makoye2009
JF-Expert Member
- Jun 12, 2009
- 2,638
- 1,218
Wana JF,
Nina hakika kwa sasa kila Mtz anasubiria kwa hamu kusikia Rais Kiwete akitaja safu ya Baraza jipya la Mawaziri baada ya mtikisiko wa Operesheni Tokomeza Ujangiri ambayo imeacha Mawaziri wanne wakifutwa kazi. Hii itakuwa ni mara ya 3 au 4 kwa Rais Kiwete kufumua Baraza lake la Mawaziri.
Pamoja na Semina na Warsha za Ngurundoto inaonekana Mawaziri hawakuwahi wala hawajawahi kuelewa somo.Kwa mtaji huo Kiwete atendeleakubadilisha Mawaziri kila wakti kwa vile inaonekana kuna tatizo kubwa katika uteuzi wa Mawaziri wa Serikali ya CCM. Ni dhahiri na siyo siri kuwa Mawaziri wengi wanapewa nafasi hizo kiundugu,kiushikaji,kiurafiki,kiudini na pengine kiumakundi ndani ya Serikali ya CCM.
Mawaziri wengi hawapewi kulingana na Uweledi wao(professionalism) katika maeneo husika(wizara).Nakumbuka Rais Kiwete kuna wati akiwahi kutamka kuwa Uwaziri HAUSOMEWI! Nafikiri hii haikuwa lugha sahihi. Pamoja na kwamba Uwaziri hausomewi ni lazima Waziri anayetuliwa kwenye nafasi husika awe na uweledi wa Wizara hiyo hata siyo core business kwenye wizara husika lakini awe na utaalamu wa Kuongoza na Kusimamia( Management and Administration). Kuna Wizara kama ya Afya, huwezi kuweka kwenye Wizara hiyo mtu ambaye amesomea UALIMU(Teaching) au SHERIA(Laws) hataweza, kuna mahali atachemka tu maana siyo profession yake!
Kuna msemo unasema hivi, ninanukuu ''PEOPLE DELIVERS WHAT YOU INSPECT NOT WHAT YOU EXPECT'' mwisho wa kunukuu. Maana yake ni nini. Kwamba watu watakuletee kitu kizuri tu iwapo wewe mwenyewe umekigua na si vinginevo. Kama unakaa tu ofisini ukitegemea uletewe kitu kizuri bila ya kukagua sahau!
Ndiyo maana leo tunazungumzia Mawaziri mizigo. Kama Waziri anakaa ofisini tu kupulizwa na kiyoyozi, kusaini mikataba ya kifisadi na kuidhinisha vocha na hundi za vikao visivyoisha vya semina,warsha,makongamano na mikukuta lazima atakuwa mzigo. Waziri anayekaa ofisini kupigwa kiyoyozi(AC) na akitoka ofisini anaingia kwenye Shangingi na na anaendelea kupulizwa na baridi ya kiyoyozi cha Shangingi halafu anategemea BIG RESULTS NOW lazima awe mzigo!
Kwa Mawaziri kama lazima itakula kwao. Operesheni Tokomeza Ujangiri imeonyesha wazi kuwa hawa jamaa 4 waliotimuliwa walikuwa ni aina hiyo ya Mawaziri! BIG RESULTS NOW imekuwa BIG RESULTS NOT!!!!
Huwezi kupata BIG RESULTS NOW kwa kujifungia ofisini! No sir. Mwalimu JK Nyerere(RIP) pamoja nakuwa Mkuu wa nchi kama Rais alikuwa anatoka kwenda kutembelea Wananchi. Kuna picha zinaonyesha alikuwa akifka kwenye mashamba ya Vijiji vya Ujamaa anashika jembe na kupiga ngwe! Huu ndiyo uongozi. Siku zote Mwalimu alikuwa akiwaambia watu kuwa kuongoza ni kuonyesha njia. Leo hii ni vigumu sana kupata viongozi aina ya Mwalimu. Inashangaza kuwa mtu akishapata madaraka whether ya Uwaziri,Ubunge,U-RC,U-DC ni kufikiria namna ya kuifisadi Tanzania kwa kutumia wadhfa aliopewa!
Chonde chonde wale mtakaoteuliwa ikiwa ni kwa sababu za kishikaji,kiurafiki,kiundugu,umakundi au kidini lazim mjipime, mtafkari na kuona kama kweli mnastahili na mtaweza kusimamia na kuongoza Wizara hizo. Kama mnafikiri Uwaziri ni kuuchinja/kuukata au kufaidi nchi basi muda si mrefu hizo ofisi mtaziona za moto na itakula kwenu. Kuongoza ni kuonyesha Njia. Kuna tofauti kubwa sana ya Kuongoza na Kutawala. Pengine ndiyo maana kila siku Chama Twawala CCM kila siku kuna kuwa na mabadiliko ya Baraza la Mawaziri kwa vile wa n Watawala na si viongozi! Mtawala hana tofauti na Dikteta. Hawa wote hutawala kwa mabavu na kwa kulazimisha mabo bila kutumia busara. Kwa mtawala au Dikteta kwake neno Demokrsia ni nadra kutamkwa. Yuko tayari kuua wale wale anaowatawala ili abakie madarakani!!!Kwa sasa Tanzania imeshaanza kuelekea kwenye mkondo huo. Tumeshuhudia Watawala wa CCM wanavyopambana na vyama vya upinzani kwa kuratibu hata mipango ya mauaji ili waendelee kutawala nchi hii milele!(kwa kauli zao wenyewe). Kumbukeni Watanzania wa sasa wameelimika, wamesoma na wanaelewa mambo kwa upana mkubwa kuliko hata baadhi ya Mawaziri.
Karibuni kwenye Baraza jipya la Mawaziri na kazi kwenu.
Nina hakika kwa sasa kila Mtz anasubiria kwa hamu kusikia Rais Kiwete akitaja safu ya Baraza jipya la Mawaziri baada ya mtikisiko wa Operesheni Tokomeza Ujangiri ambayo imeacha Mawaziri wanne wakifutwa kazi. Hii itakuwa ni mara ya 3 au 4 kwa Rais Kiwete kufumua Baraza lake la Mawaziri.
Pamoja na Semina na Warsha za Ngurundoto inaonekana Mawaziri hawakuwahi wala hawajawahi kuelewa somo.Kwa mtaji huo Kiwete atendeleakubadilisha Mawaziri kila wakti kwa vile inaonekana kuna tatizo kubwa katika uteuzi wa Mawaziri wa Serikali ya CCM. Ni dhahiri na siyo siri kuwa Mawaziri wengi wanapewa nafasi hizo kiundugu,kiushikaji,kiurafiki,kiudini na pengine kiumakundi ndani ya Serikali ya CCM.
Mawaziri wengi hawapewi kulingana na Uweledi wao(professionalism) katika maeneo husika(wizara).Nakumbuka Rais Kiwete kuna wati akiwahi kutamka kuwa Uwaziri HAUSOMEWI! Nafikiri hii haikuwa lugha sahihi. Pamoja na kwamba Uwaziri hausomewi ni lazima Waziri anayetuliwa kwenye nafasi husika awe na uweledi wa Wizara hiyo hata siyo core business kwenye wizara husika lakini awe na utaalamu wa Kuongoza na Kusimamia( Management and Administration). Kuna Wizara kama ya Afya, huwezi kuweka kwenye Wizara hiyo mtu ambaye amesomea UALIMU(Teaching) au SHERIA(Laws) hataweza, kuna mahali atachemka tu maana siyo profession yake!
Kuna msemo unasema hivi, ninanukuu ''PEOPLE DELIVERS WHAT YOU INSPECT NOT WHAT YOU EXPECT'' mwisho wa kunukuu. Maana yake ni nini. Kwamba watu watakuletee kitu kizuri tu iwapo wewe mwenyewe umekigua na si vinginevo. Kama unakaa tu ofisini ukitegemea uletewe kitu kizuri bila ya kukagua sahau!
Ndiyo maana leo tunazungumzia Mawaziri mizigo. Kama Waziri anakaa ofisini tu kupulizwa na kiyoyozi, kusaini mikataba ya kifisadi na kuidhinisha vocha na hundi za vikao visivyoisha vya semina,warsha,makongamano na mikukuta lazima atakuwa mzigo. Waziri anayekaa ofisini kupigwa kiyoyozi(AC) na akitoka ofisini anaingia kwenye Shangingi na na anaendelea kupulizwa na baridi ya kiyoyozi cha Shangingi halafu anategemea BIG RESULTS NOW lazima awe mzigo!
Kwa Mawaziri kama lazima itakula kwao. Operesheni Tokomeza Ujangiri imeonyesha wazi kuwa hawa jamaa 4 waliotimuliwa walikuwa ni aina hiyo ya Mawaziri! BIG RESULTS NOW imekuwa BIG RESULTS NOT!!!!
Huwezi kupata BIG RESULTS NOW kwa kujifungia ofisini! No sir. Mwalimu JK Nyerere(RIP) pamoja nakuwa Mkuu wa nchi kama Rais alikuwa anatoka kwenda kutembelea Wananchi. Kuna picha zinaonyesha alikuwa akifka kwenye mashamba ya Vijiji vya Ujamaa anashika jembe na kupiga ngwe! Huu ndiyo uongozi. Siku zote Mwalimu alikuwa akiwaambia watu kuwa kuongoza ni kuonyesha njia. Leo hii ni vigumu sana kupata viongozi aina ya Mwalimu. Inashangaza kuwa mtu akishapata madaraka whether ya Uwaziri,Ubunge,U-RC,U-DC ni kufikiria namna ya kuifisadi Tanzania kwa kutumia wadhfa aliopewa!
Chonde chonde wale mtakaoteuliwa ikiwa ni kwa sababu za kishikaji,kiurafiki,kiundugu,umakundi au kidini lazim mjipime, mtafkari na kuona kama kweli mnastahili na mtaweza kusimamia na kuongoza Wizara hizo. Kama mnafikiri Uwaziri ni kuuchinja/kuukata au kufaidi nchi basi muda si mrefu hizo ofisi mtaziona za moto na itakula kwenu. Kuongoza ni kuonyesha Njia. Kuna tofauti kubwa sana ya Kuongoza na Kutawala. Pengine ndiyo maana kila siku Chama Twawala CCM kila siku kuna kuwa na mabadiliko ya Baraza la Mawaziri kwa vile wa n Watawala na si viongozi! Mtawala hana tofauti na Dikteta. Hawa wote hutawala kwa mabavu na kwa kulazimisha mabo bila kutumia busara. Kwa mtawala au Dikteta kwake neno Demokrsia ni nadra kutamkwa. Yuko tayari kuua wale wale anaowatawala ili abakie madarakani!!!Kwa sasa Tanzania imeshaanza kuelekea kwenye mkondo huo. Tumeshuhudia Watawala wa CCM wanavyopambana na vyama vya upinzani kwa kuratibu hata mipango ya mauaji ili waendelee kutawala nchi hii milele!(kwa kauli zao wenyewe). Kumbukeni Watanzania wa sasa wameelimika, wamesoma na wanaelewa mambo kwa upana mkubwa kuliko hata baadhi ya Mawaziri.
Karibuni kwenye Baraza jipya la Mawaziri na kazi kwenu.