Kufunga mikanda hakuna haja, kwanini ufungishe watu wako mikanda? Wakati unaongoza watu kuwapa mafanikio na maisha Bora? Wala soko huria siyo kikwazo maana kama ni kikwazo mbona miundo mbinu ni mipango ya Nchi lakini watu wanakosa barabara? Maji, hospital, mashule nani amewazuia kujenga? Sasa hivyo vitu vidogo vidogo kama nguo watu wakivaa za nje na za hapa shida ipo wapi? Maisha mazuri ndo Mungu anapenda Kila mtu Aishi hivyo vitu vikipatikana kwa wingi ndo watu wataishi kwa kuchagua kipi watapenda kutumia maana dunia ishakuwa kijiji yule atakayetengeneza vilivyobora ndo vitu vyake vitapedwa zaidi.Soko huria, hasa hili soko huria la kulazimishana ni hatari sana kwa maendeleo ya nchi maskini.
Kanuni ya soko huria ni kuondoa vikwazo vya biashara kati ya nchi na nchi. Watetezi wake wanadai kuwa ni njia rahisi ya kuleta maendeleo. Lakini kiukweli siyo kabisa. Nchi zote zilizoendelea zilikuwa kinyume kabisa na soko huria. Zilizuia bidhaa kutoka nje kwa kuweka kodi kubwa, kusingizia usalama, ubora na marufuku. Jambo hili lilifanya viwanda vyao vya ndani kukua.
Vilipokuwa na kuweza kushindana ndipo wakaanza kuhubiri soko huria. Hiki kipindi cha protectionism ndicho kilifanya viwanda vyao vichanga kukua. Nchi zote zilizoendelea zimepitia njia hii. Hakuna nchi imewahi endelea kwa kufuata sera za soko huria.
Sababu kuu inayofanya nchi za kiafrika zote kubaki maskini ni kuruhusu soko huria. Na mbaya zaidi nchi zilizoendelea zinazilazimisha nchi maskini kufuata soko huria. Vyombo kama WTO, WB, IMF, AGOA nk vipo kwaajili ya kuhakikisha nchi zote zinafuata soko huria.
Nchi zikienda tofauti zinaadhibiwa. Nchi za EA zilipotaka kupiga marufuku mitumba ili kukuza viwanda vya ndani AGOA ilitishia kuziadhibu.
Lakini hizohizo nchi zikiona soko linawaendea vibaya wanakwepa soko huria kwa visingizio kibao. China ilizikataa Google, Facebook na paypal kwa kusingizia usalama. Marekani imeipiga marufuku Huawei kwa kusingizia usalama.
Nchi za Afrika zitaendelea zitapotambua kuwa adui yao ni soko huria na pale zitakapopata kiongozi mwenye ujasiri wa kupingana na matajiri huku raia wake wakiwa tayari kufunga mikanda ili kukuza viwanda vya ndani.