Soma majina ya waliokula hela za akaunti ya ESCRO katika ripoti ya PAC iliyomwa leo bungeni!

Hata mie najiuliza endapo waliochukua pesa watawajibika je kwa upande wa watumishi.wa mungu itakuwaje?? Mtumishi wa mungu Pengo chukua hatua na wewe kuhusu hawa watumishi kwani ni hatari pia, pia natoa ushauri kuhusu bank ya mkombozi kwa kuonekana ni bank inayotumia fedha chafu nayo meneja mkuu achukuliwe hatua ili iwe fundisho kwa wafanyakazi wengine.

Mkuu, kuna sheria za nchi na taratibu za dini husika..hata kama ni kiongozi wa dini akiua, akibaka, akifanya utapeli asihukumiwe kwa sababu ya dini?! Kusiwe na double standards..endapo inathibitika wao(Viongozi wa dini wachukuliwe hatua pia(kidini na kikatiba pia)...Hakuna aliyejuu ya sheria ('Sheria ni msumeno'). Shida ni kwamba msumeno huu hukata wanyonge tu na mafisadi wako juu ya sheria.

Hebu imagine fedha hizi angekuwa amekula mwalimu mkuu pengine fedha kwa ajili ya kutengeneza "maabara" madawati, au diwani n.k. Hii ungeisikia katika vyombo vya habari na kusimamishwa kazi mara moja na hukumu yake ingepitishwa right away. Lakini mafisadi tunawabembeleza na hadi leo wako kazini, yaani mwisho wa mwezi huu watalipwawa mshahara na bado watapokea marupurupu, hao viongozi wa dini walivyo wanafiki(No offence to their followers) wako kimya kama magogo tu na wao.

Wonderful enough watu wanategemea the highest/Worst adhabu watakayopata ni kusimamishwa kazi. Hivi kungekuwa na sera(kwa mfano) Anayethibitika ni mwizi/mbadhirifu n.k anyongwe(kama China kama sijakosea) au afungwe maisha baada ya kurudisha fedha na kufilisiwa unadhani upuuzi huu tungekuwa tunajaza thread hapa za ESCROW ESCROW ESCROW?..Hapana. Lakini kutokana na mazoea toka katika familia(mkubwa wa familia akikosea anajipa msamaha lakini watoto au wengineo wapate adhabu kali ili iwe fundisho) ndiyo hii inayotokea (mkubwa yuko juu ya sheria) ingawaje haipaswi kuwa hivyo.
 
Paul kimiti si ndie anae miliki mabasi ya network yanayo fanya safari zake sumbawanga to mbeya .kama amekula mgao afilisiwe tu ili iwe fundisho kwa wengine..
 
Kumbe pesa n kubwa kuliko hata mungu mzeee,viongoz wa dini wamekula pesa nawao eee? Wanatufundisha nn as ambao tuko huku chini mungu awape adhabu kari Hawa mafilauni,na pia wamehusishwaje?kwenye heal hz?
 
SOMA MAJINA YA WALIOKULA FEDHA ZA AKAUNTI YA ESCROW KATIKA RIPOTI YA PAC INAYOSOMWA SASA BUNGENI. Zitto:

Upande wa viongozi wa kisiasa ambao waliingiziwa fedha katika akaunti zao binafsi ni;

Mhe. Andrew Chenge (Mb)= shilingi bilioni 1.6.

Mhe. Anna Tibaijuka (Mb) na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi = shilingi bilioni 1.6.

Mhe.William Ngeleja (Mb) na ambaye alikuwa Waziri wa Nishati na Madini = shilingi milioni 40.4

Ndg. Daniel N. Yona ambaye alikuwa pia Waziri wa Nishati na Madini = shilingi milioni 40.4.

Ndg. Paul Kimiti ambaye ni Mbunge Mstaafu wa Jimbo la Sumbawanga = shilingi milioni 40.4

Dr. Enos S. Bukuku ambaye alikuwa Mjumbe wa Bodi ya TANESCO = shilingi milioni 161.7.

Upande wa Majaji

Prof. Eudes Ruhangisa, aliingiziwa milioni 404.25 na J.A.K Mujulizi aliingiziwa shilingi milioni 40.4

upande wa Watumishi wa umma,

Ndg. Philip Saliboko ambaye alikuwa mtumishi wa RITA aliingiziwa shilingi milioni 40.4

Ndg. Emmanuel Daniel Ole Naiko ambaye alikuwa Mkurugenzi Mkuu wa (TIC) aliingiziwa shilingi milioni 40.4

Ndg. Lucy L. Appollo ambaye ni Mtumishi wa TRA aliingiziwa shilingi milioni 80.8.

Viongozi wa Madhehebu ya Dini walioingiziwa fedha na Benki ya Mkombozi

Askofu Methodius Kilaini shilingi 80.9

Askofu Eusebius Nzigirwa shilingi milioni 40.4

Mchungaji Alphonce Twimann Ye Simon shilingi milioni 40.4.

Watu walienda kugawana fedha kwenye Benki tajwa wakiwa na mifuko ya rambo, sandarusi, mabox, magunia na lumbesa TegetaEscrow

Bilioni 73.5 zilitolewa na kugawanywa kwa watu mbalimbali kinyume cha Sheria ya Benki Kuu na Taasisi za Fedha ya 2006

Taarifa ya benki (bank statements) yenye majina na akaunti zote zilizoingiziwa fedha zimeambatishwa.

Kamati imebaini mawasiliano kutoka kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini na Katibu Mkuu Wizara ya Fedha

HAPO VIPI???

Source : copy and paste


Bado tu wanaitwa Waheshimiwa?
 
Hivi yule CEO wa RITA Mhe. Philip Saliboko ameachwaje na wakati alikiuka maadili ya Utumishi wa Umma?
 
WANASIASA
Andrew Chenge (MB) CCM - Bilioni 1.6
Anna Tibaijuka (MB) CCM - Bilioni 1.6
Paul Kimiti (CCM) - Milioni 40.4
William Ngeleja (MB) CCM - Milioni 40.4
Daniel Yona (CCM). - Milioni 40.4

MAJAJI
Jaji Mujulizi - Milioni 40.4
Jaji Ruhangisa - Milioni 404.25

WATUMISHI WA UMMA
Mkurugenzi Mkuu TIC, Emanuel Daniel Ole Naiko - Milioni 40.4
Lucy Appollo (TRA) - Milioni 80.8
Dkt. Enos Bukuku (Mjumbe Bodi Ya Tanesco).
Philip Saiboko (RITA) - Milioni 40.4

VIONGOZI WA DINI
Askofu Msaidizi Jimbo Katoliki La Bukoba, Methodius Kilaini - Milioni 80.9
Askofu Msaidizi Jimbo Kuu Katoliki La DSM, Alphonce Twimannye Simon - Milioni 40.4

Mkurugenzi wa TAKUKURU wakati huo alisema kuwa kurudisha fedha zilizochotwa katika akaunti ya Tegeta Escrow hakumsafishi mtu dhidi ya tuhuma za uhujumu uchumi zinazomkabili na kusisitiza kuwa ni lazima sheria ichukue mkondo wake bila kujali cheo cha mtuhumiwa.

Swali ni Je mbona ni miaka mitatu sasa tangu Kalasinga Seth na James Rugemalira wakamatwe kwa tuhuma za uhujumu uchumi, mbona hawa washirika wakuu wa ufisadi huu bado wangali uraiani wakila maisha wengine bungeni na hata wengine Makanisani?

Kwa nini walioshirikiana uhujumu uchumi na Seth na Rugemalira wao wapo mtaani wanakula maisha Bungeni na hata Makanisani?

Kwamba kushtakiwa au kutoshtakiwa nayo inahitaji connection? Kwamba ukifanya uhujumu uchumi kama huna connection ujue utakamatwa na kushtakiwa lakini kama ukifanya ufisadi na uhujumu uchumi ila una connection za kutosha wewe utakuwa salama hutokamatwa wala kushtakiwa maana kwa connection yako ukiguswa tu wataguswa mpaka wakubwa waliostaafu ambao una connection nao? Hakika bongo kila kitu kinahitaji connection, hata ukifa ili msiba wako upewe air time connection inahitaji sana. Yani kwa connection tu leo wahujumu uchumi wengine wanakula maisha ndani ya CCM, ndani ya makanisa, ndani ya bunge, ndani ya taasisi mbali mbali, mitaani huku wahujumu uchumi wasio na connection wakinyea debe magerezani. Kabla huja hujumu uchumi jiulize kwanza, je una connection?

Wakati mmiliki wa Kampuni ya Kufua Umeme ya IPTL, Kalasinga Habinder Sethi na Mfanyabiashara James Rugemarila wao wameendelea kusota rumande kwa mwaka wa tatu sasa kwa kile kinachoitwa eti ni kutokana na upelelezi wa kesi yao ya utakatishaji fedha kutokamilika katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ambapo Hakimu Mwaikambo ameahirisha kesi hiyo hadi Oktober 10, 2019 na washitakiwa wamerudishwa rumande.
_
Washitakiwa kwa pamoja wanakabiliwa na mashitaka 12 yakiwemo ya utakatishaji fedha na kusababisha hasara ya Dola za Marekani Milioni 22,198,544.60 na Sh.Bilioni 309,461,300,158.27 ambapo kwa mara ya kwanza walifikishwa Mahakamani hapo Juni 19, 2017.
...
Mtemi Andrew Chenge, Mbunge wa Bariadi (CCM) aliwahi kusema hadharani kwamba "wakumkamata yupo lakini haoni mtu wa kumshitaki". Na kweli hadi leo si kukamatwa tu bali hata kushtakiwa hajashtakiwa.

Ni katika ufisadi huu tulimsikia Anna Tibaijuka ambaye ni Mbunge wa Muleba Kusini (CCM) akisema zile bilioni 1.6 alizochotewa na Rugemalira ni " tuhela twa mboga". Tukamsikia Chenge akisema alichopewa yeye ni vijisenti tu. Yaani kama bilioni 1.6 aliyopewa Change ni vijisenti tu hebu jiulize hao wengine ambao hawatajwi katika huu ufisadi walipewa nini? Na pengine ndio sababu ya Chenge kusema wa kumkamata yupo Ila haoni wa kumshtaki kwa kuwa anajua akishtakiwa ataenda kuchomoa betrii katikati ya hekaheka za uchotaji mafuta na wote wataungulia humo. Na pengine ndio sababu badala ya Chenge kukamatwa na kushtakiwa amepewa cheo cha kua Mwenyekiti wa Bunge katika Bunge na Serikali inayojinasibu kupambana na UFISADI.

Binafsi sina tatizo na kuwekwa ndani Seth na Rugemalira, tatizo langu ni KWA NINI WALIOSHIRIKIANA NA HAWA JAMAA WAPO KITAAN WANAKULA MAISHA na hata wengine tunawaona huko Bunge? Orodha ya washirika wa ufisadi huu iliwekwa wazi na kiwango cha pesa mafisadi wenza walichochotewa, wengine ni Maaskofu. Mbona wako uraiani.

William Ngeleja, Mbunge wa Sengerema (CCM) alitangaza kurudisha fedha alizochotewa, tukasikia kila mtu akizikana si TRA sio nani. Leo nani anajua zile fedha alizotapika Ngeleja ziko wapi?

Leo nasikia na Prof. Anna Tibaijuka naye kashikwa na kichefuchefu na kutangaza kutapika zile bilioni 1.6 (hela za mboga). Sijui nazo kila mtu atazikana?

Can you imagine watu wako gerezani miaka mitatu sasa kwa kile kinachoitwa upelelezi haujakamilika, alafu leo mtu anatokea na kusema njooni kwangu mtubu enyi wenye DHAMBI na kulemewa na mizigo, mlipe mpate UHURU kwa maana nira yangu ni laini na mzigo wangu ni mwepesi. Lazima tujiulize ni nani anachelewesha kesi hizi, ni nani anachelewesha ushahidi na upelelezi. Je ni upande wa upelelezi, serikali au Mahakama? Kwa nini hatua zisichukuliwe ikiwa kuna nia ya dhati?

Ni vigumu kuamini unaweza washitaki hawa bila kuwashitaki/kuwahusisha walioshirikiana nao ambao ushahidi wa nyaraka uliwekwa wazi.

Bwana yule Mungu aje amlipe kutokana na matendo yake!!

Mwaka wa tatu eti upelelezi haujakamilika, na watu kila siku wanaingia kazini/ofisini na mwisho wa mwezi wanalipwa mishahara na posho!!

Hata kama kweli walifanya makosa, ila kuwaweka watu ndani miaka mitatu huku kila wakati mkidai upelelezi haujakamilika, si kuwatendea haki hata kidogo. Leo mnawaambia watu watubu watubu nini, kazi ya Mahakama ni nini? Nini lengo lililojificha nyuma ya pazia la hii toba? Je zile Mahakama za mafisadi zinafanya kazi? Je tunatafuta kwa nguvu fedha kwa ajili ya kampeni za uchaguzi?

Nawaona Kalasinga Seth na Rugemalira hawa wameamua KAMA ni kufa basi wacha wafe.
Wamesimamia KWELI ya nafsi zao. Mioyo yao imeota sugu, hawaogopi tena kulala chini, kuumwa na mbu, chawa, kunguni wala viroboto vya Jela. Wameheshimu Nafsi zao na kukubali kuwa kila mtu ataonja mauti.

Huenda anaewasababishia USUMBUFU huu akafa kabla wao hawajafa (Mungu ni Msiri) sana.

Hata wale walioshindwa kuvumilia mateso makali ya gerezani na kuamua kutubu hata kama wanajua hawana makosa au walibambikiwa kesi na kwa kuona kuwa hata hukumu ikija toka hawatopewa HAKI kutokana na kesi na ushahidi kuingiliwa basi nao Mungu ni muaminifu atawalipia kisasi.

Mene Mene Tekel na Peres!

Ki Ben 10
Sauti ya wasio na sauti
Screenshot_20191004-003210_Facebook-01.jpeg
 
WANASIASA
Andrew Chenge (MB) CCM - Bilioni 1.6
Anna Tibaijuka (MB) CCM - Bilioni 1.6
Paul Kimiti (CCM) - Milioni 40.4
William Ngeleja (MB) CCM - Milioni 40.4
Daniel Yona (CCM). - Milioni 40.4

MAJAJI
Jaji Mujulizi - Milioni 40.4
Jaji Ruhangisa - Milioni 404.25

WATUMISHI WA UMMA
Mkurugenzi Mkuu TIC, Emanuel Daniel Ole Naiko - Milioni 40.4
Lucy Appollo (TRA) - Milioni 80.8
Dkt. Enos Bukuku (Mjumbe Bodi Ya Tanesco).
Philip Saiboko (RITA) - Milioni 40.4

VIONGOZI WA DINI
Askofu Msaidizi Jimbo Katoliki La Bukoba, Methodius Kilaini - Milioni 80.9
Askofu Msaidizi Jimbo Kuu Katoliki La DSM, Alphonce Twimannye Simon - Milioni 40.4

Mkurugenzi wa TAKUKURU wakati huo alisema kuwa kurudisha fedha zilizochotwa katika akaunti ya Tegeta Escrow hakumsafishi mtu dhidi ya tuhuma za uhujumu uchumi zinazomkabili na kusisitiza kuwa ni lazima sheria ichukue mkondo wake bila kujali cheo cha mtuhumiwa.

Swali ni Je mbona ni miaka mitatu sasa tangu Kalasinga Seth na James Rugemalira wakamatwe kwa tuhuma za uhujumu uchumi, mbona hawa washirika wakuu wa ufisadi huu bado wangali uraiani wakila maisha wengine bungeni na hata wengine Makanisani?

Kwa nini walioshirikiana uhujumu uchumi na Seth na Rugemalira wao wapo mtaani wanakula maisha Bungeni na hata Makanisani?

Kwamba kushtakiwa au kutoshtakiwa nayo inahitaji connection? Kwamba ukifanya uhujumu uchumi kama huna connection ujue utakamatwa na kushtakiwa lakini kama ukifanya ufisadi na uhujumu uchumi ila una connection za kutosha wewe utakuwa salama hutokamatwa wala kushtakiwa maana kwa connection yako ukiguswa tu wataguswa mpaka wakubwa waliostaafu ambao una connection nao? Hakika bongo kila kitu kinahitaji connection, hata ukifa ili msiba wako upewe air time connection inahitaji sana. Yani kwa connection tu leo wahujumu uchumi wengine wanakula maisha ndani ya CCM, ndani ya makanisa, ndani ya bunge, ndani ya taasisi mbali mbali, mitaani huku wahujumu uchumi wasio na connection wakinyea debe magerezani. Kabla huja hujumu uchumi jiulize kwanza, je una connection?

Wakati mmiliki wa Kampuni ya Kufua Umeme ya IPTL, Kalasinga Habinder Sethi na Mfanyabiashara James Rugemarila wao wameendelea kusota rumande kwa mwaka wa tatu sasa kwa kile kinachoitwa eti ni kutokana na upelelezi wa kesi yao ya utakatishaji fedha kutokamilika katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ambapo Hakimu Mwaikambo ameahirisha kesi hiyo hadi Oktober 10, 2019 na washitakiwa wamerudishwa rumande.
_
Washitakiwa kwa pamoja wanakabiliwa na mashitaka 12 yakiwemo ya utakatishaji fedha na kusababisha hasara ya Dola za Marekani Milioni 22,198,544.60 na Sh.Bilioni 309,461,300,158.27 ambapo kwa mara ya kwanza walifikishwa Mahakamani hapo Juni 19, 2017.
...
Mtemi Andrew Chenge, Mbunge wa Bariadi (CCM) aliwahi kusema hadharani kwamba "wakumkamata yupo lakini haoni mtu wa kumshitaki". Na kweli hadi leo si kukamatwa tu bali hata kushtakiwa hajashtakiwa.

Ni katika ufisadi huu tulimsikia Anna Tibaijuka ambaye ni Mbunge wa Muleba Kusini (CCM) akisema zile bilioni 1.6 alizochotewa na Rugemalira ni " tuhela twa mboga". Tukamsikia Chenge akisema alichopewa yeye ni vijisenti tu. Yaani kama bilioni 1.6 aliyopewa Change ni vijisenti tu hebu jiulize hao wengine ambao hawatajwi katika huu ufisadi walipewa nini? Na pengine ndio sababu ya Chenge kusema wa kumkamata yupo Ila haoni wa kumshtaki kwa kuwa anajua akishtakiwa ataenda kuchomoa betrii katikati ya hekaheka za uchotaji mafuta na wote wataungulia humo. Na pengine ndio sababu badala ya Chenge kukamatwa na kushtakiwa amepewa cheo cha kua Mwenyekiti wa Bunge katika Bunge na Serikali inayojinasibu kupambana na UFISADI.

Binafsi sina tatizo na kuwekwa ndani Seth na Rugemalira, tatizo langu ni KWA NINI WALIOSHIRIKIANA NA HAWA JAMAA WAPO KITAAN WANAKULA MAISHA na hata wengine tunawaona huko Bunge? Orodha ya washirika wa ufisadi huu iliwekwa wazi na kiwango cha pesa mafisadi wenza walichochotewa, wengine ni Maaskofu. Mbona wako uraiani.

William Ngeleja, Mbunge wa Sengerema (CCM) alitangaza kurudisha fedha alizochotewa, tukasikia kila mtu akizikana si TRA sio nani. Leo nani anajua zile fedha alizotapika Ngeleja ziko wapi?

Leo nasikia na Prof. Anna Tibaijuka naye kashikwa na kichefuchefu na kutangaza kutapika zile bilioni 1.6 (hela za mboga). Sijui nazo kila mtu atazikana?

Can you imagine watu wako gerezani miaka mitatu sasa kwa kile kinachoitwa upelelezi haujakamilika, alafu leo mtu anatokea na kusema njooni kwangu mtubu enyi wenye DHAMBI na kulemewa na mizigo, mlipe mpate UHURU kwa maana nira yangu ni laini na mzigo wangu ni mwepesi. Lazima tujiulize ni nani anachelewesha kesi hizi, ni nani anachelewesha ushahidi na upelelezi. Je ni upande wa upelelezi, serikali au Mahakama? Kwa nini hatua zisichukuliwe ikiwa kuna nia ya dhati?

Ni vigumu kuamini unaweza washitaki hawa bila kuwashitaki/kuwahusisha walioshirikiana nao ambao ushahidi wa nyaraka uliwekwa wazi.

Bwana yule Mungu aje amlipe kutokana na matendo yake!!

Mwaka wa tatu eti upelelezi haujakamilika, na watu kila siku wanaingia kazini/ofisini na mwisho wa mwezi wanalipwa mishahara na posho!!

Hata kama kweli walifanya makosa, ila kuwaweka watu ndani miaka mitatu huku kila wakati mkidai upelelezi haujakamilika, si kuwatendea haki hata kidogo. Leo mnawaambia watu watubu watubu nini, kazi ya Mahakama ni nini? Nini lengo lililojificha nyuma ya pazia la hii toba? Je zile Mahakama za mafisadi zinafanya kazi? Je tunatafuta kwa nguvu fedha kwa ajili ya kampeni za uchaguzi?

Nawaona Kalasinga Seth na Rugemalira hawa wameamua KAMA ni kufa basi wacha wafe.
Wamesimamia KWELI ya nafsi zao. Mioyo yao imeota sugu, hawaogopi tena kulala chini, kuumwa na mbu, chawa, kunguni wala viroboto vya Jela. Wameheshimu Nafsi zao na kukubali kuwa kila mtu ataonja mauti.

Huenda anaewasababishia USUMBUFU huu akafa kabla wao hawajafa (Mungu ni Msiri) sana.

Hata wale walioshindwa kuvumilia mateso makali ya gerezani na kuamua kutubu hata kama wanajua hawana makosa au walibambikiwa kesi na kwa kuona kuwa hata hukumu ikija toka hawatopewa HAKI kutokana na kesi na ushahidi kuingiliwa basi nao Mungu ni muaminifu atawalipia kisasi.

Mene Mene Tekel na Peres!

Ki Ben 10
Sauti ya wasio na sautiView attachment 1223084
Wengine tuliambiwa na madam spika kuwa ukiwataja tu umetikisa dola . Je lengo la mapambano haya ni nini kama tunaogopa kutikisa dola. Tumeona Sudan, S Africa , Brazil , South Korea, France nk watu wa aina hiyo wakiwajibishwa mbele za sheria, na nchi zao ni stable. Tz tuking'ang'ania katiba na sheria hii hakuna sababu za watu kujinasibu kuwa wako kwenye vita vya ufisadi . Kwa itakuwa vita vyenye macho. Na tunaambiwa vita havina macho
 
Kimsingi hapo hakuna jambo la msingi isipokowa uonevu mtupu. Sasa kama nikweli jamaa ni wahujumu uchumi iweje makosa wanayo tuhumiwa nayo yawe hayana ushahidi mpaka sasa.? Huu ni uonevu mkubwa lakini nadhani majaji wetu ndio wana yalea haya kwasababu ya kuogopa kupoteza ujaji wake
 
Hivi hiyo migao walikua wanapewa kwa madhumuni yapi na kwanini hasa je, kama posho?mishahara? Faida iliyotokana na hisa walizowekeza au
 
Yule Ndugu aliyesema kuwa fedha za Escrow siyo za Serikali mbona mpaka leo yuko kimya na hajatoa tamko tena kuwa fedha hizo ni za Serikali?.
 
SOMA MAJINA YA WALIOKULA FEDHA ZA AKAUNTI YA ESCROW KATIKA RIPOTI YA PAC INAYOSOMWA SASA BUNGENI.

Zitto: Upande wa viongozi wa kisiasa ambao waliingiziwa fedha katika akaunti zao binafsi ni; Mhe. Andrew Chenge (Mb)

Zitto: Andrew Chenge aliingiziwa shilingi bilioni 1.6. Zitto: Mhe. Anna Tibaijuka (Mb) na Waziri wa 62 Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi shilingi bilioni 1.6.

Zitto: Mhe.William Ngeleja (Mb) na ambaye alikuwa Waziri wa Nishati na Madini alipewa shilingi milioni 40.4 Zitto: Ndg. Daniel N. Yona ambaye alikuwa pia Waziri wa Nishati na Madini alipewa shilingi milioni 40.4.

Zitto: Ndg. Paul Kimiti ambaye ni Mbunge Mstaafu wa Jimbo la Sumbawanga alipewa shilingi milioni 40.4 Zitto: Dr. Enos S. Bukuku ambaye alikuwa Mjumbe wa Bodi ya TANESCO aliingiziwa shilingi milioni 161.7.

Zitto: Upande wa Majaji Prof. Eudes Ruhangisa, aliingiziwa milioni 404.25 na J.A.K Mujulizi aliingiziwa shilingi milioni 40.4

Zitto: kwa upande wa Watumishi wa umma,Ndg. Philip Saliboko ambaye alikuwa mtumishi wa RITA aliingiziwa shilingi milioni 40.4

Zitto: Ndg. Emmanuel Daniel Ole Naiko ambaye alikuwa Mkurugenzi Mkuu wa (TIC) aliingiziwa shilingi milioni 40.4

Zitto: Ndg. Lucy L. Appollo ambaye ni Mtumishi wa TRA aliingiziwa shilingi milioni 80.8. Zitto: Viongozi wa Madhehebu ya Dini walioingiziwa fedha na Benki ya Mkombozi ni Askofu 63 Methodius Kilaini shilingi 80.9

Zitto: Askofu Eusebius Nzigirwa shilingi milioni 40.4 na Mchungaji Alphonce Twimann Ye Simon shilingi milioni 40.4.

Zitto: Watu walienda kugawana fedha kwenye Benki tajwa wakiwa na mifuko ya rambo, sandarusi, mabox, magunia na lumbesa TegetaEscrow

Zitto: Bilioni 73.5 zilitolewa na kugawanywa kwa watu mbalimbali kinyume cha Sheria ya Benki Kuu na Taasisi za Fedha ya 2006

Zitto: Taarifa ya benki (bank statements) yenye majina na akaunti zote zilizoingiziwa fedha zimeambatishwa.

Zitto: Kamati imebaini mawasiliano kutoka kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini na Katibu Mkuu Wizara ya Fedha

Zaidi, soma;


SUKUMA GANG walianza siku nyingi sana.

CCM ni ile ile , hakuna jipya toka tupate uhuru, tunahitaji overhauling ya serikali na katiba mpya.
 
Back
Top Bottom