Sony Wathibitisha Muendelezo wa Game ya God of War upo jikoni

Msamiati

R I P
Mar 6, 2011
1,063
697
GodofWar.jpg

Meneja Ubunifu wa studio za Sony, Bwana Cory Barlog amethibitisha rasmi kuwa Studio zao zipo kwenye maandalizi ya toleo jipya la game ya God of War.

Bwana Cory Barlog amethibitisha taarifa hizo jana kwenye tamasha la PlayStation lililofanyika Las Vegas wakati akijibu maswali ya mashabiki kuhusiana na Gamu hiyo.

Hata hivyo, mapema baadae Studio za Sony kupitia account yake rasmi ya tweeter wali tweet ujumbe uliosema,"Taarifa hizi si za kusambazwa, Alichosema Cory Barlog alikisema kimakosa kwani hakutakiwa kukizungumzia".

Hata hivyo tukijaribu kutizama jambo hili kwa jicho la tatu, alichosema Cory BarLog hakikuwa na unyeti mkubwa kiasi hicho, kwani alijaribu kuzungumzia kwa ufupi kinachoendelea kwenye ofisi zao.

Kutokana na mkanganyiko huu, Mpenzi wagame hii usijipe sana moyo ya ujio wa toleo jipya la God of War,kauli ya Barlog ilisema game lipo kwenye hatua ya awali kabisa ya matengenezo, hivyo anatarajia kutoa taarifa zaidi miaka miwili au zaidi mbele.

Toleo la mwisho la God of War kwenye mfululizo wa game hizi lilikuwa God of War Ascension toleo lililotoka kipindi cha PlayStation 3 mwaka 2013.

By Msamiati
 
Kweli dunia msongamano...wengine tunawazia buku la makoko kwa mama ntilie wengine wanawazia magame..........
 
Kweli dunia msongamano...wengine tunawazia buku la makoko kwa mama ntilie wengine wanawazia magame..........

na mwisho wa siku angalia huyo anaecheza game ana hela kumshinda huyo anaehangaika na maisha kutwa nzima. enterteinment ni muhimu kwenye maisha inafanya akili iwe active tofauti na mtu mwenye mawazo na muda wote anafkiria maisha
 
na mwisho wa siku angalia huyo anaecheza game ana hela kumshinda huyo anaehangaika na maisha kutwa nzima. enterteinment ni muhimu kwenye maisha inafanya akili iwe active tofauti na mtu mwenye mawazo na muda wote anafkiria maisha

Kweli mkuu....lakini game linakuwa tamu kawa ukiwa umeshiba......
 
Kweli mkuu....lakini game linakuwa tamu kawa ukiwa umeshiba......

Ha ha ha haaaa, sio mcheza gamu wewe ! Wenye hii kitu hawatizami hayo, fanya kazi ukikosa ukipata muda wa kupumzika unapumzika. Ukikosa usipopumzika unatengeneza matatizo mengine suo kwamba hela ndio zitakuja
 
Ha ha ha haaaa, sio mcheza gamu wewe ! Wenye hii kitu hawatizami hayo, fanya kazi ukikosa ukipata muda wa kupumzika unapumzika. Ukikosa usipopumzika unatengeneza matatizo mengine suo kwamba hela ndio zitakuja
Hivi mkuu unajua kutofautisha njaa na hamu ya kula....???
 
aisee...!!!

naisubiria moja kati ya game ambazo vichwa maji hawachezi
 
Back
Top Bottom