Sometimes the Nerd/Zoba Gets The Girl

lara 1

JF-Expert Member
Jun 10, 2012
15,700
29,111
Namasteeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee!!!! Mai tumse pyaar karta hoo! (Kama nimetukana mnisamehe lugha za watu hizi zilikuja na majahazi!)

Mjue nimekuwa so harsh and insensitive dhidi ya broke a.ss na kina lazzy billy, well leo nabadilisha upepo kidogo, ni katika kumuwish HAPPY WEDDING ANIVERSARY , broke ass mstaafu, alieiga kunya kwa tembo akafanikiwa! Najua upo humu HAPPY WEDDING ANIVERSARY BRO! Hii story nachakachua ilia nikija kusutwa na mdundiko kama sio baikoko mje mnisaidie maana walengwa siku hizi popular si utani!

Epilogue! 2004 Form six! Kayumba flani! Sillas!

Sillas: Mi bana lazima nije nioe demu kisuuu! Talk of the town, si mnajua mimi Muhaya baaana! Siwezi tu kuoa anybody, wakati nimesoma! Hata kama nisipokua na hera kaka mi naoa kisu mtaniambia!

Mob: Aaaah wapi, kwa mshiko gani? Keep dreaming!

Sillas: Tena kuna toto la kichagaa, toto la Prof..... wa Muhimbili pale, toto nalipenda lile sio baraa! Toto lipo very interrigent, famiria nzuri, harina mambo ya wanaume mi nitarioa tu! Prof lazima anikubali! Naaapa namuoa Dori!

Mob: Hahahaaaaa! Mtoto mkaree yule, maisha safi, geti kali, we unaotaaa! Shule yenyewe kayumba umuoe nani? Mmmh! Saizi yako kina mwajuma ndala ndefu!

CHAPTER 1! 2008 Daresalaam!

Dori yupo MUHAS medicine 2nd year, ana date na talk of the university, mchaga mwenzie kijana Dunccan, mwaka wa 5, kila mtu anamjua, harudii nguo, nyweli 2 weeks imefumuliwa, afu mtoto wa Prof, tena anafundisha hapo hapo, aaaah! She could never be happier!

Sillas yupo UDSM anateseka na boom hapo kidogo lipo 5000 kwa siku, kwao kanda ya ziwa, anahaha haha tu! Lakini lengo lake la kupata mutoto ya Prof liko pale pale.

Kuna kaundugu ka mbali baina ya pande hizo mbili, wakakutana kwenye harusi, Sillas karusha karata, akawa brushed off politely, the girl had manners! Akamwambia i wish but you are too late n not my type!
Lakini utapata mtu saizi yako! Mjomba Sillas akawa anacheka cheka tu! Utafanyaje? Mmmmh! When money, beauty, brains zikiungana! Masacreeee!

Basi Sillas akawa anakila kwa macho tu! Na akimcheki Dunccan nae mambo byee, money miss road, na kichwani zimo hapo final year chezea Dr.(MD) Dunccan! Hapana chezea and he is handsome too! Wapambe tulimeza wembe!

Ikabidi tumkalishe kikao Sillas tumshauri utazeeka bikra sasa, mwaka wa 2 chuo still you are not getting any? Anhahaaaaa! Its abnormal! Very abnormal! Let the fantasy go now naaah! Afterall we unajitunza huku kule kijana Dunccan anakandamiza vitu sio akili hio! Let it go, tafuta demu PSPA life should go on! You tried! We prayed for you too but it didnt work out!

Akakubali kuanza kukubali huenda it was just a dream! Akatafuta kipoozeo Udsm pale, basi maisha yakaenda!

CHAPTER 2! 2010 Daresalaam? He popped the question! And she said Yes!
Waambiwa kubwa la maadui japo sina ukaribu na toto la prof, nilikuwepo kwenye hio issue! Ilikuwa ni birthday yake bibie Dori, nikamsindikiza shosti wake mmoja, ukumbini hatuna hili wala lile! Mara Dunncan kipindi hio yuko Bullyankhulu mambo ya mgodini, aka propose on his knees! Aaaaaaw! And she said Yes! Aaaaaaaw! It was so sweet! I was so happy for her! Mwaka wa 4, she is cute, handsome responsible bf, an accomplished dad, and a ring too?!!? Life is so unfair! She had it all! Mijicho ilitutoka kama mjusi kabanwa na mlango!

Mda si mda, D akamnunulia Dori Escudo, wachaaaa! Things could never go righter for her! Pete nzitoo kidoleni, akawa anakuja huku D,Dori anaenda bully hivo yani! So sweet!

Sillas hapo ana battle with unemployment! Kachoka kaishaaaa! Broke ass wa ma broke a.ss! Anamshangaa tu Dori na baby wake! Wivu hana ila roho yamuuma! Alikondaje sasa? Siku moja nilishuhudia kwa macho yangu, Dori alitupakiza kwenye ki Escudo chake na Sillas, ilibaki nukta alie! Koo lilimkakuka mwanaume yule! Mie kijiba cha roho na wivu vilinikabaje sasa? Njia nzima Dori anaelezea how they are in love na Danny, and she cant wait to tie the knot! Safari ilikuwa ndefu balaa! Unaweza hisi Mungu hauipo na kama yupo si wako wala wa wote ni wa kina Dunccan na Dori! Mmmmmh! Akajikaza maisha yakaenda!

CHAPTER 3! Love story is over! The bi.tch karma came knocking!
Ya Mungu mengi, huku bully waambiwa kijana Danncan alifanya ka fling kidogoo, ze michepuko you know, ndani ya mwezi bibie wa huko kanda ya ziwa mjamzito, na analeta za i dont have a way out namuoa, be responsible for my actions, fuc.k you! Akaoa huko ziwani kama ,asihara! In 6 month kila kitu CHALIIIIIIII! Mmmmmh! Tukasema uchawi nini? Ndo hivo bibie kaacha! Wakawa hawaongei! Ujuanja kupata jamani sio kuwahi ooooooh! Mwezi huo huo aliooa akamtuma mtu aifate Escudo! Prof alitokwa povu la aerial maana la omo dogo! Ilisikitisha sanaaaa!

Kijana Silas kapata kazi shirika la kiserikali, mhaya yule, Mungu wake kajibu! Akashinda gari kama utani promotion sijui ya voda au airtel ile kitu double cabin! He was officially back! And he was back with a BANG! Wenye wivu tulijinyonga na big g!

Karma is a bit.ch! Akauza ile double cabin akanunua ndinga flani hivi Hyundai Tucson, weweeeeee mambo iko huku!

CHAPTER 4. The dark days!

Bibie Dori akawa mtu wa machozi tu, hana raha, hana gari, hapo yupo intern Amana hospital, ana mawazoje sasa? Alitia huruma mno mno! Basi kijana Sillas ndo akajitolea kuwa Sheuffar, kumzungusha mjini, na mitoko, kazini anapelekwa na dingi yake Prof. na kufatwa. Ila ilikaa kamati ya halmashauri za vichwa vyao kujadiliana kuwa NI JUST FRIENDS! Kijana Sillas akatoa msimamo he doesnt wanna be friends, he wants the cherry for himself. He is in no hurry, but he wants in on the deal when and if the time comes! He just wanta Dori ajue he is not just some guy or the other guy! Mambo ya kwenda kuomba jamvi watia story, anakuja mtu nyuma anaomba jamvi plainly a kuishia nalo ukiwa kati kati ya story.

Dori was indecessive! She used to be the bi.tch that runs the block, afu saivi she is just another girl next door who got dumped! Ouuuch! Yet still Sillas is not his type of guy! But he is so sweet! A chicken ooh dear! And he pays all the bills too, plus he does every thing she wants! Mmmmmmh! Interesting! Akakubaliana na terms they are dating but not in a rush! Anajikaza kaza hivo hivo?

Jumatatu mpaka jtatu full bata mwanzo mwisho, mtoto Dori akamsahau Dunccan! Akitoka kazini ni bata batani, mpaka Prof akanunaa! Hamuoni binti yake! Lakini akashukuru katoka depression!

CHAPTER FIVE! The Spot Light!
Ikawa ndo hivo kijana Sillas kajisogeza kwa Dr. Dori (MD), wako close vibaya mnooo! Alituchapa bakoraa hadi zikatukolea! Ilikuwa birthday yake, kaenda kazini hapo kapangiwa nje ya mji kazi sasa. Dr. Dori hana hili wala lilw, baby wake Sillas the former broke as.s lol! Akamwambia aje amtoe hata dinner! Karudi mwenyewe na bajaji yake kwa Sillas kakuta taa zimezimwa! Kuwashwa waambe tukajimwaga Happy Birthday!!! Weeeeeee! Haikuwa ya kitoto! Bonge la party hadi decor! Moet zilimwagwa, mhaya hapana chezeya kabisaaa! Aliteketeza kitita si utani! Waliomkataa silla walijutaje sasa? Ji party kama lile.? Nomaaa! Alilia machozi!

Akapata masters pale MUHAS tena, chezea baba yako kutangulia mjini, sasa hapo ndo watu walikomaaaa! Wauza maua wa namanga walimpendaje Sillas! Kila jnne na ijumaa baquet of fresh original roses na kadi zina delivwa darasani! "JUST BECAUSE ITS TUESDAY/FRIDAY WITH LOVE SILLA!" Mamaaae! Watu walioshwa tongo tongo! Mahusiano ya watu wengi yaliyumba, huna mia ya kula unadaiwa baquet ya rose japo mara moja kwa mwezi! Halooooooooo! Kantangazeeeeee! Hio billi ilikaa karibia miezi 6. DR. Dori weeee! We ndo umeokota fuko la hela kwenye maandamano!

Usiku, room kidogo ipate obessity, na hivi debonaires pizza walikuwa free delivery upanga, msasani, na masaki, billi ya piza siku ngapi sijui kwa week, analipa Silla! Mitoko ndo usiongeee! Ukileta nguo unauza kuganga njaa anakwambia peleka kwa Dr. Dori anazochagu mpeee hata mia, fata hela! Tobaaaa! Wahaya nawapendaje sasa.? Mko juu kama KLM! Kiukweli bwana yule msweet!

Basi ndoa ikafungwa ziwani huko, pale bukoba mjini, watu wa kamachmu walijaaje.? Ndo hivo! Siku hizi wanaishi wote mujini hapa hapa!

THE NERD GOT THE GIRL INDEED! If you really want something things have a way to work themselves! Mpaka leo Silla ana wivuuu huyo! Bado tu hajaamini he got the girl!

THE END!!!
 
Yaani hapa ulipofikia imeshakuwa nchipa au nchumali harafu unahairisha game mpaka baadaye ! Hujatenda haki!!
 
Ngoja nikamsafishe miguu muhindi najua hadi nirudi utakuwa umemalizia hadithi yako
 
Kama hadithi haijafikia mwisho basi sesemi chochote ....!!!!!!!!!!
 
I like the Thread title & comprehensive contents of the story,,,,wait to follow it up
 
Bora uzilete hivyo tujue ni 'hadisi'...!!
Hivi Nishawahi kukutumia MWALIKO MAALUMU uje usome thread yangu hata moja? Thubutuuuuuuuuuu yako! Tuondolee nzi humu! Nitaleta navotaka hata nikiamua ki hip hop, huwezi kunipangia maisha yako! TOKAAAAAAA!
 
Dah! "Itaendelea" za JF siku hizi zimekuwa ndio nitolee.Umetuonjesha halafu kwenye utamu ndio unakatiza.

Kilichomuumiza bidada ni kauli yake ya "You are not my type".
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom