Sonso ameacha maandishi ukutani, tujitafakari

Nadhani TFF wangeweka kanuni kwa vilabu vyote vya ligi kuu kuhakikisha wachezaji wote walio sajiliwa wanakuwa na Bima ya Afya ya daraja kama lile la wafanyakazi wa Serikali.

Pia tuendelee kuwekeza kwenye Academy kwa vijana, ili tupate wachezaji walio kamilika. Badala ya kuendelea kuwakumbatia wachezaji wanao amini mpaka leo katika kupigana misumari, na pia bangi kama 'booster'.
 
sonso pic


IJUMAA iliyopita amefariki dunia beki wa Ruvu Shooting, Ally Mtoni ‘Sonso’ na alizikwa Jumamosi. Sonso enzi za uhai wake aliwahi pia kuzicheza Lipuli, Yanga na Kagera Sugar. Zaidi ya hapo amewahi kuipigania jezi ya timu ya taifa.

Ni mara chache kwa taifa letu kutokea kifo cha mchezaji wa Ligi Kuu ambaye anaendelea kucheza soka. Tumewahi kushuhudia wachezaji wengi wa zamani walioacha soka wakifariki lakini sio kwa wachezaji ambao wanaendelea kucheza.

Jina lake lipo katika ofisi za TFF kama mchezaji wa Ligi Kuu na ni Novemba mwaka jana tu Sonso alikuwa amecheza pambano lake la mwisho la Ligi Kuu. Ni Novemba mwaka jana tu tunaambiwa kwamba Sonso alishapangwa katika kikosi ambacho kingecheza na Simba, lakini mguu ukaanza kumpa maumivu.

Huu ulikuwa mwanzo wa safari yake ya mwisho. Kinachosemwa ni kwamba baada ya hapo alipelekwa hospitali ya Muhimbili lakini yeye na familia yake wakamtoa hospitali na kuamua kumpeleka kusikojulikana kwa ajili ya matibabu zaidi.

Hili ni fumbo. Kusikojulikana ni wapi? Hatuwezi kufichana kuhusu matibabu. Sonso alikwenda kupata matibabu ya kienyeji. Inadaiwa kulikuwa na hisia kwamba huenda alikuwa amefanyiwa mambo ya kishirikina. Sio jambo jema.

Kumekuwa na wimbi la wachezaji ambao wanaamua kuifuata njia hii. Hatuelewi kwanini, lakini kikubwa zaidi ni elimu miongoni mwa wachezaji wetu. Wachezaji wetu wanapaswa kufundishwa kuamini katika magonjwa halisi yaliyopo na yanayoweza kutibika kitalaamu.

Advertisement

Staa mmoja wa Yanga aliwahi kupata hisia hizi. Akagomea matibabu ya hospitali. Alikwenda kusikojulikana kwa ajili ya kupata matibabu, lakini hali ikaendelea kuwa mbaya. Baadaye Yanga wakamkimbiza Afrika Kusini kwa ajili ya matibabu zaidi. Alirudi akiwa ametengemaa na maisha yake ya soka yanaendelea. Alitibiwa kitaalamu zaidi kwa mujibu wa ugonjwa wake na hali ikawa sawa.

Imewahi pia kutokea hapo zamani kwa staa wa zamani wa Simba na timu ya taifa. Aliwahi kupata majeraha ya kawaida, lakini akagoma kutibiwa katika njia za kawaida za kitabibu. Bahati mbaya alikuwa anaelekea katika siku zakeza mwisho za maisha yake ya soka. Sijui kama alienda hospitalini au vinginevyo. Namuona akicheza mechi za mitaani.

Hili ni fundisho kwa soka letu na tunahitaji kujitafakari. Tunahitaji elimu kwa wachezaji wetu. Elimu ya saikolojia na elimu ya kawaida kabisa. Itasaidia kwa wachezaji kujua kwamba mwanadamu, hasa mwanamichezo anaweza kuumia kama Cristiano Ronaldo huwa anaumia.

Unajaribu kujiuliza kwa Sonso. Ni kwanini ilifikirika hivyo? Timu kama Ruvu Shooting ina riziki gani ya kuweza kuwahangaisha wachezaji wawafanyie wachezaji wenzao mambo mabaya? Kama haikuwa hivyo Yanga vipi itokee kwa Ruvu Shooting?

Kitu kingine ambacho kinaweza kuwahangaisha wachezaji wetu ni bima ya Afya. Wachezaji wetu wana bima za Afya? Tufanye kwamba Sonso angeamua kukaa hospitalini na matibabu yake yakachukua muda mrefu. Je ni kweli alikuwa na bima ya afya?

Wachezaji wengi wa Ligi Kuu hawana bima za Afya. Sio kwa wao tu, bali pia kwa familia zao. Mchezo wa soka unaonekana kama sehemu ya kuzugia tu na sio kazi kamili. Ni kosa kubwa kwa mwanamichezo kukosa bima ya Afya hasa ukizingatia pia kazi zao zinawafanya wawe katika hatari kubwa ya kuumia.

Wengine wanaweza wasiumie kazini, lakini mtazame mchezaji kama Gerald Mdamu wa Polisi Tanzania ambaye aliumia katika ajali ya gari akiwa na timu. Baadaye ilibainika kwamba Mdamu hakuwa na bima ya Afya. Hata kama angeumia ndani ya uwanja bado angepata wakati mgumu.

Wachezaji wa Yanga, Simba na Azam wana bahati ya kwenda kutibiwa nchi za nje. Wapo wanaokwenda zaidi Afrika Kusini lakini Yanga pia wameanzisha utaratibu kwa kuwapeleka wachezaji wao Tunisia. Sio kila timu inaweza kufanya hivi. Tusisitize wachezaji kuwa na bima. Mchezaji anayefikia hadhi ya kucheza daraja la pili, la kwanza na Ligi Kuu lazima awe na bima.

Tukirudi kwa Sonso, ndani ya uwanja nitafafanua mambo mawili. Kwanza kabisa tumempoteza mchezaji ambaye alikuwa na umbo refu kabla ya kila kitu. Baada ya maumbo ya kina Bakari Malima kuondoka nchini kwa sasa tumebakiwa na wachezaji wachache warefu hasa katika maeneo ya ulinzi. Sonso alikuwa mmoja wao.

Lakini vile vile tumempoteza mchezaji aliyeweza kucheza nafasi nyingi tofauti uwanjani. Angeweza kucheza kama beki wa kushoto, pia kama beki wa kati na pia alimudu kiungo cha ukabaji yaani namba 6. Hii pengine ilitokana na matumizi sahihi ya mguu wake wa kushoto.

Hatuna wachezaji wengi wanaoweza kufanya hivi katika zama za kisasa. Wengi wanaweza kucheza nafasi moja uwanjani. Kitu ambacho kwa sasa Dickson Job au Kibwana Shomari wamekuwa wakiifanyia Yanga ni kitu adimu kwa soka letu.

Zamani tulikuwa na wachezaji wengi ambao wangeweza kucheza katika nafasi tofauti kutokana na upungufu wa baadhi ya wachezaji uwanjani. Marehemu Saidi Mwamba Kizota alikuwa mmojawao. Angeweza kucheza nafasi tatu uwanjani. Angeweza kucheza kama beki wa kati, kiungo na pia mshambuliaji. Mungu amrehemu.

Pamoja na yote haya, lakini kifo cha Sonso kimetukumbusha umoja wetu katika soka. Inawezekana Sonso hakuwa maarufu sana kama Mbwana Samatta, lakini jamii ya wanamichezo imewakumbusha watu wa fani nyingine jinsi mchezo wa soka ulivyo na nguvu.

Msiba wa Sonso ulitufanya tuwe wamoja na kuungana katika majonzi yetu. Ambao wapo katika fani nyingine na hawakumfahamu Sonso walijikuta wakimfahamu na kutaka kujua mengi yanayomuhusu. Ni heshima pia kwa familia yake.



Mungu amlaze mahala pema peponi.



eddo Kumwembe
Haya maelezo yoote yalikuwa yaandikwe paragraph moja tuu.
 
Kama kuna mtu aliuona ule mguu wa sonso,ni dhahiri hiyo ni kansa

Sent from my SM-N960F using JamiiForums mobile app
Nimeona Ile picha mdau mguu umelika kabisaa Ila wanadai alitupiwa jini.......chanzo ni kugombea namba ya moja kwa moja pale ruvu na ni yeye mwenyewe ndio alianzisha hii Vita kumloga yule beki jamaa akaona isiwe tabu kama yeye kaanza mie namaliza.......sonso kaanzisha Vita kumbe Kinga Hana ndio yakamkuta yale
 
aliye mpiga misumari huyu dogo Mungu anamuona, hata akiokoka hili la sonso ataenda nalo adi kaburini, otherwise akaiombee msamaha familia ya sonso………….
 
Asante mleta mada umegusa kitu muhimu sana bima ya afya kwa wachezaji. Kama kumbukumbu zangu zipo vizuri miaka michache iliyopita TFF ilianzisha suala la bima ya afya kwa wachezaji na timu zililazimishwa kuwakatia bima ya afya wachezaji wao wote. Na walienda mbali zaidi kwa kuvilazimisha vilabu vikate hiyo bima vinginevyo visingeruhusiwa kushiriki ligi. Sijui huo mpango uliishiia wapi. Suala la Mudamu wa Polisi liwe funzo kubwa kwenye hili.

Hivi kweli kama TFF inaweza kuvilazimisha vilabu kuwa na timu za vijana ili ziruhusiwe kushiriki ligi kuu inashindwa nini kuvilazimisha hivi vilabu kukata bima kwa wachezaji wote . Na klabu itakayoshindwa kuwakatia bima wachezaji wake wasitoe leseni ya kuwaruhusu wacheze.

Vipi nayo makampuni ya bima na mabenki mbona yamekaa kimya kwa wachezaji wa mpira lakini yote yamejikita kwenye bima za mazishi au kutoa bima kwa wacheza mpira sio biashara nzuri kwao?

Ombi langu kwa vilabu vyote vijikite kutoa elimu kwa wachezaji wetu waache kuamini ushirikina hata kwa mambo yanayo hitaji matibabu ya kawaida hospitali. Vijana wengi wanatoka na imani zao kwenye hivi vilabu vya chini ambavyo vinaamini sana ushirikina wanafika kwenye vilabu vikubwa badala ya kuelimishwa wanakuta hata vilabu vikubwa navyo vimebobea kwenye ushirikina. Matokeo yake mchezaji akiumia kidogo tu au akipata changamoto yoyote mbio kwa waganga. Japo kifo ni mpango wa mwenyezi Mungu lakini huenda Ally Sonso angepata taarifa sahihi akabaki Muhimbili hali isingekuwa kuwa kama ilivyo leo hatupo naye.

Na viongozi wa vilabu nao wajitathmini. Nikiangalia suala la Sonso lilivyoshughulikiwa na viongozi wa timu yake naona kuna shida mahali. Hivi kiongozi unashindwaje kumfuatilia mchezaji kwa karibu tangu Novemba mwaka jana mpaka hali inakuwa mbaya Februari mwaka huu? Naamini kungekuwa na ufuatiliaji wa karibu viongozi wangejua mapema Sonso anapatiwa matibabu yasiyo rasmi wapi na wangegundua mapema kuwa matibabu anayopata sio sahihih na ingekuwa rahisi kumrudisha kwenye matibabu sahihi kwa wakati muafaka.
 
Piga picha huo ukuta aliouandika maelezo mbona mengi muda mchache
 
sonso pic


IJUMAA iliyopita amefariki dunia beki wa Ruvu Shooting, Ally Mtoni ‘Sonso’ na alizikwa Jumamosi. Sonso enzi za uhai wake aliwahi pia kuzicheza Lipuli, Yanga na Kagera Sugar. Zaidi ya hapo amewahi kuipigania jezi ya timu ya taifa.

Ni mara chache kwa taifa letu kutokea kifo cha mchezaji wa Ligi Kuu ambaye anaendelea kucheza soka. Tumewahi kushuhudia wachezaji wengi wa zamani walioacha soka wakifariki lakini sio kwa wachezaji ambao wanaendelea kucheza.

Jina lake lipo katika ofisi za TFF kama mchezaji wa Ligi Kuu na ni Novemba mwaka jana tu Sonso alikuwa amecheza pambano lake la mwisho la Ligi Kuu. Ni Novemba mwaka jana tu tunaambiwa kwamba Sonso alishapangwa katika kikosi ambacho kingecheza na Simba, lakini mguu ukaanza kumpa maumivu.

Huu ulikuwa mwanzo wa safari yake ya mwisho. Kinachosemwa ni kwamba baada ya hapo alipelekwa hospitali ya Muhimbili lakini yeye na familia yake wakamtoa hospitali na kuamua kumpeleka kusikojulikana kwa ajili ya matibabu zaidi.

Hili ni fumbo. Kusikojulikana ni wapi? Hatuwezi kufichana kuhusu matibabu. Sonso alikwenda kupata matibabu ya kienyeji. Inadaiwa kulikuwa na hisia kwamba huenda alikuwa amefanyiwa mambo ya kishirikina. Sio jambo jema.

Kumekuwa na wimbi la wachezaji ambao wanaamua kuifuata njia hii. Hatuelewi kwanini, lakini kikubwa zaidi ni elimu miongoni mwa wachezaji wetu. Wachezaji wetu wanapaswa kufundishwa kuamini katika magonjwa halisi yaliyopo na yanayoweza kutibika kitalaamu.

Advertisement

Staa mmoja wa Yanga aliwahi kupata hisia hizi. Akagomea matibabu ya hospitali. Alikwenda kusikojulikana kwa ajili ya kupata matibabu, lakini hali ikaendelea kuwa mbaya. Baadaye Yanga wakamkimbiza Afrika Kusini kwa ajili ya matibabu zaidi. Alirudi akiwa ametengemaa na maisha yake ya soka yanaendelea. Alitibiwa kitaalamu zaidi kwa mujibu wa ugonjwa wake na hali ikawa sawa.

Imewahi pia kutokea hapo zamani kwa staa wa zamani wa Simba na timu ya taifa. Aliwahi kupata majeraha ya kawaida, lakini akagoma kutibiwa katika njia za kawaida za kitabibu. Bahati mbaya alikuwa anaelekea katika siku zakeza mwisho za maisha yake ya soka. Sijui kama alienda hospitalini au vinginevyo. Namuona akicheza mechi za mitaani.

Hili ni fundisho kwa soka letu na tunahitaji kujitafakari. Tunahitaji elimu kwa wachezaji wetu. Elimu ya saikolojia na elimu ya kawaida kabisa. Itasaidia kwa wachezaji kujua kwamba mwanadamu, hasa mwanamichezo anaweza kuumia kama Cristiano Ronaldo huwa anaumia.

Unajaribu kujiuliza kwa Sonso. Ni kwanini ilifikirika hivyo? Timu kama Ruvu Shooting ina riziki gani ya kuweza kuwahangaisha wachezaji wawafanyie wachezaji wenzao mambo mabaya? Kama haikuwa hivyo Yanga vipi itokee kwa Ruvu Shooting?

Kitu kingine ambacho kinaweza kuwahangaisha wachezaji wetu ni bima ya Afya. Wachezaji wetu wana bima za Afya? Tufanye kwamba Sonso angeamua kukaa hospitalini na matibabu yake yakachukua muda mrefu. Je ni kweli alikuwa na bima ya afya?

Wachezaji wengi wa Ligi Kuu hawana bima za Afya. Sio kwa wao tu, bali pia kwa familia zao. Mchezo wa soka unaonekana kama sehemu ya kuzugia tu na sio kazi kamili. Ni kosa kubwa kwa mwanamichezo kukosa bima ya Afya hasa ukizingatia pia kazi zao zinawafanya wawe katika hatari kubwa ya kuumia.

Wengine wanaweza wasiumie kazini, lakini mtazame mchezaji kama Gerald Mdamu wa Polisi Tanzania ambaye aliumia katika ajali ya gari akiwa na timu. Baadaye ilibainika kwamba Mdamu hakuwa na bima ya Afya. Hata kama angeumia ndani ya uwanja bado angepata wakati mgumu.

Wachezaji wa Yanga, Simba na Azam wana bahati ya kwenda kutibiwa nchi za nje. Wapo wanaokwenda zaidi Afrika Kusini lakini Yanga pia wameanzisha utaratibu kwa kuwapeleka wachezaji wao Tunisia. Sio kila timu inaweza kufanya hivi. Tusisitize wachezaji kuwa na bima. Mchezaji anayefikia hadhi ya kucheza daraja la pili, la kwanza na Ligi Kuu lazima awe na bima.

Tukirudi kwa Sonso, ndani ya uwanja nitafafanua mambo mawili. Kwanza kabisa tumempoteza mchezaji ambaye alikuwa na umbo refu kabla ya kila kitu. Baada ya maumbo ya kina Bakari Malima kuondoka nchini kwa sasa tumebakiwa na wachezaji wachache warefu hasa katika maeneo ya ulinzi. Sonso alikuwa mmoja wao.

Lakini vile vile tumempoteza mchezaji aliyeweza kucheza nafasi nyingi tofauti uwanjani. Angeweza kucheza kama beki wa kushoto, pia kama beki wa kati na pia alimudu kiungo cha ukabaji yaani namba 6. Hii pengine ilitokana na matumizi sahihi ya mguu wake wa kushoto.

Hatuna wachezaji wengi wanaoweza kufanya hivi katika zama za kisasa. Wengi wanaweza kucheza nafasi moja uwanjani. Kitu ambacho kwa sasa Dickson Job au Kibwana Shomari wamekuwa wakiifanyia Yanga ni kitu adimu kwa soka letu.

Zamani tulikuwa na wachezaji wengi ambao wangeweza kucheza katika nafasi tofauti kutokana na upungufu wa baadhi ya wachezaji uwanjani. Marehemu Saidi Mwamba Kizota alikuwa mmojawao. Angeweza kucheza nafasi tatu uwanjani. Angeweza kucheza kama beki wa kati, kiungo na pia mshambuliaji. Mungu amrehemu.

Pamoja na yote haya, lakini kifo cha Sonso kimetukumbusha umoja wetu katika soka. Inawezekana Sonso hakuwa maarufu sana kama Mbwana Samatta, lakini jamii ya wanamichezo imewakumbusha watu wa fani nyingine jinsi mchezo wa soka ulivyo na nguvu.

Msiba wa Sonso ulitufanya tuwe wamoja na kuungana katika majonzi yetu. Ambao wapo katika fani nyingine na hawakumfahamu Sonso walijikuta wakimfahamu na kutaka kujua mengi yanayomuhusu. Ni heshima pia kwa familia yake.

Mungu amlaze mahala pema peponi.

eddo Kumwembe
Ushirikina ni janga. Tumebobea kwenye ushirikina na unaturudi vibaya sana
 
Nadhani TFF wangeweka kanuni kwa vilabu vyote vya ligi kuu kuhakikisha wachezaji wote walio sajiliwa wanakuwa na Bima ya Afya ya daraja kama lile la wafanyakazi wa Serikali.

Pia tuendelee kuwekeza kwenye Academy kwa vijana, ili tupate wachezaji walio kamilika. Kuendelea kuwakumbatia wachezaji wanao amini katika kupigana misumari, na pia bangi kama 'booster'.
Kua na bima ya afya hakuzuii ndugu wenye imani za kishirikina kukupeleka vilingeni
 
sonso pic


IJUMAA iliyopita amefariki dunia beki wa Ruvu Shooting, Ally Mtoni ‘Sonso’ na alizikwa Jumamosi. Sonso enzi za uhai wake aliwahi pia kuzicheza Lipuli, Yanga na Kagera Sugar. Zaidi ya hapo amewahi kuipigania jezi ya timu ya taifa.

Ni mara chache kwa taifa letu kutokea kifo cha mchezaji wa Ligi Kuu ambaye anaendelea kucheza soka. Tumewahi kushuhudia wachezaji wengi wa zamani walioacha soka wakifariki lakini sio kwa wachezaji ambao wanaendelea kucheza.

Jina lake lipo katika ofisi za TFF kama mchezaji wa Ligi Kuu na ni Novemba mwaka jana tu Sonso alikuwa amecheza pambano lake la mwisho la Ligi Kuu. Ni Novemba mwaka jana tu tunaambiwa kwamba Sonso alishapangwa katika kikosi ambacho kingecheza na Simba, lakini mguu ukaanza kumpa maumivu.

Huu ulikuwa mwanzo wa safari yake ya mwisho. Kinachosemwa ni kwamba baada ya hapo alipelekwa hospitali ya Muhimbili lakini yeye na familia yake wakamtoa hospitali na kuamua kumpeleka kusikojulikana kwa ajili ya matibabu zaidi.

Hili ni fumbo. Kusikojulikana ni wapi? Hatuwezi kufichana kuhusu matibabu. Sonso alikwenda kupata matibabu ya kienyeji. Inadaiwa kulikuwa na hisia kwamba huenda alikuwa amefanyiwa mambo ya kishirikina. Sio jambo jema.

Kumekuwa na wimbi la wachezaji ambao wanaamua kuifuata njia hii. Hatuelewi kwanini, lakini kikubwa zaidi ni elimu miongoni mwa wachezaji wetu. Wachezaji wetu wanapaswa kufundishwa kuamini katika magonjwa halisi yaliyopo na yanayoweza kutibika kitalaamu.

Advertisement

Staa mmoja wa Yanga aliwahi kupata hisia hizi. Akagomea matibabu ya hospitali. Alikwenda kusikojulikana kwa ajili ya kupata matibabu, lakini hali ikaendelea kuwa mbaya. Baadaye Yanga wakamkimbiza Afrika Kusini kwa ajili ya matibabu zaidi. Alirudi akiwa ametengemaa na maisha yake ya soka yanaendelea. Alitibiwa kitaalamu zaidi kwa mujibu wa ugonjwa wake na hali ikawa sawa.

Imewahi pia kutokea hapo zamani kwa staa wa zamani wa Simba na timu ya taifa. Aliwahi kupata majeraha ya kawaida, lakini akagoma kutibiwa katika njia za kawaida za kitabibu. Bahati mbaya alikuwa anaelekea katika siku zakeza mwisho za maisha yake ya soka. Sijui kama alienda hospitalini au vinginevyo. Namuona akicheza mechi za mitaani.

Hili ni fundisho kwa soka letu na tunahitaji kujitafakari. Tunahitaji elimu kwa wachezaji wetu. Elimu ya saikolojia na elimu ya kawaida kabisa. Itasaidia kwa wachezaji kujua kwamba mwanadamu, hasa mwanamichezo anaweza kuumia kama Cristiano Ronaldo huwa anaumia.

Unajaribu kujiuliza kwa Sonso. Ni kwanini ilifikirika hivyo? Timu kama Ruvu Shooting ina riziki gani ya kuweza kuwahangaisha wachezaji wawafanyie wachezaji wenzao mambo mabaya? Kama haikuwa hivyo Yanga vipi itokee kwa Ruvu Shooting?

Kitu kingine ambacho kinaweza kuwahangaisha wachezaji wetu ni bima ya Afya. Wachezaji wetu wana bima za Afya? Tufanye kwamba Sonso angeamua kukaa hospitalini na matibabu yake yakachukua muda mrefu. Je ni kweli alikuwa na bima ya afya?

Wachezaji wengi wa Ligi Kuu hawana bima za Afya. Sio kwa wao tu, bali pia kwa familia zao. Mchezo wa soka unaonekana kama sehemu ya kuzugia tu na sio kazi kamili. Ni kosa kubwa kwa mwanamichezo kukosa bima ya Afya hasa ukizingatia pia kazi zao zinawafanya wawe katika hatari kubwa ya kuumia.

Wengine wanaweza wasiumie kazini, lakini mtazame mchezaji kama Gerald Mdamu wa Polisi Tanzania ambaye aliumia katika ajali ya gari akiwa na timu. Baadaye ilibainika kwamba Mdamu hakuwa na bima ya Afya. Hata kama angeumia ndani ya uwanja bado angepata wakati mgumu.

Wachezaji wa Yanga, Simba na Azam wana bahati ya kwenda kutibiwa nchi za nje. Wapo wanaokwenda zaidi Afrika Kusini lakini Yanga pia wameanzisha utaratibu kwa kuwapeleka wachezaji wao Tunisia. Sio kila timu inaweza kufanya hivi. Tusisitize wachezaji kuwa na bima. Mchezaji anayefikia hadhi ya kucheza daraja la pili, la kwanza na Ligi Kuu lazima awe na bima.

Tukirudi kwa Sonso, ndani ya uwanja nitafafanua mambo mawili. Kwanza kabisa tumempoteza mchezaji ambaye alikuwa na umbo refu kabla ya kila kitu. Baada ya maumbo ya kina Bakari Malima kuondoka nchini kwa sasa tumebakiwa na wachezaji wachache warefu hasa katika maeneo ya ulinzi. Sonso alikuwa mmoja wao.

Lakini vile vile tumempoteza mchezaji aliyeweza kucheza nafasi nyingi tofauti uwanjani. Angeweza kucheza kama beki wa kushoto, pia kama beki wa kati na pia alimudu kiungo cha ukabaji yaani namba 6. Hii pengine ilitokana na matumizi sahihi ya mguu wake wa kushoto.

Hatuna wachezaji wengi wanaoweza kufanya hivi katika zama za kisasa. Wengi wanaweza kucheza nafasi moja uwanjani. Kitu ambacho kwa sasa Dickson Job au Kibwana Shomari wamekuwa wakiifanyia Yanga ni kitu adimu kwa soka letu.

Zamani tulikuwa na wachezaji wengi ambao wangeweza kucheza katika nafasi tofauti kutokana na upungufu wa baadhi ya wachezaji uwanjani. Marehemu Saidi Mwamba Kizota alikuwa mmojawao. Angeweza kucheza nafasi tatu uwanjani. Angeweza kucheza kama beki wa kati, kiungo na pia mshambuliaji. Mungu amrehemu.

Pamoja na yote haya, lakini kifo cha Sonso kimetukumbusha umoja wetu katika soka. Inawezekana Sonso hakuwa maarufu sana kama Mbwana Samatta, lakini jamii ya wanamichezo imewakumbusha watu wa fani nyingine jinsi mchezo wa soka ulivyo na nguvu.

Msiba wa Sonso ulitufanya tuwe wamoja na kuungana katika majonzi yetu. Ambao wapo katika fani nyingine na hawakumfahamu Sonso walijikuta wakimfahamu na kutaka kujua mengi yanayomuhusu. Ni heshima pia kwa familia yake.

Mungu amlaze mahala pema peponi.

eddo Kumwembe
Bima Ya afya tsh 54000/= kwa mwaka
Mchezaji anashindwaje kulipa?
Uelewa mdogo tu
Yupo raisi mmoja kwenye nchi moja huko EA. alishawahi kuwaminisha watu wake kwamba dawa ya CORONA ni nyungu na maombi
 
Hujawahi kutana na ulozi broo, Sonso arogwa
Kama hosp Muhimbili walisema ugonjwa hauonekani kqbisa yaani yeye ni mzima ili hali yeye maumivu yanaendelea basi yawezekana tungewaelewa hao mandugu kumtoa hosp.
 
I see..ule mguu ulipata shida kubwa Sana..Kama Ni uchawi basi Kuna watu wanajua kuroga..Kama sio..basi Ni kansa Kama mdau alivyosema hapo juu..
 
Bima Ya afya tsh 54000/= kwa mwaka
Mchezaji anashindwaje kulipa?
Uelewa mdogo tu
Yupo raisi mmoja kwenye nchi moja huko EA. alishawahi kuwaminisha watu wake kwamba dawa ya CORONA ni nyungu na maombi
Hiyo ni gharama ya bima kwa watoto chini ya umri wa miaka 5 na bima inayotolewa vyuoni.

Pia ni 50,400
 
Back
Top Bottom