Somo la 'Historia ya Tanzania' alilotaka Magufuli lasitishwa

Hayati Magufuli naona kaangukia pua tena

Somo la historia ya Tanzania lasitishwa

Katibu mkuu wizara ya elimu amesema syllabus hiyo imesitishwa haraka na haitafundishwa kokote.

Source ITV news

==============

Waziri wa elimu Prof. Ndalichako amesitisha maboresho ya mtaala wa somo historia ambao ulianzishwa na Magufuli. Mtaala huo wa somo la historia ungeanzisha kufundisha somo la historia kwa kiswahili tangu madarasa ya awali hadi chuo kikuu. Waziri Ndalichako ameagiza kuendelea kutumia mtaala wa zamani hadi mtaala mpya utakapoandaliwa kwa kushirikisha wadau.

Source: ITV

Sijui Magufuli anajisikiaje huko aliko kwa sababu maagizo yake yanatupiliwa mbali kila kukicha!
Kwani mnamkomoa au mnajikomoa wenyewe! Kuna mimtu milofa kweli😠!
 
Lingewasaidia vip vijana wetu kujikwamua kimaisha
Hili siyo swali la kuuliza hapa barazani...

Kila mtu anawajibu kuelewa na kuijua historia yake, ya nchi yake na ya chochote kinachomhusu...?

Swali la kujiuliza siyo hilo bali ni hili:

Ina maana tangu uhuru mpaka sasa watoto wetu na sisi tuliosoma miaka ile hatukuwa tunafundishwa hisoria ya nchi yetu..?

Jibu ni, HAPANA..

Tumesoma historia ya nchi yetu. Labda kama kuna mambo yalisahaulika au tumeyaona kuwa yanafaa kuingizwa ktk mtaala wa somo la historia, basi ni kiasi cha kurekebisha tu mitaala hiyo na siyo kuanzisha somo jipya ndani ya somo la historia lililopo ambalo linafundishwa kuanzia shule za msingi hadi chuo kikuu...
 
"Waziri Ndalichako ameagiza kuendelea kutumia mtaala wa zamani hadi mtaala mpya utakapoandaliwa kwa kushirikisha wadau"-Kumbe mtaala huo wa somo la historia ulikuwa unaandaliwa bila ya kushirikisha wadau?🤔🤔🤔

Walaaniwe madikteta popote walipo!
 
Kama wakija kulirudisha tena, wasifundishe kama historia bali liwe kama Filosofia...

Wachina wana somo lao mashuleni, laitwa Chinese philosophy ambapo kwa ngazi ya chuo kikuu watu hupata degree
 
Uwezo wako umefikia hapo, dadangu hawezi kuwa historia kwangu Leo hii, na sihitaji kwenda darasani ili kutambua huyu ni dadangu.
Bado nasimama pale pale, wewe umeisoma historia ya Mkwawa nambie imekusaidia nini ktk Maisha ya kila siku? Siamini Katika kusoma historia Kwa lazima, iachwe atakayehitaji akasome mwenyewe, siyo watu wote tukawe ma-histori teller
Kwanini huwez kumuoa Dada yako?!Nani kakuonesha kuwa kufanya hivyo ni vibaya?
Wachina wanatufundisha the past Chinese culture,inafundishwa kwenye vyuo vikuu vyetu,na hii ndiyo Historia!leo tunasoma kichina,pia kunfuu au karate inaonekana ndo ustaarabu😓😓,Startimes wanatutafsiria tamthiliya zinazoonesha kuwa Mwanaume ukioa unatakiwa kwenda kuishi nyumban kwa kina mwanamke(ukweni)na maisha yanaendelea-Wanafanya hivi ili kuua cultural values (history)yetu!

Ukitaka umtawale mtu futa kumbukumbu(historia) zake!

Mimi huwa natumia historia ili kujua mgonjwa atakufa au atapona!
Historia inaniambia mtu akianguka chooni huyo haponi,hapo ni kuandaa msiba tu🤣🤣

Uongozi na utawala waufanyao viongozi wa Leo wamekopi kutoka kwa viongozi wa miaka hiyo wakibadilisha tu baadhi ya vitu!Sasa visingeandikwa wangetoa wapi?!!binadamu tunazaliwa tunaukuta Mfumo wa maisha ambao hubaki historia pale unapokamilika!
Historia hurekodi matukio makubwa na ya muhimu tu!

Mungu atupe Maisha marefu ili tushuhudie Wachina wakitutawala Mara ya Tatu,Matukio mabaya ya kihistoria yasipokomeshwa Yana tabia ya kujirudia😔😔
 
" Lifutwe haraka sana na halitafundishwa popote" huu mstari kutoka kwa katibu umenifurahisha sana daah.
 
Hayati Magufuli naona kaangukia pua tena

Somo la historia ya Tanzania lasitishwa

Katibu mkuu wizara ya elimu amesema syllabus hiyo imesitishwa haraka na haitafundishwa kokote.

Source ITV news

==============

Waziri wa elimu Prof. Ndalichako amesitisha maboresho ya mtaala wa somo historia ambao ulianzishwa na Magufuli. Mtaala huo wa somo la historia ungeanzisha kufundisha somo la historia kwa kiswahili tangu madarasa ya awali hadi chuo kikuu. Waziri Ndalichako ameagiza kuendelea kutumia mtaala wa zamani hadi mtaala mpya utakapoandaliwa kwa kushirikisha wadau.

Source: ITV

Sijui Magufuli anajisikiaje huko aliko kwa sababu maagizo yake yanatupiliwa mbali kila kukicha!
Hiki ni kifurushi cha pinduapindua 🤣🤣🤣, acha tuinue nchi kwanza
 
Hayati Magufuli naona kaangukia pua tena

Somo la historia ya Tanzania lasitishwa

Katibu mkuu wizara ya elimu amesema syllabus hiyo imesitishwa haraka na haitafundishwa kokote.

Source ITV news

==============

Waziri wa elimu Prof. Ndalichako amesitisha maboresho ya mtaala wa somo historia ambao ulianzishwa na Magufuli. Mtaala huo wa somo la historia ungeanzisha kufundisha somo la historia kwa kiswahili tangu madarasa ya awali hadi chuo kikuu. Waziri Ndalichako ameagiza kuendelea kutumia mtaala wa zamani hadi mtaala mpya utakapoandaliwa kwa kushirikisha wadau.

Source: ITV

Sijui Magufuli anajisikiaje huko aliko kwa sababu maagizo yake yanatupiliwa mbali kila kukicha!
Waziri wa elimu Prof. Ndalichako,nilijua hili zoezi hutaliweza na huna uwezo wa kulifanya hata upewe miaka mitano.
 
Back
Top Bottom