Hero
JF-Expert Member
- Aug 20, 2010
- 3,932
- 2,832
Kwani mnamkomoa au mnajikomoa wenyewe! Kuna mimtu milofa kweli😠!Hayati Magufuli naona kaangukia pua tena
Somo la historia ya Tanzania lasitishwa
Katibu mkuu wizara ya elimu amesema syllabus hiyo imesitishwa haraka na haitafundishwa kokote.
Source ITV news
==============
Waziri wa elimu Prof. Ndalichako amesitisha maboresho ya mtaala wa somo historia ambao ulianzishwa na Magufuli. Mtaala huo wa somo la historia ungeanzisha kufundisha somo la historia kwa kiswahili tangu madarasa ya awali hadi chuo kikuu. Waziri Ndalichako ameagiza kuendelea kutumia mtaala wa zamani hadi mtaala mpya utakapoandaliwa kwa kushirikisha wadau.
Source: ITV
Sijui Magufuli anajisikiaje huko aliko kwa sababu maagizo yake yanatupiliwa mbali kila kukicha!