konda msafi
JF-Expert Member
- Sep 5, 2018
- 1,666
- 8,523
Muda huu soko lililopo mbele ya Daraja la TAZARA au Mfugale upande wa kushoto kama unatokea Buguruni linateketea kwa moto.
Jina la soko silikumbuki vizuri, sijui linaitwa Vetinari. Chanzo cha habari ni mimi mwenyewe. Nimepita muda huu nimekuta soko linateketea.
Zima moto na gari lao wapo ila naona wanakodoa macho tu.
====
Soko la Vetenari lililopo eneo la Tazara jijini Dar es Salaam linawaka moto.
Kwa mujibu wa Kamanda wa Zimamoto mkoa wa kizimamoto Temeke Mrakibu Msaidizi Michael Bachubira amesema Hadi sasa Jeshi linaendelea kuuzima moto huo na kudhibiti usisambae maeneo mengine na kwamba wanaendelea kuchunguza chanzo cha moto huo.
Hii ni mara ya nne kwa masoko jijini Dar kuungua kwa mwaka huu ambapo mwezi Februari soko la Mbagala likiungua, na Soko la Karume kuungua mara mbili, mwezi Januari na Aprili
====
RC MAKALLA: HITILAFU YA UMEME CHANZO CHA KUUNGUA SOKO LA VETERINARY.
- Asema kazi ya kurejebisha Miundombinu iliyoungua itafanyika usiku na mchana.
- Awahakikishia Wafanyabiashara hakuna atakaehamishwa.
- Asisitiza Masoko kuwa na Fundi umeme anaetambuliwa na TANESCO.
- Aonya tabia ya Mamalishe kuhinjika maharage jioni ili asubuhi wakute yameiva.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Amos Makalla amesema chanzo Cha Moto uliopelekea kuteketea kwa Soko la Veterinary lililopo TAZARA Wilaya ya Temeke ilitokana na Hitilafu ya umeme.
RC Makalla amesema hayo alipotembelea Soko Hilo kujionea uharibifu wa Mali zilizoteketea moto ambapo amesema taarifa za awali zinaonyesha Moto huo umeathiri takribani vibanda 453.
Aidha RC Makalla amesema Serikali inafanya taratibu za haraka kuhakikisha kazi ya kurejesha Miundombinu iliyoharibika inafanyika usiku na mchana ili Wafanyabiashara warudi kuendelea na Biashara Kama awali ambapo ameahidi hakuna mfanyabiashara atakaeondolewa.
Hata hivyo RC Makalla ametoa pole kwa Wafanyabiashara walioathiriwa na Moto huo na kuwataka kuwa watulivu wakati Serikali yao inaendelea kutatua changamoto hiyo.
Kutokana na matukio ya Moto kujirudia Mara kwa Mara, RC Makalla ameendelea kutoa wito kwa Viongozi wa masoko kuhakikisha kila soko linakuwa na fundi umeme anaetambuliwa na TANESCO,Halmashauri kuweka Vifaa vya kudhibiti moto kwenye Kila soko, Wafanyabiashara kuacha tabia ya kuhinjika maharage jioni ili asubuhi wakute yameiva huku akisisitiza Masoko kuwa na Ulinzi.
Jina la soko silikumbuki vizuri, sijui linaitwa Vetinari. Chanzo cha habari ni mimi mwenyewe. Nimepita muda huu nimekuta soko linateketea.
Zima moto na gari lao wapo ila naona wanakodoa macho tu.
====
Soko la Vetenari lililopo eneo la Tazara jijini Dar es Salaam linawaka moto.
Kwa mujibu wa Kamanda wa Zimamoto mkoa wa kizimamoto Temeke Mrakibu Msaidizi Michael Bachubira amesema Hadi sasa Jeshi linaendelea kuuzima moto huo na kudhibiti usisambae maeneo mengine na kwamba wanaendelea kuchunguza chanzo cha moto huo.
Hii ni mara ya nne kwa masoko jijini Dar kuungua kwa mwaka huu ambapo mwezi Februari soko la Mbagala likiungua, na Soko la Karume kuungua mara mbili, mwezi Januari na Aprili
====
RC MAKALLA: HITILAFU YA UMEME CHANZO CHA KUUNGUA SOKO LA VETERINARY.
- Asema kazi ya kurejebisha Miundombinu iliyoungua itafanyika usiku na mchana.
- Awahakikishia Wafanyabiashara hakuna atakaehamishwa.
- Asisitiza Masoko kuwa na Fundi umeme anaetambuliwa na TANESCO.
- Aonya tabia ya Mamalishe kuhinjika maharage jioni ili asubuhi wakute yameiva.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Amos Makalla amesema chanzo Cha Moto uliopelekea kuteketea kwa Soko la Veterinary lililopo TAZARA Wilaya ya Temeke ilitokana na Hitilafu ya umeme.
RC Makalla amesema hayo alipotembelea Soko Hilo kujionea uharibifu wa Mali zilizoteketea moto ambapo amesema taarifa za awali zinaonyesha Moto huo umeathiri takribani vibanda 453.
Aidha RC Makalla amesema Serikali inafanya taratibu za haraka kuhakikisha kazi ya kurejesha Miundombinu iliyoharibika inafanyika usiku na mchana ili Wafanyabiashara warudi kuendelea na Biashara Kama awali ambapo ameahidi hakuna mfanyabiashara atakaeondolewa.
Hata hivyo RC Makalla ametoa pole kwa Wafanyabiashara walioathiriwa na Moto huo na kuwataka kuwa watulivu wakati Serikali yao inaendelea kutatua changamoto hiyo.
Kutokana na matukio ya Moto kujirudia Mara kwa Mara, RC Makalla ameendelea kutoa wito kwa Viongozi wa masoko kuhakikisha kila soko linakuwa na fundi umeme anaetambuliwa na TANESCO,Halmashauri kuweka Vifaa vya kudhibiti moto kwenye Kila soko, Wafanyabiashara kuacha tabia ya kuhinjika maharage jioni ili asubuhi wakute yameiva huku akisisitiza Masoko kuwa na Ulinzi.