KERO Somo la Pharmacognosy Mwaka wa 3 Chuo cha Kampala (KIUT), mhusika anaweka ‘ugumu’ ili tufeli, ‘ukimtoa’ unafauli

KERO Somo la Pharmacognosy Mwaka wa 3 Chuo cha Kampala (KIUT), mhusika anaweka ‘ugumu’ ili tufeli, ‘ukimtoa’ unafauli

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
A

Anonymous

Guest
Mimi Mwanafunzi wa Kampala (KIUT), Kozi ya Pharmacy, kuna jambo linatukera sana, kuna tabia ya Walimu kukomoa Wanafunzi, kutuwekea mazingira magumu ya kufaulu mtihani, na njia pekee ya kutoboa hapo ni “kunyoosha mkono uwe mrefu” jambo ambalo linatushinda Wanafunzi wengi, hatuna uwezo huo ikifika mpaka Shilingi 200,000 inatuumiza sanaa.

Mtu anayehusika anatuambia tukitoa mpunga hakuwekei ‘sup’ japo anafanya indirect na kwa msisitizo anasema ukipata sup yake hauwezi kuchomoa kwa kufanya mtihani, hii ndiyo kauli yake hata darasani keshawahi kutuambia, kwahiyo ni kama vitisho anatufanyia ili tutoe tu kiasi hicho cha hela.

Pia ukijulikana unashtaki kwa uwongozi wa juu akikushikilia ndiyo mtihani wake sahau kufaulu kabisa hata uki-carry or ukapata sup, ni kama anakwambia ku-graduate wewe itakuwa ngumu.

Somo husika ni Pharmacognosy Mwaka wa Tatu na pia huwa hata utungaji wake wa mtihani anatuekea mazingira magumu hata kwenye mtihani ili kuchukulia advantage ya kutoa hiyo pesa.
 
Waziri anayehusika na elimu ya juu, na timu ya uchunguzi kutoka wizarani waingilie kati na kuchunguza tatizo hili kabla undergraduate hawa hawajaathirika zaidi.
 
Serikali inatakiwa iamke kutoka usingizini ili itafute mwarobaini wa kuwadhibiti wakufunzi wa vyuo vikuu na vile vya kati, waliojigeuza miungu watu. Huu upumbavu huwezi kuukuta kwenye elimu ya msingi na sekondari ambako kuna NECTA.

Huku juu ndiyo madudu yametawala miaka nenda na hakuna hatua inayochokuliwa. Elimu ya watoto wetu imeachwa kuwa chini ya wakufunzi ambao baadhi yao wanawadhulumu watoto wa kike kingono, na wengine ndiyo hawa wanachukua rushwa ya fedha pasipokuwa na hofu yoyote ile.
 
TAKUKURU ilikuwa sehemu sahihi ya kumlambisha pesa za moto.
Hapa sijui kama mtaweza kupata ufumbuzi.
Tatizo Uhuru na mamlaka wanayopewa waalimu wa elimu za ngazi za juu.
Waafrika ukiwapa nguvu au mamlaka hayo umemkabidhi nyani shamba la mahindi. Abuse of power.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom