Nipo mjini Njombe kwa zaidi ya wiki moja sasa. Njombe ni mji mzuri wenye shughuli nyingi za uchumi. Shughuli za uzalishaji wa mbao, kilimo cha parachichi na vanilla ni miongoni mwa zile zinazobamba mno.
Nimetembelea soko kuu la Njombe ambalo jiwe la msingi la ujenzi wake liliwekwa na Mh Jafo, Agosti mwaka jana 2020. Ujenzi wa soko hili umekamilika na limeshaanza kutumika. Design ni nzuri likiwa na mifumo ya kisasa ya kuzima moto na jenereta mbili za umeme wa dharura.
Hata hivyo,workmanship ni very poor! Sakafu na plaster zimeanza kubomoka! Kwa ujumla,kwa kuangalia tu kwa macho,viwango havijazingatiwa kabisa.
Halikadhalika, jenereta za dharura hazifanyi kazi! Jazijawahi kufanya kazi! Wafanyabiashara wa soko hilo wanadai waliambiwa zinafua umeme mkali hivyo zikiwashwa zitaunguza vifaa vyao.
Kwa kuwa mradi huu umegharimu mabilioni, fedha za walipakodi au mikopo ambayo watalipa wananchi wa Tanzania,nimuombe waziri Ummy Mwalimu aunde tume ya kuchunguza mradi wa ujenzi huu, na wale wote watakaobainika kuhusuka na uzembe/ufisadi huu wachukuliwe hatua. Kwa performance hii, mkandarasi aliyetekeleza mradi huu asipewe kazi yoyote tena na serikali ya Tanzania.
Kazi iendelee.....
Nimetembelea soko kuu la Njombe ambalo jiwe la msingi la ujenzi wake liliwekwa na Mh Jafo, Agosti mwaka jana 2020. Ujenzi wa soko hili umekamilika na limeshaanza kutumika. Design ni nzuri likiwa na mifumo ya kisasa ya kuzima moto na jenereta mbili za umeme wa dharura.
Hata hivyo,workmanship ni very poor! Sakafu na plaster zimeanza kubomoka! Kwa ujumla,kwa kuangalia tu kwa macho,viwango havijazingatiwa kabisa.
Halikadhalika, jenereta za dharura hazifanyi kazi! Jazijawahi kufanya kazi! Wafanyabiashara wa soko hilo wanadai waliambiwa zinafua umeme mkali hivyo zikiwashwa zitaunguza vifaa vyao.
Kwa kuwa mradi huu umegharimu mabilioni, fedha za walipakodi au mikopo ambayo watalipa wananchi wa Tanzania,nimuombe waziri Ummy Mwalimu aunde tume ya kuchunguza mradi wa ujenzi huu, na wale wote watakaobainika kuhusuka na uzembe/ufisadi huu wachukuliwe hatua. Kwa performance hii, mkandarasi aliyetekeleza mradi huu asipewe kazi yoyote tena na serikali ya Tanzania.
Kazi iendelee.....