Ndondocha mkuu
JF-Expert Member
- Feb 17, 2014
- 2,351
- 2,732
Habari yenu wanaJF
Poleni na Majukumu ya kila siku, Leo nimekuja kusimulia mawili matatu nayopitia katika harakati zangu nishare nanyi ndugu zangu.
Wanajf mimi Ni muhitimu wa BSc Education(Mathematics and geography) , kama post zangu nyingi zilivyojieleza huko nyuma. Nilihitimu mwaka 2019 November, nilijaribu walau Kuomba tempo katika sekondari mbalimbali hapa mjini Songea lakini sikufanikiwa kupata kwa wakati ule, (labda kwavile Sikua hata na vyeti vya Masomo yangu).
Nilifanikiwa kufungua tuition centre ya Muda wa Likizo December, Nilifanikiwa kupata wanafunzi wa kutosha kwa Kipindi kile ikizingatia nilifanya promotion ya kutosha, mwaka 2020 niliendelea kufundisha tuition centre mbalimbali Nikipata kipato walau cha kununulia mswaki na matumizi mbalimbali, niliweza kufundisha hata Watoto wa Wakubwa wa Mkoa majumbani Mwao.
Muda wa Likizo ya corona nilijichanganya katika kazi ngumu ya kuopoa na kuchimba mchanga kwasababu hata tuition hazikuruhusiwa tena, ilibidi nijivue kutoka mwalimu hadi mchimba mchanga, ni muda ambao nimejifunza mengi sana na nimekutana na wengi sana.
Ipo siku ambayo Nilipata mteja wa mchanga ambaye alikuja kuchukua mchanga kwa tractor ukizingatia tractor haliwezi kubinua ilibidi nichukue Buku ya kushushia mwenyewe, nilipokua nikishusha nyumbani kwa boss nilishangazwa kuona naitwa "teacher" na msichana Mdogo aliyetokea ndani kwa boss Ni mtoto wa boss, nilishusha mzura hadi machoni nikijua atahisi kanifananisha lakini aliita tena kwa msisitizo,.
Hakuamini kuniona pale, Mzee wake alishangaa kuitwa vile, Nilimwambia hujambo Dogo, nikachukua changu nikatembea.
Ipo siku nilipeleka mchanga site nilishangaa kukutana na headmaster wa Shule fulani niliyofanyia field akiwa ndio muhusika inabidi anipatie Pesa, nilifanya maujanja hatimaye hakuweza Nitambua.
Nilikua napakia mchanga wa mwenzangu sikumoja ( nipate 2000 ta haraka) nilishangaa boss akiletwa na bodaboda ambaye nilikua nikimkimbizia Mathematics O-level, alishangaa aliniita mkuu vipi tena? Nilipandisha mzura nikamtazama Nikamwambia Tutaongea boss.
Leo hii nimepeleka mchanga sehemu nimeshangaa kukuta fundi Mkuu ni Dogo aliecha Shule miaka ile akiwa pale sekondari, aliniuliza Bro Upo Huku sikuhizi, Nilimwambia ndio Nipe Dili hizo Niishi.
Kuna MUDA inanibidi niulize kati ya form four tuliohitimu Pamoja hivi nani ni dereva ili walau AKIPATA trip za mchanga anikumbuke na Mimi.
Unajua HAYA maisha hayana huruma, unakuta sometimes unachimba mchanga na Mzee wangu labda mnauza mnapata 50 ,000 Ila unamwambia Basi Mzee Wewe Chukua 20000 mimi Nibaki na 30000 kwa sababu mimi bado najipanga kimaisha, lakini Mzee anakaza anataka 50% anakwambia yeye ndio kaleta gari, no way utafanyaje Sasa.
Maisha yana mengi sana ya kujifunza, unajua ukishamaliza Chuo kama hivi home nako wanajua unaenda kuajiriwa soon, Kuna Muda unamwambia Mzee nipatie hizi Mbao nikachonge kitanda anakwambia Je ukipangiwa kazi Mwanza utaenda nacho? Sasa najiulizaga na nisipopangiwa Mzee itakuaje?
Wazazi wengi wetu wanaamini WANAO tutaajiriwa, yaa Ni kweli, lakini mtuwezeshe PIA kwa Kipindi hiki ambacho hatuna KITU,.
Hakuna mtu asiyependa goodlife, "we need money to go, to do our family matters".
Wanajf kama umefanikiwa usimcheke asiefanikiwa, kama unauwezo basi muwezeshe, kwa kazi nazopiga mtu mwingine mwenye degree kama mimi anaweza kataa kabisa akiona ni kujidharirisha, lakini Naamini mafanikio hayana SIRI.
Naamini katika kusubiri million basi unapaswa utafute Buku.
Unaweza teseka DUNIANI na mbinguni PIA.
Ni Mimi Ndondocha mkuu.
Karibuni kwa mchanga mgumu Songea
0754350882
v
Poleni na Majukumu ya kila siku, Leo nimekuja kusimulia mawili matatu nayopitia katika harakati zangu nishare nanyi ndugu zangu.
Wanajf mimi Ni muhitimu wa BSc Education(Mathematics and geography) , kama post zangu nyingi zilivyojieleza huko nyuma. Nilihitimu mwaka 2019 November, nilijaribu walau Kuomba tempo katika sekondari mbalimbali hapa mjini Songea lakini sikufanikiwa kupata kwa wakati ule, (labda kwavile Sikua hata na vyeti vya Masomo yangu).
Nilifanikiwa kufungua tuition centre ya Muda wa Likizo December, Nilifanikiwa kupata wanafunzi wa kutosha kwa Kipindi kile ikizingatia nilifanya promotion ya kutosha, mwaka 2020 niliendelea kufundisha tuition centre mbalimbali Nikipata kipato walau cha kununulia mswaki na matumizi mbalimbali, niliweza kufundisha hata Watoto wa Wakubwa wa Mkoa majumbani Mwao.
Muda wa Likizo ya corona nilijichanganya katika kazi ngumu ya kuopoa na kuchimba mchanga kwasababu hata tuition hazikuruhusiwa tena, ilibidi nijivue kutoka mwalimu hadi mchimba mchanga, ni muda ambao nimejifunza mengi sana na nimekutana na wengi sana.
Ipo siku ambayo Nilipata mteja wa mchanga ambaye alikuja kuchukua mchanga kwa tractor ukizingatia tractor haliwezi kubinua ilibidi nichukue Buku ya kushushia mwenyewe, nilipokua nikishusha nyumbani kwa boss nilishangazwa kuona naitwa "teacher" na msichana Mdogo aliyetokea ndani kwa boss Ni mtoto wa boss, nilishusha mzura hadi machoni nikijua atahisi kanifananisha lakini aliita tena kwa msisitizo,.
Hakuamini kuniona pale, Mzee wake alishangaa kuitwa vile, Nilimwambia hujambo Dogo, nikachukua changu nikatembea.
Ipo siku nilipeleka mchanga site nilishangaa kukutana na headmaster wa Shule fulani niliyofanyia field akiwa ndio muhusika inabidi anipatie Pesa, nilifanya maujanja hatimaye hakuweza Nitambua.
Nilikua napakia mchanga wa mwenzangu sikumoja ( nipate 2000 ta haraka) nilishangaa boss akiletwa na bodaboda ambaye nilikua nikimkimbizia Mathematics O-level, alishangaa aliniita mkuu vipi tena? Nilipandisha mzura nikamtazama Nikamwambia Tutaongea boss.
Leo hii nimepeleka mchanga sehemu nimeshangaa kukuta fundi Mkuu ni Dogo aliecha Shule miaka ile akiwa pale sekondari, aliniuliza Bro Upo Huku sikuhizi, Nilimwambia ndio Nipe Dili hizo Niishi.
Kuna MUDA inanibidi niulize kati ya form four tuliohitimu Pamoja hivi nani ni dereva ili walau AKIPATA trip za mchanga anikumbuke na Mimi.
Unajua HAYA maisha hayana huruma, unakuta sometimes unachimba mchanga na Mzee wangu labda mnauza mnapata 50 ,000 Ila unamwambia Basi Mzee Wewe Chukua 20000 mimi Nibaki na 30000 kwa sababu mimi bado najipanga kimaisha, lakini Mzee anakaza anataka 50% anakwambia yeye ndio kaleta gari, no way utafanyaje Sasa.
Maisha yana mengi sana ya kujifunza, unajua ukishamaliza Chuo kama hivi home nako wanajua unaenda kuajiriwa soon, Kuna Muda unamwambia Mzee nipatie hizi Mbao nikachonge kitanda anakwambia Je ukipangiwa kazi Mwanza utaenda nacho? Sasa najiulizaga na nisipopangiwa Mzee itakuaje?
Wazazi wengi wetu wanaamini WANAO tutaajiriwa, yaa Ni kweli, lakini mtuwezeshe PIA kwa Kipindi hiki ambacho hatuna KITU,.
Hakuna mtu asiyependa goodlife, "we need money to go, to do our family matters".
Wanajf kama umefanikiwa usimcheke asiefanikiwa, kama unauwezo basi muwezeshe, kwa kazi nazopiga mtu mwingine mwenye degree kama mimi anaweza kataa kabisa akiona ni kujidharirisha, lakini Naamini mafanikio hayana SIRI.
Naamini katika kusubiri million basi unapaswa utafute Buku.
Unaweza teseka DUNIANI na mbinguni PIA.
Ni Mimi Ndondocha mkuu.
Karibuni kwa mchanga mgumu Songea
0754350882