Somo kwa Wanandoa - inawahusu waliooa na walioolewa tu

kbm

JF-Expert Member
Oct 5, 2012
5,222
1,670
NDOA YENYE FURAHA HUDUMISHA UPENDO WA DHATI

Ndoa ni nini? Ndoa ni muungano wa mwanaume na mwanamke unaokubalika kiutamaduni na kidini ambao unatarajiwa kudumu, kuwapa haki sawa za kijinsia na kutosheleza majukumu mengine ya kijamii. Katika ndoa kuna uhalali wa watoto.

Pamoja na tafasiri hiyo ya ndoa, watu wengi siku hizi wamekuwa wakiishi maisha ya ndoa kama fasheni hali ambayo imekuwa ikishusha hadhi ya ndoa. Si jambo la ajabu kusikia ndoa iliyofungwa wiki moja iliyopita imevunjika baada ya wanandani hao kutwangana makonde.

Katika ndoa kuna matabaka mawili. Tabaka la kwanza ni kwa wanandoa kufurahia ndoa yao na tabaka la pili ni la wanandoa kuijutia ndoa yao. Hakika ndoa inaraha sana na nitendo la heshima mbele za Mungu.

Hivi ulishawahi kujiuliza ni kwa nini siku ya harusi wanandoa wote huwa na furaha? Na je, furaha hiyo baadaye hupotelea wapi? Hakuna mwanandoa yeyote ambaye huwaza kama siku moja yeye na mwenzi wake wanaweza kukorofishana na kutukanana matuzi mazito ambayo hugeuka kuwa sumu ndani ya ndoa yao.

Siku ya harusi kila mmoja huisubiri kwa shauku kubwa na kuona siku kama haziendi ili wanandoa hao wawe pamoja katika jahazi la ndoa ya maisha. Lakini mambo hubadirika kwa baadhi ya wanandoa pindi wanapoanza maisha ya pamoja. Kabla sijaendelea naomba kukuuliza wewe uliyendani ya ndoa, je ulishawahi kujiuliza ni kwanini furaha mliyokuwa nayo wakati hamjaoana leo hii haipo hivyo?

Kumbuka mara nyingi penzi linalotolewa wakati wa uchumba huwa lina mbinu nyingi za kusomana tabia na kila mmoja hupenda kuficha tambia yake mbaya aliyonayo. Ni suala gumu kigodo kwa wanandoa ambao kila mmoja amekulia katika malezi tofauti kukaa na kujenga tabia moja. Wakati watu wanapokuwa katika hatua ya uchumba hushindwa kusomana vizuri tabia zao kutokana na umbali walionao. Kwa sababu kila mmoja anakuwa kwao ama kwake hali ambayo hutoa muda mwingi wa kumkumbuka mpenzi wake.

( Ama hakika ndoa ni furaha, Kabula akitamka maneno ya ahadi mbele ya mashahidi kanisani huku taaaratibu akimuvisha pete ya ndoa mme wake mpendwa George Kayala tayari kwa kuanza safari ya maisha ya ndoa yeye raha teeeeele!) Kipindi hicho wachumba hao hutumiana jumbe fufi kupitia mitandao kama simu na email ili kila mmoja kuonyesha ni kwa jinsi gani anampenda mwanandani wake mtarajiwa. Wahusika hao hujitahidi kutumika maneno mazuri na yenye kuvutia hisia ya mahaba hali ambayo uzidi kuongeza penzi kwa pande zote mbili. Maneno hayo huongeza shauku kwa walengwa hao kuwa na shauku ya kuwa pamoja wakidhani kuwa siku zote mambo yatakuwa hivyo.

Kwa kipindi hicho wachumba hao huwa wanaelewana kwa kila jambo wanalopenda lifanyike. Utamu wa uchumba huo kama nilivyosema hapo awali hunogeshwa na umbali uliopo kati ya wahusika hao. Wakati mwingi mmoja wapo anapotakiwa na mwenzake wakutane sehumu wanayoona inafaa kwa ajili ya mazungumzo yao ya faragha hulazimika kuwadanganya wazazi wao ama ndugu zao wanaoishi nao kwamba wanaenda kwa jamaa zao na atachelewa kurudi.

Na pindi mazungumzo yao yanapoanza huku muda ukizidi kwenda wachumba hao hutamani muda urudi nyuma ili waendelee kuongea na kupeana habari za hapa na pale kuhusu maisha yao ya badae. Sasa shauku hiyo ya kuwa pamoja hupotelea wapi baada ya kuoana ambapo huwa kuna muda mrefu wa kuwa pamoja tofauti na kipindi kile walipokuwa wanaona muda unaenda na mazungumzo yao bado yanaendelea?

Nadhani utaungana na mimi kwamba kwa baadhi ya wanandoa mambo hayo hupotea pindi wanapoingia ndani ya ndoa kutokana na muda mwingi kuwa pamoja. Utakuta wanaongea masuala yao mpaka yanaisha. Na kisha wanalala. Siku zote mwanadamu hakosi kuwa na madhaifu maishani mwake. Kipindi hicho wanandoa hujikuta wapo katika wakati mugumu pindi mmoja wapo anapofanya kosa hata si kwa makusudi. Inawezekana akawa ni mama akawa mkorofi ama baba ama wote kwa pamoja.

Na hiyo hutokea kila mmoja kujiona anahaki ya kufanya atakavyo na hayupo tayari kukosolewa.
Ni imani yangu kuwa kila mwanandoa siku ya kufunga ndoa huwa kunaviapo ambavyo hutamkwa na wahusika wote. Kwamba watakuwa tayari kuishi katika maisha ya raha na shida, iwe magonjwa nk. Lakini mambo huwa sivyo pindi safari ya maisha ya ndoa yanapo anza.

SUMU YA MAISHA YA NDOA

Hakuna asiyefahamu kwamba asilimia kubwa ya vitu tunavyovitumia vina sumu. Lakini hatuoni madhara ya sumu hiyo kutokana na kufuata taratibu za matumizi na vitu tunavyovitumia. Mfano mzuri ni dawa ya panado ambayo mtu anapoumwa kichwa hutumia dawa hiyo ili kuondoa maumivu hayo. Na dawa hiyo huwa haitoi madhara yoyote. Lakini dawa hiyo ukinywa kinyume na masharti yake lazima madhara uyapate kama si kufa tambua utaugua zaidi. Nimetoa mfano huo ili unielewe vizuri kwamba na katika ndoa kuna mambo ambayo yasipofanyiwa kazi huleta madhara katika ndoa.
(Ndoa ni furaha mama huyu anamvisha pete ya ndoa mmewe huku akionyesha tabasamu kubwa akiashiria maisha yenye raha teeeeele, Picha kwa hisani ya mtandao).

Mambo hao kwanza kabisa ni heshima, upendo wa dhati, mawasiliano mazuri katika familia, kusaidiana na Uvumilivu. Haya ni mambo muhimu sana kwa wanandoa. Kumbuka kwamba wanandoa wanaokosa mambo hayo muhimu ndoa yao lazima iwe mashakani na ugomvi hauwezi kuisha kamwe. Kwa wanandoa upendo unapotawala ndani ya nyumba huifanya ndoa hiyo kuchanua kila mara na hiyo huambatana na uvumilivu.

Neno jingine ambalo wengi huliona kama halina maana ni SAMAHANI pindi mmoja wenu anapokosea. Inapotokea ukamkosea mwenzako jitahidi kuomba samahani badala ya kukaa kimya na ukifanya hivyo itaonekana unadharahu. Ukiyazingatia yote hayo ni lazima ndoa yako iwe na furaha siku zote. Kwa leo niishie hapa baada ya hapa nitakulete sababu za mwanamke kwenda nje ya ndoa, na kisha mwanaume naye kwenda nje ya ndoa. Nakaribisha maoni na ushauri juu ya yale uliyoyasoma hapo juu. Pia na wewe unaruhusiwa kutoa somo ama kufundisha jambo lolote ulilonalo kwa ajili ya faida ya sisi tusiojua.

Wataalamu wa Ndoa wanasema hivi!

Kuna wataalamu 600 wa masuala ya ndoa (marriage experts) walikaa pamoja kujadili misingi (fundamentals) muhimu ya ndoa ambayo wanandoa wakiifuata ndoa zao zitakuwa imara na zenye afya hadi kifo kitakapowatenganisha. Misingi hiyo ili imeinamia zaidi kwenye imani ya Kikristo, ingawa mtu yeyote bila kufuata dini yake anaweza kuifuata na bila shaka ndoa yake itakuwa ya tofauti.

Kuna mambo mengi sana muhimu ya kufanya katika ndoa ili ndoa iwe imara na yenye mafanikio, hawa wataalamu walichambua yale ya mambo msingi tu ambayo yakifuatwa basi vitu vingine muhimu katika ndoa inakuwa ndani yake. Tumeshayaongea sana haya mambo hapa kwenye blog hii inaweza kuonekana kama kurudia, hata hivyo kuna kitu muhimu na kipya unaweza kukipata hapa leo.

Je, ni Misingi ipi hiyo?

Kwanza - Kristo kuwa Kiongozi wa Ndoa
Ndoa ambayo inaendeleza, ongeza, imarisha na kufurahia mahusiano na Yesu Kristo itakuwa na picha kamili ya Yesu na kanisa. Kila mwanandoa atakuwa na uhusiano mzuri na Kristo na atajitahidi kufanana na Kristo na matokeo yake dhambi itakaa mbali na dhambi kukaa mbali basi upendo wa kweli wa kimungu huongoza ndoa. Ndoa yenye msingi wa Kristo huwa na maombi na maombi ni mawasiliano ya wanandoa na Mungu, hivyo kwa kuwa na connection kati ya Mungu na wanandoa, Mungu atakuwa anaipa stabilization ndoa yao kila wanapokutana na tatizo, shida au jaribu.

Unajua kuna siku shetani huwa anaamua kupaka matope (mavi) mmoja ya wanandoa ili asipendwe (unajisikia kutovutiwa na mwenzako), ni kwa maombi tu unaweza kuharibu kazi za aina hii za shetani si pesa, wala elimu wala ujanja. Kwenye ndoa kuna good times na bad times na Kristo huweza kuwapitisha wanandoa vizuri kama wanamtegemea yeye, hilo halina ubishi ni amini na kweli.

Pili - Upendo wa Kujitoa

Maisha ya binadamu ni safari ndefu, si sahihi kwamba siku zote ndoa itakuwa na mapenzi yaleyale ya motomoto, au kupendana kule kule kama mwanzo, kiwango cha mahaba kupanda tu graph kila iitwapo leo; si kweli, kutokana na kuwa na malezi tofauti na mambo mengine inawezekana ndoa kupita kwenye wakati mugumu sana, kuna stress, kuna kukata tamaa, kuna business kufilisika, na kuwa wakati tu inatokea mume na mke kila mmoja hampendi mwenzake bila sababu, hivi vyote vinahitaji watu wenye Upendo wa kujitoa ili kurudi kwenye mstari.

Katika ndoa conflict na disagreement hutokea bila upendo wa kujitoa basi ndoa haiwezi kufika popote Kwenye ndoa hakuna mtu perfect wote bado tuna tumia Learner driving license kwa maana kwamba tunaendelea kujifunza na kutoa efforts za kuhakikisha ndoa inakuwa na afya na inaendelea kudumu na kudumu na kudumu. Kuna utafiti ulifanywa kwa wanandoa waliopata talaka, asilimia 40 walisema wanatamani kurudi kwenye uhusiano wao wa kwanza, hii ni kuthibitisha kwamba wangekuwa na upendo wa kujitoa basi wasingeamua kuomba talaka zao kwani kuna watu ambao conflict kidogo tu, tuachane! Hawana dogo na wengine sasa kuoa na kuolewa ni kama shopping!

Tatu - Mawasiliano

Utafiti unaonesha kwamba watoto wadogo wa kike wamebarikiwa sana (talented) na uwezo wa kuongea na lugha kwa ujumla (linguistic), huweza kuongea haraka na mapema kuliko watoto wadogo wa kiume. Hiyo tabia huendelea hadi wanapokuwa watu wazima na kwa maana hiyo wanawake na wanaume lipokuja suala la kuongea na mawasiliano kwa ujumla kuna tofauti kubwa. Inajulikana kwamba wanawake huongea maneno kati 40,000 hadi 50,000 kwa siku wakati wenzao wanaume huongea maneno 15,000 hadi 25,000 kwa siku.

Hivyo basi wanawake ni viumbe wanaohitaji mwanaume kuuongea ili na yeye aongee hayo maneno yake, ndiyo maana kwa mfano kama umetoka kazini basi mwanamke anapenda sana umwambie mambo mbalimbali kama vile unafikiri kitu gani, nini kilitokea kazini, watoto wameshindaje, unajisikiaje kuhusu yeye mwanamke nk. Wakati huohuo wanaume hujisikia sawa tu hata asipoongea chochote akifika nyumbani kutoka kazini matokeo yake mke anakuwa bored na hayo ni mawasiliano mabovu. Wanaume kushindwa kuelezea hisia zao kwa wake zao ni kitu kinachowaumiza sana.

Panga muda maalumu kwa ajili ya maongezi ya maana na mke wako hata kwa kuwa na matembezi au outing. Hata hivyo wanawake wanapaswa kufahamu kwamba kuna wanaume ambao hawawezi kuwa kama wanavyotaka wao kwani ndivyo walivyo. Mume wako hataweza kukutimizia mahitaji yako yote kwani hakuna mwanaume duniani ambaye anaweza kumpa mwanamke vyote anavyohitaji, ndiyo maana hata wewe mwanamke mwenyewe hupo perfect mia kwa mia. Kumbuka
Unapowasiliana na mume au mke;
Badilisha kile ambacho kinaweza kubadilishwa
Elezea kile ambacho anaweza kukielewa
Fundisha kila ambacho anaweza kujifunza
Patanisha kile ambacho anaweza kukubaliana
Rudia kile ambacho anaweza kukiimarisha.

DALILI ZA NDOA INAYOKUFA

Jitahidi kuhakikisha unalinda moyo wako na moyo wa mpenzi wako; usije ukaupasua na kuuumiza.
Wanandoa wengi hujikuta wamefika mahali ambapo ndoa haiwezi kuwepo tena (talaka) na tatizo kubwa ni kwamba wengi hukaa bila kuchukua hatua zinazostahili (serious) wakati tatizo au mgogoro unapojitokeza ili kumaliza tatizo.

Kutoshughulikia vizuri tatizo lolote kwenye ndoa hupelekea Chuki, Uchungu, Kinyongo, Kuumia hisia na huweza kusababisha mwanandoa mmoja kujiondoa katika muungano wa kindoa uliopo (kuanza kuishi kivyake katika kufikiria na kutenda).

Zifuatazo ni dalili mbaya sana ambazo zinaonesha ndoa inayoelekea kwenye kifo

KUFIKIRIA MAISHA KIVYAKO BILA MKE AU MUME KUMUHUSISHA
Ukiona unaanza kufikiria uzuri wa maisha utakavyokuwa bila mwenzi wako kwa maana kwamba kuwa na yeye unaona asilimia mia moja anakulostisha, au hana maana kabisa ni dalili kwamba hiyo ndoa inaelekea kwenye kifo cha ghafla. Na kama unasongwa sana na mawazo kutaka kuishi mwenye au na mtu mwingine zaidi ya huyo uliye naye na kujiona utakuwa na amani zaidi basi unaelekea kubaya kwani inaonesha umeshapoteza nafasi yake ndani ya moyo wako na kitu cha msingi waone washauri wa mambo ya ndoa ili waweze kukusaidia.

MAMBO MABAYA NI MENGI KULIKO MAMBO MAZURI KWENYE NDOA YAKO
Kama mnajikuta ndoa yenu ina mambo mabaya mengi zaidi kama vile kutokuelewana, kila mtu ana hasira, mnapishana lugha kila mara, hakuna kucheka wala kufurahishana na mambo mazuri kama kucheka pamoja, kufurahi pamoja, kujisikia bila mwenzako siku haiendi basi hiyo ni dalili kwamba hiyo ndoa inahitaji msaada na bila kuifanyia ukarabati basi itasombwa na mafuriko na hatimaye kufa.

UNAJISIKIA VIGUMU SANA KUWASILIANA NA MKE AU MUME WAKO
Je, unajisikia kupatwa na hofu au mashaka kuongea na mke au mume wako kuhusu matatizo ya ndoa yako au maisha yenu kwa ujumla? Mawasiliano ndiyo njia pekee ya kuondoa stress za ndoa na maisha kwa ujumla na hatimaye kujenga ndoa yenye afya kwa wanandoa. Kama mkiwa pamoja mnakuwa kimya bila kuongea chochote na hakuna dalili ya kutaka kuongea na mwenzako basi kuna tatizo kubwa sana, hasa kama ni tofauti sana na kawaida yenu hasa jinsi ilivyokuwa katika siku za kwanza wakati mnachumbiana. Kama hujisikii vizuri kuwasiliana na mwanandoa mwenzio basi hiyo ni dalili kwamba tayari umekosa imani kwake na ndoa huwa inakuwa katika wakati mgumu kukiwa kauna kuaminiana (trust) Pia kama wewe ni mtu wa mwisho kujua kitu chochote muhimu au kuzuri kuhusu yeye, basi hapo kuna tatizo kwani ni kawaida wanandoa kuelezana vitu vizuri vinavyotokea kwa mmoja wao.

KILA MMOJA KUKATAA KUHUSIKA NA MATATIZO AU MIGOGORO YA NDOA INAPOJITOKEZA
Kama kila mmoja anajilinda na kutothamini hisia za mwenzake hasa linapotokea tatizo na kuanza kumrushia mwenzake lawana kwamba ndiye muhusika na wote mnakuwa na msimamo huohuo, fahamu kwamba hapo ndoa inapitiliza hata tiba za uangalifu zinazopatikana ICU. Ikiwa migogoro au matatizo yanapojitokeza kuna kuwa na kushindana kwa kila mmoja kukwepa kuhusika na badala ya kupata suluhisho mnajikuta mgogoro unazidi kuongezeka basi hiyo ni dalili kwamba sasa mmeanza kubusu kifo cha ndoa.

KUJIKUTA NI WEWE PEKE YAKO TU UNAHUSIKA KATIKA KUTATUA MIGOGORO AU MATATIZO YA NDOA.
Je, umekata tamaa, au kujisikia vibaya kuongea masuala ya matatizo ya ndoa yako kwa sababu mwenzako anakurudisha nyumba, au imefika mahali na wewe umeamua kunyamaza na kuachana kabisa na kujishughulisha na tatizo lolote katika ndoa na matokeo yake hakuna hata mmoja anajali tena kushungulikia matatizo ya ndoa? Kama mpo kwenye matatizo na kila mmoja amenyamaza kimya katika kuhakikisha mnamaliza tatizo lililopo basi hii ndoa ipo ICU na kama mtabaki kimya bila kila mmoja wenu kuhusika ili kuhakikisha ndoa inarudi kwenye mstari basi ni kama bomu lililotegwa ardhini na siku mtu akikanyaga hakuna kitakachosalia.

TENDO LA NDOA
Kama mmoja wenu sasa hana hamu kabisa na tendo la ndoa, au wote kwa pamoja hamna hamu kabisa ya tendo la ndoa hiyo ni dalili kwamba somethings is wrong. Kukosa faragha ya pamoja (intimacy and affection) itawafikisha mahali ambapo ndoa inaweza kufa au kuwa na ndoa isiyokidhi haja au kukosa kuridhishana inavyotakiwa.

Je mnaishi tu kwa sababu ya watoto ndo wamewafanya msiachane?
Kama ni ndiyo basi mnahitaji kupata msaada wa washauri wa mambo ya ndoa kwani hakuna tatizo lolote kwenye ndoa ambalo halina jibu. Kama hakuna hamu ya mapenzi kwa mmoja wenu au wote maana yake hisia zenu zipo mbali sana na hiyo ni dalili kwamba kila mmoja anaenda njia yake.

KUBISHANA AU KUGOMBANA KWA KITU KILEKILE KILA MARA
Kama kubishana, kupishana, kugombana, kuanzisha zogo kila mara kunatokana na issue ileile moja bila kupata suluhisho basi hiyo ndoa imesimama haikui wala kuelekea kwenye uimara zaidi bali inatelemka kwenda kwenye shimo. Kama hakuna kitu kipya kinatokea ili kupata ufumbuzi wa hiyo hali basi tafuta mshauri wa mambo ya ndoa ili awasaidie.

HITIMISHO
Hakuna tatizo la ndoa ambalo halina jibu hapa duniani kuna washauri wa mambo ya mahusiano na ndoa, wazazi ambao hupenda mafanikio ya watoto wao, kuna wachungaji ambao wana hekima na busara walizopewa na Mungu kwa ajili ya kuwashauri hivyo hata kama kuna tatizo kubwa namna gani jibu lipo na tiba ipo. Anza kwa kuzungumza na mwanandoa mwenzako then ikishindikana nenda kwa watu mnaona wanaweza kuwasaidia, usiwe mbishi wala mbabe ndoa ni kuchukuliana na kuelewana.

Dalili kuwa mpenzi anatereza/toka nje..

Unapogundua mabadiliko fulani ambayo yanahashiria kuwa mpenzi anatereza hupaswi kukasirika wala kujenga chuki na mumeo/mpenzi bali unatakiwa kuiandika upya kama sio kuibadilisha "script" kwa vile hakuna mwanaume anatoka nje bila kujua nini anakifanya, faida au hasara zake na jinsi ya kukuficha/danganya na kujitetea ikitokea atabambwa. Kumbuka wanaume wanazungumza kama ambavyo wanawake wanafanya (hasa wakiwa hawajaoa) na swala la kutereza (cheat) linapojitokeza wote hufuata mtiririko (Script) ule ule ila wanabadili kwa kukwepa/kutofuata yale yaliyopelekea wenzao kushitukiwa kama sio kufumaniwa.

Dalili ya kwanza-
Anapopunguza "attentions" na kutumia muda wake mwingi kufanya mambo mengine ndani ya nyumba na kukufanya ujihisi/sikie "lonely in love" na unapoliweka hilo wazi anakulaumu wewe kwa kutokuwa na muda nae na wala halalamiki (najua utakavyojisikia lakini kumbuka nimesema hakuna kukasirika wala kuwa mkali) na badala yake jieleze kistaarabu kuwa huenda kufanya kwako kazi masaa mengi, kuangalia watoto au kufanya kazi nyingi ndani ya nyumba kuna kufanya uchoke sana na hivyo kutopata muda wa kuwa karibu nae lakini hiyo haina maana kuwa penzi limepungua au kuisha kwani unampenda kama mwanzo mlipokutana.

Kisha muulize ni kitu gani ambacho mlikuwa mnakifanya awali kwenye uhusiano wenu na sasa anakikosa......akimaliza kusema au kuorodhesha basi mwambie hata wewe unakosa yote hayo na ungependa mambo yawe kama yalivyokuwa awali. Na kuanzia hapo anza kujirekebisha na kufanya mambo fulani kama mpenzi na sio mume/mwenza au mama fulani. Hapa utakuwa umegundua anatereza na wakati huohuo umezuia asiendelee kwa kumpatia kilichokuwa kikimpeleka nje (usiulize kuhusu the other woman just show him how lucky he is to have u as a wife/mwenza).

Dalili ya 2 kuwa anatereza nje...
Akishuhudia tukio lolote linalohusisha uterezaji (cheating) kutoka kwa marafiki zenu au ndugu na jamaa lenye kuhusisha swala zima la kutoka nje ya uhusiano na pea husika wanataka kuachana 4 good......atasema kwa sentensi fupi tu yenye maana kuwa "kamwe sitoweza kukufanyia hivyo" alafu kamaliza. Najua utafurahi na kuamini kinachotoka mdomoni lakini anaweza kabisa akasema hivyo akimaanisha kuwa kamwe hutogundua anachokifanya kwa kujifunza mapungufu yaliyotokea kwenye tukio zima.....kama nilivyosema unachotakuwa kufanya hapo ni kubadili mtiririko mzima kwa kuanzisha maongezi yatakayohusisha tukio lililotokea/linalotokea bila kujenga hasira/ukali. Kwa vile kasema kuwa yeye kamwe hatokufanyia hivyo (hatokuumiza) basi mwambie jinsi gani unampenda na namna gani utaumia au penzi lenu kusumbuka ikiwa mmoja wenu akitereza na kisha sema hutoruhusu hilo litokee kwa vile usingependa kupoteza penzi lenu.

Halafu malizia kwa kusema, lakini ikiwa mmoja wetu kashawishika na katereza nihakikishie kuwa tutalizungumza kwa uwazi na kutafuta ufumbuzi/muafaka.......hapo utakuwa umebadilisha "script" yake na wakati huohuo wewe unatakiwa kuangalia kitu gani kimepungua kama sio hakipo kwenye uhusiano wenu na hivyo anza kuki-restore taratibu ili Uhusiano usiharibike. Pamoja na kuwa sote kazi zetu za kila siku zakutuingizia kipato ili tuendelee kuishi, kumbuka kuwa uhusiano wa kimapenzi unahitaji kufanyiwa kazi ili kuwa mzuri na wenye afya.....usitegemee penzi pekee kufanikisha hilo, unahitaji kujishughulisha kila siku ili usijisahau.(keep the fire burning).

Dalili ya 3 kuwa anachoropoka nje....
Kwa kawaida kwenye uhusiano wowote wa kimapenzi hakukosi kutofautiana na matokeo yakutofautiana ni kuzozana, sasa linapojitokeza hilo na kwa bahati mbaya hamjafikia muafaka au mmoja wenu kagoma "kukubali yaishe" au kuwa mjinga ili kutofikia pabaya basi mpenzi wako ambae "anatereza", anaweza kuibuka na maelezo/sentensi zitakazo ashiria kuwa mnaelekea pande tofauti (hamuelewani) na kama kawaida atakurushia wewe lawama kuwa humuelewi, m-bishi au hata kuwa humheshimu.

Kwa yeye kukusingizia hayo ni wazi kuwa yatakuumiza na kukufanya labda uongeze hasira (hakuna jambo baya kama kusingiziwa jambo) lakini kama nilivyokuonya awali kuwa kukasirika hakuruhusiwi kwani tunachojaribu hapa ni kubadili "mtiririko" au "script" ili kuokoa uhusiano wenu. Maelezo yake yako wazi (kumbuka niliwahi kusema kuwa wanaume most of the time husema kilicho kichwani), sasa hapo anakuambia kuwa uhusiano wenu hauko kama ulivyotakiwa kuwa na anaefanya au kusababisha ni wewe (hata kama ni yeye still atakusukumizia wewe) kwani sote tuna jua kwamba wanawake ndio wanaoweza kurekebisha mambo.....they are mothers, dont forget that! Sasa ziba/zuia au ondoa hasira zako na anza kuzungumza nae taratibu kwa upendo (kama mama na mwana, yaani jisogeze...mshike panaposjikika namuangalie usoni) na kusema kuwa ungependa nyote wawili muwe kwenye mstari mmoja naje ufanye nini ili kufanikisha hilo.

Kisha malizia kwa kusema kuwa utajitahidi kadiri ya uwezo wako ili kumuelewa na kurudisha heshima kwake. Jichunguze au chunguza kuna kitu gani kimepungua ndani ya uhusiano wenu ambacho kina mfanya ahisi kuwa heshima haipo baina yenu?, kwa nini adhani kuwa hum-elewi? n.k alafu rekebisha hizo hitilafu na mambo yatakuwa poa kabisa kwani kinachomtoa nje atakuwa anakipata nyumbani.

Jambo linapojitokeza unapaswa kulizungumzia wakati huo (itakubidi ujifunze kuzuia hasira), sio unaacha siku moja au mbili zinapita alafu unarudi nyuma.....kwa mwanaume itakuwa "unapenda kulalamika kila wakati" wakati kwako itakuwa "nilihitaji muda kufikiria na kupanga maneno yangu".
Panua uwezo wako wa kiakili au niseme upeo ili uweze kufikiri haraka na kupangilia maneno cha-chap on spot, usingonjee kesho utakuta mwana sio wako.

Jinsi ya kumfurahisha mwanamke katika tendo la ndoa

WATU wengi (hasa baadhi ya wanaume) ama hawajui au hawajali ni kitu gani wenza/mwenza wake anataka kufanyiwa au akifanyiwa kitamsisimua (Turn on) hata kama amechoka sana. Uchunguzi unaonyesha kuwa Wanaume wengi hasa kutoka nchi za Kiafrika hujali zaidi kumaliza hamu zao za mwili na kamwe hawajali kama wenza/Mwenza wake yuko tayari au la!. Mf: Inasemekama baadhi ya Wanaume wa Kiafrika ambao ni wakubwa kiumri (wa zamani), au wale ambao wanathamini sana jadi zao asilia ndani ya Afrika, kitu cha kwanza watakacho kuambia mkiwa chumbani ni "njoo hapa" au "vua nguo basi" na kisha utavamiwa kabla hata wewe mwenyewe hujawa tayari na unalazwa chini kama sio unawekewa uume mbele ya uso wako.......halafu watu mnashangaa kuambiwa "mume wangu alinibaka".

Mfano huo unaonyesha ni kwa jinsi gani baadhi ya wanaume wanavyojipendelea(wabinafsi), na mara zote huweka akilini mwao kuwa wanawake/mwanamke ni chombo cha kumridhisha / kumstarehesha/ kumfurahisha na kumliwaza yeye "mwanaume". Napenda kusema kuwa mwanamke kama mwanadamu pia anahaki ya kuridhishwa, kustareheshwa, kufurahishwa na kuliwazwa pia. Dhana hiyo potofu imepelekea baadhi ya makabila kuendeleza mila za kuwakusanya wasichana ktk umri wa kuvunja ungo (mwali) na kuwafundisha jinsi ya kuwaridhisha mwanaume kimapenzi " hao wana bahati".

Lakini kwa wale ambao hawafuati/hawana/hawazijui mila hizo wamekuwa wakifuatilia kwa makini na kuamini kila kinachoonyeshwa kwenye "Video" ailimradi tu kiwe kinahusu jinsi ya kumridhisha mwanaume kimapenzi. Inasikitisha sana kuona pia baadhi hufuatilia hatua kwa hatua kila kinachoandikwa kwenye Magazeti na baadhi yao huamua kutafuta "Kungwi" na kulipishwa ili wapatiwe ujuzi wa kufanya mapenzi ili kuwaridhisha wapenzi wao. Ninavyofahamu mimi ni kuwa , ujuzi, utundu katika kufanya mapenzi haufundishwi hata kidogo ila ni ubunifu wako,
-kujaribu,
-kuujua mwili wako na wa mpenzi wako,
-ufurahiaji wa mwili wako,
-kujiamini kwako,
-uwazi na ushirikiano wa mpenzi wako.
Ni vema jadi ikabadilishwa na swala zima la kufundishwa/fundwa liwe kwa jinsia zote mbili. Wake kwa waume wafundishe jinsi ya kuridhishana, jinsi ya kufurahia na yale mambo muhimu ya mahusiano ya kimapenzi iwe ni ndoa au mahusiano ya kudumu nje ya ndoa.
Pia ni vizuri utambue kuwa unapoamua kufanya tendo la Ndoa au Ngono ni vyema ukajua mahitaji ya mwenzio iwe mwanaume/mwanamke, jaribu kufamnyia Mwenza wako kitu/vitu tofauti na alivyokuwa akitarajia/alivyozoea ni vizuri zaidi na kutamfanya aendelee kuwa na hamu ya kuwa na wewe kwa muda mrefu "usipigwe kibuti" kwa vile unamjulia.....yaani unajua vipele vilipo na unavikuna vilivyo.

SOMO HILI NI KWA MUJIBU WA MTANDAO

Kukanda (Massage) Mwanaume

Vipele vya kumyegesha mwanaume viko vingi na sehemu tofauti na hutegemea zaidi na mwanaume mwenyewe na vilevile jinsi wewe utakavyo vitumia/chezea ili kumfurahisha mwenzi wako au "kumnyegesha" (turn on). Pamoja na utofauti wao wanaume kwa ujumla wanapenda sana kukandwa sehemu ya juu ya mgongo, kiunoni, makalio yao, miguu(hasa vikanyagio) sehemu ya nyuma ya mapaja, ile sehemu ya ndani ya mapaja bila kusahau makende na uume.

Kama mara kwa mara unamkanda a.k.a "massage" mpenzi wako(mwanaume) lakini hata siku moja hajawahi kunyegeka (na wewe ungependa kumnyegesha kwa massage) basi jaribu hii na ninakuhakikishia mambo yatakuwa mazuri kabisa. Mlaze kifudi-fudi.....kisha mkalie kiunoni (natumai huna uzito wa zaidi ya kg 60) na anza kufanyia kazi sehemu ya kichwa (pembeni kule karibu na macho) huku ukimpa maneno mazuri yakumfanya asahau matatizo yaliyojitokeza kazini au kwenye shughuli zake nyingine za kuendesha kimaisha na kuhamishia akili yake hapo alipo.

Hamishia viganja vyako taratibu sehemu ya shingo...usikae sana hapa.....then hamia mabegani namoja kwa moja mgononi tumia muda wa dk 20 hivi kumkanda mabega na mgongo na wakati huu utapaswa kujiinua kidogo ili uweze kupitisha viganja vyako kiunoni). Ukimaliza jiondoe hapo juu yake na kisha jiweke katikati ya miguu yake na ipanua miguu hiyo ili upate nafasi ya kufanya shughuli yako.

Kwa kutumia mafuta maalum kwa ajili ya "massage" au unaweza kutumia baby oli au lotion yeyote yenye asili ya mafuta (yenye asili ya maji hukauka haraka). Mwagia kiasi mafuta yao juu ya makalio yake na pitisha viganja vyako kama vile unampaka mtoto (sio kwa nguvu) ukisha eneza sehemu nzima sasa endelea kumkanda makalio yake taratibu na tumia kama dk15-20 alafu shuka taratibu kwenye sehemu ya nyuma ya mapaja yake fanyia kazi paja moja baada ya lingine.

Hongera kwa kumaliza hatua hiyo.....sasa tumia mikono yako laini yenye mafuta kupenyeza pale yalipo mapumbu (akiwa kalalia tumo utayaona) hivyo yakande taratibu usiyavute ikiwa hayajajitokeza sana kwa nyuma. Kwa kufanya hivyo kutamfanya mpenzi wako aanza kusikia raha zaidi na hivyo atainua sehemu yake hiyo ya nyuma ili kukupa nafasi wewe kuyafanyia kazi makende yake......wewe endelea kuyakanda taratibu huku ukipitisha viganja vyako sehemu ya ndani ya mapaja yake pia(wakati huu itakuwa rahisi kuyafikia kwa vile atakuwa kajiinua).....

Sasa nenda mpaka kwenye uume na ushike kama vile unavyoshikilia "kitwangio" wengine huita Mchi alafu endelea kumkanda sehemu yote hiyo kisha mgeuze taratibu na uendelee na kazi yako yamikono mpaka atakapo omba mambo fulani au endelea namkono mpakama acheke a.k.a amwage.

Kwa nini hatuna furaha katika ndoa?

NIKO katika ngwe nzito ya kujadili na kutafakari juu ya ukosefu wa furaha na amani katika ndoa zetu. Juma lililopita tuliona jinsi amani na utulivu katika ndoa zetu ilivyokuwa bidhaa adimu, kwani ndoa nyingi zimesalimishwa mikononi mwa shetani. Naomba niwashukuru wasomaji wangu hasa wale walioamua kunitumia ujumbe mfupi wa maneno ili tuweze kutafakari kwa pamoja juu maisha yetu ya ndoa.

Kutokana na wingi wa meseji hizo za simu sitoweza kumjibu kila mtu kupitia simu yake ya mkononi na badala yake nitatumia makala haya kujaribu kujadili mada tajwa.
Hata hivyo kuna mambo mawili yaliyonisukuma kuandika makala haya ya leo.

Mosi ni meseji hizi: "Bwana Ngetti, ndo kwanza namaliza kusoma makala yako juu ya ndoa. Imenigusa sana kwani pamoja na utajiri tuliojaaliwa kuwa nao mimi na mume wangu lakini sina furaha katika ndoa. Naona heri kama ningeolewa na mtu fukara lakini tukawa na furaha na amani katika ndoa". Mama wa Mwanza.

"Bollen, laiti kama watu wangeruhusiwa kubadilishana wake, ningeomba mtu amchukue huyu mke wangu ambaye nashindwa kumtofautisha na shetani katika ndoa yangu". Kinondoni

"Umewapendelea mno wanawake katika uchambuzi wako, lakini ukweli hata wanawake wamechangia mno kukosekana kwa amani na furaha katika nyumba nyingi". Msomaji - Tanga.

"Naomba kukutana na wewe kwa ushauri kwani hivi ninasoma makala yako nimetoka kupewa talaka mahakamani. Inaniuma sana kwani mume wangu ameamua kuniacha kisa nimezeeka, akatafuta sababu zisizo na msingi wowote". Mama wa Arusha.

"Kama ningeambiwa kurudia kuoa, ningemkimbia huyu mwanamke kama ugonjwa wa ukoma. Mwanamke mjeuri asiyesikia la mtu hata mimi mume wake haniheshimu". Mwita msomaji, Tarime.

"Bwana Bollen, hatuwezi kupata amani na furaha katika ndoa kama hatutamkabidhi Mungu maisha yetu ili ndiye atawale ndoa zetu". Mwinjilisti Mulaki - Kigoma.

"Ndoa Bwana Ngetti inadhibitiwa na rungu tu. Mwanamke atabaki kuwa mwanamke tu hivyo lazima adhibitiwe kwa chuma". Mwita - Mwanza.
Orodha ya ujumbe mfupi ni ndefu kiasi kwamba hatuwezi kuziorodhesha zote hapa. Lakini kimsingi meseji hizi na nyingine nyingi zimetuonyesha kuwa kuna tatizo kubwa katika ndoa zetu na hatuna budi tusaidiane kutafakari juu ya tatizo husika.

Makala iliyopita nilijadili juu ya wanandoa kufahamu juu ya ubinadamu. Hata katika makala ya leo pamoja na mambo mengine bado ninasisitiza umuhimu wa utambuzi wa ubinadamu na kutofautisha tabia na mwenendo kwani ni vitu viwili visivyoshabihiana kwa namna yoyote ile.

Wengi wamedhani kuwa ndoa ni kuvaa pete na kuwa na cheti cha ndoa. Wengine pia wamedhani ni kula na kunywa siku ya harusi, kuzaa watoto au kuwa na fedha nyingi.

Kwa hakika yote hayo ni ubatili mtupu na kamwe havitoweza kufanya ndoa zetu kuwa na furaha. Hakuna tofauti ya pete ya ndoa na hereni ya sikioni au kikuku cha mguuni.

Cheti cha ndoa hakina tofauti na cheti cha mafunzo ya mgambo na kadhalika.

Ndoa ni muunganiko wa watu wawili wa jinsia tofauti kuungana kimwili, kiroho na kiakili. Lakini tunaweza kujiuliza ni kwa vipi watu wawili waweza kuungana na kuwa kitu kimoja kimwili, kiroho na kiakili?

Hapa kwanza nitazungumzia tendo la ndoa. Ieleweke kuwa hili ni tendo linalopaswa kupewa heshima ya hali juu kwani iko kwenye orodha ya vitu vitakatifu na ndio maana niliahidi kulijadili leo.

Tendo la ndoa limehusishwa mara nyingi na ukosefu wa furaha na amani katika ndoa nyingi.

Wapo waliowafuma wapenzi wao, wapo walioshindwa kuridhika na mapenzi kutoka kwa wapenzi wao, wapo waliokosa watoto, wapo walioshindwa kuzuia tamaa zao za mwili na wapo pia waliotumia fedha vibaya na hata kufilisika wakisaka ngono ya ndoa.

Wapo pia waliopoteza maisha yao kwa magonjwa ya kufedhehesha kama ukimwi na mengine mengi ya kuambukiza. Matatizo haya yanawakumba wahusika wote wa ngono bila kubagua jinsia. Na hii inatufanya tuamini kuwa hili ni tendo linalopaswa kutazamwa kwa umakini wa hali ya juu.

Nimewahi kuandika mahali fulani kuwa ngono halali ni baina ya wanandoa tu na kinyume chake ni uhalifu wa kiasili usiofaa kwa mwenye maono chanya.
Ngono ni zawadi ya upendo kwa wanandoa na hivyo haipaswi kufanywa kwa woga, aibu wala papara. Ngono ni hitimisho ya upendo ambayo mume anampa mke na mke anamzawadia mumewe.

Kama vile tunavyoandaa zawadi kwa wale tunaowapenda na hata kuzifunga zawadi hizo kwa umakini, vivyo hivyo tunapaswa kuandaa zawadi ya ngono kwa wake na waume zetu.

Ngono ni tendo linalohusisha moja kwa moja na ubongo na hivyo ikitumiwa vibaya hata ubongo pia unaweza kuathiriwa vibaya. Hii ndiyo maana mtu huumia sana pale anapobaini kuwa mke wake au mume wake anafanya ngono na mtu mwingine tofauti naye.

Kwa kuwa ni tendo la upendo na zawadi ya pekee kwa wenzi wetu, ni maandalizi yepi tunapaswa kufanya?
Usafi umepewa nafasi kubwa kwa wanandoa wanaojiandaa kufanya tendo hilo. Vyumba vyetu vinapaswa visafishwe, viwe na nuru si mwanga na hewa safi. Shuka zetu ziwe safi na ikiwezekana ziwe za rangi zinazopendwa na wanandoa wale.

Usafi wa chumba ni pamoja na mpangilio wa vitu pale chumbani. Nguo zetu za ndani ziwe safi na za kupendeza. Waume wengi huvutiwa na "bahasha" nyeupe au pinki. Miili yetu iwe safi na hata ikiwezekana tunaweza kujipulizia marashi yenye kutoa manukato isiyokera (love perfumes).

Hata hivyo, kabla ya kuingia chumbani ambayo ni hatua ya mwisho kuna maandalizi ya awali (foreplay) ambayo ni pamoja kufanya mazoezi ya mepesi ya viungo, kula vyakula vyenye protini ili mwili uweze kujitengenezea joto la kutosha.

Tarehe kamili ya kufanya ngono ijulikane ili hamu ya kufikia siku hiyo iweze kuwa juu. Wengi wamedhani baada ya kuoa au kuolewa basi ngono huwa ni biashara ya kila siku bila kujua hathari tutakazozieleza katika aya ifuatayo.

Kwa mujibu wa mtaalamu wa maswala ya mahusiano Mosses Tony katika kitabu chake " Ujue Mwili Wako" anasema "Ndoa nyingi zimevunjika kwa sababu ya kuendekeza ngono za mfululizo kila siku hadi tendo hilo kuonekana ni la kijeuri". Ameendelea kueleza: "Hali hiyo husababisha uraibu ambao mwisho wake ni anguko la ndoa".

Ngono pia ijulikane itafanywa kwa manufaa gani kwa mantiki kwamba itafanyika kwa kufurahisha hisia za mwili au kwa lengo la kuumba binadamu mwingine. Hii iwekwe wazi ili mimba isitungwe kwa bahati mbaya na badala yake ipangiliwe vema ili mtoto atakayezaliwa awe baraka katika familia.

Wanandoa wawapo kitandani wanapaswa kuwa makini katika ngono na makandokando yake. Mfano; sauti ya kike itofautiane na sauti ya kiume ili kuleta usikivu wa maana chumbani.

Viungo vyote vya mwili vipewe uhuru wa "kuzungumza" (let your body talk). Hapa tunamaanisha ulegevu kwa viungo vya mwanamke na ukomavu kwa viungo vya mwanaume.

Pia ijulikane kuwa kwa mwanamume kuwa ni sehemu zipi za mwanamke zinapaswa kushikwa kwa nguvu na zipi zishikwe kwa mpapaso tu. Mfano; sehemu za siri za mwanamke zimeumbwa kwa ngozi laini isiyohitaji rabsha na endapo itatokea yaweza kumfanya mwanamke huyo kupoteza hisia zote za kingono.

Kila binadamu anayo sehemu katika viungo vyake ambavyo vinapochezewa kwa namna apendayo humfanya kujisikia raha mustarehe.
Hili nalo lijulikane kwa wahusika wote wa tendo hili. Mfano; yupo mwanamke ambaye bila kuhisi joto la ulimi ukeni, kamwe hawezi kufikishwa kileleni. Ni vyema akabainisha kwa mumewe ili aridhike.

Wapo pia wanaume wanaopenda kuchezewa nywele za vikwapani, hawa pia ni muhimu wakaweka wazi. Lakini pia wapo wanaume wanaopenda kugusa shanga za kiunoni japokuwa makala zijazo nitajadili matumizi ya shanga kwa kina zaidi kwani nimepata taarifa za mwanaume aliyetumia shanga kama mwendesha farasi na kumkata tumbo mwanamke.

Kifupi majadiliano juu ya hisia za ngono zijadiliwe kwa uwazi baina ya wanandoa ili kila upande ujishughulishe kumridhisha mwenzie.
Usiri katika hili umefanya wake kwa waume wengi kuugulia hali hii kwa muda mrefu hadi pale walipozidiwa na kisha kuamua kutoka nje ya ndoa. Tumesikia akina baba wakifanya ngono na wasichana wao wa kazi au wanawake walioamua kutembea na wafanyakazi wao wa kiume (houseboys).

Kuridhika katika ngono hakuwezi kuwapo kama tendo hili litafanyika kwa aibu baina ya wanandoa. Hofu na wasi wasi vinapaswa kuepukwa wakati wa tendo hili kwani fikra zote ni muhimu kuhamishiwa pale kitandani.

Tatizo jingine linalojitokeza katika utafiti wangu ni wanandoa kufanya punyeto kama njia moja wapo ya kujiridhisha kingono.
"Yani mimi kabla sijafanya ngono na mke wangu ni lazima kwanza niende bafuni kupiga punyeto ndipo nije niendelee na bao la pili", amesema mwanandoa mmoja wa Tabata na kuongeza:

"Nafanya hivi ili mke wangu anione nachelewa kufika kileleni.
"Mimi huwa najichua mara kwa mara hata kwa kutumia vitu kama ndizi na karoti kwani mume wangu hajaweza kunifikisha hata siku moja. Nimefanya hivi sasa huu mwaka wa kumi na moja na mume wangu hajui", alisema mwanamama (37) aishie maeneo ya Mikocheni 'B' Dar es Salaam.

Wataalamu wengi wa afya bado hawaamini kuwa kujichua (punyeto) haina madhara kiafya, lakini kwa hakika ni tendo lisilo la asili na humpunguzia binadamu heshima. Wakati mwingine punyeto imetajwa kama "self-abuse" kwa maana ya kujivunjia heshima. Mosses Tony anasema: "Kupiga punyeto ni sawa na kufanya ngono na mizimu, kwani kamwe mpiga punyeto hamwoni anayefanya naye ngono ya hisia".

Upigaji wa punyeto umekuwa ni matokeo ya kutoridhishana katika ngono na hali hiyo kufanywa kuwa siri baina ya wanandoa.
Najua msomaji angependa kujua ni kwa nini wengine hata ukiwafanyia yote bado hutoka nje ya ndoa.

Naam, tunapaswa kujua kuwa "hayo yote" ni yapi na yamefanyika kwa ustadi gani? Wengine wamedhani "kwenda" mara nyingi na kumwacha mwanamke au mwanamume amechoka ndiko kuridhika kingono.

Huku ni kujidanganya na punde ndoa hiyo inaweza kuyeyuka.

Kwa msomaji makini anaweza kugundua kuwa maandalizi tuliyobainisha hapo juu hayawezi kamwe kufanywa na mtu asiye wa ndoa yako kwani wezi wa ngono hutumia maeneo kama 'gesti', sehemu ambazo huwezi kufanya maandalizi tuliyoorodhesha hapo juu ambayo ndiyo njia stahiki kuridhika na uliye naye.

Na pili wengi hutoka nje ya ndoa kama wenzi walio nao hawakuwa chuguo lao kwa hakika kwani tunapaswa kujiridhisha na wachumba zetu hasa kabla hatujaingia nao katika ndoa.

Wengi wameamua kuoa au kuolewa kwa kuwa ulifika wakati wa kufanya hivyo, wengine pia kwa kulazimishwa au kujilazimisha bila kwanza kujiridhisha na wale waliotarajia kuoana nao.

Hii imesababisha ndoa nyingi kuvunjika na sasa ni ndoa vilema.

Wengi hudhani wanandoa kutoishi pamoja ndiko kuvunjika kwa ndoa bila kujua kuwa kufanya ngono na mke au mume asiye wako ni kuvunjika kwa ndoa mara dufu na hivyo kufanya wengi tunaowaona leo wakiandamana na wake zao au waume zao kuwa wajane na waseja waliojificha.

Ujane na useja wao umebaki kuwa siri kubwa hadi pale maradhi au mazingira yanapowaumbua.

Hakuna ushahidi wa kimaandishi unaoonyesha kuwa waliotoka nje ya ndoa waliweza kufanikiwa maisha kwa namna moja au nyingine isipokuwa ni kurudi nyumbani na magonjwa yasiyotibika kama ukimwi, kusambaratisha familia, kuzaa watoto ambao baadaye huteseka mitaani kwa tamaa tu ya ngono tena isiyopangiliwa.

Kupuuza maandalizi ya ngono baina ya wanandoa sasa imefawafanya wanandoa wengi kuishi kwa majuto na masononeko yasiyokwisha. Fedha na nyumba za kifahari hazikuweza kuokoa mahusiano ya wanandoa waliopuuza nguzo muhimu katika ndoa, maandalizi yafaayo.

Wengine hufikiria juu ya hisia zao pekee bila kuwajali wenzio na punde wamalizapo haja zao hima hujirusha kulala huku wake zao au waume zao wakiachwa kuweweseka kwa hashiki kali ya ngono hadi kutoona maana yoyote ya kuwa na mke au mume.

Hivyo tunasukumwa kuamini kuwa ndoa kamili ni ile ambayo mume na mke huwa na hisia zenye kulingana itokanayo na maandalizi chanya kwa ajili ya tendo hilo takatifu.

Makala ijayo nitazungumzia maboresho ya ngono; Je, kuna limbwata? Na je, ni sawa kufanya ngono na mchumba wako umpendaye? Mungu aibariki ndoa yako msomaji iwe ya amani, tulivu, iliyojaa upendo na furaha. Lakini pia tutambue kuwa sote tu wadhaifu hivyo tuchukuliane mizigo kwa huruma na upendo.

Maandalizi ya tendo la ndoa

Kabla ya hili tunda kuliwa kuna umuhimu wa kuhakikisha linaandaliwa kwa uhakika na wewe unayetaka kulila ili uweze kulifaidi vizuri, si suala na kukurupuka na kulivamia bila maandalizi mazuri na ya kutosha. Kuna tofauti kubwa sana kati ya mwanaume na mwanamke linapokuja suala la tendo la ndoa au kufanya mapenzi au sex.

Je, maandalizi ya tendo la ndoa (foreplay) ni nini?
Ni kitu kinachofanyika kati ya wakati mmetoa nguo zote na kabla ya mwanaume kuingiza uume kwenye uke.
Ni kubusiana, kugusana, na kuchezeana hadi mnakuwa mmesisimka vya kutosha kwa ajili ya tendo la ndoa.
Ni kuuungana kihisia, kiroho na kimwili kwa muda wa kutosha kabla ya tendo la ndoa
Ni msingi na kitu muhimu kwa ajili ya kuhakikisha unapata tendo la ndoa lenye kuridhisha.
Ni sanaa ya kuelezea upendo na kukaribishana kwa ajili ya tendo la ndoa.
Ni muhimu kwa ajili ya kumwandaa mwanamke kwa ajili ya tendo la ndoa.
Ni kumhusisha partner wako vizuri zaidi kupata hisia za upendo na ukaribu kimahaba yeye kujiona mtu maalumu kwako
Ni aina ya meditation (kutafakari) ambapo hukusahaulisha na mambo ya dunia (ulimwengu wa nje) na kuondoa strees na kukuwezesha ku-focus kwenye mapenzi moja kwa moja (connection)na yule umpendaye.
Pia kusoma maandishi yanayosisimua, kuangalia video na picha zinazosisimua na maongezi yanayoosisimua kimapenzi ni foreplay pia.

Je, tofauti ya kuwahi kusisimka kwa mwanaume inaweza kuleta tatizo?
Wanaume wana mzunguko mfupi sana kuamshwa kimapenzi (arousal), wakati wanawake wanamzunguko mrefu sana katika kuamshwa kimapenzi.
Ingawa pia uwezo wa kusisimka na kuamshwa kimapenzi unategemaa sana mambo yafuatayo:-
Umri - unavyozidi kuzeeka homoni hupungua hivyo kutumia muda zaidi.
Afya - kama unaumwa na dhaifu unahitaji muda zaidi.
Uzoefu na malezi - kama umelelewa na kuelezwa kama sex ni mbaya kazi ipo
Kuna matatizo mengi hujitokeza hasa kutokana na tofauti kubwa ya mzunguko wa kusisimuana na kuamshwa kimapenzi kati ya mwanaume na mwanamke na hii hupelekea hata baadhi ya wanandoa kujisikia vibaya na kutokupenda kabisa tendo la ndoa.
Kwa kuwa wanaume ndiyo husisimka haraka na kumaliza tendo la ndoa mapema kuliko wanawake ambao wakati mwingine kwanza ndo wanakuwa waanaanza kusisimka na kupata raha ya tendo.
Suala la msingi ili kuondoa matatizo ni wahusika kuwa na elimu au sayansi ya mwili na tendo la ndoa linavyokuwa.
Kama wote ni vilaza (mbumbumbu) na hawajui sayansi ya miili yao basi, mwanaume anaweza kudhani kwamba mwanamke anashindwa kuitikia msisimko anaompa, wakati huohuo mwanamke naye anaweza kudhani ana matatizo kwa kushindwa kusisimka haraka sawa na mwanaume anavyosisimka hivyo kukata tamaa na kujiona wote wana kasoro kumbe ni mzima na tatizo ni ufahamu wa miili yao wenyewe.
Hii tofauti ya kusisimka kimapenzi wakati wa tendo la ndoa wakati mwingine hupelekea kuathiri kabisa maisha ya mahaba kwenye ndoa hadi pale wote watakapofahamu vizuri mwitikio wa miili yao linapokuja suala la sex.

Je, unamchukua mwanaume dakika ngapi kufika kileleni?
Kawaida mwanaume inamchukua dakika 3 tu kuweza kufika kileleni tangu asisimke kimapenzi, wakati mwanamke humchukua zaidi ya dakika 15 kufika kileleni tangu asisimke, hii ina maana kwamba bila maandalizi mazuri ya kusisimuana mwanaume huweza kufika kileleni hata kabla mwanamke hajaanza kusisimka na muda ambao mwanamke alitakiwa kufika kileleni mwanaume anakuwa tayari alishamaliza kazi zamani.

Utafiti unaonesha ni asilimia 20 au 30 tu ya wanawake hufika kileleni na tatizo kubwa ni kutokuandaliwa vizuri na wapenzi wao (wanaume) na maandalizi mazuri ndiyo siri pekee ya mwanamke kufika kileleni na hatimaye kufaidi utamu wa tendo la ndoa.

Mahusiano mazuri maana yake ni wawili ambao wanatimiziana mahitaji muhimu na hitaji muhimu katika ndoa ni pamoja na tendo la ndoa. Suala la tendo la ndoa lina umuhimu sawa na maeneo mengine katika ndoa kama kazi, chakula nk. Ni muhimu kuwa na maarifa kuhusu mwili na tendo la ndoa kwani waingereza wanasema

Je, ni makosa gani (deadly) ambayo wanaume hufanya katika kumuandaa mwanamke?
(i) Kuwa na haraka
Wanaume wengi huwa na haraka ya tendo la ndoa bila kuzingatia umuhimu wa kumuandaa muhusika kwanza.
Wanawake hutumia muda mrefu ili kusisimka ndiyo maana unahitaji kutumia muda bila kuwa na haraka ili uweze kumsisimua na zaidi kuwa na sex nzuri na yenye kuridhishana.
Ni vizuri kutumia muda wa kutosha kumuaandaa na kama unaweza hata kumfikisha kileleni hata kabla ya kumwingilia.

(ii) Kukosa kujua sehemu muhimu za kuchezea
Zaidi ya matiti, shingo na midomo (lips) na kisimi wanaume wengi hawajui ni sehemu zingine zipi ambazo wanawake huwasisimua zaidi.
Kuna sehemu zingine ambazo mwanamke akiguswa anaweza kusisimka haraka zaidi.
Tumbo, ------, mapaja, nyuma ya shingo, mabega, mgongo, sehemu iliyopo kati ya uke na nyuma (kutumia mtandao wa Vodacom au tigo ni dhambi kubwa kabisa tena ukome kama una hayo mawazo, mwenye hekima na afahamu naongea nini)
Hizi sehemu ni muhimu sana kwake kuguswa wakati wa kumuandaa.
Pia lazima uwe mtundu kuweza kusoma lugha yake na jinsi nini anakifurahia na nini hafurahii wakati wa maandalizi.

(iii) Kuwa bubu bila kuongea maneno matamu na kumsifia
Wakati wa tendo zima la kufanya mapenzi wanawake wanategema mwanaume awe anaongea si kuwa bubu na kuongea huanzia kwenye maandalizi na kama wewe ni fundi wa kuongea basi hutachukua muda mrefu kuhakikisha moto umewaka.
Kuna maneno matamu, kwenye mapenzi maneno matamu yapo ya aina mbili, kwanza ni dirty words (mfano uke kwa jina jingine unaitaje vile au uume kwa jina jingine unaitaje vile) na pili maneno ya kumsifia juhudi yake au alivyo na umbo zuri. Dirty words husaidia kumsisimua na kupa nyege zaidi na maneno ya sifa husababisha atoe juice zaidi.

(iv) Kubusu kwa kinyaa au bila Ustaarabu
Wakati unambusu usiache mimate kila mahali uwe mstaarabu pia usioneshe kwamba una kinyaa katika kubusu baadhi ya sehemu ambazo yeye anapenda umbusu, huyo ni mke wako na yeye wewe ni mwili mmoja, yeye ni wewe na wewe ni yeye, hivyo unaruhusiwa kubusu sehemu yoyote ndiyo maana usafi ni jambo la kwanza kabisa katika mapenzi.
Kumbuka kuna msema ambao husema 'CLEANNESS IS SECOND TO GODLINESS'

MAMBO AMBAYO MWANAMKE ANAHITAJI KUTOKA KWA MWANAUME

Wapo wanaume hugongwa na magari hivihivi!
Ni mara nyingi sana tunasikia wanaume wakisema
"mke wangu wala huwa simuelewi"
Ni kweli wanaume tunahitaji kujua baadhi ya vitu kuhusu wanawake ili tuweze kuwafahamu zaidi.

Je ni mambo gani wanawake huhitaji kutoka kwa mwanaume?

Wanawake huhitaji mwanaume anayesikiliza zaidi kuliko kutoa jibu tu. Wanaume ni watu wa kutia majibu (problem solvers). Pia wanaume hujitahidi kuhakikisha mambo yanakuwa sawa kwa kila mmoja bila kusahau masuala ya mahusiano hata hivyo kuna wakati na muda wa kutoa suluhisho na pia kuna wakati ambao mwanaume anatakiwa kusikiliza tu kwa mwanamke.

Kama mke moja kwa moja amekuomba usaidie kutoa sukluhish la jambo Fulani hapo haina tatizo moja kwa moja toa jibu an fanyia kwazi. Ila kama mke anakueleza kitu ambacho amekutana nacho iwe kazini au akiwa na watoto usitoe suluhisho kabla ya kumsikiliza kwanza.

Wanawake wanahitaji kubwa la kutaka kusikilizwa na hii ndiyo tofauti kati ya mwanaume na mwanamke, wanaume hutumia ubongo tu hata bila kuongea kuhakikisha anapata tatizo la issue zake wakati mwanamke hulazimika kuzungumza na kusikilizwa ili kupata jibu la issue yake.

Kama mwanaume hutumii muda ku-discuss mambo na mke wako hiyo siyo nzuri ndiyo maana anaweza kutumia muda wake kuongea na rafiki zake kwenye simu kwa sababu hujafanikisha hitaji lake la kusikilizwa.

Mwanaume unapoongea na mwanamke hakikisha:- Unapoongea naye kwanza unamwangalia usoni (eye contact) ili ajue unamsikiliza. Anapomaliza kuongea hakikisha unaonesha ulikuwa unamsikiliza hasa kwa kurudia yale ameongea kwa mfano unaweza kusema, "kwa hiyo ulikuwa unaniambia ………"
Then muulize yeye alikuwa anafikiriaje kupata jibu la hiyo issue yake kabla wewe kutoa jibu.
Kufanya hivyo kutaonesha unajali sana hisia zake hasa suala zima la kusikilizwa na pia itamsaidia yeye mwenyewe kuangalia ni jinsi gani anaweza kuhusika kupata jawabu la issue aliyokuwa anakueleza. Wataalamu wanasema mwanamke kawaida huongea maneno 45,000 kwa siku na mwanaume maneno 15,000 kwa siku hivyo ukiwa unamkatisha kuongea na kudakia kwa kutoa jibu bila kumsikiliza kisaokolojia una muumiza na itabidi atafuta mtu mwingine wa kuongea naye.

Wanawake wanahitaji mwanaume anayemuhitaji
Wanawake wanapenda kuona wanahitajiwa na mwanaume.
Siyo tu wanapenda kujisikia wapo sexy au beautiful pia wanapenda kufahamu kwamba mwanaume ambaye anatumia muda wake mwingi pamoja anavutiwa naye kila siku.
Hapa ni suala ka mwanaume kuwa na busara kuhakikisha unamtia moyo kwani kutokana na jinsi wanwake walivyo pamoja na majukumu yao wengi wakishazaa watoto miili yao inabadilika maumbo hata wao hujisikia wapo tofauti na kupoteza ujasiri, hivyo mwanaume unahitaji kumtia moyo hata kwa kumwambia kwa sasa nakuona wamo kuliko zamani.

Na kumwambia anavutia hivyo atajitahidi zaidi kujiweka kwenye form na kuwa sexy siku zote. Kama unaweza wakati anaandaa dinner unaweza kumbusu shingo yake na kumsifia jinsi ngozi yake ilivyo nyororo, na ukamnong'oneza maneno matamu jinsi alivyo mrembo hiyo itamjengea kitu kipya kwenye mind na moyo wake hivyo atakuamini na kujiskia vizuri zaidi.

Hata wakati mkiwa faragha jitahidi kwenda na mahaba kama vile zile ziku za kwanza mlipokuwa ndo mnaoana unaweza kumueleza jinsi ngozi yake ilivyo nzuri, hips zake zilivyo bomba, miguu yake ilivyo ya uhakika, shingo yake ilivyo kiboko, na hapo chini palivyo patamu, fahamu kwamba maongezi yako yanajaza kitu muhimu sana kwenye kichwa chake na atajisihia unamuhitaji na unampa usalama zaidi.

Mwanamke anahitaji mwanaume ambaye si rafiki wa watoto tu bali ni mtu anayelinda nidhamu ya watoto.
Likija suala la kuwapa nidhamu watoto wanaume wengi hujiweka pembeni na kuwaachia wanawake peke yao, wanawake hujisikia vizuri pale mwanaume anaposhirikiana na mke wake katika kuwalea watoto kuwa na nidhamu nzuri hasa pale wanapokosea. Huwa inaumiza sana wanawake pale anapomwambia mtoto asifanye kitu fulani au anampowakataza kabisa kufanya kitu, then wakienda kwa baba yeye anawakubalia na kuwambia fanyeni.
Mwanaume huonekana kama yeye ndiye mzazi rahisi sana kwa watoto na hivyo kutengeneza mazingira ya mama kuonekana mnoko.

Hiyo huweka hasira kwa mwanamke na pia mwanaume unakuwa unarutubisha bomu ambalo siku yoyote linaweza kukulipukia wewe mwenyewe, pia kuna kitu unakijenga ndani ya mke ambacho hafurahii. Wanawake wanahitaji mwanaume anayewaamini hata kama ana wivu.
Mara nyingi mwanaume unapoondoka nyumbani unaweza kuuliza: "unaenda wapi? "na utarudi saa ngapi?" Haya ni maswali mwanamke akikuuliza anapenda umpe jibu bila tatizo kwani anataka kujua wewe mpenzi wake unaenda wapi na utarudi saa ngapi, kuna wanaume hapo huwa inakuwa ugomvi kisa unaulizwa unaenda wapi na utarudi saa ngapi.

Moja ya msingi wa mahusiano yoyote ni kuaminiana (trust)
Pia mke wako anaweza kupita sehemu na wanaume wakamsifia kwa jinsi alivyo mrembo, sasa kwa mwanaume isiwe hasira na kuanzisha zogo eti kisa wanaume wengine wamemwambia mke wako anapendeza.

Wanawake wanajisikia vizuri kuambiwa wanapendeza hata na wanaume na wanajisikia kweli mimi wamo kama hata fulani amenisifia nimependeza.
Mimi nakubaliana na najisikia vizuri kama hata wanaume wenzangu watamsifia mke wangu kwamba anavutia na nitamwambia kabisa kwamba fulani kasema unavutia sana naamini nitakuwa nimemtia moyo zaidi na atajisikia vizuri zaidi na pia atazidi kujiamini zaidi.

Wanawake wanahitaji mwanaume anayewapa uhuru.
Wanawake wanapenda sana kuwa huru na hii inafanya baadhi ya wanaume wasijisikie vizuri. Kutokana na mabadiliko ya maisha ya ,wanawake wanafanya kila ambacho kipo kwenye akili zao kwa ajili ya kuendeleza na kuimarisha familia, wanafanya kazi, wanafanya business, wanasafiri na pia wanafanya miradi yenye lengo la kuimarisha uwezo wa familia kiuchumi.

Wapo wanaume huona haiwezekana mwanamke kufanya kazi za ofisini eti atakuwa huru mno kiasi kwambaatachukuliwa na wanaume wengine. Hayo ni mawazo ya kizamani na hayana nafasi kwa karne ya leo. Unamzuia mke hata kwenda shule eti atachukuliwa na wanaume wengine.

Mimi naamini ni vizuri kumtia moyo kwanza awe anajiamini na kwamba anaweza kufanya jambo lolote akitaka kwani uwezo anao. Asipotiwa moyo na mume ni nani ataweza kumtia moyo ili ajiamini na kufanya mambo makubwa kwa ajili ya familia. Maisha ya sasa hivi yanahitaji wana ndoa ambao wanachakarika kwelikweli hivyo ni suala la kumpa mke wako uhuru ili muweze kusaidiana kuendeleza familia na maisha kwa ujumla.

Wanawake wanahitaji mwanaume anayetambua mambo muhimu madogo anayofanya.
Usione nguo zako zimenyoshwa vizuri, watoto wanasafishwa na vizuri, nguo zinafuliwa na kunukia vizuri au chakula kinapikwa vizuri, hapo mwanamke amefanya kazi kubwa na anapenda sana umpe credit kwa kazi kama hizo na kama siku ukipata nafasi unaweza kumsaidia na mkafanya pamoja hiyo inatia moyo sana.

Kuliko wewe ni kuvaa tu au kula tu na kuona ni wajibu wake, ni kweli ni wajibu wake lakini hizo kazi si mchezo zinachukua muda na nguvu. Kama mwanaume huwa husaidii kazi za nyumbani ni vizuri ukaanza sasa, huna excuse kama unataka kuwa na mwanamke ambaye anataka kujisikia ana mume anayemjali.

Hivi vitu vidogovidogo vinawafanya wanawake wajisikia raha sana mkifanya pamoja.
Pia unakuwa umempunguzia muda wake wa kufanya hiyo kazi moja na kumpa muda wa ziada hata wa kuwa na wewe mwenyewe pia. Wapo wanaume hulaumu tu mke wangu kila wakati yeye na kazi mchana na usiku na hata akiingia chumbani anakuwa amechoka, kumbe wewe mwenywe husaidii kazi ili mke apumzike.

Mwanamke huhitaji mwanaume anayefanya vitu anavyovipenda
Kama anaenda shopping unaweza kwenda naye na mkawa na muda mzuri pamoja huko kwenye shopping, kama anapenda kwenda kwenye matamasha ya miziki na michezo unaweza kwenda naye pia mkawa na muda mzuri, kama anapenda kuhudhuria semina za ndoa au neno la Mungu nenda naye pamoja.

Hii ni kuonesha kwamba na wewe wamo katika yale anapenda hiyo itaonesha kwamba unamjali sana na ina maana kubwa sana kwake. Siyo mwaka unaisha hujaenda na mke mahali yeye anapenda then unasema ninamjali sana mke wangu.

Mwanamke anahitaji mwenzi siyo Baba. Huwa inasikitisha sana kwamba mwanamke hawezi kufanya kitu chochote hata kile ambacho kipo logical mpaka apate ruhusa kwa mume. Hiyo siyo ndoa bali ni uhusianoa wa mtoto na mzazi. Kuna mambo ya msingi kama yale yanayohusu pesa hayo ni kweli yanahitaji kuwasiliana kwanza ndo mtu ufanye mfanye.

Lakini hata kama anataka kwenda kula lunch na rafiki zake wa kike lazima aombe ruhusa kwa mume hiyo kali. Mwanaume pia inabidi ujiulize je, wewe huwa unamuomba ruhusa mambo yote unayofanya?

Ka sivyo kwa nini yeye akuombe ruhusa kila kitu? Mwanamke anahitaji mwanaume ambaye hamlinganishi na mama yake. Utakuta mwanaume analalamika kwamba mama yake ndiye aliyekuwa anapika chakula kizuri, au mama yangu alikuwa anafua nguo kwa sabuni fulani nzuri zaidi au mama yake alikuwa anafanya hiki na kile.

Fahamu kwamba mke ni mtu tofauti sana na mama yako aliyekuzaa.
Ni kweli watu huwa tunakuwa na kumbukumbu nzuri sana za mambo mazuri ambayo mama zetu walikuwa wanatufanyia ila kama umeoa na unataka kila kitu kama mama yako ni vizuri ukahama na kwenda kwa mama yako mapema.
Wanawake ni watu ambao siku zote hujitahidi sana kuhakikisha mambo yanaenda na kama mwanaume hujaridhika na jinsi anavyopika, au anavyofua nguo au kulea watoto ni vizuri ukamsaidia kufanya vile unataka kuliko kumsema kwa kulinganisha jinsi mama yako alivyokuwa anafanya. Hapo una mambo ya mawili ya kufanya kwanza kumsaidia au pili fanya mwenyewe.

Mwanamke anahitaji mwanaume hot kwenye sex pia
Wanawake pia wanahitaji tendo la ndoa linalowaridhisha na kuwafikisha pale wanahitaji. Anahitaji mwanaume anaye mtimizia ndoto zake za mahaba, anafurahia na kujisikia raha jinsi Mume anavyompa mgusu wa kimwili wenye msisimko wa raha, Anajisikia vizuri kupata busu tamu, Anajisikia vizuri kukumbatiwa Anapenda kusikia maneno matamu ya kimapenzi kwenye masikio yake pia wanapenda kusikia na kuona mambo mapya kitandani siyo mazoezi ya kila mwaka mambo yaleyale, anajisikia vizuri kuwa na mwanaume mbunifu na dereva mzuri.

Hahitaji mwanaume anayempeleka kitandani na baada ya dakika mbili amemaliza. Hapo unaweza kumpotezea hamu ya tendo la ndoa ambayo ni zawadi kuu Mungu ametupa viumbe wake. Mwanamke anahitaji mwanaume anayejua kumuandaa kabla ya tendo lenyewe na pia anahitaji mume anayejua kumaliza kwa mtindo ambao anaridhika. Mwanaume unahitaji kuhakikisha tendo la ndoa linakidhi kiu yake, anaridhika na linakuwa na maana kwako na kwake na kila siku hamu inazidi kukua zaidi.


Maadui wa mwanamke kufika kileleni

Si utundu na ujanja wa mwanaume tu unaomwezesha mwanamke kupata utamu wa kufika kileleni (mshindo, orgasm, coming) bali mwanamke pia anahusika.Kufika kileleni ni nini? Ni kiwango cha juu kabisa cha utamu, hisia, raha, msisimko wakati wa tendo la ndoa wakati ambapo misuli ya uke au uume hukaza. Kwa mwanaume huambatana na kutoa manii (ejaculation).

Wengine wakifika kileleni hupiga kelele sana, wengine huongea maneno ovyo ovyo hata matusi, wengine huzimia kabisa, wengine huwakwida wapenzi wao kama vile kibaka, wengine hutulia kimya na kupitilia za usingizi na wengine ukiwauliza wanasema mahali walikuwa ni kama vile walikuwa hewani, wengine kama vile walikuwa wananamwona Bwana (Yesu) n.k ilimradi tu ni raha na utamu na ni kweli Mungu alitupa zawadi ya ajabu na hii ni kujulisha kwamba Mungu alituumba tena kwa namna ya ajabu.

Pia wengine huita kufikia mshindo, wengine huita coming n.k. Pia wapo ambao kwa tendo moja la ndoa huweza kufika kileleni zaidi ya mara moja.

Je mwanaume na mwanamke wote hufika kileleni sawa?
Kwa wanaume kufika kileleni ni suala ambalo ni automatic, halina mjadala, kitu cha msingi kwake ni kujitahidi asifike mapema kileleni ili amfikishe mke wake pale anatakiwa kufikishwa, kwani mara nyingi mwanaume akifika kileleni hupoteza uwezo wa kuendelea na tendo.
Katika nchi zilizoendelea kama USA na Canada utafiti mwingi unaonesha kwamba
Asilimia 15 % ya wanawake hufika kileleni mara zote.
Asilimia 48 % ya wanawake mara nyingi hufika kileleni.
Asilimia 19 % ya wanawake ni kawaida kufika kileleni lakini si mara nyingi
Asilimia 11 % ya wanawake ni nadra sana kufika kileleni na
Asilimia 7% ya wanawake hawajawahi kufika kileleni na hawajui ni kitu gani.
Hapa ni wanawake kutoka nchi zilizoendelea ambako elimu kuhusu mapenzi ni kubwa sana.

Je, kwetu nchi zilizogoma kuendelea hali itakuwaje?
Ukizingatia wanaume wengi bado hawajajua nini wanawake wanahitaji ili kufikishwa kileleni? Pia kuna baadhi ya wanawake ambao hata wasipofika kileleni hawana shida wanaridhika tu bora maisha yanaenda.

Nini Kitu muhimu kuhsu mwanamke kufika kileleni?
Wanawake wanaweza kuendelea kupata utamu hata baada ya kufika kileleni hivyo ni jukumu la mwanaume kuhakikisha anabaki ndani ya uke hadi anahitimisha tendo zima (conclusion) angalau kwa dakika 10 au 15 ndo ukimbie kuoga au kupiga usingizi siyo kumwacha kiumbe wa watu kwenye mataa akuugulia kwsa kumuondolea utamu na raha.
Tendo la ndoa huwa ni la kuridhisha sana hasa pale mume anapomfahamu vizuri mwanamke na kile anahitaji kwa kumfanyia utundu wote wa kuchokonoa sehemu zote ambazo zinaweza kumhakikishia kwamba atafika kileleni. Lakini pia mwanamke anasehemu kubwa sana ya yeye kujihakikishia anafika kileleni si mwanaume tu ni suala la wote.

Je maadui wakubwa wa mwanamke kufika kileleni ni nini?
Kukeketwa (Female Genital Mutilation).
Kukeketwa ni kitendo cha kukata sehemu ya uke hasa kisimi kwa wanawake. Katika Afrika kuna nchi 28 ambazo hufanya hicho kitendo cha kikatili, na pia nchi kama Yemen na Indonesia bado wanafanya. Ingawa wanawake waliokeketwa huweza kurudia hali ya kuweza kufika kileleni, walio wengi huathiriwa sana na hiki kitendo na kuwasababishia kushindwa kufika kieleleni.

Dini, jadi na utamaduni:
Kuna baadhi ya mitazamo na malezi ya dini, jadi au tamaduni huwapa wanawake mtazamo mbaya, finyu na usio na maana kuhusiana na tendo la ndoa.
Katika dini, jadi, na tamaduni nyingi ukiacha jando na unyago, elimu ya mwanamke kuhusu mwili na uzazi havifundishwa wala kutamkwa matokeo yake wanawake wengi hawaijui miili yao, kiasi ambacho unakuta kijana wa kiume anamuoa binti hajui chochote kuhusu mwili wa huyo mwanamke na mwanamke mwenyewe hajui chochote kuhusu mwili wake mwenyewe, akiguswa chuchu anakataa kwani ni kwa ajili ya mtoto, hapo utategemea afikishwa kileleni kweli?

Kisaikolojia.
Hili huchangia kwa asilimia 95 kwa matatizo yote yanayosababisha mwanamke asifike kileleni.
Adui mkubwa anayetisha sana wa mwanamke kutofika kileleni ni akili (mind.) Hofu labda ya kuachwa, mashaka, kutojiamini, kukasirika, donge moyoni, kisirani au mahusiano kutokuwa mazuri huweza kusababisha mwanamke kutofika kileleni. Kushindwa ku- concentrate kwenye tendo lenyewe na kupata hisia halisi (sensations). Kuwa na mawazo ya kitu kingine wakati wa tendo la ndoa Mawazo hasi (Negative) kuhusu tendo la ndoa, pia Kuwa mchomvu.

Kibailojia
Kama vile kuwa na mfumo ovyo wa mzunguko wa damu kwenye maeneo ya viungo vya uzazi pia huchangia. Anaweza kuwa na uvimbe au kisukari pia huchangia. pia hitilafu za viungo baada ya kufanyiwa upasuaji hasa sehemu ya uke.

Umri (Menopause)
Kuna wakati mwanamke kuanzia miaka 48 – 52 hupata mabadiliko ya upungufu wa homoni na huo upungufu husababisha sehemu ya uke kuwa kavu wakati wa tendo la ndoa. Kuwa na uke mkavu huchangia katika ufanisi wa tendo la ndoa kuwa mdogo na hatimaye kushiondwa kufika kileleni Si kweli kwamba mwanamke akizeeka uwezo wa tendo la ndoa unakuwa mdogo, muhimu ni kutumia vilainisho kama gel au KY jelly na libeneke linaendelea kama kawaida.

Kutumia madawa (Medicaments).
kama unatumia dawa za kuzuia msongo wa mawazo pia huchangia ile hamu ya tendo la ndoa (libido) na matokeo yake kukosa kufika kileleni. Pia kuna dawa za uzazi wa mpango hupunguza hamu ya tendo la ndoa hasa zile ambazo huingizwa mwilini (sindano). Pia dawa za kupunguza pressure hupunguza uwezekano wa kufika kileleni.

Pombe, madawa ya kulevya na sigara, Alkoholi na madawa ya kulevya hupunguza sana hamu ya tendo la ndoa. Huathiri mfumo wa Fahamu unaohusika na mzunguko wa hisia za mapenzi kati ya ubongo na uke. Kama inavyoathiri (alkoholi) mwanaume kudindisha vilevile huathiri mwanamke kufika kileleni. Mwonekano, urembo na umaridadi:

Kwa mwanamke jinsi anavyoonekana na jinsi mwanaume anavyoonekana kuna sehemu katika hisia za mapenzi (emotions na feelings).
Kama yeye mwenyewe anajijua kwamba hayupo vizuri kimwonekano (urembo, usafi, harufu) na pia kama mwanaume hayupo sawasawa basi anakuwa ameathirika sana kiasi ambacho hawezi kufika kileleni.
Pia wanawake wana uwezo mkubwa kunusa harufu kuliko mwanaume hivyo harufu yoyote mbaya kwake huwezi kumpeleka nje kabisa ya njia ya kwenda kileleni.

Mazingira
Kama eneo au chumba mlichopo hakina usalama kama vile anahisi mtu anachungulia au anaweza kuingia, kwa mwanamke hiyo ni issue kwani hawezi kufika kileleni kwa sababu ya usalama wake.

Je kuna jinsi ya kuondoa tatizo la kutofika kileleni?
Kujiruhusu mwenyewe kupenda tendo la ndoa na zaidi kupenda kufika kileleni kwa hamu kubwa.
Kuwa responsible kwa mambo yote yanayohusu ufanisi wa tendo la ndoa.
Kujipa elimu na maarifa kuhusu elimu ya mapenzi kwa mwanaume na mwanamke, viungo vinavyohusika na kila kitu kinachiweza kukupa tofauti katika ufanisi uimarishaji wa tendo la ndoa kama unavyosoma hapa sasa hivi.
Kuwa na mawasiliano wakati wa tendo la ndoa hasa kuhusiana na maeneo yote ambayo unasisimka pale ukiguswa au kuchezewa.
Kufanyia kazi kila tatizo lolote la kisaikolojia na kupata solution kabla ya tendo la ndoa.

Mitindo tofauti ya tendo la ndoa!

Baada ya kukuru-kakara za kuwekana sawa/tayari kwa kufurahia tendo takatifu, mlaze mpenzi wako juu ya kitanda/mkekani au kwenye sakafu (inategemea mnapenda wapi na usisahau kuwa comfy), panua na wakati huohuo shikilia miguu kitendo kitakachofanya mapaja yake yainuke pia alafu wewe jiweke kati (rejea jinsi ya kusaga "ntili" ukiwa umepiga magoti hapo juu).

Alafu sogeza mikono yako mbele zaidi ili ushike sehemu yake ya mapaja pale katika ili usije ukaangaka, mara baada ya kuwa kwenye "control" jisogeze mbele ili uume ukuingie ukeni na kisha anza kwenda mbele-nyuma taratibu huku na badilisha mwenda jinsi uwezavyo.

Wakati wewe unafanya hivyo yeye anatakiwa kuzunguusha kiuno (sio wanawake tu wanaotakiwa kukata viuno, wanaume pia wanatakiwa kujua kucheza ngoma ei zile za asilia........) au hata kujisogeza huku na huku ili agonge pombe zote za uke na kuwafanya wote mfurahie mnachokifanya.

Ikifikia wakati umechoka au unakaribia kufika kunako utamu basi jaribu kufanya kama vile unamlalia…….bila kuachia miguu/mapaja yake, kufanya hivyo kutasababisha kisimi kiguse sehemu ya juu ya eneo la uume wake na kukusababishia upate ile wanaita "Double O".

Sultan!

Katika mkao huu mwanamke anakuwa mtendaji mkuu, mwanaume hapa anatakiwa kutulizana, kufuata maelekezo na kusogea akisogezwa,kuvutika akivutwa yaani yeye ni kufurahia utendaji wako wa mwanamke.

Jinsi ya kufanya.

Mkae mkiangaliana na wakati huohuo miguu imepanuliwa kwamba yeye atapitisha miguu yake sehemu ya kiuno na hapo mnaweza kuanza kupeana mahaba kwa kukumbatiana, pigana busu, shikana, kumbatiana, papasana na hata kuambiana yale maneno matamu ambayo ukiwa nje ya chumba ni machafu si wayajua eeh? hey yaongee ikiwa unapenda au anapenda na yanawaongezea hamasa!

Taratibu mlaze mpenzi wako chali kitandani ukiwa katika mkao ule ule kwamba uko mbele yake na umepanua miguu yako (yeye akiwa katikati), ikunje miguu yako sehemu ya magoti na nyanyua miguu yake na kuiweka kwenye mabega yako jivute kwa mbele ili mboo ikuingie vema.

Ktk mkao huu kiuno kinakwenda vema kabisa kwa vile wewe ndio mtendaji mkuu na yeye atakuwa ametulia tu akisikilizia utamu, huitaji kuharakisha au kumharakisha na badala yake chukua muda kum-pamper huku wamtomba (hey hapo mwanamke anatomba japo hahahah) pia unaweza ukabadilisha mwendo kwa kupiga nje-ndani (nenda mbele na nyuma) taratibu huku ukilamba/nyonya vidole vyake vya miguuni na anapofika kileleni mnyonye kwa kuvuta dole gumba la mguuni ili kumuongezea utamu (baadhi ya wanaume hupenda hiyo hivyo mjaribu na wako).

Spoony

Baada ya kuandaliwa unalalia ubavu kisha yeye mpenzi wako analala kwa nyuma,kisha wewe unapanua mguu ili aweze kuingiza uume kisha rudisha mguu juu ya mguu mwingine (kama ulivyokuwa) na yeye anaendelea kukufanya taratibu mpaka wote mtakaporidhika au maliza haja zenu.

VITU HIVI HUONDOA RADHA YA MAPENZI

Tendo la ndoa ni tendo takatifu kwa watu waliooana na linamisingi yake ambayo ikidumishwa hakila kila mmoja atalifurahia. Kuwana baadhi ya wanawake huwa wanajisikia maumivu makali baada ya kufanya tendo la ndoa huwa kama amechanjwa na wembe.

Mara nyingi hali hii husababishwa na mwanaume mwenye kucha ndefu pindi anapokuwa katika harakati za kumwandaa. Kucha hizi kama utaziingiza sehemu za siri kwa mwanamke lazima zitamchubua na kufanya ahisi maumivu wakati wa kufanya tendo.

Mikono mikavu ambayo imeota sugu huwa kama msasa ambao humuumiza mwenzako na kusababisha michubuko kwa ndani.Vile vile unapokuwa na magonjwa ya zinaa ambayo husababisha vidonda kwa ndani na kukufanya uhisi maumivu wakati wa tendo na kushindwa kulifurahia zaidi ya maumivu muda wote.

Kingine ni kikwapa watu wengi hujisahau na kujikuta hawaheshimu tendo hili hata bila kuoga yeye anaingia kazini na kujikuta akiharibu hali ya hewa kutokana na harufu kali itokanayo na jasho la kutwa nzima.

Mara nyingi unatakiwa kuwa msafi wa mwili muda wote kwa kunyoa nywele sehemu za siri, kukata kucha huku ukihakikisha mikono yako ni misafi na laini, kuangalia afya yako kila wakati na kutibu magonjwa ya zinaa yanapokutokea, pia kuoga kabla ya tendo ili kuondoa jasho la kutwa nzima. Ni vizuri kama hujaoa ili kujiepusha na maradhi ya kuambukiza utumie kondomu kwa ajili ya kujikinga.

Tujenge utamaduni wa kuheshimu tendo la ndoa ambalo maandalizi yake yanahitaji mtu kuwa msafi tena mwenye afya bora. Nina imani mtu akizingatia yote haya ataweza kufurahia tendo lake la ndoa.

UNATEGEMEA NINI UNAPOMNYIMA MWENZIO MAKUSUDI?


NATAMANI siku moja usiku Mungu angefungua mapaa yote ya nyumba wanazolala wanandoa halafu uone namna wengi wao wanavyolala, bila shaka kama bado hauko kwenye ndoa, usingeshawishika siku moja uwe mwanandoa. Ninachotaka kusema ni kuwa ndoa nyingi zimejaa maigizo, watu wanaishi wanacheka, wengi wao wanaishi tu kwa shida, hakuna maelewano ya kutosha.

Baadhi ya nyumba kwa mfano, unaweza kuona mmoja anamlalamikia mwingine kwa kutokuwa mwaminifu nk. Baadhi ya nyumba pia utaona watu wamelala sebuleni, mmhh baba mzima au mama mzima ambaye unamuona mitaani, yanayoendelea kwenye nyumba yake kama ungeyajua bila shaka ni vigumu kuamini kama kweli huyu fulani anaweza kufanya.

Ndiyo unaweza kuona mwanaume amelala sebuleni, labda ni kwa kuwa hakuna maelewano ndani ya ndoa. Au unaweza kukuta mwanamke naye kakimbia kitanda, hataki kulala na mwanaume kwa sababu ndani ya ndoa hakuna amani. Wapo wanandoa wengine wanaombeana mabaya, hasa pale inapoonekana kwa sababu moja au nyingine ni vigumu kutalakiana.

Huenda ikawa ni kwa sababu anazijua siri fulani nzito nk. Ukitaka kujua kama fulani ana maigizo kwenye ndoa au la, ni pale ambapo mwanandoa anakuwa mbali na mke au mumewe.

Kuna watu wengi katika matembezi yao huwezi kumuona na mkewe, labda kama wanakwenda kwenye msiba na jirani au ndugu, tena mmoja anaweza kuwa hatua ya mbali, kabla ya kumfikia mwingine. Ndoa zimejaa vichekesho, kuna watu hawaelewani, wakija wageni wanajifanya wanaelewana. Je wewe ndoa yako ikoje?

Amka ndugu yangu, fanya mambo yenye kuweza kukusaidia kuwa na ndoa ya kweli, ndoa ambayo mwanaume au mwanamke anajua wajibu wake na anautekeleza. Kuna sababu nyingi za ndoa kuzifanya kuwa mbaya, lakini mojawapo ya tatizo ambalo linalizisumbua ndoa nyingi ni kutokuwa na uhakika wa tendo la ndoa. Tafiti nyingi zinaonyesha kuwa katika nyumba nyingi, liko tatizo la uhakika wa tendo la ndoa. Kuna wanawake kwa wanaume, wamekuwa wakiwanyima tendo hilo wapenzi wao, kwa sababu mbalimbali. Je wewe mwanandoa unayesoma makala hii una uhakika wa kupata tendo hili kutoka kwa mke au mumeo?

Jijibu mwenyewe, ukweli ni kwamba ikiwa unamfanya mwenzi wako asiwe na uhakika na tendo hili, jua unaiharibu ndoa yako mwenyewe. Hata kama mwenzi wako ni mtu mwema kwako kiasi gani, kama unataka kuthibitisha ubaya wake mnyime. Tafiti nyingi duniani zinaonyesha kuwa kwa sababu ya kutokuwa tayari kwa baadhi ya wanandoa katika tendo hilo, baadhi yao wamekuwa wakiona njia sahihi ni kutoka nje kusaka watu wengine ambao watakuwa tayari.

"Ni upuuzi, eti niko kwenye ndoa, mke wangu amekuwa akiniambia acha kunisumbua, jana tu nimekupa na leo unataka tena, kwani mimi ni mbwa, tena hata mbwa huwa anapumzika, niache bwana nilale," anasema mwanaume mmoja akilalamikia kitendo cha mkewe kumnyima. Kwa ujumla wanaume ndio kundi linaloongoza kwa kunyimwa, kiasi kuwa baadhi yao wamekuwa wakitumia nguvu na hata kupiga makofi wake zao wakilazimisha wafanye kile ambacho wanataka.

Hata hivyo, ukweli ni kuwa tofauti kubwa iliyoko baina ya wanawake na wanaume, ni kuwa wanawake wanaponyimwa, si wengi wanaochukua hatua mbaya kama hizi za kupiga au kwenda kwa wengine, ingawa taarifa za karibuni katika taasisi mbalimbali zinazojihusisha na utafiti kuhusu ndoa nchini Marekani, Building your Marriage inaonyesha kuwa wameanza kubadilika na baadhi yao wameibuka kusaka wanaume wanaoweza kuwapa wanachotaka.

Ambacho napenda kusisitiza katika makala hii ni kuwa unapoingia kwenye uwanja wa mpira, cheza, nikiwa na maana kuwa umeamua mwenyewe kuingia kwenye ndoa, ni vizuri kuwaza namna ya kupatiana raha, badala ya kukerana. Mnaporuhusu kukerana, maana yake ni kuruhusu akili ya mmoja au wote kutafakari njia mbadala ya kuishi, iwe ni kwa kuwa na mwingine, au kufikiria kuachana nk.

IMANI ISIYO YA KWELI: Nimekuwa nikipokea simu nyingi za wasomaji, wakitaka nizungumzie kama kuna ukweli kuwa uhusiano wa wizi-wizi ni mzuri kuliko ule wa wazi, yaani anamaanisha mwanaume au mwanamke kwenda nje ya ndoa anafuraha zaidi kuliko ndani. Jibu la swali hili ni SIYO. Ukweli ni kwamba sehemu pekee ambayo itakuwa amani ni ndani ya ndoa, unashirikiana na mtu ukiwa unamjua vema, yawezekana ni kiafya nk. Lililo la msingi ni kwa kila mmoja katika ndoa, kujifunza namna gani anaweza kumfurahisha mwenzi wake.

Je, umekuwa ukiwaza namna ya kumfurahisha mwenzi wako au mnaishi ili mradi siku zinakwenda mbele? Tafakari chukua hatua. Ni makosa kuamini raha iko nje ya ndoa. Kumekuwepo kuchokana kwa wawili walio katika ndoa na kufanya mmojawapo ajaribu kutafuta kuridhishwa nje ya ndoa, lakini ukweli ni kwamba raha ya ndoa, iko ndani, ukiikosa, usihangaike nje, badala yake suluhisha kasoro yenu, muangalie namna ya kuiboresha zaidi.
Kwa hakika kama wewe uko kwenye ndoa unapaswa kujifunza zaidi namna ya kufurahiana ndani ya ndoa, ili ndoa isibaki kuwa ni jina tu. Siri ya kuwafanya wanandoa waendelee kuelewana ni kwa wao kufanya haya ambayo ninayasema yaani kila mmoja kujiona kuwa ana deni la kumpenda mwingine.

Somo hili limeandaliwa na Dismas Lyassa ambaye ni ni mtaalam wa husiano aliyesajiliwa na serikali kutoa ushauri (social Welfare Counselor), anapatikana kwa

Je, Upoje Kitandani

Nazima Tv, halafu nakwambia kitu!! Picha kwa hisani ya inmagine. Je unadhani wewe ni mwanaume mzuri kitandani? Hapa kuna maswali kwa ajili yako.
Je ni mara nyingi mke wako huwa anakuhitaji kwa ajili ya tendo la ndoa?

Je, kila unapofanya mapenzi yeye hufika kileleni? Je unauhakika jinsi ulivyo mzuri kitandani
Basi jibu maswali yafuatayo kwa uangalifu na uhakika bila kudanganya na angalia mapendekezo ya majibu ambayo yapo kila baada ya swali.
Kama ni mwanamke basi unaweza kumuonesha mume wako haya maswali ili ajibu ajipime yupo wapi katika kukuhakikishia unapata raha inayotakiwa kitandani siku zote.

Je, ni mara ngapi huwa unajisifu sana kwamba wewe ni mzuri kitandani?
(a) Kamwe sijisifu
(b) Mara chache
(c) Kila wakati
Watu ambao hujisifu kwamba ni wazuri kitandani mara nyingi hawajiamini. Suala la tendo la ndoa ni maada sensitive sana kwa wanaume, hivyo kujisifu inawezekana ni kujaribu kufunika ukweli.

Je, nini mtazamo wako kuhusu usafi?
(a) Nipo kawaida, naoga, najinyoa ndevu na kutumia vipodozi vya wanaume na kuvaa nguo safi
(b) Kuna siku siogi, pia naweza kuvaa nguo moja hata mara mbili
(c) Nipo makini mno, naosha mikono kila wakati na sipendi kabisa kugusana na mtu mwingine asije nichafua
Kuwa msafi siku zote ni kitu kizuri sana. Wanawake wapo sensitive sana na kile wananusa kuliko wanaume.
Hii ina maana kwamba harufu mbaya huweza kumuathiri mwanamke kuliko mwanaume. Ni muhimu kuoga kila mara na kuvaa nguo safi, ingawa kuwa msafi kupitiliza kunaweza kuzima hamu ya mapenzi kwa mpenzi wako kwani huwezi kubusu kila sehemu kwa kuogopa kuchafuka.

Je, mwonekano wako upoje? Umepinda au umenyoka?
(a) Imara na mara zote mgongo umenyooka
(b) Imara sana labda niwe nimechoka basi mgongo huinama
(c) Kila wakati natembea nimeinama na kupinda mgongo
Mwonekano (posture) ovyo siku zote unahusiana na Uvivu. Na kama ni mvivu maana yake wewe si mzuri kitandani pia.
Wanaume wenye posture nzuri siku zote huwa wanasimama wima na mabega yakiwa sawa bila kuinama na pia ni wanaume ambao hupenda ku-improve vitu vingi katika maisha mojawapo ni suala la kitandani. Wanaume wenye mwonekano (posture) nzuri ni wazuri kitandani pia.

Je, ni mara ngapi unaongea na mikono
(a) Sifanyi kabisa
(b) Nafanya kila ninapoongea
(c) Mara moja au mbili kila ninapoongea
Wanaume wanaongea huku mikono nayo ikisaidia mara nyingi ni wabunifu na wafikiriaji wazuri. Hujitahidi sana kuhakikisha wanapofanya mapenzi kunakuwa na matokeo mazuri. Kama una mwanaume wa jinsi hii basi utafurahia kitandani maisha yako yote hadi uzeeni.

Je, wewe ni mbunifu kiasi gani kitandani?
(a) Nafanya kwa utaratibu uleule kila siku miaka Nenda miaka rudi
(b) Ninafanya tofauti kidogo angalau baada ya muda
( c) Najitahidi kuwa na kitu kipya angalau kila ninapofanya mapenzi
Kuwa bored ndiyo sababu kubwa ya uhusiano wa mapenzi kuwa ovyo na hata hamu kwisha kabisa. Kujaribu kitu kipya pamoja na mikao tofauti wakati wa kufanya mapenzi husaidia kitanda kuwa cha moto kila mara.
Wapo wanandoa ambao wapo kwenye ndoa zaidi ya miaka 60 na bado wana enjoy mapenzi.

Je, kuna umuhimu wowote kwako kwa mke kufika kileleni?
(a) Huwa sijali afike au asifike, ni kama hainihusu
(b) Ni vizuri akifika kileleni
(c) Nahusika sana na napenda afike kileleni na pia namsaidia kwa kiasi kikubwa kuhakikisha anafika kileleni
Kufanya mapenzi kuzuri kunategemea sana jinsi ya kutoa na kupokea kati ya wahusika. Wanaume wengi wao ni rahisi sana kufika kileleni kuliko wanawake wakati wapo kitandani. Wanawake ni viumbe wa hisia hivyo huhitaji muda zaidi ili kuweza kufika kileleni. Ingawa wanawake wengi hawapowazi kuongelea hili, bado kufika kileleni ni kitendo kinachowapa kuridhika vizuri na tendo la ndoa.
Hivyo kama huwa unahakikisha anafika kileleni basi wewe ni mwanaume mzuri kitandani.

Je, ni mahali gani unamtumia kwa ajili ya tendo la ndoa?
(a) siku zote ni kitandani kwetu chumbani
(b) Chumbani sehemu yoyote, chini au kitandani
(c) Mahali popote ambapo tunaweza
Kama kunakitu kinatakiwa kuepukwa kwa nguvu zote basi ni ile kuwa na mazoea ya kuwa na sehemu au utaratibu mmoja wa kufanya mapenzi miaka Nenda rudi. Jaribu kuwa na sehemu tofauti za kufanya mapenzi, mnaweza kusafiri au kwenda camping au sehemu yoyote.
Hawezi kusahau kumbukumbu za hizo sehemu.

Je, unapokuwa kwenye tendo la ndoa huwa unasimamamisha kwa muda gani?
(a) Dakika mbili au pungufu
(b) Kama dakika 15 hivi
(c) Hadi saa nzima kama kuna umuhimu
Hakuna ubishi uume uliodinda husaidia kumsisimua mwanamke wakati wa kufanya mapenzi. Wakati mwingine mwanamke hukata tamaa kama akijisikia wewe husisimki na matokeo yake wote mnaambulia sifuri.
Ni ukweli pia uume uliosimama na kudinda vizuri huwezi kumpa mwanamke msisimko ambao huwezesha kumfikisha kileleni.

Je, ni muda kiasi gani huwa unatumia kumuandaa mpenzi wako
(a) Sina huo muda
(b) Dakika tano hivi
(c) Hadi nihakikishe yupo tayari au amesisimka vya kutosha kiasi cha yeye kutaka.
Kama wote tunavyojua maandalizi (foreplay) ni muhimu mno kwa ajili ya tendo la ndoa.
Bila maandalizi tendo la ndoa halina ladha yoyote zaidi ya kuumizana.
Kama huwa hufanyi maandalizi yoyote hapo ni dhahiri kwamba haitawezekana kwa mkeo kufika kileleni na hatafurahia inapofika muda wa kwenda kitandani.
Na kama unatoa muda wa kutosha kwa wajili ya foreplay basi atakuwa anasubiri kwa hamu kubwa kusikia muda wa kitandani umefika.
Pia ni vizuri kufahamu kwamba mwanaume mzuri ni yule ambaye hata baada ya kumaliza tendo la ndoa si mtu wa kukurupuka na kutoa uume wakati mke hajamruhusu kwani utamu wa tendo la ndoa kwa mwanamke ni wa muda mrefu zaidi hivyo ni vizuri kubaki ndani zaidi ya dakika 10.

Je, ni mara ngapi unafanya mapenzi kwa kushtukiza?
(a) Si rahisi na kawaida
(b) Mara moja kwa mwaka
(c) Mara kwa mara tunapotaka kufanya mapenzi
Kuna raha yake kwa mwanamke kufanya mapenzi kwa kushtukiza. Utaratibu wakati mwingine huwa una bore, ni kama mazoea. Sex ya kushtukiza wakati mwingine huleta kumbukumbu nzuri zaidi na kuwa enjoyable.
Wanawake huwafurahia wanaume ambao huwapa kile wanatarajia linapokuja suala la kitandani.
Ukiwa mbunifu na mwanaume mwenye utundu kitandani basi mkeo atakushukuru na kukupenda zaidi kwa sababu unampa raha kamili.

Sehemu tofauti za utamu wa tendo la ndoa kwa wanawake


Kwa bahati nzuri wanawake wana maeneo 5 ambayo huwawezesha kusikia utamu wa kufanya mapenzi/ngono tofauti na wanaume

Sehemu maarufu ni
-kisimi na
-G spot (kipele G) lakini kuna eneo lingine linaitwa
-AFE ambalo liko mwishoni kabisa mwa uke na vile vile
-kuta za uke bila kusahau
-mwanzo wa uke.
Mwanamke anaweza kufurahi/kupata utamu wa tendo hili takatifu kwenye maeneo yote hayo ikiwa mpenzi wako anajua kuwajibika (sio kufanya kwa muda mrefu tu bali kujua kucheza na kiungo chake a.k.a uume) pamoja na utundu wake pia wewe mwanamke unatakiwa kuwa wazi na huru kumuelekeza ikiwa kagusa kusiko au kapatia kunako utamu.

Utamu wa maeneo yote hayo ni tofauti na unazidiana ikiwa umejaaliwa kuupata.
Sehemu tofauti za utamu wa ngono kwa wanawake

1.Kisimi-unapopata utamu wa kisimini kwa njia ya kusuguliwa/shikwa/chezewa kwa ulimi, kidole au kichwa cha uume. Utamu wa mahali hapa hupatikana haraka na hufanya usitamani tena tendo hilo kwa muda fulani (3-dk15) na kikiguswa tena hukupa maumivu fulani hivi (inakuwa sensitive) kwa baadhi ya wanawake ndio mpaka kesho tena.

2.Kipele G-Utamu wa mahali hapa ni wa nguvu sana mwanamke mara zote huzirai kwa muda (kuishiwa nguvu) huchukua muda wa dk20-45 kupatikana, na ukipatikana hamu haikuishii hivyo wakati wewe umezimia mpenzi anaweza kuendelea na mchezo na nguvu zikirudi basi na wewe unaendelea kutafuta goli lingine.

Ikiwa mpenzi ana uwezo wa kumaliza lakini anabaki kasimama (dinda) au anajua kujizuia basi unaweza kutandika goli tatu ktk mzunguuko mmoja (hii ni kutokana na uzoefu).

3.Mwanzo wa uke:utamu wa mahali hapa haukupotezei hamu kwani haufiki kileleni bali unasikia utamu fulani hivi....sasa ukitaka kufika kunako mwisho basi sisukumize ili uume uingie ndani zaidi ili aweze kugonga G au nguzo/kuta za uke...(kwa uzoefu)

4.Kuta za uke (kona zote kwa ndani), utamu wa eneo hili unapatikana toka mwanzo uume umeingizwa, na kadri mnavyoendelea kufanyana umoto unazidi na hatimae unamaliza (fika kileleni) ila sina uhakika kilele cha kuta za uke kina uhusiano gani na kufika kileleni.....utamu wa hapa haukumalizii hamu kwani unaweza kuendelea mara baada ya kufika kileleni as long as mpenzi bado mgumu (kadinda)....(kwa uzoefu)

5
.Mwisho wa uke (ni karibu na njia ya uzazi.....umewahi kufanya mapenzi/ngono na mpenzi wako akagonga mwisho wa uke na ukasikia maumivu fulani lakini bado unapenda aendelee na wakati mwingine unaomba afanye kwa nguvu (ili usikilizie maumivu hayo)? Je umewahi kubahatika kufika kileleni (sikia utamu) ikiwa anakufanya kwa nguvu huku ukisikia maumivu?

Kama jibu ni ndio basi huko ndio eneo la "mwisho wa uke", utamu wa huko hazimii mtu bali unaweza kutokwa na machozi kama sio kulia kilio cha furaha na maumivu, vilevile lazima utatoa ukelele wa maana sio ule wa kujifanya kumridhisha mwanaume....ukelele wa huko ni "INAUMA lakini TAMU" if u know what I mean.....pia unaweza kutokwa na damu( ni kwa uzoefu).

Utamu wa mahali hapa utakufanya utake zaidi LAKINI hakikisha unamruhusu mpenzi wako kufika huko ikiwa mnaaminiana (mko kwenye uhusiano wa kudumu na msafi kiafya) na uko tayari kuwa mama ikiwa jamaa atatereza na kuachia kidogo kwani ni mlangoni kabisa mwa njia ya uzazi.

MAMBO YA KUFANYA KWA MWANAUME WA KATI WA MAANDALIZI YA TENDO LA NDOA

Wanawake wengi huwa wanapenda kupata masimulizi mazuri na ucheshi, nasema hivyo kwa sababu huwa wapo makini sana na maneno yanayotamkwa na mumewe. Ieleweke kuwa, matamshi makali humkatisha na kumshusha hamu yake kufanya tendo la ndoa.

Baadhi ya wanawake huwa wanapenda sana kupapaswapapaswa juu ya mwili wake bila ya kubagua ni sehemu gani unayoishika.

Mume usione kinyaa kumshika mkeo zile sehemu nyeti na kuingiza vidole vyako pole pole na kuvitembeza humo, na kushika kinena na kuchezea kisimi huku ukimbusu kwa busu zuri ambalo litamfanya ajisikie raha muda wote wa maandalizi ya tendo la ndoa.

Mume usiwe na haraka kumuingilia mkeo, subiri hadi amesisimuka kiasi cha kutosha mpaka huhakikishe joto la mwili wa mke linapanda na kuanza kujitupa tupa akionesha hali ya kuhangaika hangaika kwa kuashilia nyege zimempanda.

Muandae mpaka uhakikishe kuta za ndani za uke wake na zile kuta za pembeni zinaumuka kama andazi lililokolea hamila na baadhi ya wanawake kisimi hudinda kama uume. Mbali na hili mfanyie maandalizi mpaka uke wake utatoe majimaji kwa ajili ya kulainisha maingiliano na uume uingie kwa urahisi.

Nyege za mkeo zikimpanda anakuhitani na atashika uume na kujiwekea sawa ukeni kwake mwenyewe. Fanya hivyo mpaka uhakikishe mkeo anapumua kwa haraka, mapigo ya moyo utaona yataongezeka, na kama mlikuwa mnaongea atanyamaza kimya na kuanza kutoa sauti ya kuhema na mwisho akikaribia utoshelevu hutoa sauti ya kulia. Mume usisahau kunyonya matiti yake. Baadi ya wanaume hushindwa kufanya hivyo kwa kigezo cha mwanamke kuwa na matiti yaliyo lala kama malapa. Unashauriwa hata kama ni malapa yanyonye kaha huwa anasikia raha ukifanya hivyo fanya kama unamg'ata shingoni.

Wakati wa tendo la ndoa linaendelea msizime taa hadi limekamilika na mtazame usoni bila kuoneana aibu soma kitabu cha Wimbo 7: 1-6 utapata kitu hapo.

Nitaendelea na somo hili la mwanamke kumwandaa mkewe.

MAMBO YA KUFANYA KWA WANANDOA WAWAPO CHUMBANI

Wanandoa mnashauriwa kulala mapema kama hakuna umuhimu wa kuwachelewesha kulala ili mpate muda mwingi wa kuongea na kucheza faragha. Kama nilivyosema mwanzo kuwa suala la ukubwa wenu muuvue wakati huo na kuuweka pembeni.(Picha kwa hisani ya mtandao)

Heshima ya mume na mke inatakiwa kuishia sebuleni mkifika chumbani kazi inakuwa ni moja tu. Wanandoa mnatakiwa muingie chumbani mkiwa na upendo, utii na uhuru wa kila mmoja kufamnyia lolote mpenzi wake.

Uchunnguzi unaonesha kuwa, watu wengi walioendekeza heshima wawapo chumbani wamejikuta wanang'ang'ania staili moja ya mke kulala chali maarufu kama kifo cha mende kwa kuogopa kuonekana ni wahuni pindi mmoja wapo anapodai mtindo mwingine. Ni ukweli usiofichika kuwa, kila mtindo una raha yake na utamu wake pia. Hivyo, suala la uoga kwa wanando kuomba kutumia mitindo ya aina mbalimbali limekuwa chanzo cha kuwa na wapenzi nje ya ndoa ili kuziba mapungufu ya ndani.

Linapofika suala la kufanya mapenzi msiwe na mipaka mmoja akimtaka mwenzake basi pasiwepo na kikwazo. Kitabu cha 1Kor 7: 3-5 kinasema kuwa, Mume atimize wajibu alio nao kwa mkewe, naye mke atimize wajibu alio nao kwa mumewe. Mke hana mamlaka juu ya mwili wake, bali mumewe anayo; hali kadhalika naye mume, hana mamlaka juu ya mwili wake, bali mkewe anayo. Msinyimane haki zenu, isipokuwa kama mnaafikiana kufanya hivyo kwa kitambo tu, ili mpate nafasi nzuri ya kusali. Kisha rudianeni tena mara, ili Shetani asije akawajaribu kwa sababu ya udhaifu wenu.

Mlalapo kila mmoja awe uchi kama alivyozaliwa ikiwa ni pamoja na kutumia nguo/shuka moja. Inatakiwa mwanamke na mwanaume kila mmoja apate raha kama kinavyosema kitabu cha, Ruth 1:9, 3:1, na Kumbukumbu 24:5. Tunaona hapa biblia inazungumzia raha ya mke lakini pia mume hupata raha yaani kufurahishana kwa kila mmoja.

Kabla ya kuanza kufanya tendo la ndoa kila mmoja anatakiwa kumwandaa mwenzake na kuuweka pembeni ubinafsi. Utafiti unaonesha kuwa baadhi ya wanaume huwa hawana maandalizi ya kutosha kwa wenzi wao hali ambayo husababisha raha inayotarajiwa sipatikane. Hawajali utoshelevu wa wake zao, kwa hali hiyo wake wanajiona kama vile wanatumiwa kama vyombo vya kutimizia tamaa za wanaume. Mwanamke anatakiwa kuandaliwa kwa muda wa dakika 20 ama 30 wakati mwingine saa moja wakati mwanaume anaweza kuandaliwa kwa muda wa dakika moja ama mbili na akawa tayari kwa shughuli.

Mwanamke naye hatakiwi kuwa mbinafsi kwa kumgomea mumewe akidhani kwamba ametosheka au hata kabla ya tendo la ndoa huondoa raha iliyotarajiwa. Mwanamke unatakiwa kuondoa aibu ya kumuomba mumeo pindi unapohitaji tendo la ndoa. Huha haja ya kumsemesha, anza kwa kushika sehemu ambazo unafikiri ukimgusi atatambua kuwa unamhitaji. Ongea kwa sauti laini ambayo itamshawishi azame katika tendo hilo.

Mara nyingi wanawake walioolewa wamekuwa wakizidiwa maalifa na Malaya ambao wakiwanasa waume zao huwa hawafurukuti hata kidogo. Soma Mith 7: 4- 23 ili uone jinsi Malaya wanavyoweza kuwadhibi wanandoa na kuwaona wake zao si kitu.


MAANDALIZI YA TENDO LA NDOA


Mara nyingi tendo la ndoa huwa linahitaji maandalizi ya muda mrefu. (Picha kwa hisani ya mtandao) Lakini kuna baadhi ya wana ndoa huwa wanafikiri maandalizi ya tendo la ndoa huwa chumbani peke yake pindi wanapokuwa kitandani, la hasha, suala la maandalizi ya tendo la ndoa huanza mapema na huanzia kwenye mawasiliano mazuri kati ya mume na mke tangu asubuhi hadi jioni.
Wanandoa pia wanatakiwa kula chakula cha kutosha na cha kutia nguvu ili watakapoanza mchezo huo wasichoke na kujikuta wanashindwa kuendelea na tendo hilo kutokana na mmoja wao kuchoka ama wote kwa pamoja.

Mwanamke anatakiwa kujipamba mapema ili amvutie mumewe (mume huvutiwa sana na kuona mkewe jinsi alivyojipamba ikiwa ni pamoja na kujipulizia pafyumu ambayo mumeo huwa anaipenda)

Mwanamke pia unatakiwa kufanya usafi, kuoga vizuri, kusukutua kwa dawa ili kuondoa harufu kinywani. Hili ni la kila mwanandoa hili kuondoa kukwepana kubadilishana ndimi wakati wa maandalizi ya awali kabla ya kuanza tendo la ndoa.


RAHA YA NDOA NA TENDO LA NDOA

Kuna tafasiri nyingi sana za tendo la ndoa lakini maana kubwa ni kitendo cha kukutana kimwili mume na mke yaani walio katika ndoa, tendo hilo ndilo linaloitwa TENDO LA NDOA.(Picha kwa msaada wa mtandao)

Hakuna asiyejua kuwa Mungu ndiye mwanzilishi wa ndoa na nyumba (Zab 127:1) na ndiye aliyeweka utashi ama tamaa ya kuoana ndani yetu.

Biblia takatifu inatuambia kuwa, wazo la mke na mume ni wazo la Mungu soma Mwanzo 1: 27 uumbaji haukukamilika mpaka mwanamke alipoumbwa. Na katika uumbaji wake aliwaumba kwa tofauti ambao ndiyo kivutio kati yao.

Biblia pia inatuambia kuwa, Mungu alitengeneza ndoa ili kuondoa upweke kwa mwanaume/mwanamke. Kana kwamba hiyo haitoshi naweza kusema kwamba ndoa ilipangwa na Mungu ili ilete furaha kwa wahusika na sio huzuni. Mungu alivyo wa ajabu, aliweka raha zote ndani ya watu ili wapate msisimuko, utoshelevu pamoja na upendo wa agape.

Katika masomo yangu ya ndoa ambayo nimekuwa nikifundisha nimekuwa nikigusia suala la mahusiano mazuri pindi wanandoa wawapo kitandani. Natambua kila kukicha wanandoa hudamkia katika masumbufu ya dunia hii na baadhi ya wanawake hubaki nyumbani kwa ajili ya shughuli mbalimbali hasa kwa wale ambao hawana kazi.

Katika masumbufu ya dunia wanandoa hukumbana na mambo mengi ikiwa ni pamoja na kukwazana na watu mbalimbali ndani ya daladala, ofisini ama sehemu anayopatia kipato chake cha kila siku. Hivyo basi wanandoa mnatakiwa hasira ya mchana iishie mlangoni muingiapo chumbani ili msiikose raha.
Pia ieleweke kuwa mapenzi hayana muda (mchana, jioni, usiku wa manane nk) ana hayana kikomo, mpaka mtosheke ama mtoshelezane.

KUNA TOFAUTI YA TENDO LA NDOA NA NGONO?

Ni tendo moja lenye wawakilishi wawili lakini wenye sifa tofauti. (Picha kwa mujibu wa mitandao) Wengi wanajua kuwa, tendo la ndoa na ngono ni kitu hicho hicho ila inategemea na matakwa ya mtumiaji wa matamshi hayo. Pia wapo wanaoamini kuwa, tendo la ndoa linaitwa hivyo kwa sababu huwakutanisha mwanamke na mwanaume, lakini ukweli unaweza kuwa siyo huo ingawa kwa upande mwingine ndiyo huo.

Ngono ni nini? Ngono ni kitendo cha kukutana kimwili kwa watu wa jinsia mbili ambao hawana uhalali wa kujamiiana. Kwa lugha zingine mbili ni uzinzi (kama wako katika ndoa) au uasherati (kama hawapo katika ndoa). Mfano wa watu haoa ni kama makahaba, ‘wanawake wanaouza miili’, wanaume wanaokutana na wanawake hao, watu wasiyo katika ndoa na makundi mengine yanayofanana na hayo.

Tendo la ndoa ni nini? Lakini wanapokutana kimwili watu wenye uhalali, yaani walio katika ndoa, tendo hilo ndilo linaloitwa TENDO LA NDOA. Hufanywa na mke na mume (wanaotambulika kihalali). Wako watoa mada wanaoyatumia vibaya maneno haya, wakimanisha hata wapenzi wanapokutana kimwili wanafanya tendo la ndoa. Inawezekana wako sahihi kwa upende mwingine ikiwa tu, wanamaanisha kwamba, wapenzi hao wanafanya tendo ambalo linatakiwa kufanywa na wana ndoa.

Kwa upande mwingine, na kwa maana hiyo si sahihi kabisa wanandoa wanapokutana kimwili kusema eti wanafanya ngono.! Hoja mbalimbali zimekuwa zikitolewa na watoa mada kuwa, ngono ni msemo uliozoeleka lakini ukiwa na maana moja sawa na tendo la ndoa. Hawapo sahihi kwani, watendaji wakiwa na sifa mbili tifauti ndiyo kila mmoja ana jina lake hata kama tendo ni moja. Mtu akichukua kitu cha mwenzake bila kuruhusiwa anaitwa mwizi, jina ambalo halitatumika endapo ataruhusiwa na mwenye nacho kuchukua kitu hicho, lakini tukio linakuwa moja, la kuchukua.

Ndivyo ilivyowa kwa wanaofanya ngono na tendo la ndoa, kama mwanamke hajaolewa akakutana kimwili na mwanaume, atakuwa anafanya ngono, lakini mwanaume huyo huyo akimuoa kihalali, anabadili jina, sasa atasemekana anafanya tendo la ndoa.
Ni vyema kufuatilia kwa makini kosa hii ya mahaba ili kujifunza mambo mbalimbali ambayo yatakuwa

UTUNDU WA MAANDALIZI YA TENDO LA NDOA


 Ndoa ni safari ndefu ambayo inahitaji uvumilivu wa kila namna ili kuhakikisha kila mwanandoa anaifurahia safari hiyo. Leo hii ndoa nyingi zimejaa majuto kutokana na wahusika kukosa uvumilivu katika safari hiyo na kuhisi kuwa pengine njia aliyopita siyo sahihi. Majuto ya safari hiyo yanatokana na mambo mengi, miongoni mwa hayo ni lugha mbaya kwa wanandoa, kumiliki visasi mioyoni mwao, kutosameheana, kushindwa kujishusha pindi mmoja anapokosa na kugundua kuwa yeye ndiye chanzo cha tatizo, kutoaminiana katika mahusiano yao ya ndoa, wivu uliopitiliza, kutoheshimiana nk.

Safari ya ndoa ili iwe salama na yenye baraka tele, inahitahi kutoyaruhusu hata kidogo niliyoyaelezea hapo juu. Lakini silaha kubwa kuliko yote ni msamaha, suala la kusameheana kwa wanandoa ni dawa tosha ya kuondoa mikosi ya safari ya ndoa iliyojaa kila aina ya vizingiti. Pamoja na hayo jambo lingine ambalo nalo kwa namna moja ama nyingine limechangia kuzifanya ndoa nyingi ziwe katika majuto ni wakati wa tendo la ndoa.

Eneo hili ndiyo kiungo kikubwa kwa wanandoa. Sijawahi kusikia wala kuona eti mtu ameo ama kuolewa kwa ajili ya kufanya kazi za ndani au kumnunulia nguo mkeo na kuishi kama dada na kaka. Niimani yangu kuwa, kama kungekuwa na hali hiyo, suala la kuoa na kuolewa lisingekuwa na umhimu wowote.


Hakuna raha yoyote ambayo mwanandoa huwa anaifurahia kama tendo la ndoa. Mungu aliamua kuweka kitendo hicho kwa makusudi kabisa na alijua eneo hilo ndio muunganiko wa wanandoa. Raha inayopatikana wakati wa kufanya tendo la ndoa huwa kubwa ajabu na kumfanya mtu hata kama alikuwa na mawazo furani kuyasahau ghafla na kujikuta yupo katika ulimwengu mwingine wenye raha za kila namna na hasa anapofika kileleni hata kama kutakuwa na mtu anataka kumuua kwa bunduki atakubali afe lakini haja yake itimie.

Nikisema hivyo kwa wanandoa wote naamini mnanielewa. Hata hivyo raha hiyo ukolea zaidi pindi wanandoa wanapokuwa na uelewa wa kina katika masuala ya kuandaana vema ambapo ndani ya maandalizi hayo pia wahusika hujikuta wanahama katika ulimwengu huu na kujiona wapo anga jingine kabisa. Mwanamke anapoandaliwa na kushikwa sehemu muhimu kwake naye mawazo yake huhama katika anga hii na kujihisi yupo kwenye anga yenye raha za ajabu isiyo na matatizo hata kidogo na raha hiyo hukolezwa na mwanaume anapotumia utundu wake wote wakati wa maandalizi kwa mwenza wake.

Lakini kuna baadhi ya wanandoa huwa hawaoni raha ya tendo hilo na inapofika wakati mwenzake akamhitaji hukosa raha na kuona kama ameingia kwenye safari ya mateso makali. Na hili mara nyingi huwakumba wanawake ambao waume zao hawaju kuwaandaa vema badala yake hupanda juu na kutimiza haja zake kisha anamuacha mwanamke akiwa katika maumivu makali ya kutaka afikishwe kileleni, na mfikishaji wakati huo anakuwa hoi bini taabani.

Ni vizuri utambue kuwa unapoamua kufanya tendo la ndoa ni vema ukajua mahitaji ya mwenzio iwe mwanaume/mwanamke, jaribu kufamnyia mwenza wako vitu vya tofauti na alivyovizoea ama ambayo anatarajia kuviona kwako kutokana na mazoea. Ukifanya hiyvo utamfanya aendelee kuwa na hamu ya kuwa na wewe kwa muda mrefu.

Naweza kusema mwacheni Mungun aitwe Mungu. Mara nyingi mtoto anapozaliwa kuna baadhi ya vitu huwa anafundishwa lakini baadhi ya vitu huwa havihitaji kufundishwa. Kwa mfano hakuna mtu anayemfundish mtoto kulia, kunyonya, kujisaidia, kucheka, kulala na nk. Japo kuna baadhi ya vitu ambavyo pindi akikua atatakiwa kuachana navyo na kufanya vya kiutu uzima kama suala la kujisaidia. Kwa sababu yeye hujisaidia ndani ya nguo yake ama popote pale, hivyo hufika muda akaelekezwa jinsi ya kujisaidia kuliko salama. Ndivyo hivyo na katika ndoa. Hakuna mtu aliyewahi kufundishwa jinsi ya kufanya tendo la ndoa. Wewe hapo ni shahidi, lakini kuna baadhi ya vitu hulazimishwa kufundishwa kulingana na mazingira husika. Ndiyo maana kuna baadhi ya makabila kuwafunda watoto wao kabla ya kuingia katika masuala ya ndoa.

Hivi ni baadhi ya vitu ambavyo vinaweza kukusaidia katika kuifanya ndoa yako iwe imara ya yenye fufaraha wakati wote;

A. Uwe mbunifu wa kuangalia ni sehemu ipi ukimshika mke/mumeo anasisimka
B. Ujue mwili wako na wa mpenzi wako kwa kila mmoja wapi aguswe ili asikie raha
C. Mweleze mwenzako sehemu ambapo unapenda awe anazichezea ili akupe hisia zaidi
D. Jiamini katika kutafuta mitindo ambayo itakuwa faida kwa ndoa yenu
E. Kila mmoja awe wazi kwa mwenzake na ushirikiano wa mpenzi yenu uwe mzuri.
F. Ujue sehemu za kumsisimua kwa utundu na ufundi wako mwenyewe
G. Muulize sehemu anazopata msisimko ili uzifanye naye asike raha wakati wa faragha
H. Yajue yanayomkosesha raha ya kufurahia tendo la ndoa
I . Yajue mambo yanayomletea hisia haraka za kufanya mapenzi


Ieleweke kwamba, kila mtu ana maeneo yake muhimu ya kusisimka akiguswa.
Watafiti wa masuala ya ndoa wansema kuwa, maandaalizi mazuri kwa ajili ya tendo la ndoa huchukua muda wa dakika 20 hadi 30 ili kila mmoja awe tayari kwa ajili ya tendo hilo takatifu.
Kila mmoja asiwe na haraka, tumia muda mrefu kufurahia tendo hilo kwa pamoja na mpenzi wako. Ieleweke pia kwamba kila mtu anasehemu yake ya kuguswa ambayo humfanya asikie raha wakati wa maandalizi. Ni vizuri kuwa na mawasiliano mazuri ili kila mmoja afurahie maandalizi ya tendo la ndoa.


IMENDALIWA KWA HISANI YA MASOMO YA NDOA - MAPENDO NA NDOA - MWANAUME NA MWANAMKE KATIKA MPANGO WA MUNGU
 
Yote haya na muda huu plus bayan?

Afu kwa nini watu hudhani wanamme wa kiafrika wa zamani hawawafikishi wanawake? Mko very wrong aisee kwenye hili.
 
hii ni research paper au project!!!!!!!!!!!!!!!!!!!:heh:
 
duuuuh we jamaa hauwezi kua serious yani nime copy na kupaste kwenye ms word zimefika 37 pages na sijazisort vizuri fonts etc nauhakika zinaweza fika more than 40 pages which is an equivalent to a dissertation daahhh mzeiyer umetishaaaa....!!!!
 
... Kila mtu yu na namna yake ya pekee...
===
img-thing


Tendo la ndoa:

... ndilo tendo la furaha lililo kuu kwa binadamu.Wakati tendo hilo kwa wanyama lipo kwa ajili ya kuzaa,kwa upande wa binadamu ni zaidi ya kuzaa.Mapenzi au tendo la ndoa ni sanaa hivyo inatakiwa ufundi na ubunifu ili kuweza kufurahia tendo hili.Yafuatayo ni maeneo 12 yenye msisimko na kamamwanaume utayashughulikia ipasavyo bila shaka mtafurahia uumbaji wake Mungu.
1. MIDOMO YAKE.
Tumia midomo yako,ulimi wako na meno yako kuchezea mdomo wake wa juu na wa chini na umbusu kwa msisimko mkubwa.Kunyonya ulimi pia huchangia kuongeza kasi ya mwanamke kwenda kileleni.(usafi wa kinywa kwa wote wawili ni muhimu).
2. UKE NA KINEMBE.
Tumia kidole chako cha kwanza cha mkono wa kulia polepole pitisha katika mfereji wa uke ukianzia chini (kutokea kwenye ******) ukipandisha juu,fanya hivyo mara kadhaa.Kutegemea umbo lako na urefu,unaweza kuchanganya zoezi hili na kunyonya matiti yake na hapoutaona upumuaji wake ukibadilika na majimaji yakiongezeka kwenye uke. Kwa kawaida kinembe cha mwanamke kimejificha lakini ukifanya vizuri zoezi la hapo juu na chenyewe kama uume kitajaa damu na kuinuka.Kinembe kipo juu kabisa ya mfereji wa uke na kina ukubwa wa harage au kwa wanawake wengine huwa kidogo zaidi.Tumia kidole chako cha kwanza na taratibuzungusha zungusha kidole juu ya kinembe,pandisha na kushusha kidole chako na hapo unaweza kumfikisha kwenye kilele cha utamuwa mapenzi hata kabla ya hujaiingiza uume. Wanawake wengiwatafurahia ukitumia uume wako uliosimama vizuri kupigapiga eneo la kinembe nah ii huufanya uume kuwa wa moto na unapomwingilia joto la uume wako litafanya raha ya tendo hili kuwa kubwa zaidi.
Kinembe ndio sehemu ambayo kwa asilima 80 huhusika na kazi ya kumfikisha mwanamke kileleni na kwa kuwa kinembe kiko mbali kidogo toka kwenye tundu la uke,siorahisi kwa uume kukifikia kinembe,hivyo mwanaume anatakiwa ajisukume kwa makusudikabisa kwenda mbele ili shina la uumelisugue kinembe wakati wa kuingia na kutoka kwa uume.
3. MATITI YAKE.
Matiti yake ni sehemu muhimu sana kwa mwanamke kama ilivyo kwa uke wake.Utampatia raha kamili mwanamke kama utayapapasa papasa matiti yake,utayaminyaminya kwa upole wa kimahaba,utayalambalamba na kuyanyonya.
4. MASIKIO YAKE.
Wanawake wengi hupata burudani masikio yao yanapolambwa au kunyonywa au kupigwa busu.
5. SEHEMU YA NYUMA YA SHINGO
Tumia ulimi wako kulamba sehemu ya shingo yake kwa mwendo w kutekenya tekenya.Tumia ncha ya ulimi kutekenya tekenya kwa kufanya mduara na kuendelea kuchora mduara na kurudiarudia.
6. SEHEMU YA NYUMA YA GOTI.
Sehemu ya nyuma ya goti ina miishiomingi ya mishipa ya fahamu na utashangaa jinsi ammbavyo mwanamke atapata burudani kwa kuishughulikia vyema sehemu hii.
7. SEHEMU YA NDANI YA MAPAJA.
Tumia ubapa wa kiganja chake kupapasa kwa ulaini sehemu ya ndani ya mapaja yake,fanya hivyo juu juu huku ukimbusu busu mapaja yake.
8. ****** YAKE.
Wanawake wengi wanapenda****** yao yachezewe kimahaba,anza kwa kuyapapasa papasa,endelea kwa kuyaminya minya kwa kutumia vidole.
9. MIISHO YAKE.
Miguu yake imejaa miishio ya mishipa ya fahamu kiasi ambacho baadhi ya wanawake wanaweza kufika katika kilele cha burudani ya tendo la ndoa kwa miguu yao kusuguliwa na kupapaswa.
10. USO WAKE.
Mwanamke atafurahi sana utakaposhika uso wake katika hali ya mahaba na huku ukitabasamu.Wakati ukifanya hivyo unaweza kumbusu midomo yake,mashavu na kwenye paji la uso.
11. HIPS ZAKE.
Sehemu hii ni moja ya sehemu ambazo zitamfanya mwanamke ajisikie amekubalika kabisa iwapo utashika wakati wa tendo la ndoa.
12. G-SPOT
Sehemu hii iko ndani ya uke ambayo inapata hisia kubwa sana ikibonyezwa bonyezwa,sehemu hii ipo sentimeta 5 kutoka mlango wa uke na iko katika ukuta wa juu wa uke.Sehemu hii ikibonyezwa na kuchezewa ipasavyo mwanamke anaweza akapiz mara mbili au zaidi kwa wakati mmoja.Hii ni njia rahisi ya kumfikisha mwanamke kileleni,mwanaume aingize kidole kwenye uke na kubonyeza na kusugua sehemu ya juu ya uke,sehemu hii imekaa kama sponji na huwa ngumu kwa kadiri inavyobonyezwa.Mwanamke anaweza kujisikia kama anataka kukojoa kabisa na hawezi kukojoa ila raha atakayopata ni kubwa sana.
NB.Ni muhimu kutambua kuwa sehemu hizi 12 sio kama msarafu,hutofautiana kutoka mtu namtu.Suala lililo muhimu sana ni wawili wapendanao kuwa wawazi na wawe na uhuru wa kuambiana jinsi wanavyojisikia.

... Kwa hisani ya mtandao.
 
Nia yako ni nzuri. Ungeweka kwa awamu ( yaani sehemu ya 1....ya pili n.k) maana kumeza yote hayo kwa wakati mmoja digestion inakua issue. Wengine vimchina vinaleta kadhia
 
nafikiri ingenisaidia sana kuishi vizuri na mama glory lakini inahitaji muda ili kuisoma na kuielewa, inahitaji mtu uwe na muda wa kutosha ili kuitendea haki cuz hiyo sio movie useme unaeza ku-foward na bado ukapata concept nzima, inahitaji muda kwa kweli na wala suala la uvivu
 
Ilo zoez unadhan ni dogo et, wataalam wanasema ukimaliza mshindo mmoja ni sawa na kukimbia kwa speed ya 30/km umbali wa km 4 kwa mshindo mmoja bila kupumzika,

Kwanini usilale hoi
 
Back
Top Bottom