Soko la Hisa la Dar es Salaam na orodha ya makampuni yaliyosajiliwa

Ukidhamiria mtu binafsi kununua hisa unakuwa na uhuru wa kufanya utafiti na kuona kampuni yenye mwelekeo wa uchumi mzuri ikiwa ni pamoja na kujua historia ya maendeleo ya kampuni, hayo ni muhimu si kufuata tu matangazo ya biashara, hakuna anayetangaza biashara asiyeisifia chake kuvutia wateja, ila utafiti ndio utakaokupa ukweli.

Katika shauri langu, siku na nafasi ya kuchagua au kufanya upembuzi kwa vile nchi za kibepari makampuni ya kipepari hiyo ni njia moja wapo ya kutumia pesa za wafanyakazi kwa kuongeza ufanisi wa makampuni. Ndio maana huna nafasi ya kuchagua kwa sababu hawakupi hela, inakatwa moja kwa moja na kuingizwa huko nawe unaletewa tu account number yako.

Kuna faida yake kwa nchi kama za ulimwengu wetu wa Tanzania, kwani uchumi hauyumbi sana kama ilivyo kwa mataifa makubwa. Lakini kama ulivyosema si vema kuweka pesa yote huko, bora kuweka hizo unazoona huziihitaji kwa sasa na ambazo huna malengo ya kuchuma faida ya papo kwa papo.

Mambo ya ubia ni ya wenye kipato zaidi, kwa wa kipato cha chini ni vigumu kidogo maana kiwango kinachohitajika ni kikubwa, uzungumzie kuweka mamilioni si malaki. Hata hivyo kuna makampuni madogo siku za usoni yatakayoibuka baada ya elimu hii kuwafikia wengi.

Umemema vema mkuu, naomba nisichakachue saana pointi yako, kwenye bold namaanisha kiasi cha faida utakayopata kutokana na gawio kinakua kidogo kwa kuwa na kiwango kidogo cha shea.
 
Umemema vema mkuu, naomba nisichakachue saana pointi yako, kwenye bold namaanisha kiasi cha faida utakayopata kutokana na gawio kinakua kidogo kwa kuwa na kiwango kidogo cha shea.

Yes, naelekea kuwa na maana hiyo, maana net profit inayopatikana kwenye kampuni ndio gawio linalotegemewa kupata wanahisa kadiri ya % ya kila mwanahisa, hivyo kama ni pesa kidogo hata kama kampuni imezalisha sana hakijai mkononi na aliyeweka gunia ataambulia zaidi ya uliyeweka debe.
 
Nashukuru mkuu, asante kwa kuwa tayari kuendelea kutoa mchango kuhusu suala la hisa, nimeona wenzetu wakenya hata mtu wa kawaida kabisa anawekeza na wanawanunulia watoto wao shea kwenye makampuni. Asante kwa kutoa namba zenu za simu nadhani zitakua na msaad kwa watu wengi sana. Ubarikiwe

Jambo la msingi nakupongeza kuweza kuwafungua akili wengi kwa vile hawajui vema mambo ya kununua hisa, na hata linapotamkwa jambo la hisa za makampuni au serikali wengi huona kama ni viluwiluwi vinavyoelea juu ya maji tu. Hisa ni karibu kitu kile kile ubia.

Kwa wakipato cha kati okay, lakini kwa wakipato cha chini binafsi ningeshauri kurudi nyuma kwenye fikra za nyerere kwamba ubia unaweza kufanya na watu kadhaa wakaunda kitu kikubwa kuliko kuingia kwenye hisa na makampuni makubwa.

Wajasirimali wanaweza kuwa na ubia wao kwa kuanzisha kampuni kama ya usambazaji vile, wakawa na warehouse kwa pamoja ambapo mali wanaziagiza nje kwa pamoja na kuzileta nchini kwenye warehouse yao, na kisha waziuze na nyingine kuzitawanya kwenye kanda au wakawa na zonal warehouse in future.

Wazo hili nimekuwa nalo muda ila nashindwa kupaa watu wa karibu, kwani kufanya kitu kama hicho kunahitajika kuwa na upembuzi wa kujua kila mwanahisia maana wengine uswahili nao ni taabu. Wengi wenye nafasi ya kupenya anga za North America na Ulaya bila kutaabiikia visa, lakini twaweza kupata wabia wazuri? Hapo ndo tatizo.

Lakini kuna wanaoweza inahitajika utafiti na njia hiyo imetokeza makampuni makubwa duniani, ni kujiamini na kuaminiana tu. Vijana kama watano au sita wajipinde na kupata 25 million wanaweza anza na container moja, baada ya mwaka wako mbali maana biashara ya jumla hukua haraka kuliko ya rejareja.
 
Mie sio Mjuzi wa hizo vitu ila nakushauri uende DSE kama upo Dar es Salaam ukajifunze kwa vitendo na utapata watu wa kukuelimisha. Ukiuza hisa zako unishtue.
 
Oi, topic ni ngumu kidogo na maswali yako ni mengi sana ... nafikiri ndo maana watu wameuchuna! Anyway, kuna google na wikipedia, jaribu kupita huko pia, utapata majibu yote!

Katika hali ya ukawaida sana na kwa kutumia lugha ya kiswahili, ngoja nijaribu kukujibu kwa haraka haraka then wengine wataendelea na wewe utapata moyo wa kwenda kwenye internet kutafuta majibu;

a) Hisa ni nini??
Hisa ni sehemu ya umiliki ambapo faida ama hasara mnagawana kulingana na makubaliano.

b) Naweza kuzimiliki kivipi?? ni kimaanisha umri, na kiasi na wapi?? kwa masharti gani??
-Naamini ni kwa kuzinunua tu wakati wa kwanza zinapotangazwa(IPO) ama zinapouzwa na wale waliozinunua kipindi cha awali kabisa(IPO).
-Umri nafikiri ni ule ule wa kisheria kuanzia miaka 18 ingawa unaweza pia kuwanunulia watoto i.e ukanunua kwa niaba ya watoto.
-Kiasi ni kutegema na mgawanyo uliowekwa na wenye kampuni ama kutegemea na upatikani kwani uuzani na ununuaji wake ni kama mnada vile, unaendesha na bei ya soko tu.
-Masharti yanatawaliwa na sheria za nchi zikiwemo pia zile za wenye kampuni mfano idadi ya hisa ambazo mtu mmoja atauziwa, na mwisho wa kuzinunua.

c) Nitapata faida gani kwenye umiliki wa hizo hisa??
-Faida ni nyingi sana ikiwemo kuwa na nguvu ya kufanya maamuzi ikiwemo kuajiri ama kufukuza watendaji katika kampuni husika
-Gawio la faida/fedha ya kampuni kulingana na makubaliano yenu wamiliki i.e kila baada ya miezi 3 or 6 or kila mwisho wa mwaka.
-Kupata gawio mpaka hapo kampuni itakapo kufa au kufilisika/milele
-Mara nyingi sana hisa huwa zinapanda bei kuliko kushuka hivyo ukiamua kuziuza unapata faida zaidi

d) Je nitapataje gawiwo langu kwenye umiliki wa hisa?
-Inategemea lakini wengi wanapewa cheque ama wanaingiziwa fedha kwenye akaunt zao za bank moja kwa moja

e) Hasara zipatikanazo kwa ununuzi wa hisa.
-Faida yake ni ndogo sana kwa walionunua hisa chache
-Rejesho la mtaji wako ni kila baada ya miezi 3 ama 6 ama mara moja kwa mwaka tu!
-Kampuni ikifilisika mnakuwa ni watu wa mwisho kulipwa kile ulichowekeza as wote mnahesabiwa kama wamiliki mliofeli
-Endapo zikishuka bei kwenye soko na ukahitaji kuziuza automatically utapata hasara kwa uwekezaji wako.

f) Nitaijuaje bei ya hisa ama kuna hisa zinauzwa??
-Chanzo kikuu kwa Tanzania ni kwenda Dar es salaam Stock Exchange, DSE hapa Posta Mpya ambapo ndio sokoni kwenyewe
-Angalia taarifa za habari za biashara kwenye TV ama sikiliza habari za kibiashara kwenye redio ama soma magazeti ya biashara kama vile Business Times e.t.c

g) Kwa maisha ya kitanzania is this bussiness valid and does it pay??
-Inalipa popote lakini ni lazima na vizuri sana kuwa na elimu ya kutosha ya kufanya maamuzi yote kwa ujumla


Nakaribisha wataorekebisha, kukosoa ama kuboresha,
 
munisijo kwanza kabisa naomba nikushukuru sana kwa kunifundisha, ukweli elimu ya biashara sina hasa hii ya hisa but natamani sana nijiunge hivyo unaweza kunisaidia sana nikaendelea na kusudi langu iwapo utanijibu maswali haya yafuatayo.

imagine mm gfsonwin nina biashara yangu, ambayo inaniingizia kipato cha halali kabisa, je naweza kulinganisha faida ya biashara yangu binafsi na faida niipatayo kwenye hisa??

pia je naweza kununua hisa kamaa) kikundi cha watu, b) kama kampuni ambayo labda imesajiliwa d) kama biashara tu ambayo imesajiliwa kisheria lkn sio kampuni??

what do you consider to be most benefiting investing on small/medium business or investing on buying shares in terms of cash and usumbufu??

je is it worth saving large amount of money in bank or investing on buying shares?? yaani hapa naangalia which appreciates more than the other??

usinichoke nitasoma kwenye google but nipe kwanza elimu ya msingi.
 
Last edited by a moderator:
munisijo kwanza kabisa naomba nikushukuru sana kwa kunifundisha, ukweli elimu ya biashara sina hasa hii ya hisa but natamani sana nijiunge hivyo unaweza kunisaidia sana nikaendelea na kusudi langu iwapo utanijibu maswali haya yafuatayo.

imagine mm gfsonwin nina biashara yangu, ambayo inaniingizia kipato cha halali kabisa, je naweza kulinganisha faida ya biashara yangu binafsi na faida niipatayo kwenye hisa??

pia je naweza kununua hisa kamaa) kikundi cha watu, b) kama kampuni ambayo labda imesajiliwa d) kama biashara tu ambayo imesajiliwa kisheria lkn sio kampuni??

what do you consider to be most benefiting investing on small/medium business or investing on buying shares in terms of cash and usumbufu??

je is it worth saving large amount of money in bank or investing on buying shares?? yaani hapa naangalia which appreciates more than the other??

usinichoke nitasoma kwenye google but nipe kwanza elimu ya msingi.


Very very sory gfsonwin, yaani hapa nahema juu juu na kama unauona muda its now 1656h, nilikuwa nimekujibu kwa article moja nzuri na ndefu sana ... nasikitika kukuambia kua imefutika kiajabu hapa na kwa muda huu sidhani kama naweza anza tena kuandika upya si unajua foleni zetu za Dar na hasa huku Posta, naweza fika kwangu alfajiri ...

Nitakachofanya, ingawa najua sichoulichokua ukikitaka na uniombee msamaha kwa wahusika wote wanaokuhusu especially kule MMU, nime ku-PM namba yangu ya simu, ni matumaini yangu hutaigawa na baada ya elimu utaifuta ... naahidi MUNGU akipenda kesho na nikiwa huru nitarudi kujibu kwa faida ya wote! Kama haupo vizuri, ni nitumie SMS kuwa ni wewe then nitakupigia ....
 
Last edited by a moderator:
Very very sory gfsonwin, yaani hapa nahema juu juu na kama unauona muda its now 1656h, nilikuwa nimekujibu kwa article moja nzuri na ndefu sana ... nasikitika kukuambia kua imefutika kiajabu hapa na kwa muda huu sidhani kama naweza anza tena kuandika upya si unajua foleni zetu za Dar na hasa huku Posta, naweza fika kwangu alfajiri ...

Nitakachofanya, ingawa najua sichoulichokua ukikitaka na uniombee msamaha kwa wahusika wote wanaokuhusu especially kule MMU, nime ku-PM namba yangu ya simu, ni matumaini yangu hutaigawa na baada ya elimu utaifuta ... naahidi MUNGU akipenda kesho na nikiwa huru nitarudi kujibu kwa faida ya wote! Kama haupo vizuri, ni nitumie SMS kuwa ni wewe then nitakupigia ....

dah! natamani sana urudi uje utufundishe kweli hapa niko na daftari na kalam ninaandika haya nikayasome vizuri. naskitika sana technolojia haija ni feva.
 
asante sana nimeona but inaelekea ni gharama enh!! kwa mfano hisa moja yaweza kuuzwa sh ngapi?? je kapuku kama mm anaweza kununua??

Kwa haraka haraka, bei za hisa chache pale DSE ni kama ifuatavyo ...
TOL 260, TBL 3100, TATEPA 440, TCC 5500, SIMBA 2400, SWISSPORT 1820, TWIGA 2600, DCB 600, NMB 1260, KA 990, EABL 2000, JHL 5860, KCB 440, CRDB ...

bei ya hisa inajipanga yenyewe kutegemea na demand and supply, hivyo bei inaweza kupanda ama kushuka at any time t, ni kama vile forex i.e USD

 
Kwa haraka haraka, bei za hisa chache pale DSE ni kama ifuatavyo ...
TOL 260, TBL 3100, TATEPA 440, TCC 5500, SIMBA 2400, SWISSPORT 1820, TWIGA 2600, DCB 600, NMB 1260, KA 990, EABL 2000, JHL 5860, KCB 440, CRDB ...

bei ya hisa inajipanga yenyewe kutegemea na demand and supply, hivyo bei inaweza kupanda ama kushuka at any time t, ni kama vile forex i.e USD



hizi bei ni kwa tsh ama ni kwa usd??
je ninaweza kusema labda nanunua hisa may be 1000 hivi?? anyway sijui kama unaelewa ninapokwamia kuelewa but najiona ni wapisijui na sijui nisemeje ili unielewe.
 
hizi bei ni kwa tsh ama ni kwa usd??
je ninaweza kusema labda nanunua hisa may be 1000 hivi?? anyway sijui kama unaelewa ninapokwamia kuelewa but najiona ni wapisijui na sijui nisemeje ili unielewe.

Bei zote zipo in tshs, yes unaweza kununua hisa kwa idadi yako kama unao uwezo na unamudu ...

Kwa kukuongezea, mwenye hisa nyingi kwenye kampuni ndio mwenye sauti/decision maker coz kwenye mgogoro wa kimaamuzi, hisa moja ni kura moja na uamuzi uliopata kura nyingi ndo ambao unatakiwa utekelezwe...
 
Bei zote zipo in tshs, yes unaweza kununua hisa kwa idadi yako kama unao uwezo na unamudu ... Kwa kukuongezea, mwenye hisa nyingi kwenye kampuni ndio mwenye sauti/decision maker coz kwenye mgogoro wa kimaamuzi, hisa moja ni kura moja na uamuzi uliopata kura nyingi ndo ambao unatakiwa utekelezwe...

dah! yaani kaka barikiwa sana sana, umenifunza sana but bado nina maswali bado sijui nitakuwa nakulia muda wako??
 
Well, biashara ya hisa kiukweli kwa kwetu Tanzania bado haijawa maarufu au kupewa msisitizo zaidi, inawezekana tatizo kubwa ni elimu au uelewa wa biashara hiyo.Unaponunua hisa kwenye kampuni maana yake umejiingiza kwenye umiliki wa hiyo kampuni.

Lakini nguvu na uwezo wako wa kufanya maamuzi wa hiyo kampuni inategemea na idadi ya hisa unazomiliki na pia jinsi ilivyoelezewa kenywe documents za kampuni (MEMARTS) wakati inaanzishwa.

Kwa mfano miliki anae miliki asilimia 51 na keundelea anakua uwezo wa kufanya maamuzi makubwa kuliko wamiliki wanaomiliki hisa zilizobaki hata kama wako 100.

Nachotaka kumaanisha ni kwamba unapokuwa na hisa nyingi ndio unakua na sauti zaidi. Mfano kampuni ina hisa 2000 na inaziuza kila moja kwa sh 100 ukinunua hisa 100 kwa sh 10000 mana yake utakuwa unamiliki 0.05% ya kampuni husika.

Hivyo basi inapotokea kampuni imefika muda wa kutoa gawio lake aidha imepata faida au hasara itagwanywa kulingana na asilimia ya umiliki wako kwenye hiyo kampuni.

Kiukweli ukiwa na hisa chache unapata gawio dogo sana ukilinganisha na muda.

Kwa sasa na hayo tu mkuu
 
munisijo

imagine mm gfsonwin nina biashara yangu, ambayo inaniingizia kipato cha halali kabisa, je naweza kulinganisha faida ya biashara yangu binafsi na faida niipatayo kwenye hisa??

je is it worth saving large amount of money in bank or investing on buying shares?? yaani hapa naangalia which appreciates more than the other??

Pale pekundu
Kulinganisha faida ya hisa (za public companies) na biashara yako binafsi ni rahisi. Unalinganisha returns. Magawio ya hisa zifanyazo vizuri zaidi hapa Tanzania (TBL, Sigara, nk) ukikokotoa unakuta pesa uliyowekeza inarudisha asilimia 10 - 20 kwa mwaka. Hisa nyingine zinarudisha chini ya hapo, hadi 0% (mfano TOL). Biashara nyingi zinazoenda vizuri zinalipa kuliko hisa.

Pale pa blue
Hapa pia ni kulinganisha returns. Kwa ujumla hisa za kampuni zifanyazo vizuri zinalipa zaidi sana kuliko pesa kukaa benki, kwa vile ni mara chache kukuta benki zikitoa faida ya zaidi ya asilima hata5 kwa mwaka.

Nyongeza
(1) Pamoja na biashara nyingi nzuri kulipa zaidi ya hisa za public companies, bado wafanyabiashara huwekeza sehemu ya fedha zao katika hisa - labda kwa sababu ya risk ndogo zaidi kulinganisha na biashara binafsi.

(2) Tatizo la anayeanza kuingia katika mambo ya hisa ni kujua kampuni nzuri - hapa ndipo mawakala wa soko la hisa watakapokusaidia

(3) Unaweza kusambaza risk kwa kuwekeza katika hisa za kampuni mbalimbali, kwenye amana za benki, nk kwa wakati moja kwa kuwekeza katika mifuko ya Unit Trusts.

Uzoefu wangu kwa Unit Trust of Tanzania ni kwamba returns hazipungui 12% kwa mwaka, ambayo bado ni bora sana kuliko kuweka fedha benki, lakini ni nyuma ya biashara nyingi za uhakika.
 
.
btw ukiwa umenunua hisa ndogo ina maana wewe ndo unakuwa kibaraka wa wenye hisa nyingi??

Hisa ni kama biashara nyingine. Ukiwekeza kidogo unavuna kidogo. Kwa dokezo la mbali returns (magawio) za hisa zetu hapa Tanzania ni kati ya 0% (kwa hisa zisizopeform kama TOL) hadi karibu 20% kwa mwaka (kwa best peformers).
 
Bei zote zipo in tshs, yes unaweza kununua hisa kwa idadi yako kama unao uwezo na unamudu ... Kwa kukuongezea, mwenye hisa nyingi kwenye kampuni ndio mwenye sauti/decision maker coz kwenye mgogoro wa kimaamuzi, hisa moja ni kura moja na uamuzi uliopata kura nyingi ndo ambao unatakiwa utekelezwe...

Kuongezea tu alichosema mkuu, Soko la awali hisa (zitokapo mara ya kwanza) ndipo huwa na kiwango cha juu aruhusiwacho mtu, lakini katika secondary market (soko la hisa) hakuna limit ya juu.

Lakini mara nyingi ununuapo mara ya kwanza utaambiwa uanzie na si pungufu ya hisa 50, au 100 kulingana na kampuni. Kizingiti kinaweza tu kuwa upatikanaji - maana unauziwa hisa auzazo mtu.
 
Ni kweli kwamba biashara iliyo nzuri - uwezekano mkubwa italipa vizuri kuliko mapato ya hisa katika kampuni. Lakini watu, na hata wafanya biashara wakubwa, bado huwekeza katika hisa, labda kwa sababu ya risk iliyo ndogo kuliko katika biashara zao.

Lakini pia sio wote tunaweza kufanya biashara kwa mafanikio. Mimi binafsi kwa sababu mbalimbali naogopa kufanya biashara moja kwa moja, na wengi pia huogopa. Na katika wanaofanya biashara wengi tu huishia kupoteza mitaji bila kuambulia kitu. Ukishanunua hisa, pamoja na faida kutokuwa kubwa sana, huhangaiki kusimamia, na risk ni kidogo.

Umeuliza nini Unit Trusts - Hii ni mifuko ya uwekezaji wa pamoja inayoendeshwa kitaalamu na kisheria. Wewe unanunua vipande, na unafaidika kwa au magawio au kukua kwa thamani au vyote.

Hapa Tanzania tuna Tanzania Unit Trust ambao wanauza vipande vyao vya mifuko kama Umoja, Jikimu, wekeza maisha na kadhalika. Unaweza kwenda Sukari House Dar makao yao makuu kwa maelezo zaidi.
 
Back
Top Bottom