyekiti wa wanawake hao kwa njia ya kura.

Ni Sophia huyu huyu, aliyewahi kukaririwa na vyombo vya habari akiwatetea wafanyabiashara wakubwa wanaotuhumiwa kwa ufisadi na kuzua gumzo na kuharibu upepo wa nchi wakati huo.

Sophia Simba, kwangu ni mwanamama anayekurupuka. Ni Waziri asiyejipa muda wa kutafakari na kueleza anachokifahamu. Wakati mwingine nahisi anatumika ama kwa nia ovu au kwa maslahi ya taifa ili kuharibu mwelekeo ama kuwasahaulisha walalahoi kero zinazowakabili.

Ni Sophia, aliyejaribu kucheza ngoma tofauti ya vita dhidi ya ufisadi iliyoanzishwa na viongozi wa vyama vya upinzani kabla ya kupokelewa kwa shangwe wa wakuu wa chama chake, akiwemo rais aliyemteua kushika nafasi ya uwaziri.

Ni Sophia aliyewashangaza wasomi na wasio wasomi, pale alipojiinua na kuishambulia familia ya wanasiasa, akiwemo mkongwe, Mzee Malecela.

Ni huyu Waziri Sophia aliyewaacha vinywa wazi wachambuzi, wajuzi na wananchi wa kawaida pale alipowashambulia kwa tuhuma mbalimbali wanasiasa wenzake.

Ni wapi alipokuwa Sophia kiasi cha kuzikalia tuhuma nzito za wanasiasa hao na kujinasibu kwamba ndani ya chama chao cha CCM hakuna msafi, wote ni mafisadi?

Ni imani yangu kwamba Sophia anahitaji kubanwa ili aanike tuhuma zote anazozifahamu, pengine atalisaidia taifa na kulirejesha kwenye mstari ili walalahoi waone raha na faida ya kuzaliwa juu ya ardhi ya Tanzania.

Pamoja na yote, nina ushauri kwa mkuu wake wa kazi. Kwanza amfukuze kwa sababu amejidhihirisha kwamba hafai kuwa kiongozi wa wanyonge kwa sababu ameshindwa kusimamia mienendo ya watumishi wa umma.

Sophia aanze kufuatiliwa, ahojiwe na Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (TAKUKURU), Polisi na Usalama wa Taifa.

Ni huyu sophia Simba aliyesema (akiwambia UWT members) kuwa kama Mumeo hapendi CCM basi usimpe unyumba.. Anaonyesha wazi kuwa Ngono kwake yeye ni jambo muhimu zaidi kuliko kuendelea na misimamo sawia ya kinchi na utaifa.:A S cry:

Ni Imani yangu kwamba kuondolewa kwa waziri huyu katika nafasi aliyonayo, kutabadili fikira zangu kwamba analipwa fadhila za mema machache aliyoyatenda wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu wa mwaka 2005(kumpitisha JK pale CCM).

nawasilisha
Source: freemedia:israel:
 
Nitashangaa sana sana jk akimrudisha huyu kilaza mwenzao uwaziri...nitashanga sanaa.....uwaziri sio size yake huyu labda secretary wa makamba pale lumumba.
 
huyu hawezi waza zaidi ya ngono, worst ever minister i saw inTZ history, mmmhh chaguo la JK..!!!!!! na hii yote ndio mjue WHOOOOOOOOOOOO ISSSSSSSSSS JJJJJJJJKKKKKKKKKK
 
Nitashangaa sana sana jk akimrudisha huyu kilaza mwenzao uwaziri...nitashanga sanaa.....uwaziri sio size yake huyu labda secretary wa makamba pale lumumba.

lakini kwa uwezo wa kufikiri wa raisi huyu wa ccm hakuna la kushangaa tegemea uozo
 
Kwa CCM huyu Sophia Simba ndiye anafaa kuwa Rais. Hukumsikia JK anakwambia Makinda kafungua mlango na sasa kinamama wanaweza kutwaa nafasi ya juu kabisa.

Kwani Sophia Simba ana tofauti gani na JK? Angalau Sophia Simba anaonekana ni imara kuliko JK.

What matters doesn't matter in CCM!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Jamani leteni mada za maana badala ya kuwashambulia watu mmoja mmoja, hii ni forum makini na sio chama cha mashoga au wasagaji
 
Jamani leteni mada za maana badala ya kuwashambulia watu mmoja mmoja, hii ni forum makini na sio chama cha mashoga au wasagaji

Kwanini wewe usilete hizo unazoziona za maana. Unasubiri uletewe...mbona hiyo ndiyo tabia ya mashoga na wasagaji!!!!!!!!
 
Nitashangaa sana sana jk akimrudisha huyu kilaza mwenzao uwaziri...nitashanga sanaa.....uwaziri sio size yake huyu labda secretary wa makamba pale lumumba.


mimi nitashangaaa akimnyima uwaziri, JK neve stop to amaze me, kile ambacho waungwana wanatarajia hatafanya yeye ndio anakifanya.
 
WAZIRI wa zamani Nchi, Ofisi ya Rais (Utawala Bora), Sophia Mnyambi Simba, huko nyuma amewahi pia kutoa kauli zenye ukakasi akimshambulia mfanyabiashara (Mengi kuwa sio mwanaCCM )na mmoja wa wafadhili wa chama tawala kilichomweka waziri huyo madarakani.

Ni huyu huyu Sophia ambaye chama chake kimekanusha matamshi aliyotatoa mbele ya kadamnasi kuwashambulia wabunge wa kuchaguliwa walio mume na mke – John Malecela na Anne Kilango Malecela.

Ni huyu Sophia mwenye dhamana ndani ya wizara nyeti ya Utawala Bora, yenye wajibu wa kusimamia mienendo ya watumishi wa umma, iliyo chini ya Ofisi ya Rais.

Ni Sophia ndiye anayewajibika katika kusimamia na kutekeleza kiapo chake cha utii na kumshauri vema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, katika masuala mbalimbali yenye maslahi kwa taifa, bila migogoro yoyote.

Ni huyu Sophia, ambaye ndani ya chama chake, amekabidhiwa dhamana ya uenyekiti wa Jumuiya ya Wanawake (UWT) - wanaokiamini, kukipenda na kukitumikia chama tawala, yaani CCM.

Ni huyu Sophia aliyedaiwa kumwangushia kipigo, aliyekuwa mwenyekiti wa jumuiya hiyo, Janeth Kahama, wakati wa mchakato na kampeni za kumtafuta mwenyekiti wa wanawake hao kwa njia ya kura.

Ni Sophia huyu huyu, aliyewahi kukaririwa na vyombo vya habari akiwatetea wafanyabiashara wakubwa wanaotuhumiwa kwa ufisadi na kuzua gumzo na kuharibu upepo wa nchi wakati huo.

Sophia Simba, kwangu ni mwanamama anayekurupuka. Ni Waziri asiyejipa muda wa kutafakari na kueleza anachokifahamu. Wakati mwingine nahisi anatumika ama kwa nia ovu au kwa maslahi ya taifa ili kuharibu mwelekeo ama kuwasahaulisha walalahoi kero zinazowakabili.

Ni Sophia, aliyejaribu kucheza ngoma tofauti ya vita dhidi ya ufisadi iliyoanzishwa na viongozi wa vyama vya upinzani kabla ya kupokelewa kwa shangwe wa wakuu wa chama chake, akiwemo rais aliyemteua kushika nafasi ya uwaziri.

Ni Sophia aliyewashangaza wasomi na wasio wasomi, pale alipojiinua na kuishambulia familia ya wanasiasa, akiwemo mkongwe, Mzee Malecela.

Ni huyu Waziri Sophia aliyewaacha vinywa wazi wachambuzi, wajuzi na wananchi wa kawaida pale alipowashambulia kwa tuhuma mbalimbali wanasiasa wenzake.

Ni wapi alipokuwa Sophia kiasi cha kuzikalia tuhuma nzito za wanasiasa hao na kujinasibu kwamba ndani ya chama chao cha CCM hakuna msafi, wote ni mafisadi?

Ni imani yangu kwamba Sophia anahitaji kubanwa ili aanike tuhuma zote anazozifahamu, pengine atalisaidia taifa na kulirejesha kwenye mstari ili walalahoi waone raha na faida ya kuzaliwa juu ya ardhi ya Tanzania.

Pamoja na yote, nina ushauri kwa mkuu wake wa kazi. Kwanza amfukuze kwa sababu amejidhihirisha kwamba hafai kuwa kiongozi wa wanyonge kwa sababu ameshindwa kusimamia mienendo ya watumishi wa umma.

Sophia aanze kufuatiliwa, ahojiwe na Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (TAKUKURU), Polisi na Usalama wa Taifa.

Ni huyu sophia Simba aliyesema (akiwambia UWT members) kuwa kama Mumeo hapendi CCM basi usimpe unyumba.. Anaonyesha wazi kuwa Ngono kwake yeye ni jambo muhimu zaidi kuliko kuendelea na misimamo sawia ya kinchi na utaifa.:A S cry:

Ni Imani yangu kwamba kuondolewa kwa waziri huyu katika nafasi aliyonayo, kutabadili fikira zangu kwamba analipwa fadhila za mema machache aliyoyatenda wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu wa mwaka 2005(kumpitisha JK pale CCM).

nawasilisha
Source: freemedia:israel:


chezea Mwanakijiji.
 
umenikuna lakini umewasahau Dk Shukuru Kawambwa & Hawa Ghasia sijaona walichofanya TRL,ATCL,bandari hakuna kitu kero kero kero na utumishi wa uma ndo yale yale mauozo hata Mhe Jenista Mhagama alisha sema .wakitemwa ntafanya sherehe ntawambia venue
 
Kwa JK hakuna lisilowezekana, Megji -mmoja wa mafisadi wa EPA-kesharudi mjengoni! Na bado kina masha, buriani, worse still EL anaweza kupewa wizara!
 
Back
Top Bottom