Songwe: Askari waliovuka mpaka kuingia Malawi kinyume cha sheria wafukuzwa kazi

Askari 7 wanamfukuza bodaboda mmoja, ila hawa ndugu sijui hata wanawaza nini

PGO ndio yanapoanzia matatizo yote, kama mimi Raia najua kuvuka mpaka wa nchi nyingine ukiwa na silaha za moto, mavazi au sare za kijeshi au kuvuka bila kutimiza vigezo ni kosa wao walishindwa nini kujua hilo
 
Septemba 15 askari Polisi wa Tanzania waliingia Malawi kinyume cha sheria wakimfukuza bodaboda waliyedhani amebeba biashara ya magendo ambapo walipoingia Malawi walipigwa mawe na wamalawi na kuokolewa na Polisi wa Malawi

Askari 7 wa Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Ileje mkoani Songwe wamefukuzwa kazi kwa kosa la kuvuka mpaka na kuingia nchini Malawi wakiwa na mavazi ya kijeshi na silaha za moto kinyume na taratibu za kijeshi

Kamanda wa Polisi Mkoani Songwe Janeth Magomi amethibitisha tukio hilo

Pia soma: Polisi wa Tanzania wanasa Malawi wakifuatilia wahalifu
Eti waliona piki piki wakaikimbiza wakizani ina magendo.... ujinga mtupu yaani sijui wanakuwa trained vipi hawa jamaa. Hapo utakuta walikuwa wanakimbiza wapate rushwa.
 
Happy hakuna tofauti na wale wafanyakazi wa TRA waliopoteza maisha Kwa ajili kukimbiza magendo. Tofauti ni kwamba wale wamepoteza maisha, Hawa wamepoteza kazi Ila wote walikuwa wanakimbiza ili kupata Cha juuuu!!!!
 
21 SEPTEMBER 2021
ILEJE, SONGWE
TANZANIA

ASKARI WA POLISI WATANZANIA WALIOINGIA MALAWI WAFUTWA KAZI, PIA WALIKIMBIA NA KUTEKELEZA SILAHA ZAO





WALIKUWA KATIKA OPERESHENI AMBAYO HAIKUFUATA KANUNI ZA GPO

Askari 7 wa kituo cha Polisi cha Ileje bila kutoa taarifa kokote wala kibali cha IGP wa Tanzania waliingia katika nchi ya Malawi wilaya Chitipa wakidai kufukuzia magendo wakiwa na silaha 2 za SMG kila mmoja ikiwa na risasi 30 na gari moja la jeshi la Polisi la Tanzania.

Kufuatia kitendo hicho walikumbana na wananchi wa wenye hasira kali Malawi kupelekea askari polisi 4 kukamatwa pamoja na silaha mbili, risasi 60 na gari la polisi lenye usajili PT kushikiliwa nchini Malawi.

Askari hawa kwa kushindwa kufuata sheria ya utekelezaji kazi, kupata ruhusa, kutumwa / kupewa idhini halali toka ofisa wa Cheo cha juu kama zilizoainishwa na kanuni za GPO (general police orders), jeshi la Polisi kupitia mkuu wa Polisi mkoa wa Songwe amewafukuza kazi askari kwa kudhalilisha Jeshi la Polisi na pia kuifedhehesha nchi kwa vitendo vyao kufanya kazi bila kufuata GPO zinavyotaka.

Source : MATUKIO DAIMA TV

RPC anasema waliwashtaki hao Polisi kwa kufuata Kanuni zao zinazowaongoza Jeshi la Polisi yaani PGO.

Kesi ya kina RPC Kiangi na wenzake ni ngumu sana, kama hawakufuata Sheria zilizopo kwenye PGO na wao watakuja kushtakiwa na kufukuzwa kazi.
 
RPC anasema waliwashtaki hao Polisi kwa kufuata Kanuni zao zinazowaongoza Jeshi la Polisi yaani PGO.

Kesi ya kina RPC Kiangi na wenzake ni ngumu sana, kama hawakufuata Sheria zilizopo kwenye PGO na wao watakuja kushtakiwa na kufukuzwa kazi.

Hii kitu kanuni za PGO inawasumbua sasa, wanatakiwa kuisoma, kuifahamu na kuitumia katika kazi zao

Tanzania Police Force in modernisation strides - Daily News

7 Aug 2020 — TANZANIA Police Force (TPF) is on the verge of reviewing its Police General Order (PGO) that would incorporate addressing administration
 
Lakin pia pongez kwa wananch wa malawi sio mazombi. Kitendo cha kuwatwanga hao vilaza walioingia kwako ni cha kizalendo na kujielewa..

Njoo sasa huku kwetu kwa mazombi, kule Tarime one time police wakenya walivuka mpaka kuwakamata boda boda waliokuwa wanavuka mpaka kwenda Kenyaa..

Mazombi ya tz yakawa yanasema tu mbona wamevuka mpaka..mbona wanawashika..alaf yamekaa tu kutazama..
Vichwa wa wabongo vimejaa simba na yanga tu..shwaini
Uko sahihi.
 
Safi saaaan ukisikia polisi zero ndio hao hata km sijasoma sheria nisingekuwa na akil hizo za kuingia mpakan mwa watu bila kibal kwenda kuwakamata
 
askari wetu hamna kitu wanajua yani ni tatizo la mfumo kuingizana kwa baba kanituma wapo wapo tu haishangazi wakifanya makosa makubwa kama hayo.
hata movie hawaoni hahaha unaingiaje nchi nyingine kwa namna hiyo ndo mana risasi wanapiga 10 inafika mwilini 1
 
PGO, PGO Kuhusu mtuhumiwa akikimbilia nchi jirani inasemaje?

Naomba kazi nikafundishe PGO kama building capacity kwa jeshi letu afadhali.
 
Hizi njaa zitawamaliza polisi. Wengine watwangwa risasi na Hamza wakitaka kumpora, wengine wamejisahau kama wamevuka mpaka wako nchi ya watu wakiwa mbioni kumpora mtu mali zake.
 
Bodaboda alistiriwa vizuri na Wamalawi, lakini wananzengo wakaambulia kipigo. Kwa nini Wamalawi hawakumkabidhi mhalifu wao wakaamua kuwashushia kipondo vijana wetu? Kwa nini isiwe vinginevyo? PGO haikusomwa? Hii inatafakarisha sana.
 
Back
Top Bottom