Somo la kijinga kutoka kwa mjinga kwenda kwa wajinga!

Mbona panya ni chakula kizuri,niwewe tu hutaki kuijadili ID yangu karibu sana
Mmawia na wamawia wote nawapendea kwa kuwa social sana. Nabaki nacheka.....hasira tupa kule

Ningekuwa bar tayari ushaletewa windhoek yako
 
Last edited by a moderator:
Mmawia na wamawia wote nawapendea kwa kuwa social sana. Nabaki nacheka.....hasira tupa kule

Ningekuwa bar tayari ushaletewa windhoek yako

Ungenambia castle lager bariiiidiiiiiii,ninge kupa like kuuubwa
 
Last edited by a moderator:
Mwaka huu wa uchaguzi ni wa kijinga sana.

Ni mwaka wa wajinga kuambiana ujinga na kukubaliana katika ujinga.

Mbaya zaidi wajinga hawakai kimya kwa kuwa werevu hawataki kuwaambia wajinga kama wanafanya ujinga kwa kufanya ujinga.

kuna mjinga mmoja alifanya ujinga akidhani werevu na wajinga wote ni wajinga.

kuna werevu wakajitahidi kuwaeleza wajinga ingawa walieleza kijinga kuwa kuna mjinga alifanya ujinga kijinga sana.

Basi werevu na wajinga wakaamka kwa hamaki na kujidai kukataa ujinga na kulazimisha mjinga ajione mjinga na kusema huu ulikuwa ujinga wa wajinga wenzangu lakini sitaki kuuelezea sana kwani wajinga hamtakiwi kuujua ujinga huu na mjinga mwengine huku akifikiria mjinga mwenzake akiondoka ataendelea kuwafanya wajinga waendelee kuwa wajinga.

Kumbe yule aliyeonekana mjinga alijanjaruka na kuamua kuwa mwerevu hata kama ni kijinga.

Huyu mjinga mwingine alihisi mjinga mwenzake bado ataendeleza ujinga waliokubaliana kumbe mwenzake alishatoka kwenye ujinga na kuamua kuwa mjanja.

Wajinga na werevu walikuwa wakiangalia tu michezo ya kijinga inayoendelea huku wakipiga kelele za kiwerevu.

kumbe kwenye group la waliodhaniwa kuwa werevu kuna wajinga wengi waliokuwa wakicheza na akili za wajinga na werevu.

Ujinga ukaendelea mpaka 2015 mpaka pale mjinga na mjanja walipofanyiana ujinga.

Ebo...! Katika kundi la wale waliodhaniwa kuwa werevu pakaibuka mjinga mmoja au wawili hivi wakaamua kukubaliana na mjinga ili aje kuendeleza ujinga kwenye Taifa la werevu,wajanja na wajinga.

He...mjinga huyu akaamua kumpaisha mjinga mzoefu ili awasimamie werevu,wajanja na wajinga katika kutupeleka kwenye nchi ya kijinga.

mbaya zaidi kuna wajinga wanataka kukubaliana na ujinga kisa mjinga kazidiwa kete na mjanja.Hapa mwerevu ameshtuka sana na kamwe hataki kuona wajinga wakiendelea kufanya ujinga na wajanja wakiendeleza ujanja!

Kazi ya mwerevu itakuwa moja tu mwaka huu...kukataa ujinga ushike nafasi.

werevu wawe tayari kuukubali ujanja kwa mara nyingine kuliko ujinga!!

Hili somo ni gumu sana kwa mjinga,mwerevu na mjanja.

Tunasubiri mtihani wa mwisho ambapo mwerevu atakuwa namba moja akifuatiwa na mjanja(huyu ataigiliza kwa mweravu) na mjinga atashika mkia tu na ujinga wake.


KWA HISANI YA MTU WA TANZANIA!
Nimependa ushauri huu!! .
.
WANA CCM NISIKILIZENI..!!
Nina ushauri kwa wana CCM wenzangu; Lowasa kuhamia CHADEMA msipaniki. Kama kweli tulimaanisha kuwa hafai, ana uchu wa madaraka, alikiuka kanuni na maadili ya chama, ni mwizi na tena ni fisadi basi inabidi tushangilie kuondoka kwake, kwani kuvuja kwa pakacha sio ndio nafuu ya mchukuzi? Ila kama tulimkata kwa maslahi ya watu wachache na ikiwa tulitumia akili ndogo kulikata jina lake basi itabidi tujilaumu wenyewe kwa lolote tusilolitarajia litakalotokea.
Na tukiendelea kutumia akili ndogo za kudhani tutashinda kwa "magoli ya mikono", basi tunakwenda na maji mchana kweupe!
.
Tukijidanganya kuwa matusi, kejeli, mipasho, maneno ya kwenye kanga na nyimbo za Komba kwamba zitabadilisha huu upepo, pia tutajikuta tunakuwa chama cha upinzani bila hata kujiandaa kisaikolojia. Mwana CCM utakuwa unajichanganya kuushambulia uamuzi wa Lowasa kuhamia CHADEMA kwa sababu kimsingi CCM yetu ilishabariki vijana kadhaa wamshambulie majukwaani ili aonekane hafai na hao vijana wakazawadiwa vyeo. Mtu tuliemuona hafai kwetu inatuuma nini akiondoka kwetu? Ukioa mke kisha ukamtuhumu mbele za watu kuwa ni mzinzi na mshirikina; kisha mkaachana na akaolewa na mume mwingine, unaanzaje kuhangaika nae tena huko alikoenda? Tuwaache wapiga kura waamue kama ni sisi CCM ama UKAWA. .
.
Hata Mh. Mwenyekiti JK alishasema kila mtu ana haki kuongoza hii nchi; tunategemea kushinda lakini haitakuwa ajabu UKAWA wakitwaa madaraka kutokana na makosa yetu kimkakati. Wana CCM tusipaniki, kukomaa kisiasa ni pamoja na kuhimili na kukubali usichotarajia!
Wenu,
Mfurukutwa wa Shina.
😂😂👆
 
Nimependa ushauri huu!! .
.
WANA CCM NISIKILIZENI..!!
Nina ushauri kwa wana CCM wenzangu; Lowasa kuhamia CHADEMA msipaniki. Kama kweli tulimaanisha kuwa hafai, ana uchu wa madaraka, alikiuka kanuni na maadili ya chama, ni mwizi na tena ni fisadi basi inabidi tushangilie kuondoka kwake, kwani kuvuja kwa pakacha sio ndio nafuu ya mchukuzi? Ila kama tulimkata kwa maslahi ya watu wachache na ikiwa tulitumia akili ndogo kulikata jina lake basi itabidi tujilaumu wenyewe kwa lolote tusilolitarajia litakalotokea.
Na tukiendelea kutumia akili ndogo za kudhani tutashinda kwa "magoli ya mikono", basi tunakwenda na maji mchana kweupe!
.
Tukijidanganya kuwa matusi, kejeli, mipasho, maneno ya kwenye kanga na nyimbo za Komba kwamba zitabadilisha huu upepo, pia tutajikuta tunakuwa chama cha upinzani bila hata kujiandaa kisaikolojia. Mwana CCM utakuwa unajichanganya kuushambulia uamuzi wa Lowasa kuhamia CHADEMA kwa sababu kimsingi CCM yetu ilishabariki vijana kadhaa wamshambulie majukwaani ili aonekane hafai na hao vijana wakazawadiwa vyeo. Mtu tuliemuona hafai kwetu inatuuma nini akiondoka kwetu? Ukioa mke kisha ukamtuhumu mbele za watu kuwa ni mzinzi na mshirikina; kisha mkaachana na akaolewa na mume mwingine, unaanzaje kuhangaika nae tena huko alikoenda? Tuwaache wapiga kura waamue kama ni sisi CCM ama UKAWA. .
.
Hata Mh. Mwenyekiti JK alishasema kila mtu ana haki kuongoza hii nchi; tunategemea kushinda lakini haitakuwa ajabu UKAWA wakitwaa madaraka kutokana na makosa yetu kimkakati. Wana CCM tusipaniki, kukomaa kisiasa ni pamoja na kuhimili na kukubali usichotarajia!
Wenu,
Mfurukutwa wa Shina.
😂😂👆

CCM haiwezi kupanic kwa kuwa walishajua mazungumzo ya lowassa na Mbowe siku nyingi!
 
Back
Top Bottom