JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,302
- 5,439
Kundi la Al Shabaab la Somalia limeshambulia kambi ya wanajeshi wa Umoja wa Afrika (AU) katika Mkoa wa Shabelle katikati mwa nchi hiyo, ikidaiwa raia watatu wamepoteza maisha katika mapigano hayo.
Mkazi mmoja anayeishi katika kijiji kilicho karibu na eneo la tukio, alisema baadaye aliona helikopta mbili zikipita na milio ya risasi ikitoka kwao.
Kamanda wa Jeshi wa Shaballe, Col Muse Hassan wapiganaji wa Al-Shabaab wakiwa na silaha nzito walishambulia katika nafasi tofauti. Walitumia gari lililokuwa na bomu likavunja geti ndipo wakaingia na kurushiana risasi kwa saa moja.
Al-Shabaab wamekiri kuhusika na kusema wameua wanajeshi 59 lakini mamlaka zimegoma kutoa idadi ya wanajeshi waliofariki.
Source: CNN