Hivi karibuni nilisafiri kutoka Dar kwenda mikoa ya kusini. Ndani ya gari nikakuta nimekaa siti moja na mdada mmoja mdogo, umri waweza kuwa kati ya miaka 16-18. Kawaida yangu huwa siyo mzungumzaji sana, labda mpaka mtu mwingine aanzishe mada. Kwa mvao na mwonekano wake alikuwa amependeza vizuri tuu, lakini ikaonekana hakuwa vizuri kiuchumi. Alikuwa ananunua vitu rahisi sana, hata maji alikuwa anauliza kama kuna ya 300.
Tukafika sehemu tukashuka kwa mapumziko ya dk kumi kununua mahitaji na kuchimba dawa. Nikafanya manunuzi ya chakula na vinywaji mara mbili ili nimgawie na yeye. Akafurahi sana na tukajaribu kufahamiana. Nikataka kujua anafanya nini. Akaniambia kuwa aliacha shule akiwa form 2 mwaka jana kwa sababu za kiuchumi, ndo akawa ameenda Dar kutafuta kazi za kuuza duka.
Nikampa pole kwa maswahibu yaliyomkuta. Tulivyokaribia kushuka akaniuliza kuwa nafanya kazi wapi? nikamweleza, akaniomba namba. Tukaachana huku akinishukuru sana kwa msaada wa chakula njiani. Ikawa kila siku usiku ananibip ili nimpigie. kimsingi hakuna hata mada serious za kuzungumza, basi tu kujuliana hali. Baadaye akaanza kunitumia msg za kuniita mpenzi, baby, etc. Akaanza kuniambia ametokea kunipenda, na anataka nimtumie hela na vitu vingine kibao. Jamani, hivi mtu akikusaidia ndo inakuwa automatic gear ya kuwa wapenzi? Mmmh!!!
Tukafika sehemu tukashuka kwa mapumziko ya dk kumi kununua mahitaji na kuchimba dawa. Nikafanya manunuzi ya chakula na vinywaji mara mbili ili nimgawie na yeye. Akafurahi sana na tukajaribu kufahamiana. Nikataka kujua anafanya nini. Akaniambia kuwa aliacha shule akiwa form 2 mwaka jana kwa sababu za kiuchumi, ndo akawa ameenda Dar kutafuta kazi za kuuza duka.
Nikampa pole kwa maswahibu yaliyomkuta. Tulivyokaribia kushuka akaniuliza kuwa nafanya kazi wapi? nikamweleza, akaniomba namba. Tukaachana huku akinishukuru sana kwa msaada wa chakula njiani. Ikawa kila siku usiku ananibip ili nimpigie. kimsingi hakuna hata mada serious za kuzungumza, basi tu kujuliana hali. Baadaye akaanza kunitumia msg za kuniita mpenzi, baby, etc. Akaanza kuniambia ametokea kunipenda, na anataka nimtumie hela na vitu vingine kibao. Jamani, hivi mtu akikusaidia ndo inakuwa automatic gear ya kuwa wapenzi? Mmmh!!!