Soka na Matangazo live ya TV kupitia Computer

BabaDesi

JF-Expert Member
Jun 30, 2007
6,028
3,943
Kwenu Wataalamu JF. Nina maswali mawili ambayo wengi wenu mnaweza kuyaona ni rahisi lakini kwa sisi ambao tumeanza ;kucheza' na Computer baada ya kustaafu kazi ofisi za serikali zisizo na Computer (siku hizi ndio nasikia wanajitahidi kuziweka maofisini!) ni maumivu matupu kutokana na kutokuwa computer savvy. Tuvumiliane.


-Nimekuwa nikiona thread zinazoonyesha link ambazo zitakuwezesha kuona mechi za soka kupitia computer yako. swali. unapoingia katika link hii na kuanza uangalia mpira bila shaka kinacholika ni hela iliyomo kwenye kifurushi cha internet nilicho nacho. Je mechi moja ya dakika 90 inaweza kuwa ni MG ngapi?? Kama nimeweka kifurushi za Zain cha MG 400 kwa shilingi 2300, naweza kuangalia mpira hadi mwisho??


-Nimesoma mahali humu kwamba naweza kupata matangazo live ya vituo vya televisheni kupitia kwenye computer yangu ambayo ni Dell Optiplex GX 620. Je ninahitaji ku-install nini ili kupata matangazo hayo?? Je hicho ninachotakiwa ku-install naweza ku-download na ku-install?? Je nitakapopata matangazo hayo live ya TV nitalazimika kuweka Aerial ili kupata picha safi ama yanakuja yameishajichuja??
Wataalamu, nitashukuru kwa majibu yenu na natanguliza shukurani.
 
Mkuu achana tuu na hiyo habari kama link yako ya Internet ni ya kihivyo...nitafanya research ili kukupa jibu makini ila kwa sasa ushauri wangu ndio huo. Ungekuwa una lipia kwa mwezi na hauna limitation ya download ningekushauri uendelee na mpango wako huo otherwise ni more economical kufunga DSTV!!
 
Kwenu Wataalamu JF. Nina maswali mawili ambayo wengi wenu mnaweza kuyaona ni rahisi lakini kwa sisi ambao tumeanza ;kucheza' na Computer baada ya kustaafu kazi ofisi za serikali zisizo na Computer (siku hizi ndio nasikia wanajitahidi kuziweka maofisini!) ni maumivu matupu kutokana na kutokuwa computer savvy. Tuvumiliane.


-Nimekuwa nikiona thread zinazoonyesha link ambazo zitakuwezesha kuona mechi za soka kupitia computer yako. swali. unapoingia katika link hii na kuanza uangalia mpira bila shaka kinacholika ni hela iliyomo kwenye kifurushi cha internet nilicho nacho. Je mechi moja ya dakika 90 inaweza kuwa ni MG ngapi?? Kama nimeweka kifurushi za Zain cha MG 400 kwa shilingi 2300, naweza kuangalia mpira hadi mwisho??


-Nimesoma mahali humu kwamba naweza kupata matangazo live ya vituo vya televisheni kupitia kwenye computer yangu ambayo ni Dell Optiplex GX 620. Je ninahitaji ku-install nini ili kupata matangazo hayo?? Je hicho ninachotakiwa ku-install naweza ku-download na ku-install?? Je nitakapopata matangazo hayo live ya TV nitalazimika kuweka Aerial ili kupata picha safi ama yanakuja yameishajichuja??
Wataalamu, nitashukuru kwa majibu yenu na natanguliza shukurani.

Yes kuangalia Live streaming unahitaji kuwa na bandwidth ya kutosha. Na kwa sababu ni video streaming inahitaji bandwidth kubwa zaidi kuliko Audio streaming.

Zipo site nyingi kama ustream.tv,justin.tv, atdhe.net, etc zote hizi unaweza kuona though not at best quality kama kwenye Televison receiver

Sasa kujua Kisio la unahitaji kiasi gani cha bandwidth jaribu kutembelea Bandwidth Calculator | Web User

Hpo kwenye hiyo site kuna kipengele cha Online radio streamining.

Kwa mujibu wa hiyo site listening online radio kwa masaa mawili utahitaji 30 Mb

So unaweza ku approximate kwa kungalia online /Live video streaming ya dk 90 utahitaji not less than 40 Mb kwa kila mechi

NB: Video trasmision and reception consume more bandwidth than Audio
 
Mkuu kama alivyosema mdau hapo juu, hii habari ya kuangalia mpira au Tv kwny intrnt sababu ni gharama sana na pia bandwithth za hizi network zetu ni ndogo, ndo maana unaweza ukakuta pesa zako zinakwisha na hakuna unachoona sbb ya kusimama simama kwa picha...kwa mfano mechi moja ya dk 90 ni kama GB 1.2, kwa hiyo hizo MB zako 400 ziwe mara tatu
 
Steaming video zinatofautiana quality na quality kubwa zaidi inahitaji bandwidth kubwa zaidi, quality link kama unataka uangalia kwa raha ni around 700-1000Kbps so cha kwanza ni provider wako aweze kukupa hiyo speed consistently kwa mechi nzima, maana ikiwa slower ndo video inaanza kuganda.

Cha pili ni inagharimu kiasi gani.

So tukichukua stream ya 700Kbps for 90 min.

700 x 60 x 90 ÷ 8 ÷ 1024 =
461 MB approx

Stream ya 1Mbps = 675 MB
 
* Maelezo yafuatayo yanatokana na experience yangu.

Kuangalia mpira/soka online ni jambo linalowezekana, na ni kweli kuwa linahitaji bandwidth kubwa na pia uwe na ulimited plan ama bundle kubwa kwa bei nafuu. Kuna streaming website nyingi kama zilizoainishwa hapo juu, ila kwa kuwa nina personal project ya ku-study streaming capabilities na uwezo wa internet providers wetu, kuna software naitumia inayokusanya links nyingi sana kwa mecho moja. Software yenyewe ni SportPlayer 5, ni free, unaipata hapa, SportPlayer - Free software downloads and software reviews - CNET Download.com

Kuhusu kiasi cha MB unachotumia kwa mechi moja, inategemea na quality ya signal/picture ya mechi yenyewe kama ilivyosema hapo juu. Kwa uzoefu wangu, kwa quality iliyo nzuri, unaweza tumia kati ya 3MB mpaka 4MB kwa dakika, which means kwa 90 minutes ni kati 270MB mpaka 360MB kwa mechi.

Hii ina maanisha kwa bundle ya airtel (airtel internet strongly recommended kwa live streaming), ya 400MB kwa shilingi 4500 inakutosha kabisa kuangalia mechi nzima.

Kwa kuwa mimi kwangu ni study, najaribu kuangalia value for money ya kutumia internet kuangalia mpira, naweza kusema somehow ni viable kwa sababu kunaweza kuwa na scenario za mbili:

1) Kwamba wewe ni mtu wa kuangalia mpira kwenye sehemu za kulipia, kiingilio chake kama huku kwetu ni kinywaji, ambacho kama ni soda ni shs 1000 kwa moja, iwapo utakunywa mbili + time yako ya kutoka/kurudi nyumbani inaweza ikarudi kuwa around same 2500/- au zaidi, hasa hasa kwa zile mechi za usiku

2) Iwapo unatumia dstv ambayo ina vary kati ya $70 na $100, iwapo wewe ni mtu wa kungalia labda mechi mbili kwa siku au maximum nne, unaweza ukawa unatumia kati ya shs 5,000 - 10,000 kwa wiki (au maximum ya shs 40,000 kwa mwezi), advantage yake ikiwa unaangalia kile unachotaka tu, siyo kujaziwa channel kibao na dstv usizozihitaji.

Of course kuna suala kubwa zaidi, ambalo ni legality ya unachoangalia, kuna watu wana copyright zao kwenye mpira, huko mbeleni unaweza kukumbana nao.
 
... pia unaweza kutumia TTCL Banjuka internet ikitulia inakuwa poa, usiku ni 500 kwa saa, unlimited usage.
 
So unaweza ku approximate kwa kungalia online /Live video streaming ya dk 90 utahitaji not less than 40 Mb kwa kila mechi

kwa mfano mechi moja ya dk 90 ni kama GB 1.2, kwa hiyo hizo MB zako 400 ziwe mara tatu

Cha pili ni inagharimu kiasi gani.

So tukichukua stream ya 700Kbps for 90 min.

700 x 60 x 90 ÷ 8 ÷ 1024 =
461 MB approx

Stream ya 1Mbps = 675 MB

Kuhusu kiasi cha MB unachotumia kwa mechi moja, inategemea na quality ya signal/picture ya mechi yenyewe kama ilivyosema hapo juu. Kwa uzoefu wangu, kwa quality iliyo nzuri, unaweza tumia kati ya 3MB mpaka 4MB kwa dakika, which means kwa 90 minutes ni kati 270MB mpaka 360MB kwa mechi.

Hii ina maanisha kwa bundle ya airtel (airtel internet strongly recommended kwa live streaming), ya 400MB kwa shilingi 4500 inakutosha kabisa kuangalia mechi nzima.
.
Kwa mujibu wa majibu ya kiasi gani kinatumika kwa mechi moja, utofauti huu unaonyesha inategemea mambo mengi pengine streaming tv unayotumia na speed ya ISP wako. maana kuna kuanzia 40 Mb hadi 1.5 Gb per mechi.
Swali ambalo sijaona jibu lake ni je unahitaji kuinstal software yoyote ili uweze kuona hizo live tv?
 
Kwa mujibu wa majibu ya kiasi gani kinatumika kwa mechi moja, utofauti huu unaonyesha inategemea mambo mengi pengine streaming tv unayotumia na speed ya ISP wako. maana kuna kuanzia 40 Mb hadi 1.5 Gb per mechi.
Swali ambalo sijaona jibu lake ni je unahitaji kuinstal software yoyote ili uweze kuona hizo live tv?

Kuangalia mpira/soka online ni jambo linalowezekana, na ni kweli kuwa linahitaji bandwidth kubwa na pia uwe na ulimited plan ama bundle kubwa kwa bei nafuu. Kuna streaming website nyingi kama zilizoainishwa hapo juu, ila kwa kuwa nina personal project ya ku-study streaming capabilities na uwezo wa internet providers wetu, kuna software naitumia inayokusanya links nyingi sana kwa mechi moja.

http://download.cnet.com/{value=http://www.download.com/sportplayer/3000-2136_4-75328359.html
 
Kuangalia mpira/soka online ni jambo linalowezekana, na ni kweli kuwa linahitaji bandwidth kubwa na pia uwe na ulimited plan ama bundle kubwa kwa bei nafuu. Kuna streaming website nyingi kama zilizoainishwa hapo juu, ila kwa kuwa nina personal project ya ku-study streaming capabilities na uwezo wa internet providers wetu, kuna software naitumia inayokusanya links nyingi sana kwa mechi moja.

SportPlayer - Free software downloads and software reviews - CNET Download.com
Mkuu ntaipakuwa hii software niijaribu na mimi, natumia sasatel kwa bundle ya 1.5 Gb kwa sh7500 kwa wiki inanitosha sana.
Kuna maelezo yoyote ya ziada kuhusu utumiaji wake, maana umesema inakusanya link nyingi kwa mechi moja
 
Mkuu ntaipakuwa hii software niijaribu na mimi, natumia sasatel kwa bundle ya 1.5 Gb kwa sh7500 kwa wiki inanitosha sana.
Kuna maelezo yoyote ya ziada kuhusu utumiaji wake, maana umesema inakusanya link nyingi kwa mechi moja

Ukisha install, click kwenye updates, kisha click mechi uitakayo, hasa zenye status ya live
 
Ukisha install, click kwenye updates, kisha click mechi uitakayo, hasa zenye status ya live
Mkuu ipo powa, inaonyesha safi kabisa ila kwambali sana inakatika katika (ISP anadai anatoa 3.1 Mbps),any way ntaifanyia utafiti jioni nikiwa home
But all in all it worth watching
 
Kwa mujibu wa majibu ya kiasi gani kinatumika kwa mechi moja, utofauti huu unaonyesha inategemea mambo mengi pengine streaming tv unayotumia na speed ya ISP wako. maana kuna kuanzia 40 Mb hadi 1.5 Gb per mechi.
Swali ambalo sijaona jibu lake ni je unahitaji kuinstal software yoyote ili uweze kuona hizo live tv?

Yah inategema lakini sijui wataalam wengine wamepataje hizo takwimu. ile link niliweka naona iko broken kuna nyingine hii inatoa simple but clear picture https://ben.cheetham.me.uk/resources/net/data-usage-calculator

Lakini kusikiliza au kuona streaming kama ulivyosema inategemea zaidi na quality ya ISP. yaani uwez wa modem kudowload/kuuplaod.

Mfano tembelea hapa the World Family of Radio Maria

Ukienda kwenye Radio maria Tanzania utaona wana stream matangazo yao katika High quality na low quality. Wanaposema Low quality sana sana ni kwamba msikilizaji atachelewa kidogo kupata matangazo tofauti na yule anasikiliza katika high quality. Sasa hii Low a high quality ni viwango vya warushaji ambayo inaweza kuathiriwa na Uwezo wa mpokeaji (ISP). Kama ISP wako hakupi Dowload ya kutosha unaweza usione tofauti ya high quality na low quality streaming

So inachanganya saababu inategemea mrushaji na mpokeaji. Na kwa upande wa hapa bongo tunaweza usema ISP na modem zetu bado uwezo wake ni very low quality in terms handling Live event streaming


Kuhusu software sio lazima uwe na software maalum zaidi ya flashplayer ila sometime inabidi inategema unata kungalia kupitia streaming tovuti gani

Mfano


 
Back
Top Bottom