Yericko Nyerere
JF-Expert Member
- Dec 22, 2010
- 16,977
- 20,243
Nichukue fursa hii kumfunza kijana Nape katiba ya chama kilichomlea tangu azaliwe na kinachomuweka mjini leo hii:
Bahati mbaya sana kwa ccm, siku ya kufa nyani miti yote huteleza,
CCM ipo HOI bin Taabani na inahitaji msaada wa hali na mali kuurejelea uzima.
Lakini nani wa kuleta tumaini la uhai wa ccm? Hili ndilo swali kuu walilojiuliza mwezi jana walipokutana pale Dodoma wahafidhina wa chama hiki mufilisi.
Ilikuwa ni kazi ngumu hasa kumpata msemaji wao kwani ilihitaji mtu makini na mwenye weledi si wa makengeza.
Hili linatokana na uwazi kuwa mtu huyo ndie atakuwa msemaji pia kwenye mitandao ya kijamii inayoaminika kuwa vijana wengi wazalendo na wasomi wa elimu za juu wameweka vituo vya ukombozi wa nchi yao dhidi ya mkoloni mweusi ccm kwenye mitandao hii.
Ajabu na nikweli, nafasi hiyo ilirejea kwa yuleyule ambae siku za nyuma alikimbia vita ya kisiasa mitandaoni na si mwingine ni NAPE NNAUYE
Kijana huyu aliye mjuvi wa siasa angavu ilihali anaombwe kichwani, amekuja na staili mpya ambayo inamfanya awe kituko mbele ya tuzijuazo siasa za kisasa na siasa za maji taka.
Kwa hoja na matamko yake anayo iwakilisha ccm, Niseme wazi Nape Haijui Katiba ya CCM.
Najiuliza huyu kweli kama haijui katiba ya Chama chake je, ataijua ILANI ya chama hicho? Je ataijua Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania?
Nimeonelea busara nianze kwa kumfunza kitu kimoja kimoja, na nimeanza na vifungu vichache muhimu vya katiba ya CCM ambavyo ndivyo vilivyosababisha nitambue kuwa kijana huyu hajui chochote ndani ya chama chake, si katiba wala ilani za chama hicho.
Naaaam naanza hivi:
Soma Katiba ya CCM toleo la mwaka 2010. Ibara ya 13. kifungu (1).
Inahusu WANACHAMA NA VIONGOZI.
Uanachama utakwisha kwa:
(a) Kufariki.
(b) Kujiuzulu mwenyewe.
(c) Kuachishwa kwa mujibu wa Katiba.
(d) Kufukuzwa kwa mujibu wa Katiba.
(e) Kutotimiza masharti ya uanachama.
(f) Kujiunga na Chama kingine chochote cha siasa.
(2) Mwanachama ambaye uanachama wake unakwisha kwa sababu yoyote ile hatarudishiwa kiingilio alichokitoa, ada aliyotoa wala michango yoyote aliyoitoa.
Sasa nikufahamishe kuwa, Dr Slaa alijiunga na chama kingine cha siasa zaidi ya miaka 15 iliyopita (Nape ulikuwa hujamaliza hata darasa la saba)
Amekuwa mbunge wa kuchaguliwa kupitia chama kingine cha siasa (CHADEMA) kwa miongo kadhaa.
Leo hii Nape & co mnauliza kadi yake ya CCM?
1. Nape na wenzake mnaijua vema katiba ya CCM? wanaelewa masharti ya uanachama?
2. Ni kifungu gani cha katiba ya CCM kinachosema kuwa ili uanachama wa CCM ukome sharti mhusika arudishe kadi?
NB
Shukrani kwa FJM
Bahati mbaya sana kwa ccm, siku ya kufa nyani miti yote huteleza,
CCM ipo HOI bin Taabani na inahitaji msaada wa hali na mali kuurejelea uzima.
Lakini nani wa kuleta tumaini la uhai wa ccm? Hili ndilo swali kuu walilojiuliza mwezi jana walipokutana pale Dodoma wahafidhina wa chama hiki mufilisi.
Ilikuwa ni kazi ngumu hasa kumpata msemaji wao kwani ilihitaji mtu makini na mwenye weledi si wa makengeza.
Hili linatokana na uwazi kuwa mtu huyo ndie atakuwa msemaji pia kwenye mitandao ya kijamii inayoaminika kuwa vijana wengi wazalendo na wasomi wa elimu za juu wameweka vituo vya ukombozi wa nchi yao dhidi ya mkoloni mweusi ccm kwenye mitandao hii.
Ajabu na nikweli, nafasi hiyo ilirejea kwa yuleyule ambae siku za nyuma alikimbia vita ya kisiasa mitandaoni na si mwingine ni NAPE NNAUYE
Kijana huyu aliye mjuvi wa siasa angavu ilihali anaombwe kichwani, amekuja na staili mpya ambayo inamfanya awe kituko mbele ya tuzijuazo siasa za kisasa na siasa za maji taka.
Kwa hoja na matamko yake anayo iwakilisha ccm, Niseme wazi Nape Haijui Katiba ya CCM.
Najiuliza huyu kweli kama haijui katiba ya Chama chake je, ataijua ILANI ya chama hicho? Je ataijua Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania?
Nimeonelea busara nianze kwa kumfunza kitu kimoja kimoja, na nimeanza na vifungu vichache muhimu vya katiba ya CCM ambavyo ndivyo vilivyosababisha nitambue kuwa kijana huyu hajui chochote ndani ya chama chake, si katiba wala ilani za chama hicho.
Naaaam naanza hivi:
Soma Katiba ya CCM toleo la mwaka 2010. Ibara ya 13. kifungu (1).
Inahusu WANACHAMA NA VIONGOZI.
Uanachama utakwisha kwa:
(a) Kufariki.
(b) Kujiuzulu mwenyewe.
(c) Kuachishwa kwa mujibu wa Katiba.
(d) Kufukuzwa kwa mujibu wa Katiba.
(e) Kutotimiza masharti ya uanachama.
(f) Kujiunga na Chama kingine chochote cha siasa.
(2) Mwanachama ambaye uanachama wake unakwisha kwa sababu yoyote ile hatarudishiwa kiingilio alichokitoa, ada aliyotoa wala michango yoyote aliyoitoa.
Sasa nikufahamishe kuwa, Dr Slaa alijiunga na chama kingine cha siasa zaidi ya miaka 15 iliyopita (Nape ulikuwa hujamaliza hata darasa la saba)
Amekuwa mbunge wa kuchaguliwa kupitia chama kingine cha siasa (CHADEMA) kwa miongo kadhaa.
Leo hii Nape & co mnauliza kadi yake ya CCM?
1. Nape na wenzake mnaijua vema katiba ya CCM? wanaelewa masharti ya uanachama?
2. Ni kifungu gani cha katiba ya CCM kinachosema kuwa ili uanachama wa CCM ukome sharti mhusika arudishe kadi?
NB
Shukrani kwa FJM