Soda vs uzito, utipwtipwa na unene kupita kiasi

Fadhili Paulo

JF-Expert Member
Sep 1, 2011
3,211
988
SODA VS UZITO NA UNENE KUPITA KIASI:

Baada ya kuona namna kutokunywa kwetu maji na kutokujishughulisha na mazoezi hasa ya kutembea kwa miguu kunavyochangia kuongezeka kwa unene, utipwatipwa na uzito kupita kiasi katika post iliyoenda kwa kichwa: 'Chanzo cha vitambi, uzito na unene kupita kiasi', sasa tuone namna unywaji soda unavyochangia kuongezeka kwa tatizo hili. Twende pamoja.

kwa mjibu wa utafiti wake, dr.Batmanghelidj, anasema, ingawa soda hazina kalori inayoweza kuainika, zinaweza kuwa kisababisho cha kuongezeka uzito kupita kiasi kwa wale wanaozinywa kwa malengo ya kudhibiti uzito wao.

Kitendawili hiki katika uelewa wetu juu ya uhusiano baina ya unywaji wa vimiminika ambavyo havichangii moja kwa moja uchukuaji wa kalori wa mwili na kuongezeka kwa uzito, kinahitaji ufafanuzi. Kwa mjibu wa utafiti huo, kuna watu wengi waliochukua uamuzi wa kunywa soda ili kudhibiti uzito, lakini matokeo yamekuwa kinyume chake.

Viwanda vya vinywaji vinakuwa kwa kasi kubwa (apace), jarida la The Nation la aprili 27, 1998 liliripoti kuwa, watoto na vijana walio wengi wanakisiwa kunywa mpaka galoni 64 za soda kwa mwaka, kiasi ambacho kiliongezeka mara tatu zaidi tangu mwaka 1978, kikaongezeka mara mbili zaidi kwa mafungu ya umri kati ya miaka 6-11 na kuongezeka kwa robo kwa watoto chini ya miaka 5(chanzo: utafiti, kitengo cha kilimo 1994, marekani).

Inavutia pia kuandika hapa kuwa, kuongezeka huku kwa matumizi ya soda kwa watoto chini ya miaka 5, kuweza kuwa ndiyo sababu ya kuongezeka mara tatu zaidi ya ugonjwa wa pumu (asthma) kwa watoto wa umri huo kati ya mwaka 1980 na 1994.

Utafiti mmoja katika kampasi ya chuo kikuu cha pennsylvania nchini marekani, ulionesha baadhi ya wanafunzi kunywa soda 14 kwa siku, msichana mmoja alitumia soda 37 kwa siku mbili. Wengi wamekiri kuwa hawataweza kuishi bila vinywaji hivi baridi.

Ikiwa vinywaji hivi vitaondolewa sokoni, watu hawa wataonesha dalili zilizosawa na zile zinazowatokea waliokuwa wategemezi kwa madawa mengine ya kulevya.

Jarida la Boys Life, liliwatafiti wasomaji wake na kugunduwa kuwa, asilimia 8 ya wasomaji wake wanakunywa soda 8 au zaidi kwa siku. Viongozi wa kambi moja ya skauti (boy scout jamboree), walikusanya chupa 200,000 tupu za soda kwa ajili ya matumizi mengine (recycling), chama cha vinywaji baridi kimefanya utafiti juu ya matumizi ya vinywaji hivi baridi mahospitalini nchini marekani na kugunduwa zaidi ya asilimia 85 wakihudumia wagonjwa chakula pamoja na vinywaji hivi baridi.

Kwa kiasi kikubwa, imeaminika kuwa vinywaji hivi vinaweza kuwa mubadala wa mahitaji ya mwili kwa maji. Imedhaniwa kuwa, kwa sababu tu vinywaji hivi vina maji, mwili utakuwa umekamilishiwa mahitaji yake ya maji. Dhana hii ni potofu.

Kuongezeka kwa matumizi ya soda zenye kafeina,kunaunda vyanzo vingi vya matatizo ya kiafya kwenye jamii zetu. Imani hii potofu kwamba vimiminika vyote ni sawa na maji kwa mahitaji ya mwili, ndiyo chanzo kikuu cha magonjwa kwa mwili wa binadamu ikiwa ni pamoja na kuongezeka kwa uzito kupita kiasi.

Ili kuielewa dhana hii, inatubidi kutambua baadhi ya kanuni rahisi za kianatomia na kifizioloji za ubongo ambazo huongoza hisia za kula na kunywa.

Umbile kubwa la mwili bila mpangilio kwa kusanyiko la mafuta, ni hatua ya mwanzo ya kuanguka kwa mwili wa binadamu, na kwa mjibu wa maoni ya dr.Batmanghelidj, ni matokeo ya kuchagua kusiko sahihi kwa uchukuaji wa vimiminika. Baadhi ya vinywaji vina madhara zaidi ya vingine.

Kafeina, moja ya vitu mhimu katika soda nyingi, ni dawa ya kulevya!!!.

Hii ndiyo sababu kwa wale waliozoea kunywa chai ya rangi asubuhi wasipokunywa hujisikia kichwa kuuma (they are addicted).

Ina sifa ya kumfanya mtu mtegemezi kwayo sababu ya matendo yake moja kwa moja kwenye ubongo. Inaingilia pia katika ini na kusababisha kuongezeka kwa uzarishaji wa mkojo.

Hivyo, kafeina ni kikojoshi (diuretic).

Kifiziolojia, kafeina ni wakala mkausha maji mwilini. Hii ndiyo sababu mtu analazimika kunywa soda nyingi kwa siku bila kutosheka. Maji hayabaki mwilini kwa muda mrefu.

Wakati huo huo, watu wengi wanajichanganya kwa kutokutambua hisia zao za kiu kwa kudhani kuwa wamekunywa maji ya kutosha toka katika soda, wanajihisi kuwa ni wenye njaa na kuanza kula chakula zaidi ya mahitaji yao ya mwili. Kwa hiyoupungufu wa maji (dehydration) uliosababishwa na vinywaji baridi venye kafeina, kwa muda utasababisha kuongezeka kwa uzitokutokana na kula kupita kiasi ambako ni matokeo ya moja kwa moja ya kushindwa kuzielewa hisia za njaa na kiu.

Kafeina, ni kiamsho (pick-me-up), husisimua ubongo na mwili hata wakati mtu amechoka. Inajionesha kuwa, kafeina hupunguza udhibiti wa stoo ya kwanza ya ubongo (ATP). Hifadhi hii ya kwanza hutumika kwa baadhi ya kazi ambazo kwa kawaida zisingeweza kufikiwa kunapokuwa na usawa uliosawa wa hifadhi hii.

Ikitokea soda imeongezwa sukari, walau baadhi ya mahitaji ya ubongo kwa sukari hufikiwa. Ikiwa kafeina inatoa nguvu toka stoo ya kwanza ya nguvu za ubongo kusaidia ufanyikaji kazi, walau sukari yake itarudishia baadhi ya akiba za stoo ya kwanza hata kama matokeo ya mwisho ni matumizi hasi ya ulalo (deficit) ya stoo ya kwanza kwa ubongo.

Mwanzoni mwa miaka ya 1980, kiongeza utamu cha kutengenezwa (artificial sweetener) kiitwacho 'aspartame', kilianza kutumika kwenye viwanda vya vinywaji baridi. Aspartame ina utamu mara 180 zaidi ya utamu wa sukari ya kawaida, bila nguvu yeyote (kalori) izarishwayo nayo.

Aspartame sasa inatumika kama kitu kisicho na madhara kwa sababu Taasisi ya Madawa (Federal Drug Administration ya marekani) imeitetea (deemed it) kama kitu kisicho na madhara kikitumika kama mubadala wa sukari.

Ndani ya utumbo mdogo, aspartame inabadilishwa kwenda transimita nyurolojia mbili, asidi amino aspartame na phenylalamine, vivyo hivyo methyl alikohol au formaldehyde. Inatetewa kuwa Ini huichukulia methyl alikoholi kuwa si sumu. 'Binafsi nafikiri madai haya hutolewa kunyamazisha sauti zinazopinga biashara za vyakula vilivyotengenezwa viwandani vijulikanavyo kuwa na kemikali hatari kwa binadamu - dr.Batmanghelidj'.

Kafeina huibadilisha Adenosine Triphosphate (ATP) kwenda Adenosine Monophosphate (AMP) ambayo ni nishati iliyokwishatumika (ash) na aspartate huibadilisha GuanosineTriphosphate (GTP) kwenda Guanosine Monophosphate (GMP).

Adenosine monophosphate na Guanosine monophosphate zote ni nishati zilizokwishatumika (ash) na husababisha kiu na njaa ili kuzirudishia stoo za nguvu nishati iliyopotea kwenye seli za ubongo. Kwahiyo, unywaji soda husababisha matumizi yasiyo ya busara ya hifadhi za nguvu za seli za ubongo.

Ni ukweli unaojulikana kisayansi kuwa, nishati iliyotumika AMP, huleta hisia za njaa. kafeina husababisha utegemezi (addiction), na watu wanaoitumia mara kwa mara wanatakiwa wajihesabu kama wanatembea katika soda (sodaholics).

Hivyo matumizi ya soda zenye kafeina kwa watu wasiofanya mazoezi lazima yatapelekea kuongezeka uzito, kwa kuzunguka, unywaji wa soda unasisimua kula zaidi sababu ya ubongo kulazimishwa kutumia hifadhi zake za nguvu.

Kumbuka ni baadhi tu ya thamani ya nguvu ya chakula itachukuliwa na ubongo. Sehemu kubwa ya nguvu iliyochukuliwa itahifadhiwa katika mfumo wa mafuta ikiwa haitatumika katika shughuli za mishipa (mazoezi).

Matokeo haya ya uzito kuongezeka kupita kiasi ni moja kati ya matokeo mengine mengi yatokanayo na matumizi ya soda. Kafeina hupatikana pia katika chai ya rangi, kahawa na katika vinywaji vingine vingi vya viwandani.

Tabia moja mhimu inayokuja kujiimarisha ni mwitikio wa ubongo kwa radha za utamu. Lugha ya kitaalamu inayotumika kuelezea mwitikio huu ni, 'cephalic phase response'. Mwitikio huu wa kulazimishwa unakuja kujengwa kama matokeo ya mazoea ya muda mrefu kwa radha zenye utamu zinazoambatana na utambulishaji wa nguvu mpya ndani ya mwili.

Wakati radha zenye utamu zinaposisimua katika ulimi, ubongo unaliamuru Ini kujiandaa kupokea nguvu mpya (sukari) kutoka nje. Ini nalo litasimama kutengeneza sukari toka hifadhi ya protini na wanga ya mwili, na kuanza kuhifadhi nishati ya kimetaboli inayozunguka kwenye mzunguko wa damu.

Kama Michael G Tardoff, Mark I Friedman na wanasayansi wengine, wameonesha kuwa 'cephalic phase' huwa na matokeo ya kuongeza shughuli za kimetaboli ili kuhifadhi lishe, nishati inayopatikana kwa ajili ya mabadiliko hupungua na kusababisha kuongezeka kwa njaa.

Ikiwa ni sukari hasa ndiyo inayosisimua ulimini, matokeo kwenye ini yatakuwa ni urekebishaji wa hicho kilichoingia mwilini. Ingawa ikiwa radha ya utamu haina lishe ndani yake, hisia za kutaka kula zitakuwa ndiyo matokeo yake.Ni Ini ndilo linalotengeneza hisia za kula. Kadiri radha utamu bila kalori ndani yake zinavyosisimua kionjea radha, vivyo hivyo zinavyokuja zaidi hisia za kutaka kula.

Matokeo ya 'cephalic phase' kwa radha za utamu yamethibitishwa katika majaribio kwa wanyama kwa kutumia 'saccharin' (dawa yenye utamu kama sukari). Kwa kutumia aspartame, wanasayansi kadhaa wameonesha matokeo yanayofanana ya kutaka kula kupita kiasi kwa binadamu.

Blundel na Hill wameonesha kuwa viongeza utamu visivyo na kalori hasa aspartame huongeza njaa na kuongeza uchukuaji wa chakula kwa muda mfupi. Wanaripoti, ''baada ya kunyweshwa aspartame, wapendwa waliachwa na njaa iliyobaki ikilinganishwa na walivyoachwa baada ya Glukozi. Njaa hii iliyobaki husababisha kuongezeka kwa matumizi ya chakula''.

Tardoff na Friedman wameonesha kuwa hisia hizi za kutaka kula zaidi chakula baada ya viongeza utamu vya kutengenezwa vimetumika, zinaweza kudumu mpaka dakika 90 baada ya kinywaji kitamu hata wakati majaribio yote ya damu kuonesha thamani ya kawaida. Wameonesha kuwa hata wakati usawa wa damu kwa insulini, usawa wa juu ambao unafikiriwa kuwa unasababisha njaa, umefikia usawa wa kawaida, majaribio kwa wanyama yameonesha hitaji la kutaka kula zaidi ya udhibiti.

Hii inamaanisha kwamba ubongo unashikilia kwa muda mrefu zaidi hisia za kutaka kula inapotokea tezi za kuhisia sukari zimesisimuliwa bila sukari kuwa imeingia kwenye mfumo. Radha utamu husababisha ubongo kuliamuru ini kuhifadhi ziada badala ya kuitumia toka katika akiba za mwili.

Kimsingi, mwitikio huu wa kifiziolojia kwa viongeza utamu bila kuwa na kalori ambazo mwili unazitumainia, unamlazimisha mtu kutafuta kalori hizo kokote na hatimaye kuhitaji kula.

Wakati kafeina na aspartame vimeingia mwilini, huanza kuonesha (dictates) matokeo yake ya kusisimua kwenye fiziolojia ya seli kwenye ubongo, kwenye ini, kwenye figo, kwenye kongosho, kwenye tezi mbalimbali na kadharika.

Aspartame hubadilishwa kuwa 'phenylalanine' na 'aspartate', zote huwa na matokeo ya moja kwa moja ya usisimuaji kwa ubongo. Kwa haraka matokeo ya kafeina na aspartame yanajenga namna mpya za kazi kwa ubongo, kwa sababu vinapatikana kwa kujirudia kwa kiasi kikubwa zaidi ya kile ambacho pengine kingeleta usawa wa kifiziolojia.

Transimita nyurolojia zilizo nyingi, ni mazao ya pili kutoka moja au asidi amino zingine. Hata hivyo aspartate ni moja kati ya jozi ya asidi amino za pekee ambazo hazihitaji kubadilishwa kuwa zao la pili ili kufanya kazi kwenye ubongo. Kuna nukta zinazopokea (receptors) hizi asidi amino mbili kwenye neva seli maalumu ambazo huathiri fiziolojia ya mwili haraka zaidi.

Matumizi ya viongeza utamu kwa usisimuaji wake wa kimakosa wa miishio ya neva ambayo husajili usambazaji wa kuingia wa nguvu kwenye mwili, yana matokeo mengine zaidi yasiyotarajiwa zaidi ya kusababisha kuongezeka uzito kupita kiasi.

Kwa muda wote, kemikali hizi zinaning'inia kwenye fiziolojia ya mwili kwenye mwelekeo unaoamuliwa na mfumo wa neva zinazozisisimua. Matumizi yake bila uelewa wa matokeo yake ya muda mrefu mwilini sababu tu yanasisimua tezi za radha, bado hayajaainishwa.

Utafiti umeonesha kuwa mapokezi ya aspartame yanapatikana pia kwa baadhi ya mifumo ya fahamu ambayo matokeo yake husisimua pia ogani za uzazi na matiti. Usisimuaji wa kudumu kwa tezi za matiti bila sababu nyingine zinazohusiana na ujauzito, unahusishwa kama moja ya sababu za kuongezeka kwa saratani ya matiti kwa wanawake.

Homoni iitwayo prolactini ndiyo inahusika zaidi katika mwelekeo huu. Moja ya vitu ambavyo havijafanyiwa utafiti wa kutosha juu ya madhara ya aspartame, ni matokeo yake ya madhara yanayoweza kupelekea kutokea kwa saratani ya ubongo. Majaribio kwa panya na wanyama wengine, yote yameonesha aspartame kuhusika kutengeneza uvimbe kwenye ubongo.

Dr.H.J.Roberts ameyaainisha baadhi ya matatizo ya kiafya yanayosababishwa na aspartame, na kuyaita yote kwa pamoja kama, 'magonjwa ya aspartame',katika kitabu chake; ''Breast Implants or Aspartame Diseases?'', ameyataja baadhi ya magonjwa kama vile kuumwa kichwa, kizunguzungu, kukosa usingizi, kuchanganyikiwa, kupoteza kumbukumbu, uchovu sugu, kushuka kwa damu sukari, maumivu ya maungio, nywele kupotea, na kadharika, kama ni magonjwa yasababishwayo na aspartame. Ameandika makala na vitabu vingine vingi juu ya mada hii.

Sayansi ya sasa ya kudhibiti kuongezeka uzito kupita kiasi inayohusisha ukatazaji wa baadhi ya vyakula, hata kama baadhi ya kilo zitapungua, zitaongezeka tena baada ya muda mfupi. Cha kushangaza zaidi ni fasheni mpya inayojitokeza siku hizi, mtu anakuwa mtumwa wa kuchagua chakula hiki au kile kama mbwa mnusaji hasa katika suala la helemu (cholesterol).

Usishituke!, ''tofauti na imani iliyojengeka ya kupunguza au kuondoa kabisa matumizi ya mayai katika milo yetu, mimi nakula mayai mengi nitakavyo – dr.Batmanghelidj''. Mayai yana protini nzuri iliyosawazishwa. Anasema, anaelewa pia ni namna gani utengenezwaji wa kolesteroli unavyohusiana na upungufu wa muda mrefu wa maji mwilini (prolonged dehydration).

Ikumbukwe kuwa, kafeina ni dawa ya kulevya(addictive drug) ambayo matumizi yake yamehalarishwa. Watoto wadogo kwa upande wao wanatokea kuwa wategemezi kirahisi zaidi kwa vinywaji vyenye kafeina. Hii ndiyo sababu ya kwanza watoto wengi mashuleni siku hizi hawafundishiki, tunabaki kuwalaumu bure.

Usisimuaji huu wa miili kwa vinywaji vyenye kemikali kwa watoto, hupelekea baadhi yao kuwa wategemezi wa madawa ya kulevya makubwa zaidi wakati wanapokuwa wakubwa.

Kama tulivyofafanua muda wote, mwili hutoa ishara anuwai unapokuwa na maji chini ya kiwango. Wakati huu (uzito unapozidi), mwili unakuwa unahitaji maji pekee.Mwili unaanza kuchanganya habari wakati mtu anapoamua kutumia vinywaji vya kutengenezwa kama mubadala wa mahitaji ya mwili kwa maji.

Kwa hiyo, utumiaji wa muda mrefu na wa kudumu wa soda, lazima uchukuliwe kama moja ya visababisho vya matatizo mengi ya kiafya katika jamii zetu.

"kujielimisha ni kutafuta ukweli wa mambo, kwenda shule hutusaidia tu, japo hatuwezi kwenda shule, twaweza kujielimisha – Mwl.J.k.Nyerere".

Kumbuka kutembelea; www.maajabuyamaji.net
 
Thanx, ni ndefu ila ina mafundisho lukuki inside it......u made it.
 
Thanx Fadhili for another great piece of work..endelea kufikiria kuhusu kuandika columns kwenye gazeti!
 
fp, unaweza kuongelea kidogo kuhusu artificial sweeteners?manake kuna hizi diet drinks na ile sweetex. niliona mahali wanasema inachangia kuhifadhi zaidi kwa mwili.naona umeongelea stimulation ya ini hapo.
 
fp, unaweza kuongelea kidogo kuhusu artificial sweeteners?manake kuna hizi diet drinks na ile sweetex. niliona mahali wanasema inachangia kuhifadhi zaidi kwa mwili.naona umeongelea stimulation ya ini hapo.
I will, ngoja nipekuwepekuwe. thanks
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom