Songea mbona haibadiliki? Kuna tatizo gani na mmekuwa na Mawaziri toka miaka ya 1960?

Airfryer

JF-Expert Member
Sep 17, 2021
430
1,032
Nimefika mkoa wa Ruvuma hapa mjini Songea baada ya miaka 18 tangu mwaka 2004, sioni mambo mapya kabisa wala ukuaji wa mji.

Hapa mjini naona majengo ni yale yale tu zaidi majengo kidogo sana yameongezeka kama pale opposite na Bank ya NMB zamani tulisema ni eneo la TANESCO. Kitu gani kinazuia majengo marefu hapa Songea mjini?

Huu mji kwa maendeleo ya vitu naona ni negative growth hasa infrastructure, zaidi ya miaka 18 niliyoondoka huku no changes!

Boda boda zipo nyingi sana hapa mjini tofauti na wakati huo nilipoondoka, sijajua watu wanatembea kwa umakini kiasi gani maana boda boda na watu ni kama idadi sawa au ngoma droo hapa mjini.

Soko la majengo kule zamani tuliita mitumbani hakuna mabadiliko makubwa sana zaidi ya bara bara za hapa na pale lakini wakati huo kulikuwa na lami yenye mashimo mashimo.

Mjini hakuna barabara za maana zaidi ya barabara itokayo bombambili mpaka Mbinga huko. Mji haujapanuka kabisa, Unatembea nusu saa tu umemaliza, hakuna sehemu za kuvutia na sehemu za mitoko zaidi ya bar.

Songea ukisema leo natoka ni kwenda bar, hakuna amsha amsha niliyoiona hapa Songea mjini.

Wazoefu wa miji, huu mji una tatizo gani?

Nilipita Njombe imebadilika sana sana tofauti na Njombe ile ya miaka 18 iliyopita. Hii ni Songea mjini lakini ni kama upo kwenye wilaya za ndani ndani huko za baadhi ya mikoa.

Soko la hapa Songea Mjini hata silielewi vizuri ni kasoko kadogo sana na kamejibana sana, kwanini wasiliamishe soko hilo?!

Kulikuwa na kampeni za kujenga masoko na stand wakati wa JPM, sijajua kwanini waliamua kuacha soko la mtindo huu.

Kuna stand mpya lakini haivutii kabisa kabisa zaidi ya kuweka lami, hakuna jengo kubwa la maana la abiria kwenye stand mpya.

Wamejenga stand mpya mbele ya msamala ukitokea mjini lakini bado wamefeli vibaya sana ni kama kituo cha daladala hivi.

Bar zipo zipo sana labda ndio sehemu ya starehe lakini hazina quality inayotakiwa kwa watu wala bata na matanuzi.

Mikoa hii ya kusini kuna tatizo kama hata stand mikoa walipata nao pesa za mgao wamejenga stand nzuri na za kisasa sana.

Kwa hiyo Songea hata ukapeleka mabilioni ya pesa za Serikali bado huu mji unalala usingizi tu, Kwa miaka 18 niliyotoka nimesikitika sana.

Jumatatu naelekea Lindi, nipo mapumzikoni hivyo natembea tembea kwenye hii mikoa nilianzia safari Dodoma.
 
Unaenda Lindi? Bora ughairi.

Mi ndio nipo hapa same kama wewe nimekuja kuzurura. Aisee. Nilikua nimejiandaa kwamba Lindi pakiwaki ila nimekuta pakiwaki zaidi tena na tena.

Nilipanga nikae 2 days niende N'twara sahivi nipo kwenye gari nasepa. Ngoja nikaone iyo Mtwara na Masasi.

Tukirudi kwenye mada: Songea tatizo ipo mbali na kila mkoa aisee. Imejitenga kinoma. Imagine Songea to Njombe.
 
Unaenda Lindi? Bora ughairi.

Mi ndio nipo hapa same kama wewe nimekuja kuzurura. Aisee. Nilikua nimejiandaa kwamba Lindi pakiwaki ila nimekuta pakiwaki zaidi tena na tena.

Nilipanga nikae 2 days niende N'twara sahivi nipo kwenye gari nasepa. Ngoja nikaone iyo Mtwara na Masasi.

Tukirudi kwenye mada: Songea tatizo ipo mbali na kila mkoa aisee. Imejitenga kinoma. Imagine Songea to Njombe.
songea-nombe ni parefu sana aisee sitaki hata kukumbuka kile kipande
 
Siyo Songea tu ni mkoa mzima wa RUVUMA.

Nimetembea Njombe, Kahama na miji mingine kadhaa ya kanda ya ziwa lakini hauwezi kufananisha na Songea.
Mkoa wa Ruvuma hasa mji wa Songea Kuna mambo hayapo sawa.

1. Wananchi wengi wa Ruvuma hawakupendi kwao. Mngoni au mmatengo akifanikiwa huko kurudi kwao ni ndoto na hukana kabisa kuwa yeye siyo wa Mbinga, Songea au Tunduru(UKWELI MCHUNGU). Hili suala udhoofisha uwekezaji wa wazawa wenye kipato kwenye shughuri za kilimo, uvuvi na misitu ambazo ndiyo shughuri KUU za uchumi.

2. Mkoa wa Ruvuma umechelewa sana kufunguliwa kimiundo mbinu hasa Ile ya usafirishaji, Ruvuma Ina deposit kubwa sana ya makaa ya mawe na Chuma, Lakini Bado ni ngumu sana utajiri huo kufika, kuvunwa na kupelekwa sokoni. Kabla ya miaka hamsini ya uhuru tulitegemea kungekuwepo na reli hata chakavu kutoka bandari ya Mbamba bay impaka bandari ya Mtwara. Hii ingeifanya Songea kuwa mji mkubwa sana kusini mwa Tanzania, kutokana na muingiliano wa watu na biashara.
 
Nimefika mkoa wa Ruvuma hapa mjini Songea baada ya miaka 18 tangu mwaka 2004,Sioni mambo mapya kabisa wala Ukuaji wa mji

Hapa mjini naona majengo ni yale yale tu zaidi majengo kidogo sana yameongezeka kama pale opposite na Bank ya NMB zamani tulisema ni eneo la Tanesco

Kitu gani kinazuia majengo marefu hapa Songea mjini?

Huu mji kwa Maendeleo ya vitu naona ni negative growth hasa infrastructure, Zaidi ya miaka 18 niliondoka huku no changes

Boda boda zipo nyingi sana hapa mjini tofauti na wakati huo nilipoondoka, Sijajua watu wanatembea kwa umakini kiasi gani maana boda boda na watu ni kama idadi sawa au ngoma ndroo hapa mjini

Soko la majengo kule zamani tuliita mitumbani hakuna mabadiliko makubwa sana zaidi ya bara bara za hapa na pale lakini wakati huo kulikuwa na lami yenye mashimo mashimo

Mjini hakuna barabara za maana zaidi ya barabara itokayo bombambili mpaka Mbinga huko

Mji haujapanuka kabisa, Unatembea nusu saa tu umemaliza, Hakuna sehemu za kuvutia na sehemu za mitoko zaidi ya Bar

Songea ukisema Leo natoka ni kwenda Bar, Hakuna amsha amsha niliyoiona hapa Songea mjini

Wazoefu wa miji, Huu mji una tatizo gani?

Nilipita Njombe imebadilika sana sana tofauti na Njombe ile ya miaka 18 iliyopita

Hii ni Songea mjini lakini ni kama upo kwenye wilaya za ndani ndani huko za baadhi ya mikoa

Soko la hapa Songea mjini hata silielewi vizuri ni kasoko kadogo sana sana na kamejibana sana sana, Kwanini wasiliamishe soko hilo

Kulikuwa na kampeni za kujenga masoko na stand wakati wa JPM, Sijajua kwanini waliamua kuacha soko la Mtindo huu

Kuna Stand mpya lakini haivutii kabisa kabisa zaidi ya kuweka lami, Hakuna jengo kubwa la maana la abiria kwenye stand mpya

Wamejenga stand mpya mbele ya msamala ukitokea mjini lakini bado wamefeli vibaya sana ni kama kituo cha dala dala hivi

Bar zipo zipo sana labda ndio sehemu ya starehe lakini hazina quality inayotakiwa kwa watu wala bata na matanuzi

Mikoa hii ya kusini kuna tatizo kama hata stand mikoa walipata nao pesa za mgao Wamejenga stand nzuri na za kisasa sana

Kwa hiyo Songea hata ukapeleka mabilioni ya pesa za Serikali bado huu mji unalala usingizi tu, Kwa miaka 18 niliyotoka nimesikitika sana sana

Jumatatu naelekea Lindi Nipo mapumzikoni hivyo natembea tembea kwenye hii mikoa nilianzia safari Dodoma


Mods badilini Title ni haibadiliki
Pichaaaaaa ziko wapi mkuu weka picha picha watu tunapenda picha tuonyeshe palivyo tuone
 
Kifupi kama umetokea dar huko kwingine kote ni vijijini mwaka Jana nilienda Mbeya Dec nikiamni nitaenjoy aisee nilichoka anyway kitu pekee nilifurahia ni upishi mzuri sana wa kitimoto nje ya hapo hakuna kitu
Shida ndio inaanza maeneo ya kutoka na Familia kula upepo hakuna kabisa Songea

Mbeya Sijajua kama kumebadilika huko Nilitoka mwaka 2016 nina miaka sita sasa

Mbeya hakuna mipango miji, Watu wamejenga hovyo hovyo tu hakijulikani ni njia ya gari au ya miguu mtaani

Mbeya ni centre ya uchafu
 
Umeponda hakuna maendeleo.Lakini umekubali kuna stend mpya nk safi.
Mkuu stand kama kituo cha Makumbusho au pale mawasiliano Dar es Salaam, Kumbuka hiyo ni centre ya mkoa mkuu

Na ni mkoa una Mawaziri kila awamu ya uongozi tangu uhuru

Mpaka sasa wana huyo Jenista Mhagama na yule Jamaa mfupi mfupi Ndumbaru Waziri wa katiba kabla alikuwa utalii
 
Siyo Songea tu ni mkoa mzima wa RUVUMA.

Nimetembea Njombe, Kahama na miji mingine kadhaa ya kanda ya ziwa lakini hauwezi kufananisha na Songea.
Mkoa wa Ruvuma hasa mji wa Songea Kuna mambo hayapo sawa.
1. Wananchi wengi wa Ruvuma hawakupendi kwao. Mngoni au mmatengo akifanikiwa huko kurudi kwao ni ndoto na hukana kabisa kuwa yeye siyo wa Mbinga, Songea au Tunduru(UKWELI MCHUNGU). Hili suala udhoofisha uwekezaji wa wazawa wenye kipato kwenye shughuri za kilimo, uvuvi na misitu ambazo ndiyo shughuri KUU za uchumi.

2. Mkoa wa Ruvuma umechelewa sana kufunguliwa kimiundo mbinu hasa Ile ya usafirishaji, Ruvuma Ina deposit kubwa sana ya makaa ya mawe na Chuma, Lakini Bado ni ngumu sana utajiri huo kufika, kuvunwa na kupelekwa sokoni. Kabla ya miaka hamsini ya uhuru tulitegemea kungekuwepo na reli hata chakavu kutoka bandari ya Mbamba bay impaka bandari ya Mtwara. Hii ingeifanya Songea kuwa mji mkubwa sana kusini mwa Tanzania, kutokana na muingiliano wa watu na biashara.
Lakin mbona NBS inautaja kuwa top five ya mikoa tajiri nchini kwa GDP kuzidi mikoa maarufu kama Kilimanjaro, kagera nk

NBS inataja mkoa wa Ruvuma kama mkoa wa nane nchini kwa maisha bora sasa sijui wanatumia vigezo vip

Sent from my SM-A032F using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom