Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 269,633
- 697,782
Sehemu ya pili muhimu imeshapita. Maamuzi yaliyotolewa na kamati kuu. Sakata lilianzia pale mazungumzo binafsi yaliyovujishwa. Zikafuatia tuhuma. Kishapo barua za kulalamika na hatimaye kuitwa kwenye kamati ya maadili.
Mpaka hapo walikuwa pamoja. Walikuwa wamoja, lakini wakaanza kuachana siku ya tukio. Huyu mmoja akatii na kuwahi. Hawa wawili wakawa wanasuasua. Pengine kuna mmoja alikuwa anambembeleza mwingine. Itajulikana tu
Watoa maamuzi kidogo wakajiongeza. Wakaona tukiwaacha hawa wakawa wamoja watatusumbua sana. Sasa tufanyeje!? TUWATAWANYE. Waache waingie mlango mmoja lakini tuwafanye kila mmoja atoke na mlango wake. KWISHA HABARI YAO!
Mmoja akaomba msamaha kwa maandishi. Mmoja akapewa KARIPIO kali. Mmoja akatimuliwa.
Chungu hakiinjikwi na figa moja ama mawili, ni matatu.
Moja, ni binafsi haina majuto. Haina shirika. Mbili, ina ukinzani. Inaweza kuleta lawama na moja.
Tatu, ni wingi. Ni kikowa. Maamuzi si thabiti tena na majuto huwa mengi.
Wametawanywa. Wakatawanyika. Sasa kila mtu na lwake. Tunaambiwa kwenye misahafu: Siku ya mwisho watakutwa wawili kondeni. Mmoja atatwaliwa, mmoja ataachwa.
Maamuzi na aina za adhabu, vimewatengenisha, vimewanyamazisha na pengine vimewafarakanisha!
SOMO MUHIMU LA MAISHA
Katika maisha kuwa wewe. Usimtegemee mtu, usitegemee maamuzi ya wengine. Kuwa na maamuzi binafsi kwakuwa haya pekee ndio utakayoweza kuyatetea na kuyasimamia. Usiwe bendera fuata upepo.
Usiyumbishwe. Usikubali wengine waamue badala yako. Usishawishike na kushawishiwa.
Kwanza kuwa na misimamo binafsi kabla hujakubali maamuzi na misimamo ya kikoa.
Hili litakusaidia sana shida itakapotokea mbeleni. Hapo ndio utakapoona rangi halisi za watu. Ila kama ulishafanya maamuzi binafsi hutaumia wala kuteseka sana.
Jambo la kikoa linapofanikiwa na kutimia kamwe hatuwezi kuwaza upande wa pili.
Lakini jambo hilo linapogeuka kuwa batili na mambo kuharibika. USALITI huanzia hapo.
Si kila mtu ana kifua kama ulichonacho wewe. Si kila mtu ana uwezo wa kuhimili pressure kama ulivyo wewe.
Si kila mtu ana uwezo wa kusimania maamuzi kama ulivyo wewe. Wengine wakitikiswa kidogo tu wanafunguka. Wengine wakifinywa kidogo tu hawabakishi kitu
Kuwa wewe! Baki wewe! Kama hujanielewa mrejee yule aliyesema:
I HAVE FAMILY TO FEED NOT A PUBLIC TO IMPRESS.
MSALITI...
USALITI...
Jr™️
Mpaka hapo walikuwa pamoja. Walikuwa wamoja, lakini wakaanza kuachana siku ya tukio. Huyu mmoja akatii na kuwahi. Hawa wawili wakawa wanasuasua. Pengine kuna mmoja alikuwa anambembeleza mwingine. Itajulikana tu
Watoa maamuzi kidogo wakajiongeza. Wakaona tukiwaacha hawa wakawa wamoja watatusumbua sana. Sasa tufanyeje!? TUWATAWANYE. Waache waingie mlango mmoja lakini tuwafanye kila mmoja atoke na mlango wake. KWISHA HABARI YAO!
Mmoja akaomba msamaha kwa maandishi. Mmoja akapewa KARIPIO kali. Mmoja akatimuliwa.
Chungu hakiinjikwi na figa moja ama mawili, ni matatu.
Moja, ni binafsi haina majuto. Haina shirika. Mbili, ina ukinzani. Inaweza kuleta lawama na moja.
Tatu, ni wingi. Ni kikowa. Maamuzi si thabiti tena na majuto huwa mengi.
Wametawanywa. Wakatawanyika. Sasa kila mtu na lwake. Tunaambiwa kwenye misahafu: Siku ya mwisho watakutwa wawili kondeni. Mmoja atatwaliwa, mmoja ataachwa.
Maamuzi na aina za adhabu, vimewatengenisha, vimewanyamazisha na pengine vimewafarakanisha!
SOMO MUHIMU LA MAISHA
Katika maisha kuwa wewe. Usimtegemee mtu, usitegemee maamuzi ya wengine. Kuwa na maamuzi binafsi kwakuwa haya pekee ndio utakayoweza kuyatetea na kuyasimamia. Usiwe bendera fuata upepo.
Usiyumbishwe. Usikubali wengine waamue badala yako. Usishawishike na kushawishiwa.
Kwanza kuwa na misimamo binafsi kabla hujakubali maamuzi na misimamo ya kikoa.
Hili litakusaidia sana shida itakapotokea mbeleni. Hapo ndio utakapoona rangi halisi za watu. Ila kama ulishafanya maamuzi binafsi hutaumia wala kuteseka sana.
Jambo la kikoa linapofanikiwa na kutimia kamwe hatuwezi kuwaza upande wa pili.
Lakini jambo hilo linapogeuka kuwa batili na mambo kuharibika. USALITI huanzia hapo.
Si kila mtu ana kifua kama ulichonacho wewe. Si kila mtu ana uwezo wa kuhimili pressure kama ulivyo wewe.
Si kila mtu ana uwezo wa kusimania maamuzi kama ulivyo wewe. Wengine wakitikiswa kidogo tu wanafunguka. Wengine wakifinywa kidogo tu hawabakishi kitu
Kuwa wewe! Baki wewe! Kama hujanielewa mrejee yule aliyesema:
I HAVE FAMILY TO FEED NOT A PUBLIC TO IMPRESS.
MSALITI...
USALITI...
Jr™️