Mchaga
JF-Expert Member
- Apr 11, 2008
- 1,378
- 204
Soma Majibu ya Selebu wa Kibongo, Hemed Akihojiwa na Zamaradi
Hemed Suleiman ni mmoja wa waigizaji filamu na sinema nchini Tanzania.
Katika video hii, Zamaradi Mketema, mtangazaji wa kituo cha runinga cha CloudsTV anamwuliza maswali kadhaa katika sehemu ya "Mtu Kati" ya kipindi anachokiendesha katika kituo hicho cha runinga.
Mojawapo ya swali aliloulizwa ni, "Umepata nini kupitia sanaa?"
Jibu:
"Kiukweli sanaa imenipa mafanikio mengi.
Aaa, lakini nisingependa yoote niyataje kwa sababu si lazima vitu vingine uongee.
Vitu vingine vinakuwa vyako wewe mwenyewe personal.
Maisha yako unavyoishi, mambo yako unavyoyafanya, vitu ulivyovipata kupitia sanaa, vinakuwa ni maisha yako mwenyewe binafsi.
Lakini kikubwa ambacho ninajivunia kiukweli kuhusu sanaa ni kuzidi kuniweka karibu na mabinti.
Eeh, sanaa inanifanya kila siku naonana na mabinti.
Sanaa inanifanya naongeza upendo kwa mabinti. Kwa sababu mimi kila movie yangu ikitoka, huwa nahesabu ni wanawake wangapi wamenitafuta kupitia hiyo movie, japokuwa movie zinazidiana kwa hiyo kuna movie imenifanya nimetokewa na wasichana wengi kuliko movie nyingine kwa hiyo nina rekodi yangu ambayo ninaiandika kwenye diary.
Kwahiyo in short, sanaa naishukuru, nashukuru sanaa kwa kunipatia mademu."
Kweli mire*** siku hizi hawafanyi kazi
Last edited by a moderator: